Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Nasikia leo polisi wamemuita Mchungaji Mtikila na kumuonya aache maneno ya uchochezi

Polisi ni wazembe kabisa
Kwanini wanashindwa kudhibiti hii hali ya uvunjifu wa amani inayoletwa na huyu mchungaji,Nadhani wanasubiri watu wauwae ndo wachukuwe hatua.Si mara ya kwanza huyu mchungaji kusema maneno ya uchochezi kwenye majukwaa,anatumiwa na watu wachache kwa maslahi yao.
Huyu tumemstukia kuwa anavunja amani,anasubiri watu wafe ndo amwage upupu na kujipatia sifa za kutanganza habari za wafu.
Mara marehemu Kolimba(R.I.P) kauwawa,mara amkashifu baba wa Taifa(R.I.P),Mara aibue ya chacha (R.I.P)
Ya uchochezi wa kifo cha kolimba na ya kumkashifu baba wa Taifa pale Singida polisi walimsekwa lupango,kwa nini hili la Tarime bado wanamuacha anatanua????Manumba vipi?
Kwa nini Huyu mchungaji asiwalishe maelezo yake polisi wayafanyie kazi?nini kazi ya polisi huko Tarime?
 
Pole sana Mtikila,
Ulituletea Mgombea Binafsi.

Doubt Yangu ni kwa nini ulichukua million tatu mkopo kwa fisadiiiiiiii?????

Ungekuja kwangu ningekukopesha hata million 10 kwa ajili ya politics.

Mie sina chama, sijaamua niwe NCCR, CUF, Chadema au CCM.

Nataka kugombea mgombea Binafsi. Am Mp admire
 
Mtikila ameminywa kona mbaya maana kesi walimfutia lakini badala ya kufunguwa kesi ya kudai fidia kama alivyofanya Mrema...Yeye amekopeshwa milioni tatu na msharti kwamba aongee maneno ya uchochezi.
Na kwasababu yuko kwenye mtego mbaya na maisha yake pia yanaweza kuwa hatarini kwa pande zote...yani upande wa wananchi kama akiendelea na uchochezi na upande wa huko alikochukuwa huto tusenti tudogo sana na kuuza uhuru wake...Huko wataminya saana tu kwani keshakuwa kama kijitumwa flani hivi...Hana njia ya kukwepa kuwafanyia kazi waliomtuma na maisha yake kisiasa yamefikia pengine ukingoni.....Nachelea lisije kuwa neno zito...Lakini maneno yake na yeye ni mazito na yanaweza kupelekea vurugu kubwa sana.
Kwanini asiwaachie ccm na serikali hiyo kazi ya kuzungumzia kuhusu kifo cha Wangwe kama huyu mtu si PANDIKIZI HATARI?
 
Huko ni TARIME ,hao WAKURYA wana misimamo hawadanganyiki na propaganda kama hizo
Angalia usije ukafia huko
 
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Democratic(DP) Mch. Christopher Mtikila kushambuliwa kwa mawe mkutanoni Tarime, ameibuka na kusema leo atalipiza kisasi kwa unyama waliomfanyia wabaya wake.

"Nitalipiza kisasi na ninajua watashindwa. Siwezi kuchukua mawe na kujeruhi watu lakini kisasi changu ni kuzidi kufunua mipango mingine ya siri ya mauaji ya wapigaji wazalendo wa nchi hii," amesema.

Ameapa kwamba pamoja na kujeruhiwa, leo ataendelea na mkutano wake na hata kama Polisi isipompa ulinzi wananchi tayari wanaomuunga mkono wamejitolea kumlinda vya kutosha.

Akizungumza na Dar Leo kwa njia ya simu kutoka Tarime leo asubuhi, Mtikila amesema tukio la kupigwa kwake ni la kupangwa siku nyingi na alishajua hilo litatokea kwa kuwa alikwishapewa taarifa na wananchi wema.

"Watu waliosuka mpango wa mimi nishambuliwe katika mkutano nawafahamu na tayari nimeshatoa taarifa Polisi na nimezungumza na Mkuregenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na mchana huu wapinzani wote tutakutana naye kujadili hali ya kampeni inavyokwenda,"anasema Mtikila.

Alisema kushambuliwa kwake haina maana yale aliyokuwa amekusudia kuwaambia wananchi wa Tarime katika mikutano yake ya hadhara itakuwa mwisho bali sasa anajipanga zaidi ili aweze kuwafikia wananchi wote kuwaeleza mwenendo mzima wa mambo ya siasa yanayofanywa na vyama vingine vya siasa.

"Kwa bahati mbaya Polisi wa Tarime hawataki kunipa ulinzi lakini nitaendelea kufanya kazi yangu kama kawaida, wananchi wamejitolea kunipa ulinzi na wengine wamejitolea kunipa Landcruiser ili niwafikie wananchi wengi zaidi kueleza yale ninayofahamu mchungaji wao,"amesema Mtikila.

Amesema kushambuliwa kwake kumetokea baada ya kuzungumzia ukweli anaoufahamu kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe (CHADEMA)

"Wasijidangenye kwamba wamenifunga mdomo nitakachofanya sasa ni kuchapisha nakala nyingi zaidi zinazozungumzia kifo hicho na kuzisambaza kwa wananchi wengi zaidi," amesema na kusisitiza:

"Nimekuja kuwaeleza wananchi maovu yanayofanywa na wanasiasa kwa wananchi wa Tarime na nitalipa kisasi cha kushambuliwa kwangu kwa hoja kwa kueleza wananchi ukweli."

Alipoulizwa kama wakati anashambuliwa Polisi walikuwepo eneo la tukio, Mtkila amesema kwa bahati mbaya amekuwa hapewi ushirikiano na polisi katika suala la kumpatia ulinzi lakini pamoja na hali hiyo wananchi wameamua kumlinda ili aweze kufanya mikutano yake vizuri.

Anaongeza kuwa anashindwa kuelewa kitu gani ambacho wapinzani wenzake wanataka kutoka kwake kwani kila chama kinafanya kampeni zake bila kupangiwa na chama kingine ndio maana wapo wanazungumzia ufisadi na yeye ameamua kuzungumzia yale anayoyajua yeye.

Mwandishi Wetu kutoka Tarime anaripoti kuwa Mkuu wa Kitengo cha Operesheni Maalum Venance Tossi ameagiza kufikishwa mahakamani watu wanne wanaodaiwa jana kumpiga mawe Mtikila.

Amesema leo asubuhi kuwa tataribu zilikuwa zikifanywa maafisa wa polisi kuwafikisha mahakamani watu hao ambo ni Mussa Peter, Mwita Chacha, Hafidh Stanslaus na Mwita Kiongo wakazi wa Tarime mjini.

Kwa mujibu wa Tossi, watu hao ambao ni wafuasi wa vyama vya upinzani walikula njama na kumpiga jiwe Mtikila wakati akihutubia mkutano wa Kampeni katika Viwanja vya Sabasaba mjini Tarime.

Mtikila alipigwa jiwe kisogoni kutokana na kauli yake kwamba Rais Jakaya Kikwete alimkumbatia mmuaji Ditopile na kwamba ana ushahidi kwamba Chacha Wangwe aliuawa kutokana na mpango uliosukwa na Chadema.

Baadhi ya wananchi waliohojiwa jana jioni walimtaka Mtikila kuondoka mara moja kabla hajadhurika kwani kutumia kifo cha Wangwe kunaweza kugharimu maisha yake.

Hata hivyo ilidaiwa na baadhi ya viongozi wa vyama upinzani kwamba anatumiwa na Chama Cha Mapinduzi CCM na kwamba siasa hizo zitaifanya Tarime iwe kama Kenya na ishindwe kukalika, endapo vyama vitatumia kifo cha Wangwe badala ya kutumia sera.

Source;Dar leo.

Msisitizo wangu uko kwenye highlights nyekundu...Ina maana kuwa sababu ya yeye kupigwa mawe ni chadema na JK....
Pia madai kuwa wapinzani wote wanakutana..Wapinzani wote minus chadema? Wanakutana na nani eti? Kuzungumzia usalama wa nani?
Na anajidai kuwa hana sapoti ya ccm na polisi na kuwa ana sapoti ya upinzani ambao wanakutana na mkurugenzi wa usalama wa NEC.
Huko Tarime ni hayo madini?
Na wanasiasa wameenda kupiga kambi kabisa...Kazi ipo.
Wakati Mtikila akisema kuwa amepigwa mawe kwa kusema ukweli kuhusu kifo cha Wangwe na chadema....Kamanda Tossi na yeye anadai kuwa alipigwa mawe kwa kusema JK na Ditopile walikumbatiana....
Kwahiyo hapo ina maana tunaweza ku assume kuwa Mtikila analipiza kisasi kwa JK dhidi ya chadema?
 
Mtikila is just crayz....u can see how ditopile akawa ana ushaidi wakati dito kafa kabla ya cha wangwe....very confused na ndio maana huwa anashida kesi zake mara kwa mara kwa kuwa watu hawa pay attension kwenye mazungumzo yake...check hapo alivyo changanya?

Yaani at the end of the day huwa hana la maana,na mbona hasema kuhusu mgombea wa udiwa ni tarime peter zakaria...huyu ndio balaa,sujui CCM watajifunza lini wewe mtu mfanya biashara(mabasi ya zakari,agent wa coca) .... lingine sisemi...then awe diwani...

AU ndio aongeze mchango katika mfuko wa ushindi...zamani mtu huyu alikuwa ameshika biashara zote wilaya ya tarime...hata mabasi wa wengine yalikuwa yanaishia musoma yeye yake ndio yanakwenda mpaka tarime ,sirari...leo hii ukitaka kuwa agent wa coca wilayani tarime na vijiji vingine..lazima upate kibali kwake(Zakari) na if fact huwezi pata kwa kuwa na yeye ni agent na swahiba wake Gachuma..huu si ufisadi.....hafai hata kuwa mwenyekiti wa nyumba kumi.
 
Na sasa Mtikila anasema anakwenda Mahakamani kwa sababu waliompiga anawajua
 
Basi hizi ni siasa za kitoto I may say. Pamoja na kuwa Mtikila anaweza kutofautiana nao CHADEMA sioni sababu ya wao kufurahia yeye kupigwa mawe.

Shame on their bones (whomever celebrates Mtikila's stoning).

🙁

Inv.... Mimi ningependa kuonyesha hisia zangu wazi wazi, kwa kweli kama kuna mtu atakayeninyooshea kidole na aninyoshee tu lakini ukweli ni kwamba

NIMEFURAHI SANA KWA HUYU JAMAA KUFANYIWA ALIVYOFANYIWA MAANA AM FEDUP NA SIASA ZAKE ZA KUWA KIBARAKA ALWAYS, HE DESERVSE KUWA HAPO ALIPO KWA SASA, SIONI SABABU YA KUMUONEA HURUMA MTU AMBAYE ANATUMIWA KUHATARISHA MAISHA YA WATU ZAIDI YA 100,000, WHO ARE HIM AONGEE MANENO YA KIIZUSHI TU NA WATU WAMUANGALIE WHILE WAMEISHA SAHAU.
NOTE:- WANGWE ALIKUWA ANAPENDWA SANA NA WANANCHI WA JIMBO LAKE YEYE LEO AENDE KUONGEA KUWA ALIULIWA NA WATU FULANI WHILE MJADALA ULISHAFUNGWA KWA POLISI KUTOA JIBU KUWA ILIKUWA NI AJALI TU, KAMA HAUAMINI HUYU MCHUNGAJI ANATUMIWA HEBU SIMAMA WEWE KAMA WEWE INVISIBLE ALAFU PAYUKA KUWA MBOWE AMEUWAWA NA WATU FULANI THEN UONE KAMA UTAENDELEA KUTANUA KAMA ANAVYOTANUA SASA.

Nashukuru nimesema lile ninalolifikiria maana always huwa sipenzi kudhulumu hisia zangu
 
Unajua kwa nchi za Kiafrika ukiwa chama cha upinzani, kitu kimoja ambacho ni muhimu ku avoid ni kufanya vurugu. CHADEMA inatakiwa wawe wanaongoza kupiga kelele za kuonewa na wala sio wao kuongoza kufanya vurugu.

Hii mnawapa CCM nafasi ya kupiga watu.

Kuna waheshimiwa watakuja hapa na kusema Mtikila kaponzwa na ulimi wake.

Vurugu ndio zimewaponza CUF hasa kwa upande wa bara. Watu wanaopenda vurugu ni wachache kuliko wapenda amani, hivyo ukiamua kuji position kwenye wenye vurugu, sidhani kama strategy kama hiyo inaweza kukuongezea kura.

sasa sijui ni nani atakayethibitisha kama ni wafuasi wa CHADENA waliofanya hizo vurugu. Pia nae ULIMI WAKE UMEMPONZA. Hivi mbona mtu mzima kama mtikila natumia kifo kama stepping stone ktk siasa bila kufikiria kwamba ni kiasi gani hadhira inakwazika na maneno au matendo yake?

Pia,nadhani watu makini wangweweza kufikiria mbele zaidi na kuona kwamba hata CCM wanweza kuwa wamefanya dili la kuandaa vijana ili kuichafua CHADEMA kwa kuanzisha vurugu huku wakijifanya wafuasi wa CHADEMA.


Pia, Inawezakana kukawa na watu ambao ni Neutral lakini hawataki kusikia siasa za kuchafuana na mbaya zaidi mtu kama Reginald Mengi anapohusishwa ktk mazingira ambayo hayaeleweki.Mengi nin mtu ambae amelisaidia sana taifa letu lakini inapotokea mtu anaropoka kwa maslahi yake tu,huwa hatuwezi kumuonea huruma sana maanake ni mtu mbinafsi asiyejali maslahi ya watanzania walio wengi.Kwa kawaida mimi sipendi hizi siasa za vurugu lakini haki inapohujumiwa basi hapo kikomo cha uvumilivu wangu ni hapo.
 
Hapana mleta habari kutupasha kwa mbwembwe kuwa Mtikila yamemkuta hayo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na Chadema ndio waliomuua Wangwe. Hapo by implication hao watakuwa ni mashabiki wa Chadema,,,

sijajua kama hapa jamvini tuna watu wenye akili nyembamba hivi.Uko shallow sana mzee.Duh!
 
Kumbe umekubali kua kamanda wa POLISI ni GENIUS kwa kupeleka polisi wengi sehemu hiyo.Sasa ulikua unalalamika nini kuhusu polisi kuongezeka??

Kamanda ongeza watu huko wakakamate WAHALIFU maana inaonekana FFU hawatoshi ,400 kwa wilaya nzima ni wachache sana.


Nadhani hiyo nguvu wanayotumia CCM huko tarime wangeweza kuitumia pia angalao nusu yake dhidi ya wahujumu uchumi wa taifa letu,naam Mafisadi wa EPA na Richmond.

Nadhani kama msekwa ni makamu mwenyekiti wa chama chenye nia nzuri na taifa letu,anekua tayari ameshatoa wito kwa Jk kuwashughulikia wahalifu wa BOT kama alivyoonyesha uzalendo wake ktk kuhimiza polisi kuwashughulikia wahalifu wa Tarim.Hope hata wewe mkuu unaona hivyo,au bado?
 
Ni haki yako kama ambavyo mimi ninavyoona wewe ni punguani mzee Duh!


Ndiyo,ni haki yangu kabisa wala hujakosea. Nadhani inabidi nielewe kwenye msafara wa mamba kenge nao wamo.Hayo mawazo yako mepesi usituambukize mzee,ni hatari kwa ustawi wa taifa letu maanke akili imedumaa mno.You are just here for clapping!
 
Ndiyo,ni haki yangu kabisa wala hujakosea. Nadhani inabidi nielewe kwenye msafara wa mamba kenge nao wamo.Hayo mawazo yako mepesi usituambukize mzee,ni hatari kwa ustawi wa taifa letu maanke akili imedumaa mno.You are just here for clapping!

The best u can do kila unapoona post yangu wewe usisome nisije "nakaku dumaza" na mawazo yangu myepesi.....
 
Ben,

Hapo ndipo ninapowashangaa CHADEMA, badala ya kukubali ukweli kwanini mwenyekiti wenu hajaenda Tarime mnaanza kuja na hadithi za Abunuwas kibao.

Sawa endeleeni kujidanganya, ila tu wengine hamuwezi kutudanganya kama mnavyojidanganya kwenye lile la wabunge wa kuteuliwa.


Mkuu,

Ungekua mgumu kudanganyika basi usingekua mgumu kuelewa namana hii.
 
Nashauri tuendelee na mjadala maneno na vijembe mnaweza kuanza mada yake .Hili la Tarime ni maisha ya watu tafadhali tuachieni mjadala
 
Lunyungu,

Mbali ya kukandiana. ukweli unakuja kuwa mtikila alikuwa anachochea maasi. HILI LIPO WAZI, labda rafiki yangu Masatu tu ndio halioni.

Mimi nimefurahia Mtikila kula kichapo toka kwa wananchi, at the same time nawalaumu POLISI. Ilitakiwa wamchukue akalale sero kwa USALAMA WAKE MWENYEWE.

Wananchi wamechoka na mahakama ambazo kesi inachukua miaka kuisha.

Mbali ya kupigwa Mtikila amejitakia mwenyewe.
 
Polisi wanasema waliompiga mawe Mch. Mtikila ni balozi wa nyumba kumi wa CCM na vijana 3 wa DP. Hakuna mhusika kutoka CHADEMA wala chama kingine cha siasa. Hapo utaona kwamba suala la Mtikila kupigwa halihusishi chama cha siasa bali uchochezi anaouhubiri kwa ujasiri bila aibu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom