Uchafuzi wa Sensa 2022

Hali ipo hivihivi kila mahali jamaa, tusikate tamaa Luna maisha baada ya vishikwambi.
 
Wewe umewahi ona wapi msaili naye ni muhitaji wa hiyo nafasi uliyoomba pia huyo msaili ana ndugu jamaa au marafiki hawezi kukuweka ww chilinyinda aache kumuweka mwanae au ndugu yake .kuwapa mandate viongozi wa kata kuwa ndo waaproove waombaji ni kosa ambalo athari yake tumeiona waziwazi kwenye sensa hii.Kilichokuwa kinatakiwa wasaili ilitakiwa watoke mbali ili kuepusha mgongano wa kimaslahi
 
Hata wa mbali nao wana changamoto.
Watakuta majina yapo mezani na kibunda.
Wooote ni yale yale
 
Mimi ndio maana sikujisumbua kabisaaa. Mungu wangu alinijaalia kuyafahamu yajayo mapema na kwa taarifa yenu hata hizo pesa baada ya zoezi la sensa kuna watu watadhulumiwa.
Ogopa sana kazi ambazo zinahusisha watendaji hawa wa vijiji,wala usihangaike..ni kujuana tu..wengine wameingiza mpaka wake na michepuko yao.
 
Hii Nchi ngumu Kweli kweli, mtoto wa diwani anapoteza haki zake za msimgi kisa TU ni mtoto wa diwani?

Je huyo mwanaye Diwani amechukua nafasi zawatu wangapi?
Na walio itwa kwenye usahili niwangapi?

Mawazo kama haya yanapo shabikiwa na jamii kubwa, yanaiweka mashakani, freedom of speech.

Kwasababu yasaidie kujenga Bali yanaeza chuki.
 
Mkiambiwa andamana kushikiza katiba mpya mnaanza kusema atangulie Mbowe na familia yake wenye mabilion ndani!!. Haya pambaneni wenyewe...
Hiyo katiba itaweka namna yakuptikana makalani wa sensa?
 
Sa itakuaje 😀 tutapiga kelele wakubwa washaziba masikio huko, M wakija kwangu kuhesabu hawanikuti kabsa 😀
 
wakuu sio kwa ubaya ila wekeza nguvu ZAKO kwenye mishe mishe zako apa unajichora tu

you can't stop what you can't see
 
Hivi naomba kuuliza hivi hawa makarani wa sensa watalipwa shilingi ngapi? make naona vilioni vimekuwa vingi sana. hATA kama itakuwa milioni moja na baada ya hapo ukarudi mtaani kuhustle bado haina msaada kivile
 
Kipaumbele n walimu, jamaa na ndugu. Polen mliokosa na hongereni mliopata.

Hii nchi ngumu sana wenye ajira ndio wanapata ajira mpya. Inatia uchungu sana, Vijana wamemamiza chuo wapo mtaani, wanashindana kuomba ajira za muda na walioajiriwa. Waajiriwa/ walimu wanawasaili walimu wenzao. Unategemea nini?
Ushauri wangu kwa mlioumizwa na hili zoezi la sensa, msikate tamaa maisha yaendelee kwani hali halisi mmeshaiona. Nanyi mkipata nafasi za uongozi huko juu msiendeleze undugu na rushwa mtaumiza kama ninyi mnavyoumia Leo.

Nawasilisha
 
Mimi ndio maana sikujisumbua kabisaaa. Mungu wangu alinijaalia kuyafahamu yajayo mapema na kwa taarifa yenu hata hizo pesa baada ya zoezi la sensa kuna watu watadhulumiwa.
Hivi wanalipwa sh ngapi? Maana nami Mungu mwema ,sijawahi jishughulisha, na Mambo haya ya kuumiza vichwa,
 
Pole sana chuo ulimaliza lini??
 
Sensa ya mwaka huu itakua na kasoro lukuki....Hawa watu walioomba wangepewa nafasi kuliko hii michezo.
Hapana. Tuliopata tuna sifa na vigezo kama ninyi Ila sisi tunawazidi kigezo cha connection.

Watu wameomba 30,000 wenye sifa wako 20,000 nafasi zipo 2,000. Unadhani hapo unawapataje wateule? Lazima itumike connection. Siku nyingine mjipange
 

Hivi, naomba kuuliza! Hii kazi ya sensa ambayo mnalialia na usaili kuwa ni wa rushwa ni ajira ya kudumu au ya wki mbili au tatu tu! Mbona mnajifedhehesha sana? Kwani mliyegemea kila atakayetokea kwenye usaili atachaguliwa? Njoo hapa nikupe shamba na jembe na shoka ufanye kazi ya kudumu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…