Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Haya mambo watu wanajifanya kumlaumu Mtikila hawajui kibao kinaweza geuka.
Mtikila KASEMA na anayeona hatendewi haki angechukua vipeperushi hivyo akatinga navyo mahakamani
Sitoshangaa na siku zaja
Pale DR SLAA atakapobondwa mawe kwa kuwaita jamaa MAFISADI maana atakua naye ni mchochezi.
Ama siku hiyo mtasema ambaye hakupendezwa na maneno yake angeenda polisi na mahakamani??
1. Kusema mtu amemuua mwingine ni kosa la jinai. Mwenye wajibu wa kufungua kesi ni jamhuri. Sio Mbowe, Mengi, Slaa, Mnyika wala Zitto. Hivyo, polisi wamkamate Mtikila.
Keep it to yourself kwa kuwa nishaijua hiyo ya kwako na undoubtly itakuwa bias!
Kwa sheria ipi hiyo mkuu? Hilo sio kosa la jinai. Ukiachia makosa madogo madogo, makosa ya jinai ni kama hapa chini.
Kanuni ya Adhabu ya Tanzania imegawanya makosa ya jinai katika aina mbalimbali. Lakini aina kuu ni makosa dhidi ya serikali kama vile uhaini na ujajusi; makosa yanayohusiana na mali kama vile wizi, makosa yanayokiuka itikeli mathalan kulawiti na kubaka; na makosa dhidi ya mwili kama vile mauaji ya kukusudia na yasiyo ya kukusudia pamoja na ujambazi.
Kwa alichosema Mtikila, polisi wanaweza kumhoji ili kama ana ushahidi zaidi basi aisaidie polisi si lakini si vinginevyo.
Lazima pia ujue huko nyuma serikali wamewahi kutumia sheria mbalimbali za kimabavu kumshitaki mtikila kwa matamshi yake kama vile kwenye kifo cha Kolimba na bado hawakufanikiwa kwasababu sio rahisi kumshitaki mtu kwa makosa kama hayo kwa kutumia sheria ya makosa ya jinai.
exactly, anayevunja sheria au ukihisi umevunjiwa sheria nenda polisi! Ukiona polisi hawakusikilizi tumia haki yako ya kujitetea.
kuna makosa ya maneno kama libel, defamation of character n.k. Lakini kwenye nchi yetu bado tuna sheria za kikoloni zinazohusu "uchochezi" na believe me zingekuwa zinafuatwa wengi wangekuwa hawasemi wanayosema leo.
Lakini mtu akidai "x ni mwizi" halafu watu wakamkimbilia yule mtu na kumpiga mawe kwa kuamini kilichosemwa kuwa "x ni mwizi" nani ana makosa? Vipi kama hakuwa mwizi? Je yule aliyetoa wito huo kuwa "x ni mwizi" ana wajibika kwa maneno yake hayo?
haki ipi ya kujitetea ? Kama una silaha ufyatue kama unaweza mapigano mpigane ?
mwanakijiji asante kwa kufafanua hili , nimeona watu wengi mitaani huko akikuchoka ni kuitana mwizi kibaka na cha moto utakiona kuna umuhimu wa sheria hizi kuangaliwa kwa makini
sijawahi kusikia mtu ameshitakiwa kwa kumwita mwenzake mwizi akashitakiwa hata sikumoja
Lakini mtu akidai "x ni mwizi" halafu watu wakamkimbilia yule mtu na kumpiga mawe kwa kuamini kilichosemwa kuwa "x ni mwizi" nani ana makosa? Vipi kama hakuwa mwizi? je yule aliyetoa wito huo kuwa "x ni mwizi" ana wajibika kwa maneno yake hayo?
Mwanakijiji,
Mfano wako una uhusiano gani hapa? Kama Mbowe angepigwa kwasababu Mtikila kasema hivyo japo ningeelewa. Mbona hao vijana hawakumpiga Msekwa kwa kusema maneno karibu na hayo?
Mbowe na hao viongozi wengine wanaodaiwa na Mtikila kwamba wameua, waende mahakamani na huko ndiko haki inapatikana.
Adhabu nyingine ni ya kisiasa kwa wananchi wa Tarime kumdharau Mtikila na kuwanyima kura wale anaowaunga mkono.
picha hiyo ya Mhe. mch. Mtikila baada ya kupata matibabu yaliyotokana na kipigo.
HALI imezidi kuwa mbaya kwenye kampeni za uchaguzi wa mbunge na diwani wilayani Tarime, baada ya Mwenyekiti wa chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila kupigwa mawe na kujeruhiwa baada ya kudai kwenye mkutano wa hadhara kuwa Chadema ilimuua mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Chacha Wangwe.
Mashambulizi hayo yamekuja siku moja baada ya Kamanda wa Operesheni ya Jeshi la Polisi, Venance Tossi, kutangaza kuwa atatumia nguvu kudhibiti wafuasi wa vyama vya upinzani -Chadema na CUF- kwa madai kuwa wana vurugu, na pia ikiwa ni siku moja baada ya kiongozi wa Chadema kuuawa kwa risasi katika mapigao yanayodaiwa kuwa ya ukoo.
Mtikila, ambaye ni maarufu kwa kutoa tuhuma kali bila ya woga, aliwahi kutoa tuhuma hizo kwa Chadema mapema mwezi huu, akihusisha kifo cha mbunge wa jimbo la Tarime na mgongano wa kikabila ndani ya chama hicho na kumuhusisha mfanyabiashara mmoja maarufu.
Lakini jana, hakupewa nafasi ya kuendelea na tuhuma hizo kwa Chadema na badala yake wale waliokuwa akiwahutubia waliamua kumshambulia kwa mawe na kumjeruhi kiasi cha kushonwa nyuzi saba.
Mchungaji huyo wa makanisa ya ufufuo alikuwa ameanza kueleza kifo cha Wangwe ambaye alifariki kwenye ajali ya gari ndogo wakati akisafiri kutoka Dodoma kuelekea Dar es salaam kuhudhuria mazishi ya mfanyabiashara Bhoke Munamka.
Wakati akiendela kuwahutubia wananchi na kuituhumu Chadema kuwa ndio iliyomuua mbunge huyo wa zamani wa jimbo hilo, ghafla alipondwa na jiwe baada ya kuwa amegeukia upande wa kulia na hivyo kujeruhiwa kichwani.
Shambulizi hilo lilisababisha mkutano huo wa hadhara kukatishwa wakati wasaidizi wake walipoanza harakati za kutafuta usafiri wa kumkimbizia hospitali ambako alitibiwa na kushonwa nyuzi saba.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 11:00 jioni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Sabasaba mjini Tarime.
Kifo cha Wangwe kilizua utata mkubwa kutokana na uhusiano wa muda mfupi baina yake na kijana anayedaiwa kuwa alikuwa akiendesha gari hilo, Deus Mallya, ambaye kwa sasa amefunguliwa mashtaka ya makosa yanayohusiana na usalama barabarani, mazingira ya ajali hiyo na mtu hasa aliyekuwa akiendesha gari hilo.
Awali ilisemekana kuwa Wangwe, ambaye alikuwa akijulikana pia kwa kuzua hoja tata bungeni, aliuawa kwa kupigwa risasi, lakini baada ya uchunguzi ilibainika kuwa kifo chake hakikutokana na kushambuliwa kwa risasi.
Lakini Mtikila amekuwa akishikia bango kifo hicho na wiki chache zilizopita aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kuwarushia shutuma viongozi wa Chadema na mfanyabiashara mmoja kuwa ndio waliosuka njama za kumuua Wangwe, ambaye alikuwa akiripotiwa kuwa na mgogoro na viongozi wenzake wa chama hicho kiasi cha kusimamishwa wadhifa wake wa makamu mwenyekiti.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutibiwa,Mtikila alisema analitupia lawama Jeshi la Polisi kutokana na shambulio hilo la mawe ambalo anadai kuwa alishataarifu mapema kuwa kulikuwa na njama ambazo alidai zilipangwa na Chadema.
Mchungaji huyo matata alisema mara baada ya kufika mjini Tarime alipata taarifa za kufanyika kwa mkutano wa kiongozi mmoja wa Chadema na kwamba katika mkutano huo, kiongozi huyo aliwaagiza wafuasi wake kuhakikisha wanamshambulia kwa mawe ili kumdhibiti yeye asisambaratishe chama hicho.
Nilitoa Taarifa mapema kwa msimamizi wa Uchaguzi na OCD, niliwaeleza juu ya agizo la mimi kupigwa mawe, lakini nashangaa polisi hawakuweza kuleta ulinzi mkali kwangu licha ya kutoa taarifa hiyo, alieleza mchungaji huyo.
Alisema kitendo cha kupigwa mawe si cha kiungwana na kwamba kimemsikitisha kwa kuwa anaamini kuwa siasa ni majibizano na hoja na wala si vurugu.
Hata hivyo, mchungaji mtikila alisema kuwa hatasitisha kampeni zake na kwamba leo ataendelea na kampeni za chama chake kumnadi mgombea wake mchungaji, Denison John Manyika.
Kabla ya mkutano huo, Mtikila alifanya mkutano katika kijiji cha Nyamwaga na Sirari ambako alikuwa akisisitiza na kueleza kuwa marehemu Wangwe ameuawa.
picha hiyo ya Mhe. mch. Mtikila baada ya kupata matibabu yaliyotokana na kipigo.
Si mara ya kwanza Mtikila kupata matatizo kutokana na Kauli zake*****Kama kiongozi na Mchungaji anapaswa kujua anazungumza nini? na anazungumza na nani?****Kama ana uhakika kuwa Wangwe kauawa na watu wa Chadema,kwa nini asipeleke ushahidi huo Mahakamani?****Alitegemea nini kusema kuwa "Chadema wamemuua Wangwe?" na kibaya zaidi maneno hayo unayasemea Tarime.....ambako wamethubutu kutupia mawe hata gari la Makamu wa Mwenyekiti wa Chama Tawala?.
Nampa Pole zangu Mtikila...Lakini pia nae anapaswa kusoma Wakati *****Huwezi kwenda kuhubiri mambo ya Ukatoliki, Jalalabad au kufungua Duka la nyama ya Nguruwe Mecca....