Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
TAARIME.
1. Kuna mabasi mawili ya Zakaria yanatokea jijini mwanza yakiwa yamewabeba wafanyakazi wa kiwanda cha Coca cola ambacho ni cha Gachuma na huku wakisindikizwa na escort ya magari mawili ya polisi moja nyuma na jingine mbele yanaelekea Tarime , kufanya nini , stay tuned.

2.Jana usiku ziliandaliwa hujuma eneo la mgodi kule Nyamongo na wamekamatwa vijana zaidi ya 120 , kwa kile kilichoitwa kuwa mgodi ulivamiwa .......

3.Usiku wa leo maeneo ya vijijini zimeandaliwa hujuma kuwa mifugo itaibiwa na haswa Ngombe ili kesho wanatarime badala ya kwenda kupiga kura basi wawe wanafuatilia mifugo yao na kata hizo zitakazohusika ni zile ambazo CHADEMA wananguvu kubwa na hilo ni kuhakikisha kuwa wapiga kura wanapungua.

4.Hujuma nyingine ambayo imeandaliwa kufanyika maeneo ya mijini ni kuwa CCM wamehimizana kwenda kupiga kura asubuhi na ikifika saa tano basi polisi watazua mtafaruku na kuanza kutumia nguvu kuhakikisha kuwa hakuna watu kwenda kupiga kura na hivyo kuipa CCM ushindi.

5.Mawakala wa NCCR NA DP wamekubaliana na wale wa CCM kuwa watoe tamko kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki , na hakuna kilichovuruga uchaguzi huo ,hata kama polisi watatekeleza mpango wa 4 hapo juu, .

CHADEMA wamejiandaa kukabiliana na jambo hili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi wa Tarime, wananchi wamejiandaa kulinda kura zao na haki zao .

kesho ntaweza kuwapa updates za kila wakati kuhusiana na upigaji kura , matukio kwenye vituo na kuhusu matokeo na hali halisi .



kesho sijui keshokutwa kapigeni kura zeru ,haya mambo ya kutanguliza vilio yamepitwa na wakati.

Kila kituo kutakua na mwakilishi wenu kuthibitisha matokeo.Na kama mmegundua ccm wapige asubuhi kura zao basi ninyi waambieni wafuasi wenu wawe wa kwanza kwenye mstari ili wa ccm wawe wa mwisho.
 
•Leo ni leo Tarime (Majira)

*Mchuano mkubwa ni kati ya CCM, CHADEMA
Mgodi wafungwa kuhofia kuporwa
Kilaini awafananisha wagombea na mafisadi
Gorogosi: Watanzania tuombee amani nchi yetu
Na George John, Tarime

HATIMAYE wakazi 146,919 katika jimbo la uchaguzi la Tarime mkoani Mara, leo wanatarajia kupiga kura katika uchaguzi mdogo wa ubunge, baada ya kazi ya kampeni iliyoanza Septemba 14 kukamilika jana jioni.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Bw. Trasias Kagenzi, aliwaaambia waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa jana kuwa maandalizi yote ya kuwezesha kufanyika uchaguzi huo yamekamilika na kwamba shughuli za usambazaji wa vifaa zilitarajiwa kuanza jana katika kata 20 za jimbo hilo.

Alisema vituo 406 vimeandaliwa na idadi ya wapiga kura imeongezeka kutoka 130,000 waliopiga kura mwaka 2005, na awali katika uchaguzi huo mdogo, ilitarajiwa wapiga kura wangekuwa 146,510 lakini idadi hiyo imeongezeka baada ya maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Bw. Kagenzi alisema baada ya maboresho hayo kufanyika, majina ya watu 501 yameondolewa katika Daftari hilo kutokana na vifo huku 20 wakiondolewa kutokana na umri na 11 kubainika kuwa si raia wa Tanzania.

"Tume ya Uchaguzi tumejiandaa vya kutosha, hatutarajii tatizo, kwani la majina yaliyodaiwa kutoonekana tumesawazisha kwa kuwa kompyuta iliruka baadhi ya majina na sasa tumetumia teknolojia ya Afrika Kusini ya kutumia simu ya mkononi kwamba kama mtu hakuona jina anatuma ujumbe na kupata majibu ya kuonesha sehemu anayostahili kupiga kura," alisema Bw. Kagenzi.

Aliongeza kuwa uchaguzi huo unakwenda pamoja na uchaguzi wa udiwani katika Kata ya Tarime Mjini, ambayo pia imekuwa wazi kutokana na kifo cha Bw. Chacha Wangwe.

Aliongeza kuwa hadi sasa hakuna malalamiko kutoka kwa wapiga kura na tayari ofisi ya Tume imetangaza namba 0753123179 za simu itakayotumika kusaidia watu watakaokumbwa na matatizo, likiwamo la ukosekanaji wa majina kwa kutuma ujumbe wa maandishi na kupata majibu papo hapo.

Alisema matokeo ya ubunge yatatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo huku ya udiwani yakitangazwa na wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata.

Jana jioni vyama vya CCM na CHADEMA vilihitimisha kampeni zao mjini hapa kwa CCM kuwa katika uwanja wa mpira huku CHADEMA ikiwa katika uwanja wa Shule ya Msingi Nyamisangura. Kinyang'anyiro kikubwa ni baina ya CCM na CHADEMA.

Waangalizi wawasili

Wakati huo huo, waangalizi wa kimataifa tayari wamewasili mjini hapa, kwa ajili ya kushuhudia uchaguzi huo, kutokana na malalamiko ya upendeleo kwa vyombo vya Dola juu ya mwenendo mzima wa kampeni hizo.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Lewis Makame, alithibitisha jana kuwasili kwa waangalizi hao mjini hapa ikiwa ni wiki moja baada ya mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani, kufika hapa kushuhudia kampeni, kukutana na baadhi ya vyama vya siasa, Jeshi la Polisi na Msimamizi wa Uchaguzi huo.

Nchi zilizotuma waangalizi ni Uingereza, Kanada, Uswidi, Zambia na Malawi. Majira jana ilishuhudia zaidi ya magari matano yakiwa na waangalizi hao yakienda katika ofisi za Tume.

Katika hatua nyingine, Tume imetangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 11 nchini na ubunge katika jimbo la Tarime leo.

Akitangaza uamuzi huo kwa waandishi wa habari mjini hapa jana, Jaji Makame, alisema madiwani hao watachaguliwa baada ya kata zao kubaki wazi kwa sababu mbalimbali zikiwamo za vifo.

Alisema maandalizi ya uchaguzi huo mdogo wa ubunge na udiwani yamekamilika na katika jimbo la Tarime, ulinzi umeimarishwa, ili kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa amani na utulivu.

Jaji Makame alisema pamoja na vituo kuwa 406 huku idadi ya askari kutoka nje ikiwa ni 450 haina maana kuwa idadi hiyo haitatosha kwa maelezo kuwa bado kuna askari wengine wa mkoa wa Mara ambao pia watahusika kuhakikisha usalama unakuwapo wa kutosha.

Taratibu za kupiga kura

Alisisitiza wananchi baada ya kupiga kura waondoke mara moja vituoni, ili kuepusha vurugu, na baada ya upigaji wa kura kukamilika, wasimamizi wasaidizi wabandike matokeo katani na nakala zake wapewe mawakala wa vyama vinavyoshiriki kabla ya Msimamizi Mkuu kutangaza mshindi baada ya matokeo kujumlishwa.

Aliongeza kuwa Tume imesikitishwa na vurugu zilizojitokea katika kampeni na kuvitaka vyombo vya Dola kuchukua hatua kwa wahusika bila haya.

Uchaguzi huo mdogo unafanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa Tarime na diwani wa Tarime Mjini, Bw. Wangwe kilichotokea Julai 28 mwaka huu, katika eneo la Pandambili wilayani Kongwa, Dodoma.

**Mgodi wafungwa

Habari zaidi zinaeleza kuwa mgodi wa dhahabu wa North Mara uliopo eneo la Nyamongo, Tarime, mkoani Mara umefungwa kwa muda usiojulikana kuhofia vurugu kutokea wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime.

Mmoja wa wafanyakazi wa mgodi huo ambaye hakutaka jina lake litokee kwenye gazeti, alilieleza Majira Jumapili jana kuwa mgodi huo umefungwa juzi na wafanyakazi wote wamepewa likizo ya muda.

"Hapa unaponiona tayari niko likizo tangu juzi mgodi ulipofungwa na wafanyakazi wengine tayari wamesafirishwa kwa magari kurudi kwao kwa kuhofia kutokea vurugu zinazoweza kusababisha maafa," alielezea mfanyakazi huyo ambaye alikutana na mwandishi wetu kwenye mghahawa wa Girango mjini Tarime.

Alisema hawajaambiwa ni lini mgodi huo utafunguliwa ingawa kwa kipindi chote watakachokuwa likizo watakuwa wanalipwa.

"Eneo la Nyamongo lisikie hivi hivi brother, ni hatari hasa wakati kama huu wa uchaguzi, wale jamaa ni kawaida kuua maana hata usipokuwepo uchaguzi tayari matokeo kadhaa ya mauaji yamefanyika ambapo kuna walinzi, viongozi wa kampuni pamoja na baadhi ya wafanyakazi wameshawahi kuuawa," alisema.

Alitaja moja ya matukio mengine yaliyofanywa na wachimbaji wadogowadogo kuwa ni pamoja na helikopta moja ya kampuni ya Barricks inayomiliki mgodi huo ilipigwa mawe na kusababisha maafa.

Alipoulizwa kwa njia ya simu juu ya kufungwa kwa mgodi, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Bw. Stanley Kolimba, kwanza alikana kusikia suala hilo lakini baada ya muda alikubali na kueleza kuwa taarifa alizonazo ni kwamba mgodi huo umefungwa kwa muda kutokana na uzalishaji wake kushuka na si kuhofia vurugu za uchaguzi.

Mwandishi wetu alipowasiliana kwa simu na Meneja Uhusiano, wa Kampuni ya Barrick, Bw. Tewelli Tewelli, alisema mgodi umefungwa baada kusikia fununu kuwa kunaweza kutokea vurugu za kuvamia mgodi wakati wa uchaguzi na sababu nyingine ni baadhi ya wafanyakazi wa mgodi huo kuwapa fursa ya kwenda kupiga kura.
 
Mbona Chaguzi Ndogo zina kuwa na fujo na Mbwembwe nyingi kuliko uchaguzi mkuu? what is so special na Uchaguzi mdogo tofauti na kile tunachokuwa nacho kwenye uchaguzi mkuu?
 
TAARIME.
1. Kuna mabasi mawili ya Zakaria yanatokea jijini mwanza yakiwa yamewabeba wafanyakazi wa kiwanda cha Coca cola ambacho ni cha Gachuma na huku wakisindikizwa na escort ya magari mawili ya polisi moja nyuma na jingine mbele yanaelekea Tarime , kufanya nini , stay tuned.

2.Jana usiku ziliandaliwa hujuma eneo la mgodi kule Nyamongo na wamekamatwa vijana zaidi ya 120 , kwa kile kilichoitwa kuwa mgodi ulivamiwa .......

3.Usiku wa leo maeneo ya vijijini zimeandaliwa hujuma kuwa mifugo itaibiwa na haswa Ngombe ili kesho wanatarime badala ya kwenda kupiga kura basi wawe wanafuatilia mifugo yao na kata hizo zitakazohusika ni zile ambazo CHADEMA wananguvu kubwa na hilo ni kuhakikisha kuwa wapiga kura wanapungua.

4.Hujuma nyingine ambayo imeandaliwa kufanyika maeneo ya mijini ni kuwa CCM wamehimizana kwenda kupiga kura asubuhi na ikifika saa tano basi polisi watazua mtafaruku na kuanza kutumia nguvu kuhakikisha kuwa hakuna watu kwenda kupiga kura na hivyo kuipa CCM ushindi.

5.Mawakala wa NCCR NA DP wamekubaliana na wale wa CCM kuwa watoe tamko kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki , na hakuna kilichovuruga uchaguzi huo ,hata kama polisi watatekeleza mpango wa 4 hapo juu, .

CHADEMA wamejiandaa kukabiliana na jambo hili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi wa Tarime, wananchi wamejiandaa kulinda kura zao na haki zao .

kesho ntaweza kuwapa updates za kila wakati kuhusiana na upigaji kura , matukio kwenye vituo na kuhusu matokeo na hali halisi .



Mpaka Kisieleweke,
Hizi updates zako za kichochezi wala hatuzitaki. Sijui una masikio, macho, miguu mingapi maana mara unahabari za gari la coca cola, habari za migodini, siri za kuiba ng'ombe, siri za vurugu za CCM, siri za NCCR, DP & CCM n.k.

Hivi wewe ni nani ukayeyajua yote haya, hata yaliyo siri za wengine, kama sio mzushi? Watu wa aina hii ndio wanaotuletea vurugu nchini kwa majungu yao.
 
Mpaka Kisieleweke,
Hizi updates zako za kichochezi wala hatuzitaki. Sijui una masikio, macho, miguu mingapi maana mara unahabari za gari la coca cola, habari za migodini, siri za kuiba ng'ombe, siri za vurugu za CCM, siri za NCCR, DP & CCM n.k.

Hivi wewe ni nani ukayeyajua yote haya, hata yaliyo siri za wengine, kama sio mzushi? Watu wa aina hii ndio wanaotuletea vurugu nchini kwa majungu yao.

Mzeee umetumwa ? kwanini wewe usiwe mzushi? hutaki kuamini chcochote kutoka kwa Mpaka kieleweke? keep calm
 
Date::10/11/2008
Tarime roho juu: Wapiga kura 400 waongezeka ghafla
Frederick Katulanda na Musa Juma, Tarime
Mwanannchi

BAADA ya kampeni nzito za kuwania ubunge wa Jimbo la Tarime zilizojaa vitimbi na uhasama, leo wananchi wa jimbo hilo wanatengua kitendawili cha nani atakuwa mbunge wao baada ya kukamilisha zoezi la kupiga kura.

Hata hivyo, hali imezidi kuwa tete katika jimbo hilo na habari za hivi karibuni zinaeleza kuwa, Mgodi wa North Mara umefungwa kwa muda usiojulikana kwa hofu ya vurugu kutokea leo na siku ya kutangazwa matokeo.

Katika kampeni hizo zilizodumu kwa mwezi mmoja sasa, wagombea wa vyama vinne vinavyoshiriki walijinadi kwa wapiga kura huku viongozi wakuu wa vyama hivyo wakihamia Tarime, kuongeza nguvu na kukoleza kampeni zao.

Hata hivyo, kampeni hizo zilitawaliwa na vitimbi vingi na uhasama uliosababisha baadhi ya watu kukamatwa na polisi na wengine kujeruhiwa kwa mapanga na mawe kutokana na vurugu kadhaa zilizokuwa zikitokea.

Wagombea wote jana walicheza kete zao za mwisho kwa kuhitimisha kampeni zao mjini Tarime, huku wakitoa ahadi nyingi za kuwapatia maendeleo wananchi iwapo watachaguliwa kuingia bungeni.

Mgombea wa Chama cha Demokarsia na Maendeleo (Chadema), Charles Mwera Nyanguru alihitimisha kampeni zake kwa kufanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Nyamisangura na kuhudhuriwa na viongozi karibu wote wa juu wa chama hicho akiwamo, Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe.

Kwa upande wake, Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Christopher Ryoba Kangoye alihitimisha kampeni zake katika Uwanja wa Sabasaba ambako mbali ya yeye kujinadi, pia viongozi wa juu wa chama hicho walimnadi kwa wapiga kura.

Mgombea wa Democratic Party (DP), Mchungaji Johnson Makanya alifanya mkutano wake katika eneo la Mtaa wa Starehe wakati mgombea wa NCCR-Mageuzi, Enock Marwa Makubo alihitimisha kampeni zake katika Uwanja wa Mpira wa Sabasaba.

Tukio kubwa lililotokea katika kampeni hizo ni la vyama vya CCM na Chadema kutumia helikopta katika kampeni zao, ambalo lilisababisha wafuasi wao kupigana na baadhi yao kujeruhiwa wakigombea eneo la kutua helikopta ya Chadema.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imepiga marufuku wafuasi wa vyama kutobakia katika vituo vya kupiga kura baada ya kupiga kura kama ambavyo, wamekuwa wakielezwa na baadhi ya wanasiasa.

Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Lewis Makame alionya kuwa, kubaki vituoni ni kinyume na utaratibu na sheria za uchaguzi na kuonya kuwa, watakaofanya hivyo Jeshi la Polisi litawashughulikia.

Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kisha kuondoka baada ya kupiga kura.

Kwa mujibu wa Makame, maandalizi ya uchaguzi yamekamilika ikiwa ni pamoja na vifaa kuwasili katika maeneo yote. Watu 146,919 wanatarajiwa kupiga kura katika vituo 406 vilivyopo katika kata 20 za Wilaya ya Tarime.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Tarime, Trasiansi Kagenzi alisema mwaka 2005 waliokuwa wamejiandikisha ni 130,000, lakini kutokana na maboresho ya daftari la wapiga kura wameongezeka hadi kufikia 146,919.

Alisema katika maboresho hayo waliwaondoa katika daftari watu 501 baada ya kuthibitika kufariki dunia, wengine 20 kutokana na umri wao kuwa chini ya miaka 18 na 19 ni raia wa Kenya.

Wakati huo huo, kumeibuka utata wa idadi ya watu wanaopaswa kupiga kura baada ya kudaiwa kuwa watu 400 wamezidi idadi ya watu 146,510 iliyokuwa inatarajiwa na kufikia 146,919.

Akizungumzia utata huo, Kagenzi alisema, watu 409 wameongezeka kutokana na uhakiki mwingine ambao umefanywa na NEC baada ya watu kulalamika kwamba, hawaoni majina yao.


Hata hivyo, Kagenzi alisema kati ya wapiga kura 200 ambao walilalamikia majina yao kutoonekana hakuna hata mmoja aliyefika ofisini kwake, bali malalamiko yametoka kwenye vyama vya siasa.

"Haya marekebisho yamefanyika kwa umakini, kwani awali kompyuta iliwatema hawa wapigakura 409 na sasa wamerejeshwa, hivyo tuna imani kila mtu atapata nafasi ya kupiga kura kesho(leo)," alisema Kagenzi.

Vile vile kumezuka utata wa vituo vya kupigia kura baada ya kuongezea kimoja kutoka 406 hadi 407 na baada ya kufanyika marekebisho katika mkutano na waandishi wa habari, Jaji Lewes Makame ilielezwa kuwa vituo vitakuwa 406.

Wakati huo huo, Waangalizi wa nje kutoka balozi mbalimbali nchini zikiwamo za Ulaya wamewasili mjini Tarime pamoja na wa kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu chini ya Kaimu Mkurugenzi wake, Fransis Kiwanga.

Nchi ambazo zimetuma waangalizi wake ni Uingereza, Canada, Sweden, Zambia na Malawi .

Katika hatua nyingine, Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, uliopo Nyamongo wilayani Tarime, umefungwa kwa muda usiojulikana kutokana na hofu ya kuibuka kwa vurugu leo na siku ya kutangaza matokeo ya uchaguzi.

Habari zilizopatikana jana mjini Tarime na kuthibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Stanley Kolimba, zimeeleza kwamba mgodi huo umefungwa kwa muda usiojulikana.

Wakizungumza jana na gazeti hili baadhi ya wafanyakazi wa mgodi huo walisema wako katika harakati za kurejea makwao.

Kolimba alisema kuwa, kulingana na taarifa alizonazo, mgodi huo umesimamisha uzalishaji kwa muda na kukanusha si kutokana na uchaguzi.

Naye Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Barric, Teweli Teweli alisema jana kuwa mgodi huo umefungwa kwa ajili ya kuhofia vurugu na kuwaruhusu wafanyakazi wao kupiga kura.

Tambo za wagombea:

Mgombea wa Chadema Mwera anasema leo ana uhakika wa kutangazwa kuwa mbunge na kuwaomba polisi wasiwe chanzo cha vurugu za uchaguzi na kwa kujiingiza katika siasa za kulazimisha ushindi kwa wagombea wa CCM.

Mwera mwenye umri wa miaka 49 ambayeni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, anasema utendaji wake mzuri katika halmashauri hiyo kwa kipindi cha miaka miwili na nusu unampa imani kwamba atashinda.
 
Date::10/11/2008
Waziri Chilligati atimuliwa hospitali Tarime
*Majeruhi aliyekwenda kumuona ahamishiwa Bugando

Mpoki Bukuku na Mussa Juma, Tarime
Mwananchi

KATIBU mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati na Mbunge wa Musoma, Vedasto Matayo jana walitimuliwa hospitali wakati walipokwenda kuwajulia hali vijana waliojeruhiwa kwa mapanga katika vurugu zilizotokea juzi wilayani Tarime.

Tukio hilo lilitokea jana asubuhi wakati Chiligati, ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, alipowasili kwenye zahanati ya Tarime kuwatembelea vijana hao waliokatwa mapanga wakati kulipotokea mapambano baina ya wafuasi wanaoaminika kuwa wa CCM na Chadema, lakini akapokelewa na vijana waliomzuia kuingia hospitalini.

“Toka hapa hakuna mtu mwenye shida na nyie... mimi nitamuuguza mdogo wangu sihitaji msaada wenu,” alisikika mmoja wa jamaa waliokuwa sehemu ya mapokezi ya hospitali hiyo, wakionekana dhahiri kuwa walipania kutoruhusu viongozi na wafuasi wa CCM kuona majeruhi hao.

Hilo lilitokea baada ya Chiligati kuongea na waandishi wa habari jana kuhusu tukio hilo lililotokea kwenye Uwanja wa Sabasaba wakati vijana wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chadema walipokuwa wakiandaa eneo ambalo ndege ya kukodi wanayoitumia kwa kampeni ingetua na kuzuiwa na vijana wanaoaminika kuwa wafuasi wa CCM.

Jana asubuhi, Chiligati alikwenda kwanza Hospitali ya Wilaya ya Tarime, lakini akaambiwa kuwa vijana hao walikuwa hawajafikishwa hospitalini hapo na hivyo kuambiwa ajaribu kwenda zahanati hiyo ya binafsi.

Baada ya kutoka hapo alielekea moja kwa moja katika zahanati hiyo iliyo katikati ya mji, akiwa ameongozana na Mathayo, ambaye pia ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM.

Walipoingia mapokezi wakiwa wamevalia sare za CCM, kundi la watu lilitoka ndani ya hospitali hiyo na kuanza kupiga kelele kupinga kitendo chao cha kwenda hospitali hipo.

Hali ilianza kuwa mbaya baada ya vijana zaidi waliokuwa nje kuanza kujazana na wengine wakitishia kuwapiga iwapo wasingeondoka mara moja katika eneo hilo.

“Hata kama umekuja na gari la milioni 400, ni lako na wenzako sisihatuhitaji msaada... toka kabla hatujakuchenjia,” alisema mmoja wao. Pamoja na jitihada za Chiligati kuwasihi kuwa walikuja mahali hapo kwa nia njema ya kutaka kuwajulia hali vijana hao, hakuna aliyewaelewa na kuzidisha amri ya kuwataka watoke nje na kuondoka.

Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, Chiligati alitoka nje ambako, pia alizongwa na kurushiwa maneno ya kashfa yeye na chama chake, kabla ya kuingia garini na kuondoka.

Baada ya kutoka eneo hilo, Chiligati alionyesha wazi kukerwa na kitendo
hicho na kusema kuwa kitendo hicho hakikuwa cha kistaarabu na kwamba watu wenye akili timamu wasingeweza kufanya hivyo.

“Suala la kumjulia hali mgonjwa halina itikadi. Tumekuja kwa nia njema, lakini naona hawa jamaa wanashindwa kuelewa,” alisema baadaye kabla ya kwenda mjini Sirari ambako alishiriki kumnadi mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM, Christopher Kangoye.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema jana, Chiligati alieleza kusikitishwa na mapambano yaliyohusisha mapanga, akisema hata chama chake, CCM hakikufurahishwa na vurugu hiyo.

Lakini akageukia vyombo vya habari na kusema: "Watu waliojeruhiwa ni watatu tu, lakini magazeti yameandika kana kwamba Tarime nzima wamekatwa mapanga."

Wakati huohuo, majeruhi Genya Sabai alitarajiwa kuhamishiwa hospitali ya rufani ya Bugando baada ya hali yake kuwa mbaya.

Sabai ambaye alikuwa amekatwa panga la shavu la kushoto, jana alianza kuvuja damu kutokea masikioni licha ya kushonwa katika jeraha lake.

Daktari mfawidhi wa zahanati ya Tarime, ambako majeruhi huyo amelazwa, Dk Philemon Hungiro alisema hali yake sio nzuri na hivyo anapaswa kuhamishiwa hospitali ya rufani ya Bugando.

“Jana tulimshona nyuzi za ndani sita na nje nyuzi 19, lakini leo damu zinatoka hivyo tunashauri apelekwe Hospitali ya Rufani ya Bugando,” alisema Dk Hungiro.

Alisema hali za majeruhi wengine Masham Edward(23) mkazi wa Rebu, Athuman Selemani (22) mkazi wa Ronsoti na Joseph Daniel(25) Songambele zinaendelea vizuri na wameruhusiwa kutoka hospitali.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana, ndugu wa Sabai, Paulo Agostine na dada wa Modesta Mwita, walisema walilazimika kumkatalia Waziri Chilligati kuonana na ndugu yao kutokana na kuamini kuwa CCM ndio waliomshambulia.

“Amekuja hapa Chiligati akiongozana na Mbunge wa Musoma Mjini, Vedastus Matayo, lakini tumewafukuza na tumewaambia kwanza wawakamate watuhumiwa,” alisema Mwita.

Alisema anawajua kwa majina vijana ambao walimshambulia Sabai na wenzake.

“Leo asubuhi mimi nimewakuta hawa watuhumiwa wakiwa ofisi za CCM na wanalindwa na viongozi, sasa tunashangaa iweje huyu Chiligati aje kumuona mgonjwa,” alisema Mwita.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Leberatus Barlow alisema juzi kuwa bado wanawasaka watuhumiwa hao, ili kujibu shitaka linalowakabili na tayari gari lililotumika linashikiliwa.

Wakati huohuo, kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, zinahitimishwa leo katika mikutano itakayofanyika mjini Tarime na eneo la Nyamongo ambapo kuna migodi ya machimbo ya dhahabu.

Kuhitimishwa kwa kampeni hizo kunatazamiwa kuwa kwa aina yake baada ya CCM kushusha helikopta ya pili kupambana na helikopta moja ya Chadema.

Jana Chadema walikuwa wakiendelea kutumia helikopta yao moja ikiwa imembeba mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, mgombea wa ubunge, Charles Mwera, kada aliyehamia Chadema toka CCM, Mwita Mwikwabe Waitara na Tundu Lissu.

Wakati CCM inatarajia leo kuhitimisha kampeni katika uwanja wa michezo Sabasaba, Chadema leo watakuwa na mikutano mitatu tofauti ambayo itamalizikia katika machimbo ya Nyamongo na mjini Tarime.

Naye Festo Polea anaripoti toka Dar es Salaam kuwa, baadhi ya wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoa wa Dar es Salaam, wameshinikiza mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe kujiuzulu mara moja.

Wanachama hao jana walifanya maandamano ya amani kwa lengo la kushinikiza mwenyekiti huyo kujiuzulu na kusema endapo mwenyekiti huyo atashindwa kufanya hivyo wataitisha mkutano mkubwa ili kumshinikiza.

Wanachama hao pia walitaka chama hicho kiitishe kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Chadema chenye lengo la kujadili mustakabali wa chama kwa madai kuwa, kwa sasa chama hicho kimekuwa kikiyumba kutokana na ukabila unaoonyeshwa.
 
Kikao cha CCM kimemalizika jana saa tano usiku katika hoteli ya CMG. Kimeamua mambo mazito matatu yafuatayo:

1) Vituo vya sirari, tarime mjini, nyamongo, nyamwaga, bumera, trm sec na vituo vya itiryo ambako chadema wana nguvu mawakala wa ccm wamepewa laki tatu ya kuwapa mawakala wa chadema na wasimamizi wa vituo wanapewa laki tano.

2) Polisi wameambiwa kuhoji barua za mawakala wa chadema na hivyo kuwazuia kuingia kwenye kituo kwa muda wakati zoezi la kupiga kura likiwa linaendelea. Ingawa sio jukumu la polisi kufanya hivyo lakini mkakati ni kwamba wakati polisi wanawazuia mawakala nje ya kituo huko ndani msimamizi anapata muda wa kuweka mambo sawa.

3) wasimamizi kutohoji picha za wapiga kura na wanatakiwa wafuate majina ya wapiga kura yaliyobandikwa nje ya kituo ambako vijana wengi majina yao hayapo. pia kuwazuia mawakala wa chadema kutumia daftari la kudumu lenye picha ya kila mgombea waliopewa na chama chao.
 
Kikao cha CCM kimemalizika jana saa tano usiku katika hoteli ya CMG. Kimeamua mambo mazito matatu yafuatayo:

1) Vituo vya sirari, tarime mjini, nyamongo, nyamwaga, bumera, trm sec na vituo vya itiryo ambako chadema wana nguvu mawakala wa ccm wamepewa laki tatu ya kuwapa mawakala wa chadema na wasimamizi wa vituo wanapewa laki tano.

2) Polisi wameambiwa kuhoji barua za mawakala wa chadema na hivyo kuwazuia kuingia kwenye kituo kwa muda wakati zoezi la kupiga kura likiwa linaendelea. Ingawa sio jukumu la polisi kufanya hivyo lakini mkakati ni kwamba wakati polisi wanawazuia mawakala nje ya kituo huko ndani msimamizi anapata muda wa kuweka mambo sawa.

3) wasimamizi kutohoji picha za wapiga kura na wanatakiwa wafuate majina ya wapiga kura yaliyobandikwa nje ya kituo ambako vijana wengi majina yao hayapo. pia kuwazuia mawakala wa chadema kutumia daftari la kudumu lenye picha ya kila mgombea waliopewa na chama chao.

makubwa haya, tusubiri na tuone
 
Sala Maalumu.
Baba yetu ulie mbinguni naomba CHADEMA ishinde na CCM ishindwe mana maovu ya wana wako yanasababishwa na CCM. Naombea kila la kheri CHADEMA watete jimbo na iwe mwanzo wa CCM kuporomoka. kwa jina la BABA, MWANA na ROHO MTAKATIFU.

Ameni
 
For those with any new development of the elections in Tarime (voting, results, celebrations etc) please update them here; at the end of the elections this thread will be merged with the main Tarime thread. We are trying to avoid multiple new threads of whatever new thing that will come out of Tarime today.


Matokeo rasmi:

Vituo - 406
Idadi - 146,919
Waliopiga Kura - 67,733
Kura Halali - 64,765
Zilizoharibika - 2,938


UDP - 305
NCCR - 949
CCM - 28,696 - 42.6%
CHADEMA - 34,545 - 51%
 
Mpaka Kisieleweke,
Hizi updates zako za kichochezi wala hatuzitaki. Sijui una masikio, macho, miguu mingapi maana mara unahabari za gari la coca cola, habari za migodini, siri za kuiba ng'ombe, siri za vurugu za CCM, siri za NCCR, DP & CCM n.k.

Hivi wewe ni nani ukayeyajua yote haya, hata yaliyo siri za wengine, kama sio mzushi? Watu wa aina hii ndio wanaotuletea vurugu nchini kwa majungu yao.

Wew nani kwanza? Mkuu kama hutaki kuzisikia mbona bado unaganda kwenye post zake?

Wewe ndiyo mzushi na unaharibu thread,acha vurugu bro.
 
... matokeo Tarime kutangazwa `live`
2008-10-11 21:04:38
Na Emmanuel Lengwa, Jijini


Wakati uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime ukitarajiwa kufanyika kesho, wapigakura wa wilayani Tarime wanaweza kujua vituo vyao vya kupigia kura kwa kutumia simu zao za mkononi huku matokeo yatakayowasilishwa toka katika kila kituo yakitarajiwa kurushwa moja kwa moja kupitia Kituo cha Luninga cha TBC1.

Teknolojia hiyo mpya imetangazwa leo asubuhi na Msimamizi wa Uchaguzi huo mdogo wa Tarime Bw. Trasias Kagenzi, wakati akizungumza \'live\' kwenye luninga leo asubuhi.

Bw. Kagenzi amsema maandalizi yote ya uchaguzi huo yamekamilika na kuwa tayari dosari zote zilizokuwa zimejitokeza zimerekebishwa na sasa mambo yote yanakwenda vizuri.

Akifafanua jinsi mpigakura anavyoweza kupata taarifa zake za sehemu ya kupigia kura kwa kupitia kilongalonga chake, Bw. Kagenzi amesema kuwa mwenye simu anafungua sehemu ya kuandika meseji kwenye simu yake, anaadika namba tatu, anaweka alama ya koma ikifuatiwa na namba ya shahada yake ya kupigia kura kisha anatuma kwenda namba 0753 123 179.

Akasema mpigakura akishatuma ujumbe wake kwenye namba hiyo atatumiwa jina lake, kata yake kituo chake cha kupigia kura na namba ya mlango atakaoingia wakati akienda kupiga kura.

Aidha Bw. Kagenzi amewaondoa shaka wananchi wa Tarime kuwa ile dosari ya baadhi ya majina kutokuonekana kwenye orodha ya wapiga kura imeshaondolewa na kuwa sasa majina yote yapo na wananchi wote wenye sifa watapiga kura.

Amesema katika uchaguzi huo mdogo wa Tarime vipo vituo 406 vya kupigia kura ambavyo vimewekewa ulinzi wa kutosha na vitendea kazi vyote ili kufanikisha uchaguzi huo.

Bw. Kagenzi amesema vifaa vyote vinasambazwa leo vituoni na kesho asubuhi kazi zote zitaanza kwa wakati bila tatizo lolote.

Akizungumzia zoezi la kuhesabu kura, Bw. Kagenzi amesema kura zote zitaanza kuhesabiwa vituoni kama ambavyo sheria inasema na kisha kusafirishwa hadi kituo kikuu cha kujumulishia kura.

Akasema kuanzia wakati wa kupiga kura na kuhesabu kura vituoni, lazima wawepo mawakala wa vyama vyote vyenye wagombea na kuwa baada ya hapo mgombea anaweza kuteua wakala wake kusindikiza kura hadi kwenye kituo kikuu cha kujumulishia matokeo.

Akasema hata wakati wa kujumulisha matokeo, mawakala wa kila chama watakuwepo ili kuondoa wasiwasi wa kuibiwa kwa kura na kumridhisha kila mshiriki.

Msimamizi huyo ametoa rai kwa wananchi wa Tarime kuwa watulivu, kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kukubali matokeo baada ya uchaguzi.

SOURCE: Alasiri
 
... matokeo Tarime kutangazwa `live`
2008-10-11 21:04:38
Na Emmanuel Lengwa, Jijini


Wakati uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime ukitarajiwa kufanyika kesho, wapigakura wa wilayani Tarime wanaweza kujua vituo vyao vya kupigia kura kwa kutumia simu zao za mkononi huku matokeo yatakayowasilishwa toka katika kila kituo yakitarajiwa kurushwa moja kwa moja kupitia Kituo cha Luninga cha TBC1.
SOURCE: Alasiri

Kwa nini Matokeo nayo wasipewe kwenye simu ya lika kituo baada ya kumaliza kuhesabu weka kwenye simu. Mwanzo mzuri nadhani wanweza kufanya zaidi, kuweka daftari la wapiga kura online, matokeo online, vituo online, hii si kazi kubwa sana nahisi kwa NEC
 
nmejaribu hiyo namba ni kweli inafanya kazi, tena kwa nchi nzima, huenda baadayehili likasaidia kupunguza wizi wa kura
 
Wakuu mlioko Tarime
inaelekea saa saba, mtuhabarishe jamani maana wanademokrasia tuna kiu kubwa kujua yanayojiri huko.
 
Wagombea wa CCM na Chadema katika uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Tarime unaotarajiwa kufanyika kesho, juzi usiku waliwavunja moyo watazamaji wa Star Tv baada ya kukwepa mdahalo ulioandaliwa kwa ajili yao.

Mdahalo huo ulikuwa uwakutanishe wagombea kutoka vyama hivyo, NCCR-Mageuzi na DP ambao wanachuana kuwania ubunge katika uchaguzi huo unaofanyika kuziba nafasi ya Chacha Wangwe aliyekufa ajalini Julai mwaka huu.

Akitoa utetezi wa kwa nini mgombea wao hakuonekana katika mdahalo huo, Katibu Mwenezi wa CCM John Chiligati alisema waliona mdahalo huo hauna tija na hauwezi kuwaongezea au kuwapunguzia kura
Source habari leo toleo la October 11,2008

wamekacha mdahalo na baadaye wanakuja na sababu za kitoto kama hivi? Lakini pia katika kikao chake na waandishiwa habari mjini Tarime Chiligati, Kapteni wa Jeshi anayejua zaidi kuongoza vita, anasema midahalo inafaa nchi za wenzetu, hapa kwetu wananchi walio wengi hawana upeo wa kuchanganua hoja zinazotolewa kwenye midahalo.
 
Akitoa utetezi wa kwa nini mgombea wao hakuonekana katika mdahalo huo, Katibu Mwenezi wa CCM John Chiligati alisema waliona mdahalo huo hauna tija na hauwezi kuwaongezea au kuwapunguzia kura
Source habari leo toleo la October 11,2008

wamekacha mdahalo na baadaye wanakuja na sababu za kitoto kama hivi? Lakini pia katika kikao chake na waandishiwa habari mjini Tarime Chiligati, Kapteni wa Jeshi anayejua zaidi kuongoza vita, anasema midahalo inafaa nchi za wenzetu, hapa kwetu wananchi walio wengi hawana upeo wa kuchanganua hoja zinazotolewa kwenye midahalo.

Haya ya Chiligati ni zaidi ya matusi ya nguoni! Anamaanisha nini? Watu wa Tarime ni mbumbumbu sana, mdahalo hauwezi kuchangia chochote katika maamuzi yao? Kwa hiyo bwana kepteni Chiligati mnategemea nini katika kupata ushindi: takrima na vitisho? Ama kweli akutukanaye hakuchagulii tusi, lolote linalomjia kinywani anakurushia tu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom