Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Mkuu Belo, hakuna vita Tanzania, bali kuna ushindani, ingependeza kusema kuwa 'ingawa ushindani ni mgumu".

Nambari wani ni CCM.

Keep on dreaming. CCM ni nambari wani kwa kukumbatia mafisadi, kusaini mikataba mibovu isiyo na maslahi kwa Watanzania, kama hutaki kuliona hilo utajiju. Kigumu chama cha mafisadi, kigumu!!!!
 
Naona sasa JF inatumika kama chombo cha propaganda za CHADEMA. Iwapo moderators hawatakuwa macho juu ya hili credibility ya JF kwa jamii itashuka. Kichwa cha habari hii hakiko sahihi na kina ladha ya propaganda za CHADEMA, MODS mko wapi???

JF haitumiki kama chombo cha propaganda za CHADEMA, bali ni chombo cha kuhakikisha Tanzania tuna demokrasi ya kweli na pia tunajenga Tanzania njema isiyo na mafisadi. Kwa hiyo hapa JF kupambana na mafisadi wanaokupua mabilioni ya pesa za walipa kodi , kusaini mikataba mibovu kupindisha sheria na demokrasi ndani ya nchi yetu ndiyo shughuli yetu kubwa hapa. YES WE CAN, just play your part.
 
Kama ni kweli CHADEMA mmeshinda, basi 'hongereni zenu'.
CCM tulishasema kuwa tutakubali matokeo.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Kidumu Chama Tawala

Ndugu yangu Ladslaus,

Hebu pitia thread ya Re: Zakaria ni nani huyu Tarime?. Halafu jiulize kwa nini CCM kiendelee kujiita Chama Cha Mapinduzi na si Chama Cha Mafisadi kama aina ya watu inayowakumbatia mifano yao ndiyo hiyo.

Inahitaji moyo wa kijasiri kweli kweli kujitotokeza hadharani na kukitetea chama hiki kama kweli una uchungu wowote na hatima ya nchi yako. Nakubali ni uhuru wa mtu kujiunga na chama chochote lakini uhuru nao wakati mwingine una madhara yake - ndio maana wengine tumeamua kutanguliza maslahi ya nchi kabla ya chama.

The stark naked truth is that either you are with them or against them. Hii thread naomba ibaki kama ilivyo pamoja na kwamba uchaguzi umekwisha kwa sababu inatufungua macho wengine jinsi hivi vita dhidi ya udhalimu ulivyvo mgumu. Kwa kunyumbulisha yote yaliyoandikwa kabla na baada ya uchaguzi na matokeo tunapata picha ya mwamko wa wananchi kutokana na michango ya makundi matatu;

1. Waliotaka CCM ishinde
2. Waliotaka Chadema ishinde
3. Waliotaka Haki ishinde.

Naamini katika uchaguzi huu iliyoshinda ni haki na hii inaonyesha wana Tarime na Chadema walikuwa upande upi. Haki inaweza ikaminwya, ikabezwa na ikadhulumiwa lakini mwisho wa siku ikainuka na kujitangazia ushindi bila kusubiri matakwa ya vikundi. Mwenye haki ukimdhulumu inabakia swala la muda tu na kamwe haki yake haitapotea daima.

Haki ni nguvu ya umma ambayo hakuna nguvu ama silaha inayoweza kuikandamiza na kuitokomeza asilani. Haki inaweza kupewa dozi ya usingizi na mafashisti lakini ole wao siku hiyo haki ikiamka kutoka usingizini. Naamini hii haki imeanza kunyosha vidole vyake na si muda utaanza kuonyesha makali ya makucha yake.
 
Kwanza mods na mkuu invisible mmeniudhi sana leo hii!

Mbona mmebadilisha heading? Tafadhali rudisha heading "chadema yaibwaga ccm tarime"

au "ccm yaangukia pua tarime"

au "ccm yaona cha mtemakuni mbele ya chadema"



Ukiangalia kwa upande mwingine, moderator wanajaribu kuwa friendly to MAFISADI. Wanasema adui ukae karibu naye utayafahamu zaidi ya undani wake na udhaifu wake.

Siku yaja ambapo hapa patakuwa ni uwanja wa majadiliano kati ya wananchi na wanasiasa waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali za nchi.





.
 
Hongereni sana CHADEMA kwa ushindi mnono mlioibuka nao Tarime. Iwe ni changamoto ya kukiimarisha chama na kuachana na migogoro inayowakwamisha kusonga mbele. Ukombozi si kitu cha siku moja, taratibu tu tutafika!
Tumechoka kuonewa na mafisadi waliojimilikisha nchi yetu na kugawa rasilimali zetu kwa wageni. Viongozi wetu wa chama tawala wamejisahau sana na kuona kama hii nchi ni ya kwao tu. Upinzani madhubuti ndio utajenga na kurudisha uzalendo halisi.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ikomboe nchi yetu kutoka katika mikono ya mafisadi!
 
Kwanza mods na mkuu invisible mmeniudhi sana leo hii!

Mbona mmebadilisha heading? Tafadhali rudisha heading "chadema yaibwaga ccm tarime"

au "ccm yaangukia pua tarime"


au "ccm yaona cha mtemakuni mbele ya chadema"


Acha 'shari' mkuu.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Kidumu Chama Tawala (Kitawale Tanzania hadi mwaka 2100)

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki CCM.
 
Keep on dreaming. CCM ni nambari wani kwa kukumbatia mafisadi, kusaini mikataba mibovu isiyo na maslahi kwa Watanzania, kama hutaki kuliona hilo utajiju. Kigumu chama cha mafisadi, kigumu!!!!

I am not dreaming mkuu!

Nambari wani ni CCM

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Kidumu Chama Tawala
(CCM itawale Tanzania hadi mwaka 2100).

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki CCM
 
I am not dreaming mkuu!

Nambari wani ni CCM

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Kidumu Chama Tawala
(CCM itawale Tanzania hadi mwaka 2100).

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki CCM

Wana ccm wenzako wengi wamekimbia forum kuanzia jana mkuu, Msekwa na wengine walikimbia toka Tarime kabla hata matokeo hayajatangazwa rasmi na msimamizi wa uchaguzi. Anyway, ingawa huu ni ushindi mmoja tu kati ya viti vingi sana bungeni, ni vizuri ijulikane hapa kuwa wana-Tarime wamefanya la muhimu sana kwa demokrasia Tanzania.

Labda watanzania wengi sasa watajifunza hapa na kusema NO pale ambapo mambo yanakuwa yamewafikia shingoni huku ccm na mafisadi kama jambazi hili la Tarime - Zakaria wakiwaonyesha vipesa pesa vya wizi.
 
Mwisho, niseme kwamba uchaguzi huu unaashiria mwisho wa siasa za ujanjaujanja. Siasa za akina Tambwe, Makamba na Akwilombe hazitawasaidia huko tuendako. Huko tuendako kinachotakiwa ni umakini, ukweli na uwezo.

Kwa wakuu wote JF, kwanza heshima mbele sana, na pia kama mwanachama hai na mkereketwa wa CCM, nitoe heshima zangu nzito kwa kuutambua ushindi wa chama chetu cha taifa cha wananchi yaani Chadema, kwa ushindi mkubwa sana huko jimbo la ubunge la Tarime, infact jana nilikuwa sehemu ambapo pia alikuwepo Mama Migiro, ambaye at one point aliniuliza "...vipi huko JF, Tarime tupo wapi?..." nikamjibu kuwa hatujawahi kuwa popote huko zaidi ya chini, I mean:-

1. CCM tumeshindwa Tarime, vibaya sana tena sana na ni aibu tena kubwa sana, ukijumlisha maovu yote yaliyofanywa huko na baadhi ya viongozi wa CCM ambao nusu yao nimeongea nao leo, kwa kweli ni aibu kubwa sana, and I hope kwamba huu uchaguzi sio min-refferendum ya 2010, maana nina wasi wasi sana kwamba it is a refferendum tena kwa 100% ya uchaguzi wa 2010.

2. Huu ushindi ni ujumbe tosha kwetu CCM, kwamba get rid of rogue leaders kama Makamba, na Msekwa get them out tena now, maana hawa ni kundi la mafisadi, I mean wachawi wako within us kwa sababu hawana uwezo wa kuongoza taifa kwenye level ya chama kinachotawala, sasa nashangaa Rais Kikwete akiwachekea hawa fukuza now!

3. Mwenyekiti Rais Kikwete, sasa baada ya huu ujumbe kusiwe na kuchekeana tena, otherwise tunakwenda down tena kwa kasi kali sana kwa sababu this is a true picture ya what to come mbele ya safari, Republicans waliposhindwa viti vichache tu ndani ya Congress pamoja na kwamba walikua bado ni majority, walimtoa mbio Spika Gingrich, sasa CCM tuache kuechekeana kwa sababu hakuna excuse hapo, CCM nzima ilikuwepo huko Tarime, sasa iliyoshindwa hapa ni CCM sio anybody else!

4. CCM tunapaswa kuwaomba radhi wananchi wa Tarime, kwa sababu nina uhakika kwa 100% kwamba niliyoyasikia kutoka huko yaani maovu yetu ni kweli yamefanyika, lakini simply politics ni kwamba wananchi wamekataa ujinga na uongo period!

5. CCM this time tuna viongozi wabovu sana, tena sana wakumbatiaji wa rushwa na mafisadi, wasiokuwa na uwezo wa kuongoza, wasiokuwa na uwezo wa kuona mbali, I mean Mheshimiwa rais wakati mwingine sijui unapewa ushauri na nani kwamba Msekwa, aliyekuwa spika kwa karibu miaka 15 kiongozi wa chama na serikali kwa miaka karibu 40, halafu siku moja anapigwa chini kisiasa na kukosa kila kitu na kuwa jobless, leo unamuona huyu anafaa kua makamu wako wa kuongoza chama tawala taifa?

- Eti ni mwanasiasa gani wa kweli asiyeweza ku-navigate political fate yake mwenyewe? Sasaa leo unampaje ku-navigate CCM taifa kama sio kufilisika kwa hao washauri wako wa siasa?

- Waziri ameacha jiji halina umeme, anakimbilia kupiga kampeni za uchaguzi hivi hawa wananchi wa Tarime, wanatakiwa kuwa wajinga kiasi gani jamani?

- Tizama akili ya siasa ya Mkamba, hivi kweli unaweza kumtumia Mtikila kushinda uchaguzi wa jimbo la wananchi wenye akili timamu kama Tarime?

6. Hawa ni viongozi gani wa chama ambao hawana hata heshima ndani ya chama chao kutoka kwa viongozi wengine wenzao kwa sababu ninaambiwa kuwa ilifika mahali wakagundua kua hawana uwezo wa kuongoza CCM kushinda huko Tarime, wakaanza kujaribu kuwashawishi baadhi ya viongozi wengine kwenda huko Tarime, lakini hata kusaini hizo barua za kuwaomba wameshindwa badala yake wakajaribu kusingizia kuwa zimeandikwa na kikao cha sekretarieti chini ya mwenyekiti wa CCM, ambaye kila mwananchi anajua kuwa hakuwepo wakati zikiandikwa licha ya hao viongozi waliotumiwa, what kind of leadership is this kama sio a joke?

I mean CCM tumeshindwa this one na it hurts badly, kwa sababu hakuna reasonable excuse hapa, zaidi ya kukosa dira na muelekeo kisiasa na kiuongozi, sasa ni wakati wa viongozi wasiokuwa na uwezo kuwajibika au wawajibishwe, ninasema hivi kwa wanachama wote wa CCM, tusijidanganye hapa kua eti hili ni jimbo moja tu, hapana haba na haba hujaza kibaba period! Huu ni mwanzo tu kama CCM hatujiangalii kwenye kioo, hata 2010 itakuwa aibu kubwa zaidi ya hii,

Na tusidanganyane hapa hii aibu inakwenda straight kwako mwenyekiti, rais wa jamhuri kabla ya mtu yoyote mwingine, ni kwamba tuna viongozi wabovu wasiokuwa na uwezo kabisaa, sasa waondolewe kabla ya aibu zaidi,

Halafu as a nation imefika wakati wa kuliangalia tena suala la ruzuku in general, mimi ninafikiri umefika wakati wa ku- do away na ruzuku kwa sababu zinasaidia one thing only, nacho ni ku-off balance ushindani wa kweli wa kisiasa kwa taifa letu, na kudhoofisha kabisa upinzani wa kweli wa kisiasa nchini iondolewe au itafutwe njia nyingine ya kuleta balance haiwezekani chama kimoja kipate shillingi millioni 99, na vingine millioni 10, mpaka 30 halafu ukategemea kuwepo na ushindani ambao ni balanced na politically heathy kwa taifa.

Kwa kumaliza ninapenda kutoa heshima zangu kwa Chadema, kwa huu ushindi mzito sana, kutoka jimbo la mkoa aliozaliwa Baba wa Taifa letu, mhasisi wa CCM, hiyo ni aibu kubwa sana kwa viongozi wetu wote wa CCM, mlioshirki huko Tarime, shame on you, yaani kwa mara ya kwanza kuona uchaguzi mdogo ambao mmeshindwa hata kumshawishi mwenyekiti wa CCM kushirki, sasa kama mwenyekiti mwenyewe amewashitukia itakuwaje wananchi wa huko? Kwa nini mwenyekiti hakuenda huko? Maana yake ni moja tu kua hawaamini hawa wasaidizi wake, sasa mheshimiwa rais unangoja nini kuwaondoa mara moja?

Again heshima kwa Chadema kwa ushindi wenu mzito, ambao kwa jinsi nilivyoambiwa na waliokuwepo kwa maneno ya kizungu, ilikuwa ni no contest na mimi ninaamini kwa 100% kuwa ni kweli!

Mungu Aibariki Tanzania.
 
Maneno mazito sana hayo FMES, asante sana nadhani ujumbe utafika kwa mwenyekiti ....
 
maneno mzito sana mkuu fmes..lakini i beg to differ kuhusu ushiriki wa mwenyekiti wa chama.....mwenyekiti wa chama hangoji mwaliko ...kama amiri namba moja wa chama akisikia mbiu anaenda..ukizingatia safari ndefu alizokuwa nazo nje ..bado asingeshindwa kuchelewa mbeya kwa siku moja zaidi ili angalau afanye mkutano mmoja pale tarime...[mbona muda wa kwenda serengeti huwa anapata tena bila ratiba??]...tukubaliane kwa hili la kutohudhuria mwenyekiti pia anayo sehemu ya lawama....

Mwenyekiti alipewa taarifa ya mwenendo mmbovu wa kampeni ,mara tu aliporudi toka marekani ..amabapo makongoro nyerere alimfuata ikulu the first thing ..na kama tunavyomjua mako si mtu wa kutafuna maneno atakuwa alimpa inside story...lakini i believe sababu kuu iliyomzuwia jk kwenda tarime ni intelligence report....inawezekana ut hawakuona kama jk kwenda tarime wakati huu ilikuwa in the interest of the nation au his character.....

Pia awali nilihoji kitendo cha ccm - zanzibar kushindwa kuonesha mshikamano uchaguzi huu kwa kushindwa kutuma hata top brass mmoja.....

Uchaguzi wa tarime umekuwa kama wa temeke 1998......maximum force has been deployed without any ultimum results....the will of the people has prevailed...basi!!!

Udhaifu mwingine nakuunga mkono ni wa kutumia hoja mufilisi..kifo cha wangwe,wajane wake,kuwapandisha kaka zake jukwaani ets..hizo kamwe haziwezi kuleta ushindi popote...ccm imepoteza mwelekeo tangu ilipoanza kuwatumia wana propaganda wa kuokota ...wakati magwiji wa propaganda kama [remind me yule mzee wa mazumzo baada ya habari]....wanakufa njaa....kikwete binafsi ni kada na anajuwa propaganda....zilizokuwa zikifundishwa pale kivukoni,urusi,bulgaria ..ets...
 
Wakurya siku zote hawana masihara. Once they decide hata ukiwagecha still they will stick. Ni majasiri sana watu hawa. Hawaogopi bwana. They are warriors of Change. ni wang'amuzi wa machafu na rafu za walio madarakani. Jamani CCM CHANGA LA MACHO. KAZI KIMBELEMBELE TU KUFUNGUA MATAWI UGHAIBUNI NO SENSE!! Well done CHADEMA. Hope majimbo mengine yatajifunza kutoka Tarime. MURA! TATA BHAISAKORO TAHNK YOU.
 
Nakubaliana na FMES kwa kiwango fulani ila nataka kuongezea tu kwa kusema kuwa ni afadhali kuwasha kamshumaa kadogo tu kuliko kulaani giza. Giza halifukuzwi na giza bali mwanga. Hili zimwi CCM ni giza lililotanda nchini kiasi cha wananchi kubaki wanapapasa hawajui waelekee wapi. Viongozi on the other hand wamevaa miwani inayowawezesha kuona gizani na hivyo kufanya vitendo vyao vichafu bila bugudha. Hawana tena haja ya kujificha na hasa pale wanapokuwa na vibaraka, kama tunavyoshuhudia, vinavyowafuta kwa kunusa harufu ya mapochopocho vinayotupiwa.

Uonevu popote pale ni adui namba wani wa haki na pale upeo wa binadamu unapofunikwa na giza, maamuzi yasiyo busara hujikita. Ujinga hutawala mpaka atakapotokea mtu na kuwasha taa kama walivyowasha wana Tarime. Inapofikia hatua hii dawa ni moja tu, kung'oa mzizi wa fitina kwa kuitosa mfadhili wa giza, CCM. CCM haijijui kwa sababu haijimuliki na ni kama mwenye mbwa anayepima kukubalika kwake katika kijamii kwa kuangalia mbwa wake anavyomtii na kumfuata bila maswali.

Nachukua nafasi hii kuwaomba wote, tutafakari hatma ya nchi yetu na tujiulize kama kweli bado tuna imani kuwa CCM inatupeleka tunakotaka kwenda. Kama jibu ni ndiyo basi tukae tusubiri labda tutafika lakini kama jibu ni hapana tuonyeshe azma yetu kwa vitendo kwa kufuata nyayo za wana Tarime - Tuikatae CCM, tukatae kutumiwa, tukatae kudhulumiwa na tuwashe mshumaa kila kona ya nchi hili giza nene litokomee.
 
Mkuu PM,

Habari nilizonazo za ndani ni kwamba mkulu alipoambiwa kwamba wabunge wote wasiokumbatia ufisadi wamegoma kwenda Tarime, akaamua kuwa hataki anything to do na huko, lakini ninakubali hoja yako kama ulivyosema kua hakutakiwa kusubiri kuitwa, alitakiwa kuwa wa kwanza kufika huko

Tena nyeti zaidi nasikia Makamba na wenzake walivizia jana usiku wa saba, ndio wakaondoka kimya kimya huko Tarime, kurudi Dar. Halafu nasikia nyeti zaidi ni kwamba hawa viongoziw a mafisadi wanashukuru sana majimbo mawili yaliyobaki Biharamulo na Mwibara, hayatagombewa mapaka next uchaguzi kwa sababu CCM walipitisha mswaada unaokataza uchaguzi wa majimbo madogo in two years kabla ya uchaguzi mkuu, sasa vipi kina Zitto wakishinikizwa kuuulilia huo mswaada ubatilishwe ili na hayo majimbo yafanyiwe uchaguzi sasa? Tujue ukweli ulipo au?
 


...

Halafu as a nation imefika wakati wa kuliangalia tena suala la ruzuku in general, mimi ninafikiri umefika wakati wa ku- do away na ruzuku kwa sababu zinasaidia one thing only, nacho ni ku-off balance ushindani wa kweli wa kisiasa kwa taifa letu, na kudhoofisha kabisa upinzani wa kweli wa kisiasa nchini iondolewe au itafutwe njia nyingine ya kuleta balance haiwezekani chama kimoja kipate shillingi millioni 99, na vingine millioni 10, mpaka 30 halafu ukategemea kuwepo na ushindani ambao ni balanced na politically heathy kwa taifa.

......

Mkuu Field Marshall ES,

Katika hili la ruzuku nakubaliana nawe asilimia mia moja. Natumaini wanasiasa wa vyama vyote watakubaliana nawe katika hili.
 
maneno mzito sana mkuu fmes..lakini i beg to differ kuhusu ushiriki wa mwenyekiti wa chama.....mwenyekiti wa chama hangoji mwaliko ...kama amiri namba moja wa chama akisikia mbiu anaenda..ukizingatia safari ndefu alizokuwa nazo nje ..bado asingeshindwa kuchelewa mbeya kwa siku moja zaidi ili angalau afanye mkutano mmoja pale tarime...[mbona muda wa kwenda serengeti huwa anapata tena bila ratiba??]...
PM
Huyu anakwenda Serengeti kwenye mapumziko katika ile hoteli ileeee!
(ambayo wewe na mimi hatuwezi kuingia)
 
Wana ccm wenzako wengi wamekimbia forum kuanzia jana mkuu, Msekwa na wengine walikimbia toka Tarime kabla hata matokeo hayajatangazwa rasmi na msimamizi wa uchaguzi. Anyway, ingawa huu ni ushindi mmoja tu kati ya viti vingi sana bungeni, ni vizuri ijulikane hapa kuwa wana-Tarime wamefanya la muhimu sana kwa demokrasia Tanzania.

Labda watanzania wengi sasa watajifunza hapa na kusema NO pale ambapo mambo yanakuwa yamewafikia shingoni huku ccm na mafisadi kama jambazi hili la Tarime - Zakaria wakiwaonyesha vipesa pesa vya wizi.

Hata kuaga wenyeji wao hawakuwaaga. Kushindwa kubaya hasa ukitilia maanani walitumia mapesa chungu nzima, FFU, Polisi, vipigo na vitisho, helikopta mbili, wakamnunua na Mwendawzimu Mtikila ili awachafue viongozi wa juu wa CHADEMA. Sijui watamlaumu nani kwa kipigo walichokipata Tarime.
 
......Chimbugila marashi ya maramara.....pop corn zangu huyooo nasubiri winter nianze kuteleza tu kuzitafuta pavements.ccm bwana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom