Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.

Hivi wakurya wanaweza kumchagua mwanamke!


.....ndiyohiyo
 
Hivi wakurya wanaweza kumchagua mwanamke!


.....ndiyohiyo


Hawawezi...wakurya karibu wote ninaowafahamu (nawafahamu wengi, nimekua nao..!!!) bado wana mtazamo wa kumuangalia mwanamke kuwa hawezi kuwa kiongozi.

Kwa sababu hiyo sitegemei Chadema wampitishe Esther Matiko kugombea kwa tiketi ya Chama chao. Ila naamini hii kutaka kugomea Tarime ni plan ya Esther kujiweka kwenye top ranks za Chadema ili 2010 agombee tena Viti Maalum.
 

Viti maalum Chadema vina wenyewe...
 
Masatu,Gustanza-The,Mwanakijiji,Rev.K,FMES,YeboYebo,Habari-ndiyo-hiyo,.....

..kwa kweli huyu Dada amenifurahisha na kunipa matumaini.

..kwanza hoja zake zimetulia, halafu elimu imepanda kiuhakika.

..wana-Tarime wakimchagua Esther Matiko watafuta ile dhana kwamba mwanamke hana nafasi sawa na mwanaume huko kwao.
 

Well, I'd rather vote for this woman than voting for Mwita whatever anayedhani kuwa tatizo la Tarime ni ukosefu wa viongozi ambao wanaweza kushirikiana na serikali kuu.

P.S. But she need to be fully vetted kabla ya kupata endorsement yangu.
 
Hatari hatari Tarime.

Vurugu zilizomkuta Dr. Mvungi zinaashiria kitu kikubwa sana katika siasa za Tanzania.
Kwanza watanzania wanaamini kuwa upinzani ni dawa ya kutosha ya kuondoa matatizo ya watanzania.
Pili watanzania wanaamini kuwa nguvu ya upinzania iko katika kuungana. Kwa hiyo kama kukitokea lolote linaloashiria kutokuungana watanzania wanapata hisia mbaya kuwa huo utakuwa upenyo wa CCM kushinda.

Na mimi ninaamini kuwa watanzania walifarijika sana vyama vinne vilipoanzisha ushirikiano. Waliamini kuwa taratibu vyama vingine ambavyo si vya kimamluki vitajiunga. Nguvu ya vyama hivyo kwa pamoja itakuwa kubwa wanaposhirikiana katika majukwaa. Mtizamo wa wananchi kwa vyama hivyo unakuwa kwamba vyama vya upinzani sasa vinafanya siasa ya kulinda maslahi ya taifa zaidi kuliko ya vyama vyenyewe na ya watu binafsi.

DR. Mvungi Rabsha iliyokukuta katika uwanja wa Sabasaba ni ujumbe kuwa wananchi wanawataka mrudi haraka mkakae kwa kuheshimu ushirikiano wa vyama 4 muweke mgombea mmoja. Ni hakika kuwa wanaTarime wanajua chama kilicho na nguvu zaidi pale kwao. Wahojini mapema.

Dr. Mvungi wananchi wanajua mbinu zinazotumiwa na CCM kudhoofisha vita dhidi ya mafisadi. Hatua zinazochukuliwa na wananchi ni utambuzi wa heshima ya makamanda wa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi.
Chonde chonde lipeni chochote ili muiimarishe vita dhidi ya ufisadi.
 

Viti maalumu? Labda abadili jina au aolewe na mtu wa mkoa mmoja kaskazini! kwi kwi kwi!!!
 
kushambuliwa kwa Dr. Mvungi wa NCCR huko Tarime Mara na wanaosemekana ni wafuasi wa CHADEMA Dr. Slaa amebuka na kuwaunga mkono wananchi wa Tarime kweani kauli za mvungi ndio zilimponza. Dr. Slaa amesema haungi mkono vurugu lakini uvumilivu ukifika kikomo yanaweza kutokea yaliyotokea. ameambambia Dr. Mvungi asilaani wananchi bali alaani ulimi wake
 

Sasa hivi imekuwa war for Tarime!Kila chama kinaona ndio wakati wake!
Jamani wapinzani sasa kama jimbo moja tuu ndilo linalowagombanisha mtaweza kweli kuungana na kuwa kitu kimoja kwenye uchaguzi mkuu?
Mnavunja watu moyo kweli ndio maana hata morale ya kuwaunga mkono inapungua watu wanaamua CCM wapete tuuuuuuuu!
 
kwa kauli hizi na yaliyomtokea Dr. Mvungi huko... nini hatma ya upinzania nchini?
 
kwa kauli hizi na yaliyomtokea Dr. Mvungi huko... nini hatma ya upinzania nchini?

Ndivyo upinzani unavyotakiwa kuwa, na sio vyama kuungana na kushindana na CCM tu
Bali kila chama kitumie jitihada zake kukishinda chama kingine chochote kilichosajiliwa
 
Kwa mtindo huu CCM itarudisha jimbo la Tarime katika himaya yake.Vita ya panzi furaha ya kunguru.
 
Ndivyo upinzani unavyotakiwa kuwa, na sio vyama kuungana na kushindana na CCM tu
Bali kila chama kitumie jitihada zake kukishinda chama kingine chochote kilichosajiliwa

That will nevr happen in TZ.Unless they unite they will never get anyway coz as they always put it "Stand Together Coz You Are Stronger United"
 
Taabu ni kuwa kuna viongozi wa upinzani ambao ni mamluki na haya yalionekana hata wakati wa msiba wa Wangwe,walipotumika kuwachafua wengine kwa kutumia kifo kile.
Sasa msiba umekwisha na watu wametulia na kutafakari nini kilitokea, Kiongozi akija na kutaka kutumia Habari ya kifo cha Wangwe(RIP) kama karata ya kupata kura anajitafutia kupigwa mawe bure.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…