Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
ha-ha-ha-hah!
Makamba sijui tumfananishe na nani.



.
...Tena nina wasi wasi na IQ ya huyu mzee maana wakati mwingine ukisikiliza anachozungumza utashindwa kuelewa kama alienda hata shule kidogo au ndio bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi...

I wish ningepata CV yake nione alikotokea......
 
Watu kama Msekwa, Kingunge na Makamba ni bora wafe tu kuliko kuwa hai maana ni kero na mzigo kwa wananchi wa Watanzania. Wanakula kodi za watanzania na bila aibu wanatukejeri.
 
[Source Tanzania Daima]


Vijana 30 wa CHADEMA waswekwa ndani


na Mwandishi Wetu, Tarime


ZAIDI ya vijana 30 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamekamatwa na polisi wilayani Tarime kwa kile kilichodaiwa kuwa ni operesheni kamata wazembe na wazururaji.

Operesheni hiyo ilianza jana asubuhi ambapo askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), walimwagwa katika mitaa yote ya mji mdogo wa Tarime, hususan katika vijiwe maarufu vya wafuasi wa CHADEMA.

Vijana hao ambao hadi sasa bado wapo ndani, walifikishwa katika Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Tarime ambapo Mkuu wa Kituo hicho (OCD), aliwataka viongozi wa chama hicho waliokuwa wakiwafutilia vijana hao, kuacha kumwingilia katika kazi zake.

Akizungumza katika mikutano mitatu ya kampeni katika vijiji vya Mrito, Karende na Kewanja, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema kitendo cha Serikali kumwaga polisi wengi katika jimbo hilo, kinawatisha wananchi.

Dk. Slaa ambaye alikuwa akimnadi mgombea wa CHADEMA, Charles Nyanguru, alilalamikia kauli za Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa na Katibu Mkuu, Yusuph Makamba, kwamba wametumwa na Rais Kikwete, kuangalia hali ya vurugu ili wamjulishe rais.

“Kauli hiyo ni ya vitisho na kamwe hapaswi kutolewa na viongozi hao. Tunasema serikali ndiyo inayojenga mazingira ya hofu katika uchaguzi huu, wakati wananchi hawana mpango wa kuanzisha vurugu,” alisema.

Dk. Slaa alisema katika mkutano huo kuwa ana ushahidi wa kikao cha Makamba cha Septemba 19 kwamba Jimbo la Tarime liwe mikononi mwa CCM kwani wana pesa na polisi, hivyo hawana sababu ya kushindwa.

Alisema kutokana na hali hiyo, ndiyo maana polisi mjini hapo, wamekuwa wakitekeleza maagizo ya CCM ya kuwakamata vijana wanaoonyesha alama ya vidole viwili, inayotumiwa na CHADEMA.

Dk. Slaa alisema serikali inataka kulifanya Jimbo la Tarime kama visiwa vya Zanzibar katika uchaguzi kwani matokeo wanayoyafanya, yanaonyesha ni jinsi gani wanataka kuleta vurugu.

Katika mkutano huo, Dk. Slaa, alimlaumu Rais Kikwete kuwa amekuwa bingwa wa kusuluhisha matatizo ya nchi jirani kama vile Kenya na Zimbabwe wakati Zanzibar ikibaki katika uhasama na sasa hali hiyo inataka kupandikizwa Tarime.

Aliwataka wananchi hao kuacha kumpigia kura mgombea wa CCM kwani hataweza kuwaletea maendeleo na badala yake wamchague mgombea wa CHADEMA ili kumalizia kazi iliyoachwa na marehemu Chacha Wangwe.

Naye mgombea CHADEMA, Nyanguru, aliwaahidi kuwatetea vijana, hasa katika operesheni za aina hiyo ambazo alisema ni za kinyanyasaji.

Uchaguzi katika jimbo hilo utafanyika Oktoba 12.

Hizi habari za kuwa na ushahidi wa vikao za Dr. Slaa zinatia shaka. Dr., tafadhali kuwa makini na usemayo, tuko wengi tunaotegemea nguvu za maneno usemayo.
 
Oyaa,
Baada ya ile debate kati yangu nawe kwenye suala la Mtikila na maneno yote uliyotoa, ilibidi nichukue muda wa kutosha kukusoma ili nijue na-debate na mtu wa aina gani. So far nina very good picture of you kutokana na nilichosoma.

Inaelekea unao muda mwingi wa kupoteza maana kusoma postings >1000 sio mchezo, halafu bahati mbaya bado umeibuka na wrong conclussion. Sijui kwenye debate unaangalia sura au unajadili yaliyoandikwa. Shinda hoja kwa hoja lakini ukitaka ku-debate tu na mtu atakayesifu yale uliyoandika, basi mimi sio mmoja wao. Kwangu siangalii sura, naangalia maandishi. Tunaweza tukawa upande mmoja leo, halafu kesho tukapambana kwenye opposite sides.



Yaani ndicho kinachofanyika - na ndicho baadhi ya watu waliojaribu kuuliza hili kule Nyamongo "walipatikana na hatia ya kuwa mgodini bila kibali". Ambacho bado sijakupata vizuri ni - unataka picha za matukio au unataka kujua kiasi kilichomwagwa? au unataka kujua siku ngapi kwa wiki inamwagwa, au data unazotaka hapa ni zipi hasa?
Asante

Kumwaga maji ndani ya mto tokea mgodini sio kitu cha ajabu na sio kosa. Kosa ni kumwaga hayo maji yakiwa hayajasafishwa. Sasa kama unao ushahidi kuwa maji yanayomwagwa yana CN utufahamishe.

Kama uliwahi kuyafanyia test hayo maji wanayomwaga, au labda kuna watu/wanyama waliokufa au kujeruhiwa na hiyo sumu, hizo ndio shahidi unazotakiwa kutueleza kuwa unazo. Vinginevyo unayoongea ni porojo tu.

Mtu kama hana kibali cha kuingia ndani ya eneo la mgodi ni lazima akikutwa atakamatwa na hiyo sio kielelezo cha kuwepo kwa CN.
 
Nijuavyo mimi sio kawaida kwa rais kwenda ku kampeni kwenye chaguzi ndogo. Ninategemea kiongozi wa upinzani aende labda kuwe na sababu kubwa sana.

Pia Mbowe nilisoma hapa kwamba anapendwa sana Tarime, sasa kwa mtu anayependwa si ndiye anafaa kwenda kuongoza kampeni?

Hakuwepo wakati wa mazishi ya Wangwe, asipoenda kwenye kampeni, huhitaji kuwa genius kujua maana yake.

Kuna sehemu nilisoma kama Mbatia emeenda au anaenda. Sina taarifa kuhusu Lipumba, je CUF pia wameweka mgombea wao?

kwi kwi kwi kwi kwi kwi

anasubiri kupeleka mashambulizi ya angani na HELKOPITA kama alivyoshambulia KITETO akateketeneza na wanajeshi wake.

Nilifikiri ameshatua kumbe bado hajatokea tu.

kwi kwi kwi kwi
 
Hivi Mbowe, mwenyekiti wa CHADEMA ameenda Tarime kwenye kampeni?


Kwani ni Lazima? Kwa hiyo unataka tuwe kama CCM kuprleka chama chote kule? Mkuu hujajua tu kwamba CHADEMA ni tofauti sana na CCM? Hata rangi tu zinatosha kutofautisha kwi kwi kwi!

Btw: Dawa ya CCM kutumia Dola ni ndogo sana.Wao ndio hawajali kabisa damu ya wananchi,sina la kuwashamgaa maanke hata huo moyo wa huruma wangekua nao wasingelifilisi taifa hivyo.Nitakuja kuwaonyesha kwa vitendo kwamba Watanzania wanataka haki.

Idumu Nguvu ya umma
 
Kwani ni Lazima? Kwa hiyo unataka tuwe kama CCM kuprleka chama chote kule? Mkuu hujajua tu kwamba CHADEMA ni tofauti sana na CCM? Hata rangi tu zinatosha kutofautisha kwi kwi kwi!

Btw: Dawa ya CCM kutumia Dola ni ndogo sana.Wao ndio hawajali kabisa damu ya wananchi,sina la kuwashamgaa maanke hata huo moyo wa huruma wangekua nao wasingelifilisi taifa hivyo.Nitakuja kuwaonyesha kwa vitendo kwamba Watanzania wanataka haki.

Idumu Nguvu ya umma

Ben,

Hapo ndipo ninapowashangaa CHADEMA, badala ya kukubali ukweli kwanini mwenyekiti wenu hajaenda Tarime mnaanza kuja na hadithi za Abunuwas kibao.

Sawa endeleeni kujidanganya, ila tu wengine hamuwezi kutudanganya kama mnavyojidanganya kwenye lile la wabunge wa kuteuliwa.
 
Inaelekea unao muda mwingi wa kupoteza maana kusoma postings >1000 sio mchezo, halafu bahati mbaya bado umeibuka na wrong conclussion. Sijui kwenye debate unaangalia sura au unajadili yaliyoandikwa. Shinda hoja kwa hoja lakini ukitaka ku-debate tu na mtu atakayesifu yale uliyoandika, basi mimi sio mmoja wao. Kwangu siangalii sura, naangalia maandishi. Tunaweza tukawa upande mmoja leo, halafu kesho tukapambana kwenye opposite sides.

Sielewi tofauti ya wewe kuangalia maandishi na mimi niliyeangalia maandishi yako katika posts zako >1000 ni ipi ila inaonekana mwelekeo wako kwa hoja ni ule ule katika kila thread. Katika hili, endelea na kazi yako mkuu, wewe u katika mengi hapa ila mimi nimechagua issue moja tu kwa sasa - mambo ya Tarime.

Kumwaga maji ndani ya mto tokea mgodini sio kitu cha ajabu na sio kosa. Kosa ni kumwaga hayo maji yakiwa hayajasafishwa. Sasa kama unao ushahidi kuwa maji yanayomwagwa yana CN utufahamishe .

Ushahidi upo mkubwa sana wa hili, yote haya ni suala la muda tu kabla watu wa Tarime hatujachukua hatua zinazostahili. Inaumiza tu wapambanaji wanne kati ya wengi waliokuwa wanafuatilia hili suala (akiwemo Wangwe na Maisa) kwa sasa ni marehemu "kutokana na ajali za gari".


Kama uliwahi kuyafanyia test hayo maji wanayomwaga, au labda kuna watu/wanyama waliokufa au kujeruhiwa na hiyo sumu, hizo ndio shahidi unazotakiwa kutueleza kuwa unazo. Vinginevyo unayoongea ni porojo tu.

Ndio maana nilikuuliza kama uko makini kwenye hili jambo kabla ya kuanza kukupa habari kamili (au kama ni kuendeleza ubishi kama ilivyo kawaida yako kwenye posts zako zingine). Inaonekana hata hujui inachukua muda gani na vitu gani kwa cyanide kufanya/kuleta madhara. Chukua muda kusoma mambo yote yaliyowahi kuandikwa kuhusu cyanide na utajua kinachoendelea Tarime na probably kwenye migodi yote Tanzania na ujue itachukua muda gani au vitu gani kufanyika ili madhara yaanze kuonekana kwa viumbe hai wanaoishi karibu na migodi hii.


Mtu kama hana kibali cha kuingia ndani ya eneo la mgodi ni lazima akikutwa atakamatwa na hiyo sio kielelezo cha kuwepo kwa CN.

Unategemea kampuni ya madini itakupa kibali wewe au yeyote yule kwenda mgodini na kukagua treatment ya CN? Inawezekana una imani zaidi kwenye system au unahitaji ajali kujua kinachoendelea Tarime na migodini Tanzania.

No wonder Tanzania bado inapata chini ya asilimia 3.
 
Ushahidi upo mkubwa sana wa hili, yote haya ni suala la muda tu kabla watu wa Tarime hatujachukua hatua zinazostahili.
.....Ndio maana nilikuuliza kama uko makini kwenye hili jambo kabla ya kuanza kukupa habari kamili. Inaonekana hata hujui inachukua muda gani na vitu gani kwa cyanide kufanya/kuleta madhara.
...........Inawezekana una imani zaidi kwenye system au unahitaji ajali kujua kinachoendelea Tarime na migodini Tanzania.

Magabe,
Humu mtandaoni tupo watu wa taaluma mbalimbali na uelewa wetu wa mambo pia ni tofauti. Gold Cyadination ni process inayoeleweka vizuri sana pamoja na madhara yake. Na pia CN haichukui muda kuleta madhara ya kiafya kwa mtu. K.m. maji kiasi ya kijiko cha chai yenye 2% ya CN inaweza ikaondoa roho ya mtu.

Sasa kama kweli ushahidi mkubwa upo wa matumizi mabaya ya CN na kumwagwa kwenye vyanzo vya maji, basi ulete ili tujenge hoja ya kuwaadhibu hao wachimbaji. Lakini kama hakuna, basi tuachane na porojo za mitaani. Kuamini au kutoamini 'system', ni position ya kuchukua kulingana na hoja, lakini tukumbuke pia kuwa, ni rahisi sana kujenga uzushi.
 
Yule mchungaji matata anayeitwa Mtikila, hivi pundwe amepelekwa hospitali kulazwa na kushonwa nyuzi baada ya kupigwa mawe na wananchi wenye hasira. Mtikila alipata dhahama hiyo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na CHADEMA yake ndio waliomuua Chacha Wangwe.

.......ndiyohiyo
 
Wananchi walipandwa na hasira na kuwaomba polisi wamkamate kwa kufanya uchochezi lakini polisi wakamuacha aendelee kusema na kugawa makaratasi yenye maneno yake kuwa Mbowe, Mengi, Ndesa, Slaa, Mnyika na Zitto ndio waliopanga na kumuua Chacha Wangwe kwa kutuma vijana wamchome Kisu na baadaye kumpiga na nyundo. Hapo ndipo wananchi wakamgeukia na kumpiga mawe

..............habarindiyohiyo
 
Wewe furahia tu siku watakapopigwa mawe Mbowe, Slaa, Zito au Mnyika usije kusema wametumwa na CCM.
 
Unajua kwa nchi za Kiafrika ukiwa chama cha upinzani, kitu kimoja ambacho ni muhimu ku avoid ni kufanya vurugu. CHADEMA inatakiwa wawe wanaongoza kupiga kelele za kuonewa na wala sio wao kuongoza kufanya vurugu.

Hii mnawapa CCM nafasi ya kupiga watu.

Kuna waheshimiwa watakuja hapa na kusema Mtikila kaponzwa na ulimi wake.

Vurugu ndio zimewaponza CUF hasa kwa upande wa bara. Watu wanaopenda vurugu ni wachache kuliko wapenda amani, hivyo ukiamua kuji position kwenye wenye vurugu, sidhani kama strategy kama hiyo inaweza kukuongezea kura.
 
Wananchi walipandwa na hasira na kuwaomba polisi wamkamate kwa kufanya uchochezi lakini polisi wakamuacha aendelee kusema na kugawa makaratasi yenye maneno yake kuwa Mbowe, Mengi, Ndesa, Slaa, Mnyika na Zitto ndio waliopanga na kumuua Chacha Wangwe kwa kutuma vijana wamchome Kisu na baadaye kumpiga na nyundo. Hapo ndipo wananchi wakamgeukia na kumpiga mawe

..............habarindiyohiyo
Haya ndiyo matatizo ya Mtikila, kwanini hakuacha Polisi wafanye kazi yao? I see, Mengi naye anamuunganisha kama mwanasiasa vile? Kaazi kwelikweli
 
Wewe furahia tu siku watakapopigwa mawe Mbowe, Slaa, Zito au Mnyika usije kusema wametumwa na CCM.
Si tulishasikia Mbowe mwenyewe alikimbizwa kwa mawe hukohuko Tarime? Hawa hawajatumwa na CCM wala CHADEMA, labda kuna zaidi
 
Si tulishasikia Mbowe mwenyewe alikimbizwa kwa mawe hukohuko Tarime? Hawa hawajatumwa na CCM wala CHADEMA, labda kuna zaidi

Invisible,

Hakuna sababu yoyote ya kupiga watu. Kama Mtikila anaongea hayo maneno, si wachukue video na kupeleka mahakamani?

Vyama vya upinzani vikianza kupiga watu, CCM wataishia kupiga mara kumi. Watakaodhurika ni watu wa kawaida na ambao wanachotaka ni amani na maendeleo kwenye nchi yao. Kwa nchi maskini kama TZ ni rahisi mno kwa matajiri na wanasiasa kuwanunua vijana ili wapige wabaya wao. Je tunataka ujinga kama huo?
 
Yule mchungaji matata anayeitwa Mtikila, hivi pundwe amepelekwa hospitali kulazwa na kushonwa nyuzi baada ya kupigwa mawe na wananchi wenye hasira. Mtikila alipata dhahama hiyo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na CHADEMA yake ndio waliomuua Chacha Wangwe.

.......ndiyohiyo



Mungu amjalie apone haraka.
 
Hold on a minute; riots na vitu kama hivyo siyo suala la watu wa Tarime tu. Vinatokea sehemu nyingi duniani na ndio maana tunakuwa na Polisi.

a. Mtu anayevunja sheria ni mhalifu. Period hakuna udhuru wa Chama wala siasa katika hilo. Kama hawa watu wamempiga mawe hakuna cha kudai ni wana Chadema au wana CCM; hawa ni wahalifu na sheria ichukue mkondo wake.

b. Kama Mtikila alikuwa anaeneza habari hizo na kudai kwa uthabiti kuwa x,y,z wamemuua Wangwe na kueneza habari hizo ili kupanda chuki miongoni mwa wananchi au kuchezea hisia zao hilo linaweza kuwa kwenye uhuru wa maoni. Lakini tukijiuliza kama angesema Makamba, Kikwete na Msekwa wamemuua Mbatia mnafikiri kweli Polisi wangeacha asambaze habari hizo au angetiwa pingu kwa "uchochezi"?

Sasa kama habari hii kuwa "Wananchi walipandwa na hasira na kuwaomba polisi wamkamate kwa kufanya uchochezi lakini polisi wakamuacha aendelee kusema na kugawa makaratasi yenye maneno yake kuwa Mbowe, Mengi, Ndesa, Slaa, Mnyika na Zitto ndio waliopanga na kumuua Chacha Wangwe kwa kutuma vijana wamchome Kisu na baadaye kumpiga na nyundo. Hapo ndipo wananchi wakamgeukia na kumpiga mawe" Ni kweli, tunajiuliza sasa Polisi waliomwagwa huko ni wa nini?

c. NI kutokuwa makini kuwawajibisha CHadema au mtu mwingine yeyote kwa vitendo vya watu wenye akili na utashi wao. Kila mtu lazima ajifunze kubebeshwa mzigo wake yeye mwenyewe. Kwanini mzigo huu wa watu kupiga watu wengine mawe wabebeshwe Chadema au CCM for that matter? Kwanini wasibebeshwe wahalifu wenyewe na kuwajibishwa.

Kama aliyechochea watu hao hasira kwa maneno yake ni Mtikila kwanini Mtikila asiwajibishwe kwa kuchochea hasira za watu namna hiyo kwa maneno ya kichochezi?

Kama Polisi walikuwepo na waliona uchochezi unaodaiwa kufanywa na Mtikila kwanini wao wenyewe wasiwajibishwe kwa hilo. Kama watadai ni uhuru wa maoni, hebu mtu athubutu huko Tarime aanza kusambaza vipeperushi kuwa CCM, Kikwete na Makamba walipanga njama za kumuua Wangwe wakaajiri wauaji kutoka Afrika ya Kusini ambao walistage accidenti na mmoja wa watu waliosimimamia operesheni hiyo ni Mbunge maarufu wa Chama hicho akishirikiana na Kamishna mmoja wa Polisi. Na ya kuwa yule daktari mpya wa Mkoa wa Dodoma aliletwa pale kwa ajili ya kuficha ushahidi kwani ilikuwa ni siku chache tu tangu afike Dodoma ndiyo kifo cha Wangwe kilitokea. Mtu huyo aeneze uvumi huu kwa kugawa makatarasi kwenye kampeni na muone kama Msekwa na Jeshi zima la Polisi halitashuka Tarime.

Tusiwe na haraka ya kuhukumu watu wengine kwa makosa ya wengine. Kila mtu abebeshwe mzigo wake yeye mwenyewe.

On the other hand, kwanini watu hawa wa wafanye kitu kana kwamba wanamtetea Mbowe na Chadema huko Tarime?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom