Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Pole sana "mchungaji"

Mimi nafikiri waliompiga walifanya vizuri tu. Hivi yeye hana sera za kuwaambia wananchi? Atuambie DP itafanya nini ikiwa watapewa jimbo la Tarime, sio kutuambia fulani kaua. Hata kama fulani kaua na anweza kuleta maendeleo ya Tarime kuna shida gani? Hiyo kazi ya kaua au hapana inabidi waachiwe polisi, na wanasiasa watuambie sera.
 
Mambo ya Tarime yanatisha sana .Nilionya majuzi kati.Tossi anatosa wana Tarime kwa jina la CCM kutwaa Jimbo .Mtu yeyote anaye chukia ujinga Tarime leo aki act ataibwa Chadema simply he is not siding with those crooks .Wazungu wa Barrick wanafanya wawezalo kumpata mtu wao ambaye CCM wanachukua chao mapema kabisa .Mtikila he deserve what he had. Ni sawa tu
 
Mtanzania unajuaje kuwa ni "vyama vya upinzani" ndio vimeanza "kupiga watu" badala ya hawa watu wenyewe kubebeshwa lawama hizo.
naona wanataka kubebesha CHADEMA mzigo kiuonevu. mbowe nae alikimbizwa kumbuka, mvungi nae alipata kichapo na CCM nao juzi wanalalamika walifanyiwa fujo. wahukumiwe wahusika wenyewe bila kutumia majina ya vyama
 
Invisible,

Hakuna sababu yoyote ya kupiga watu. Kama Mtikila anaongea hayo maneno, si wachukue video na kupeleka mahakamani?

Vyama vya upinzani vikianza kupiga watu, CCM wataishia kupiga mara kumi. Watakaodhurika ni watu wa kawaida na ambao wanachotaka ni amani na maendeleo kwenye nchi yao. Kwa nchi maskini kama TZ ni rahisi mno kwa matajiri na wanasiasa kuwanunua vijana ili wapige wabaya wao. Je tunataka ujinga kama huo?
....Siasa za dunia ya Tatu hizo!!!!!!!!!!!! Upuuzi mtupu..
 
Hi Pastor Mtikila
Praise be to Tarime people
The reward of sin is death, but what God freely gives is eternal life,You have reaped what you sow in Tarime land.
God bless us
 
Mungu amjalie apone haraka.


Ameyataka mwenyewe!!!!!!!! Simpi pole!!!!!!!!! Katika kampeni eleza jinsi Sera na Mkakati wako unavyoweza kuibadilisha jamii hiyo kwa kuleta mabadiliko au marekebisho ambao wengine wameshindwa na Si kufanya kampeni uchwara za maneno ya uchochezi yasiyofanyiwa upembuzi yakinifu. Soorryyyy.

Huko ndiko kutosoma alama za nyakati. Pale Tarime wenye nguvu ni CCM na Chadema. Period. Halafu wewe Mtikila unaenda kuongelea siasa za chama minority kama DP!!!!!!!!!!!!!! kama nimekosea jina la chama chake nisahihisheni.

The other side of the coin, inawezekana wanaofanya vurugu si wana CHADEMA!!!! Hizo tunasema ni mbinu za kisiasa na kwa sasa CCM imejipanga at any cost and means the jimbo is lao this time. Bon voyage CHADEMA. I am presenting my views as a neutral observer.
 
Hongera wana tarime kwa kumkongori anayejiita mchungaji kumbe ni tapeli linalotumia dini na siasa kujinufaisha, makamba na msekwa watafutieni dawa pia ikibidi muwatumie popobawa
 
Hongera wana tarime kwa kumkongori anayejiita mchungaji kumbe ni tapeli linalotumia dini na siasa kujinufaisha, makamba na msekwa watafutieni dawa pia ikibidi muwatumie popobawa

Kutoka ndani ya moyo wangu nimefurahia sana mkongoto alioupata tapeli huyu, kwanza naona hawajampatia ingefaa wamtoe chongo ndo akili imrudie aache kuuza utu wake kwa mafisadi kwa ajili ya vijisenti! Bravo wana Tarime


If at all anao ushahidi kesi iko mahakamani ya Mallya aende akautoe huko sio kupandikiza chuki kwa watu na kuwafanya kama vile wao hawawezi fikiria!
 
Tangu aingizwe mkenge na kuumbuliwa na Rostam, Mtikila alishajipaka kinyesi usoni na anajaribu kutumia kila njia kurudi katika ulingoni wa siasa, ikiwemo kuropoka. Ama kwa kujua au kutokujua Mtikila anatumika.

Then, waliomponda Mtikila ni wananchi wa kawaida wenye uchungu na Tarime yao na ambao hawataki ujinga wa kutumia msiba wa Wangwe kujipatia umaarufu wa kisiasa. Kwa maoni yangu ni kukataa kufikiri kufikia uamuzi kwamba waliompiga Mtikila ni wafuasi wa CHADEMA au chama kingine cha upinzani. In any case, hata kama waliompiga ni wafuasi wa vyama vya kweli vya upinzani, hawakufanya hivyo kwa kutumwa na mtu yeyote. Hawa ni watu waliokuwa provoked na wakachukua hatua walizochukua.

Wanasiasa wetu waache uzembe wa kutamka maneno. Wanachi wameshaamka; careless talk is increasingly becoming costly!
 
Natumaini misimamo yetu tunayoionyesha kwenye mada hii, itaendelea hivyo hivyo hata pale 'matapeli' au viongozi wengine wa vyama aidha vya upinzania au CCM watakapopata kipigo kutoka kwa 'wananchi' ambao wamechukizwa na 'kuropoka' kwa mwanasiasa awaye yote.
 
Nasikia leo polisi wamemuita Mchungaji Mtikila na kumuonya aache maneno ya uchochezi
 
Hili la kushangilia kupigwa kwa Mtikila linaonyesha upeo wa wengi ndani ya JF... ushabiki bubusa!
 
Hili la kushangilia kupigwa kwa Mtikila linaonyesha upeo wa wengi ndani ya JF... ushabiki bubusa!

wapo wanaoshangilia kupigwa Mtikila; wapo wanaoshangilia kuona Chadema inahusishwa; na wapo wanaoombea kipigo kama hicho kiwatokee Chadema ili waone watu watasemaje.

Na tupo sisi wengine tunaopinga vitendo vya uhalifu kwa yeyote yule. Wewe haukemei uhalifu wowote dhidi ya mtu yeyote. Unaangalia mambo kwa minajili ya vyama vyama hivi.
 
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Democratic(DP) Mch. Christopher Mtikila kushambuliwa kwa mawe mkutanoni Tarime, ameibuka na kusema leo atalipiza kisasi kwa unyama waliomfanyia wabaya wake.

"Nitalipiza kisasi na ninajua watashindwa. Siwezi kuchukua mawe na kujeruhi watu lakini kisasi changu ni kuzidi kufunua mipango mingine ya siri ya mauaji ya wapigaji wazalendo wa nchi hii," amesema.

Ameapa kwamba pamoja na kujeruhiwa, leo ataendelea na mkutano wake na hata kama Polisi isipompa ulinzi wananchi tayari wanaomuunga mkono wamejitolea kumlinda vya kutosha.

Akizungumza na Dar Leo kwa njia ya simu kutoka Tarime leo asubuhi, Mtikila amesema tukio la kupigwa kwake ni la kupangwa siku nyingi na alishajua hilo litatokea kwa kuwa alikwishapewa taarifa na wananchi wema.

"Watu waliosuka mpango wa mimi nishambuliwe katika mkutano nawafahamu na tayari nimeshatoa taarifa Polisi na nimezungumza na Mkuregenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na mchana huu wapinzani wote tutakutana naye kujadili hali ya kampeni inavyokwenda,"anasema Mtikila.

Alisema kushambuliwa kwake haina maana yale aliyokuwa amekusudia kuwaambia wananchi wa Tarime katika mikutano yake ya hadhara itakuwa mwisho bali sasa anajipanga zaidi ili aweze kuwafikia wananchi wote kuwaeleza mwenendo mzima wa mambo ya siasa yanayofanywa na vyama vingine vya siasa.

"Kwa bahati mbaya Polisi wa Tarime hawataki kunipa ulinzi lakini nitaendelea kufanya kazi yangu kama kawaida, wananchi wamejitolea kunipa ulinzi na wengine wamejitolea kunipa Landcruiser ili niwafikie wananchi wengi zaidi kueleza yale ninayofahamu mchungaji wao,"amesema Mtikila.

Amesema kushambuliwa kwake kumetokea baada ya kuzungumzia ukweli anaoufahamu kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe (CHADEMA)

"Wasijidangenye kwamba wamenifunga mdomo nitakachofanya sasa ni kuchapisha nakala nyingi zaidi zinazozungumzia kifo hicho na kuzisambaza kwa wananchi wengi zaidi," amesema na kusisitiza:

"Nimekuja kuwaeleza wananchi maovu yanayofanywa na wanasiasa kwa wananchi wa Tarime na nitalipa kisasi cha kushambuliwa kwangu kwa hoja kwa kueleza wananchi ukweli."

Alipoulizwa kama wakati anashambuliwa Polisi walikuwepo eneo la tukio, Mtkila amesema kwa bahati mbaya amekuwa hapewi ushirikiano na polisi katika suala la kumpatia ulinzi lakini pamoja na hali hiyo wananchi wameamua kumlinda ili aweze kufanya mikutano yake vizuri.

Anaongeza kuwa anashindwa kuelewa kitu gani ambacho wapinzani wenzake wanataka kutoka kwake kwani kila chama kinafanya kampeni zake bila kupangiwa na chama kingine ndio maana wapo wanazungumzia ufisadi na yeye ameamua kuzungumzia yale anayoyajua yeye.

Mwandishi Wetu kutoka Tarime anaripoti kuwa Mkuu wa Kitengo cha Operesheni Maalum Venance Tossi ameagiza kufikishwa mahakamani watu wanne wanaodaiwa jana kumpiga mawe Mtikila.

Amesema leo asubuhi kuwa tataribu zilikuwa zikifanywa maafisa wa polisi kuwafikisha mahakamani watu hao ambo ni Mussa Peter, Mwita Chacha, Hafidh Stanslaus na Mwita Kiongo wakazi wa Tarime mjini.

Kwa mujibu wa Tossi, watu hao ambao ni wafuasi wa vyama vya upinzani walikula njama na kumpiga jiwe Mtikila wakati akihutubia mkutano wa Kampeni katika Viwanja vya Sabasaba mjini Tarime.

Mtikila alipigwa jiwe kisogoni kutokana na kauli yake kwamba Rais Jakaya Kikwete alimkumbatia mmuaji Ditopile na kwamba ana ushahidi kwamba Chacha Wangwe aliuawa kutokana na mpango uliosukwa na Chadema.

Baadhi ya wananchi waliohojiwa jana jioni walimtaka Mtikila kuondoka mara moja kabla hajadhurika kwani kutumia kifo cha Wangwe kunaweza kugharimu maisha yake.

Hata hivyo ilidaiwa na baadhi ya viongozi wa vyama upinzani kwamba anatumiwa na Chama Cha Mapinduzi CCM na kwamba siasa hizo zitaifanya Tarime iwe kama Kenya na ishindwe kukalika, endapo vyama vitatumia kifo cha Wangwe badala ya kutumia sera.

Source;Dar leo.
 
"Watu waliosuka mpango wa mimi nishambuliwe katika mkutano nawafahamu na tayari nimeshatoa taarifa Polisi na nimezungumza na Mkuregenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na mchana huu wapinzani wote tutakutana naye kujadili hali ya kampeni inavyokwenda,"anasema Mtikila.
Confused...!


Amesema kushambuliwa kwake kumetokea baada ya kuzungumzia ukweli anaoufahamu kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe (CHADEMA)

------

Mtikila alipigwa jiwe kisogoni kutokana na kauli yake kwamba Rais Jakaya Kikwete alimkumbatia mmuaji Ditopile na kwamba ana ushahidi kwamba Chacha Wangwe aliuawa kutokana na mpango uliosukwa na Chadema.
Confused here too!


Hata hivyo ilidaiwa na baadhi ya viongozi wa vyama upinzani kwamba anatumiwa na Chama Cha Mapinduzi CCM na kwamba siasa hizo zitaifanya Tarime iwe kama Kenya na ishindwe kukalika, endapo vyama vitatumia kifo cha Wangwe badala ya kutumia sera.
Confused again!
 
WHERE ARE OUR ESTEEMED PSYCHIATRIC EXPERTS?

MTIKILA NEEDS ADMISSION, HILI KANISA LAKE ANAONGOZA MISA SAA NGAPI?

mtm
 
i hope atapata ulinzi wa kutosha mana la sivo anaweza asiongee kama hapo alivosema na kuwa mpole kabisaaa!!

all the best,tunasubiri more news tu
 
wapo wanaoshangilia kupigwa Mtikila; wapo wanaoshangilia kuona Chadema inahusishwa; na wapo wanaoombea kipigo kama hicho kiwatokee Chadema ili waone watu watasemaje.

Na tupo sisi wengine tunaopinga vitendo vya uhalifu kwa yeyote yule. Wewe haukemei uhalifu wowote dhidi ya mtu yeyote. Unaangalia mambo kwa minajili ya vyama vyama hivi.

Hili si sahihi mimi ni muumini mzuri wa haki na sheria nimekuwa/nitaendelea kukemea uhalifu bali kujali itakadi za vyama. Ni bahati mbaya sana umeshanichagulia upande lakini kwa taarifa yako sina chama
 
Hili si sahihi mimi ni muumini mzuri wa haki na sheria nimekuwa/nitaendelea kukemea uhalifu bali kujali itakadi za vyama. Ni bahati mbaya sana umeshanichagulia upande lakini kwa taarifa yako sina chama

katika hili hujakemea. Na sijasema una chama ila una mtazamo wa kichama. Badala ya kukemea kitendo cha kihalifu dhidi ya Mtikila umejaribu kuscore points za kichama chama (whatever that chama is)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom