Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Huyu jamaa hamumjui, ni bonge ya mbumbumbu. Aliishia darasa la 7 hivyo hesabu ya 65+35+5=100 kumpiga chenga tusishangae jamani
 
case ya nyani kumpelekea tumbili, wamoja hao. Ngawaiya kweli anaweza kufanya utafiti wa kisiasa bila kuwa biased na CCM yake?

Ngawaiya na utawala bora?
 
fidel,

mimi sina tatizo na chama au historia ya Ngawaiya. Mambo ya unazi wa vyama ndiyo yanaturudisha nyuma kila siku Tanzania na Afrika kwa ujumla hivyo sina tatizo na alikotoa majibu ya utafiti wake.

Tatizo liko kwenye math ya Ngawaiya - asilimia 65 kujumlisha asilimia 35 na kisha kujumlisha asilimia 5 - jibu lake linakuwa asilimia 105.

Sijui kuna uwezekano gani wa Tarime kuwa na asilimia 105 na wapiga kura.


Mkuu mimi naona alikuwa anapiga kwa asilimia 200 ndo maana hesabu zake zika goti kwenye 105....kazi tunayo nchi hii bora kwenda Rwanda au Burundi tu.
 
labda alifikiri wanaposema asilimia wanamaanisha namba yoyote mbele ya mia as long as asili yake iwe ni mia..!
 
Kuna watu wanaugua ugonjwa wa chuki katika forum hii. Wanapoona CHADEMA inapata nguvu na kuikabili CCM vilivyo huko Tarime wananuna kwa sababu wenyewe walishapitisha hukumu kwamba vyama vya upinzani havina kitu. Inawezekana ni kweli nyie wenzetu kwenye huu mtandao hamjasikia sera kutoka kwa wagombea. Hata hivyo wapiga kura wa Tarime wamezisikia. Wamesikia jinsi uongozi wao wa halmashauri chini ya CHADEMA ulivyoboresha maisha yao katika kipindi cha miaka miweli na nusu, ikiwemo kutoa elimu ya sekondari bure. Wamesikia mikakati ya kuwabana wawekezaji wa machimbo ya madini ya Nyamongo ili kuhakikisha kwamba mali asili hizi zinawanufaisha wananchi wa Tarime, na ndio maaana wameamua kuchukua "risk" ya kupigania haki zao na kuiunga mkono chadema.

Nasema tena poleni sana maoundits wenzangu wa online forum. Nawataarifu tu kwamba sisi wenzenu tuliopata nafasi kidogo ya kuonana na wananchi, yaani wapiga kura, tunaona jinsi ambavyo wananchi wameamua kuikumbatia CHADEMA kama chama mbadala. Inawezekana nyie wenzetu katika internet hamtambui hilo, lakini habari njema ni kwamba wananchi wapiga kura na hata CCM wenye wametambua hilo vizuri sana.

Haya nyie endeleeni kupiga ramli na kutoa laana, ngoja sisi tuendelee kufanya kazi ya wananchi. Ngoja nisogee tukampokee kiongozi mwingine anayekabidhiwa kadi ya chadema leo katika hizi kampeni. Andaeni kejeli na laana zingine, lakini tunaendelea kukata mbuga hadi kitakapoeleweka!
 
Kuna watu wanaugua ugonjwa wa chuki katika forum hii. Wanapoona CHADEMA inapata nguvu na kuikabili CCM vilivyo huko Tarime wananuna kwa sababu wenyewe walishapitisha hukumu kwamba vyama vya upinzani havina kitu. Inawezekana ni kweli nyie wenzetu kwenye huu mtandao hamjasikia sera kutoka kwa wagombea. Hata hivyo wapiga kura wa Tarime wamezisikia. Wamesikia jinsi uongozi wao wa halmashauri chini ya CHADEMA ulivyoboresha maisha yao katika kipindi cha miaka miweli na nusu, ikiwemo kutoa elimu ya sekondari bure. Wamesikia mikakati ya kuwabana wawekezaji wa machimbo ya madini ya Nyamongo ili kuhakikisha kwamba mali asili hizi zinawanufaisha wananchi wa Tarime, na ndio maaana wameamua kuchukua "risk" ya kupigania haki zao na kuiunga mkono chadema.

Nasema tena poleni sana maoundits wenzangu wa online forum. Nawataarifu tu kwamba sisi wenzenu tuliopata nafasi kidogo ya kuonana na wananchi, yaani wapiga kura, tunaona jinsi ambavyo wananchi wameamua kuikumbatia CHADEMA kama chama mbadala. Inawezekana nyie wenzetu katika internet hamtambui hilo, lakini habari njema ni kwamba wananchi wapiga kura na hata CCM wenye wametambua hilo vizuri sana.

Haya nyie endeleeni kupiga ramli na kutoa laana, ngoja sisi tuendelee kufanya kazi ya wananchi. Ngoja nisogee tukampokee kiongozi mwingine anayekabidhiwa kadi ya chadema leo katika hizi kampeni. Andaeni kejeli na laana zingine, lakini tunaendelea kukata mbuga hadi kitakapoeleweka!

Kitila,

Kumbe uko kwenye kampeni? Mafanikio mema mkuu. Tarime ni jimbo lenu na inatakiwa mshinde, mkishindwa hapo, mtawatia wasiwasi watu wengi sana.
 
Mpaka leo sijasikia jambo la maana linalozungumziwa kuhusu mwananchi wa Tarime kutoka pande zote zinazogombania uchaguzi huu. Wamebaki kutambiana na kuonyeshana ubabe.

Mkuu hapa tupo pamoja. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba inaelekea wanaopiga kampeni huko Tarime wanajifikiria zaidi wao wenyewe kuliko wanaTarime. Kila mtu ana majigambo na kejeli dhidi ya mtu mwingine, haijasikika kwa ufasaha kabisa watawafanyia nini wapiga kura wa tarime iwapo watachaguliwa. lakini nadhani wananchi wa tariome wenyewe wana akili na wanajua la kufanya
 
Taarifa za leo kutoka huko Tarime zinasema Chiligati ameomba radhi kwa niaba ya CCM kutokana na wafuasi wake kucharanga watu mapanga jana
 
Taarifa za leo kutoka huko Tarime zinasema Chiligati ameomba radhi kwa niaba ya CCM kutokana na wafuasi wake kucharanga watu mapanga jana

MN,

Kuomba radhi hakutoshi, lazima wachukuliwe hatua pia. Karne ya 21 bado watu wanafikiri watashinda hoja kwa mapanga? Serikali lazima iwe strict na ujinga kama huo.
 
MN,

Kuomba radhi hakutoshi, lazima wachukuliwe hatua pia. Karne ya 21 bado watu wanafikiri watashinda hoja kwa mapanga? Serikali lazima iwe strict na ujinga kama huo.

TAmbwe Hiza anasema matokeo yatangazwe haraka maana kuna uwezekano wa wapinzani kupinga matokeo wakishindwa wakidai kuibiwa kura!!!!???? Tayari wizi unaandaliwa.

Jambo lingine ni kwamba, CCM wameshindwa kujitokeza katika majukwaa, wakati Mbowe anaonekana katika TV anahutubia mkutano wa hadhara, TAmbwe na mgombea wa CCM wanamwaga sera katika mkutano wa waandishi wa habari TArime.

Alama za nyakati
 
Thomas Ngawaiya, Salum Msabaha, Tambwe Hiza nk. Unadhani watasema nini, wamerudi CCM si kuwa hawajui CCM wanawafanyia nini waTZ, bali kwa maslahi yao. Yale waliyokuwa wanayapinga wakiwa upinzani sasa ndio wanayashabikia. Wote wanaangalia watagombe wapi Ubunge ili kuzidisha maslahi. Shame on them!
 
Kuweza kuhisi matokeo ya uchaguzi siyo kuangalia helikopta, mikutano ya watu n.k siri iko kwa nani atajitokeza kupiga kura. Turn out ya election kwangu ndiyo msingi wa mambo yatakavyokuwa.

a. Endapo turnout ya mjini Tarime itakuwa zaidi ya au karibu ya asilimia 50 ya wapiga kura na nje ya Tarime (vijijini) ikawa chini ya asilimia 40 na zaidi basi Chadema itashinda uchaguzi mzima kwa kati ya asilimia 60 na zaidi.

b. Endapo turnout ya mjini Tarime itakuwa karibu ya asilimia 50 lakini kule vijijini ikawa zaidi ya asilimia 50 vile vile CCM itaweza kushindwa kwa margin ndogo sana a little under 50.

c. Endapo hata hivyo vyama vingine vilivyosimamisha wagombea ukiondoa CCM na Chadema vikiweza kupata asilimia 10 ya kura zote (which I really doubt) basi CCM itashinda!

Mwanakijiji,
Hiyo analysis yako iko based na data zipi? Why 50% and not 60%, 70%, 80% n.k.? Population ya mjini ni kiasi gani vs ya vijijini? Chadema na CCM wanagawanaje hao voters?

I hope you didn't dream those figures. The analysises you see on CNN, NBC etc. in the US elections, are based on well collected figures and analysed for many years. How about your analysis??
 
Kuna watu wanaugua ugonjwa wa chuki katika forum hii. Wanapoona CHADEMA inapata nguvu na kuikabili CCM vilivyo huko Tarime wananuna kwa sababu wenyewe walishapitisha hukumu kwamba vyama vya upinzani havina kitu. Inawezekana ni kweli nyie wenzetu kwenye huu mtandao hamjasikia sera kutoka kwa wagombea. Hata hivyo wapiga kura wa Tarime wamezisikia. Wamesikia jinsi uongozi wao wa halmashauri chini ya CHADEMA ulivyoboresha maisha yao katika kipindi cha miaka miweli na nusu, ikiwemo kutoa elimu ya sekondari bure. Wamesikia mikakati ya kuwabana wawekezaji wa machimbo ya madini ya Nyamongo ili kuhakikisha kwamba mali asili hizi zinawanufaisha wananchi wa Tarime, na ndio maaana wameamua kuchukua "risk" ya kupigania haki zao na kuiunga mkono chadema.

Mkuu asante kwa post. Nashangaa hata mimi kuona watu hapa JF wanaleta analysis zisizo na kichwa wala miguu. Kuna mmoja amenichekesha eti:

a. Endapo turnout ya mjini Tarime itakuwa zaidi ya au karibu ya asilimia 50 ya wapiga kura na nje ya Tarime (vijijini) ikawa chini ya asilimia 40 na zaidi basi Chadema itashinda uchaguzi mzima kwa kati ya asilimia 60 na zaidi.

b. Endapo turnout ya mjini Tarime itakuwa karibu ya asilimia 50 lakini kule vijijini ikawa zaidi ya asilimia 50 vile vile CCM itaweza kushindwa kwa margin ndogo sana a little under 50.

c. Endapo hata hivyo vyama vingine vilivyosimamisha wagombea ukiondoa CCM na Chadema vikiweza kupata asilimia 10 ya kura zote (which I really doubt) basi CCM itashinda!

Huyu aliyetoa hizi analysis anastahili kupewa pole. maana ukweli wa mambo ni kwamba: Chadema ina nguvu zaidi huko vijijini zaidi hata ya mjini Tarime. Why? Kwasababu watu wa vijijini wamenufaika zaidi na matunda ya uongozi wa Chadema [rejea post ya Kitila Mkumbo].
 
Ati Chiligati kaomba radhi?
Sasa huo ndio uthibitisho wa CCM kushiriki katika huo unyama,cha muhimu sasa hao jamaa watoke na wafuate hatua za kisheria kutaka fidia.

Je,hao jamaa wangekufa Chiligati bado angejitokeza hadharanai kuomba radhi?
 
TAARIME.
1. Kuna mabasi mawili ya Zakaria yanatokea jijini mwanza yakiwa yamewabeba wafanyakazi wa kiwanda cha Coca cola ambacho ni cha Gachuma na huku wakisindikizwa na escort ya magari mawili ya polisi moja nyuma na jingine mbele yanaelekea Tarime , kufanya nini , stay tuned.

2.Jana usiku ziliandaliwa hujuma eneo la mgodi kule Nyamongo na wamekamatwa vijana zaidi ya 120 , kwa kile kilichoitwa kuwa mgodi ulivamiwa .......

3.Usiku wa leo maeneo ya vijijini zimeandaliwa hujuma kuwa mifugo itaibiwa na haswa Ngombe ili kesho wanatarime badala ya kwenda kupiga kura basi wawe wanafuatilia mifugo yao na kata hizo zitakazohusika ni zile ambazo CHADEMA wananguvu kubwa na hilo ni kuhakikisha kuwa wapiga kura wanapungua.

4.Hujuma nyingine ambayo imeandaliwa kufanyika maeneo ya mijini ni kuwa CCM wamehimizana kwenda kupiga kura asubuhi na ikifika saa tano basi polisi watazua mtafaruku na kuanza kutumia nguvu kuhakikisha kuwa hakuna watu kwenda kupiga kura na hivyo kuipa CCM ushindi.

5.Mawakala wa NCCR NA DP wamekubaliana na wale wa CCM kuwa watoe tamko kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki , na hakuna kilichovuruga uchaguzi huo ,hata kama polisi watatekeleza mpango wa 4 hapo juu, .

CHADEMA wamejiandaa kukabiliana na jambo hili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi wa Tarime, wananchi wamejiandaa kulinda kura zao na haki zao .

kesho ntaweza kuwapa updates za kila wakati kuhusiana na upigaji kura , matukio kwenye vituo na kuhusu matokeo na hali halisi .

 
CHADEMA wamejiandaa kukabiliana na jambo hili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi wa Tarime, wananchi wamejiandaa kulinda kura zao na haki zao .


hao chadema wanamejiandaaje kukabiliana na hujuma ulizozoorodhesha? Isije wakapigwa dafrao kwenye uchaguzi halafu waanze kualalamika baada ya kushindwa!
 
TAARIME.
1. Kuna mabasi mawili ya Zakaria yanatokea jijini mwanza yakiwa yamewabeba wafanyakazi wa kiwanda cha Coca cola ambacho ni cha Gachuma na huku wakisindikizwa na escort ya magari mawili ya polisi moja nyuma na jingine mbele yanaelekea Tarime , kufanya nini , stay tuned.

2.Jana usiku ziliandaliwa hujuma eneo la mgodi kule Nyamongo na wamekamatwa vijana zaidi ya 120 , kwa kile kilichoitwa kuwa mgodi ulivamiwa .......

3.Usiku wa leo maeneo ya vijijini zimeandaliwa hujuma kuwa mifugo itaibiwa na haswa Ngombe ili kesho wanatarime badala ya kwenda kupiga kura basi wawe wanafuatilia mifugo yao na kata hizo zitakazohusika ni zile ambazo CHADEMA wananguvu kubwa na hilo ni kuhakikisha kuwa wapiga kura wanapungua.

4.Hujuma nyingine ambayo imeandaliwa kufanyika maeneo ya mijini ni kuwa CCM wamehimizana kwenda kupiga kura asubuhi na ikifika saa tano basi polisi watazua mtafaruku na kuanza kutumia nguvu kuhakikisha kuwa hakuna watu kwenda kupiga kura na hivyo kuipa CCM ushindi.

5.Mawakala wa NCCR NA DP wamekubaliana na wale wa CCM kuwa watoe tamko kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki , na hakuna kilichovuruga uchaguzi huo ,hata kama polisi watatekeleza mpango wa 4 hapo juu, .

CHADEMA wamejiandaa kukabiliana na jambo hili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi wa Tarime, wananchi wamejiandaa kulinda kura zao na haki zao .

kesho ntaweza kuwapa updates za kila wakati kuhusiana na upigaji kura , matukio kwenye vituo na kuhusu matokeo na hali halisi .


Hivi hata kama busara zimeondoka basi hata akili za kufikiria madhara ya kufakamia uhuni huu CCM wamekosa. CCM ijue wazi kuwa kwa hali ya kisiasa sasa madhara ya kutumia uhuni kupora jimbo la TARIME ni makubwa kuliko watakapokubali washindwe ama washinde kihalali....

Uhuni wowote wa kulazimisha ushindi tarime utawakimbiza wengi CCM na hata kuwalazimu wale waliojiamulia kukaa kimya kuunga mkono upinzani kujitokeza kwa ari kubwa.....

Uhuni ukipelekea CHADEMA kushindwa utawasaidia zaidi CHADEMA zaidi ya kuwamaliza kama magwiji mikakati wa CCM wanavyojitapa......

Vilevile CCM watambue kuwa wako nyuma kipropaganda haswa kwenye matumizi ya vyombo vya habari. Hivi karibuni watajikuta kuwa ile dhana ya kuwa upinzani ni hatari kwa usalama wa nchi itageuka kuwa UHUNI wa CCM ni hatari kwa usalama wa wananchi......

Tanzanianjema
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom