Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Hivi waliopiga kura online toka igunga kwenye hiyo poll ni wangapi?

Ni vigumu kuwafahamu, ila kama ingekuwa ni nchi za wenzetu ambazo hakuna uchakachuaji ungekuta wanaigunga wangebadilika na kuona waTZ wote wanahitaji kitu gani. Issue ya msingi hapa ni hata wanaCCM hawawapi kura wagombea wao kwani wamechoka na hii hali, Swala la umeme kutikuwepo na bei ya mafuta kupandishwa kwa maslahi ya wafanya biashara linatosha kabisa kwa waTZ kutowapa kura hawa jamaa.
 
Nafikiri haya yanaweza kweli kuwa matokea ya Igunga kwasababu zifuatazo;
Kati ya majimbo magumu kwa Chadema basi hili ni mojawapo, kwanini:
1. Chadema, Mbowe, Slaa na wengine wameshindwa kufunguka na kumuattack Rostam moja kwa moja wakijua wazi kuwa huyu jamaa alikuwa anakubalika sana huko, kumuattack kungepoteza mvuto.
2. CDM wameshindwa kuongelea ufisadi kwa upana wa Nchi ambao ndio sera kuu, hii inatokana na hofu hiyohiyo kwani RA ameokena ndo kubwa la majambazi kwahiyo wamejikita kuiattach halmashauri ya Igunga na kukiri kuwa serikali imepeleka pesa nyingi Igunga lakini hakuna kilichofanyika, another weakness.
3. Vita ya ndani ya CCM imepotezewa, wamechukua watu neutral ili kuwapumbaza wana Igunga, wote waliokuwa wanampiga madongo RA wamewekwa kando.
4. Wananchi wa Igunga kubali usikubali watapiga kura in favour of RA,
5. RA yuko mtegoni, akiwapiga chini magamba wenzake wanaweza kumgeuzia kibao kwenye dili zake, akiwafagilia CDM watamuumbua baadae kwahiyo anatakiwa kusuka au kunyoa lkn kwa politics za TZ ni bora aende sawa na magamba yasije kumdhuru baadae kwasababu bado wameshikilia dola.
6. CDM wangeungana na vyama vingine labda wangekuwa kwenye sehemu nzuri ya kuichallenge CCM lkn kwa hali ya sasa ni ngumu.
7. Najua CDM kinawezaz kuwa chama makini na kuyatambua haya hivyo uwezekano wa kubadilisha matokeo ukawepo kama tu karata zao watazichanga vizuri.
Ingekuwa jimbo jingine huu ungekuwa ushindi wa wazi kwa CDM lkn kwakuwa huyu mstaafu alikuwa kisiki, jimboni ndani ya CCM na hata serikalini japo hakuwa kiongozi tusubiri tuone matokeo.
 
Wakuu,

Wengi tumeshangaa Rais mtaafu kupanda tena jukwaani, kwa kawaida tulikuwa tumezoea kuliona Tingatinga la CCM (Samweli Malecela) kuwa front na kukata kata magogo, mizizi, miamba na miti ili kuchonga barabara.

Cha ajabu namwona Mkapa naye anapiga front Igunga, ndiyo najiuliza VIPI HILI NDIYO TINGATINGA JIPYA LA CCM ? kama kweli hili limetengenezwa toka China, Japan au Ujerumani? Je litahimili misukosuko ya miamba ardhini na kusonga mbele?

Binafsi watu tunamuheshimu sana huyu Rais wetu katufanyia mengi sasa kupanda jukwaani ni ishara kuwa sasa anataka mashambulizi yote ya kiasiasa yaanze kuelekezwa kwake? Je bado anaweza purukushani za kisiasa za majukwaani? Je atavumilia makombora toka kwa vijana wa CHADEMA? hatakasirika?

Tunamkaribisha sana igunga ila asije akatuambia sisi vijana tunamkosea adabu maana kaingia mwenyewe ulingoni kwa mara nyingine tena.

MY TAKE: CCM acheni wazee wapumike, kulikuwa hakuna haja yoyote ya kumsumbua mzee wa watu, kashawatumikia wananchi miaka 10 akiwa rais na mingine mingi tu. Huu ni muda wake wa kupumzika. Kama Mmewakosea wananchi na mna uhakika hawatawapeni kura angalieni mlipojikwaa lakini si kuwasumbua wazee wetu. Mtamponza mzee wa watu.
 
Hii bado haitoi taswira ya ushindi kwa CDM, kazi bado tunayo ingawa tuna nafasi kubwa sana ya ushindi. Tukifanya hivyo, basi hata gazeti la RAI litakua sahihi.


Kwa mujibu wa RAI hayo ndiyo matokeo.

Chama kipi kitashinda Igunga


  • CUF (46%, 81 Votes)
  • Chadema (43%, 75 Votes)
  • CCM (10%, 17 Votes)
  • SAU (1%, 1 Votes)
  • UDP (0%, 1 Votes)
Total Voters: 175
 
Rais aliyeuza utu wa watanzania kwa kudalali mali zote kwa kuanzisha kampuni ya uuzaji yenye jina Wizara ya Ubinafsishaji.
 
Kwahiyo MBOWE NA SLAA ni matingatinga ya CHADEMA????/
Rais Mstaafu ana hadhi yake na ndiyo maana watanzania tunamuheshimu sana, Najiuliza Ufisadi wote huo alikuwa wapi kuukemea- leo hii ndiyo kapata nguvu ya kupanda jukwaani kwenye kampeni? CCM have failed to address even the basic needs of most Tanzanians, sasa mnahaha huko na huko kusumbua hadi wazee ambao walishastafu siasa wawasaidie kampeni tena kwa ngazi ya JIMBO. Tunamheshimu sana huyu Rais mstaafu ila awe tayari kurushiwa makombora na vijana wadogo na asinune.
 
Kweli Mkapa Raisi wetu alitakiwa apumzike tu jamani. Namkumbuka kwa sera zake nzuri za uchumi. Alichukua nchi mfumuko wa bei ukiwa asilimia nne na aliondoka madarakani ukiwa asilimia nne.
 
Rais Mstaafu ana hadhi yake na ndiyo maana watanzania tunamuheshimu sana, Najuluza Ufisadi wote huo alikuwa wapi kuukemea- leo hii ndiyo kapata nguvu ya kupanda jukwaani kwenye kampeni? CCM have failed to address the basic needs of most Tanzanians, sasa mnahaha huko na huko kusumbua hadi wazee ambao walishastafu siasa wawasaidie kampeni. tunamheshimu sana huyu Rais mstaafu ila awe tayri kurushiwa madongo na vijana wadogo na asikasirike.

na sisi tunamheshimu Dr Slaa , uzee wake wote hakupaswa kwenda igunga
au ndo inatuziilishia kuwa chadema bado wachanga?
 
Kwahiyo MBOWE NA SLAA ni matingatinga ya CHADEMA????/


Viongozi wa chadema wanatafuta kushika dola ya hii nchi Mkapa anatafuta nini sasa hivi?

Mkapa naona anafanya hivyo kwa sababu anajua madhambi aliyoyafanya ndiyo maana hawezi kumbishia JK akimwambia wasadiane kujibu mapigo. Kimsingi Mkapa angekuwa msafi kamwe asingehangaika anavyofanya leo. Anajua kama Chadema wakichukua hii nchi hayuko salama kwa ufisadi wake alioufanya.

Anaongea mbele ya umma kwa kujiamini akijua kuwa wanannchi wa kawaida hasa vijijini hawajui ufisadi wake. Amesahau kuwa habari huwaingia watu taratibu na Chadema wanaendelea kupenyeza habariza zake taratibu. Mambo yatakapokuwa hadharani kamwe hatadhubutu kuongea na hii Jeuri anayaoinyesha leo.

Ngoja tusubiri tuone kama ataweza kuhimili mashambulizi!
 
Kawatumikia wananchi wap kwa uadilifu?, kwa kujiuzia Kiwira kwa bei ya kutupwa? Wizi mkubwa umefanyika zama zake huu ndio uadilifu. Hizi ni sifa za marehemu
 
Kweli Mkapa Raisi wetu alitakiwa apumzike tu jamani. Namkumbuka kwa sera zake nzuri za uchumi. Alichukua nchi mfumuko wa bei ukiwa asilimia nne na aliondoka madarakani ukiwa asilimia nne.

mmeona makombora yamekuwa mazito ndo mnaanza huruma...... hahahaha funga mdomo ...... kimbunga kinakuja ....ukombozi uko igunga
 
Viongozi wa chadema wanatafuta kushika dola ya hii nchi Mkapa anatafuta nini sasa hivi?

Mkapa naona anafanya hivyo kwa sababu anajua madhambi aliyoyafanya ndiyo maana hawezi kumbishia JK akimwambia wasadiane kujibu mapigo. Kimsingi Mkapa angekuwa msafi kamwe asingehangaika anavyofanya leo. Anajua kama Chadema wakichukua hii nchi hayuko salama kwa ufisadi wake alioufanya.

Anaongea mbele ya umma kwa kujiamini akijua kuwa wanannchi wa kawaida hasa vijijini hawajui ufisadi wake. Amesahau kuwa habari huwaingia watu taratibu na Chadema wanaendelea kupenyeza habariza zake taratibu. Mambo yatakapokuwa hadharani kamwe hatadhubutu kuongea na hii Jeuri anayaoinyesha leo.

Ngoja tusubiri tuone kama ataweza kuhimili mashambulizi!

kwani mkapa chama gani???
 
Jamaa wamefulia sana, huyo Chinga haoni aibu pamoja na kashfa zote alizonazo bado tu anajitokeza mbele ya watu, mi nadhani kuonekana kwenye KK yao ambayo karibia wote ni wachafu sio mbaya lkn mbele ya macho ya watz sio sahihi. Aone AIBU duuuh!
 
Hii haina masirahi kwa taifa

jenga Taifa kwanza majungu baadaye

Tutamkumbusha "NET GROUP SOLUTION", "Mgodi wa Kiwira" alojiuzia na Yona, wakakopa pesa benki ambazo hawakuzitolea maelezo wala kuzifanyia kazi ya maana zaidi ya kuzihamishia kwenye account zao binafsi.
 
[/LIST]SAU na UDP wamepata kura mojamoja.
Iyo pasenti imekaaje? Hata hesabu kama hizi lazima kupika?

hapo hata utumie kanuni gani jibu hupati kama hilo, labda u''assume
 
Ameshasahau aliyoyafanya na ana wake sasa anafikiria na sisi watz tumesahau, kwani ben ulisahau nini kwenye majukwaa ya siasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom