Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Mtu unalinganisha apple na chungwa? Sasa masuala ya uchaguzi Igunga na uchumi wa Marekani yanahusiana nini? Hueleweki kabisa mkuu.
mkuu sijazungumzia kabisa kuhusu uchumi wa Marekani kama sehemu ya mada yangu. ukichunguza nilichokizungumzia ni tofauti ya misingi ya mijadala kati yetu na Marekani. wao wanazungumzia masuala muhimu ya jamii yao na sisi kazi yetu ni kuonyesha chama kipi ni kizuri au kibaya kuliko kingine kama vile chama kinaweza kuwa na watu wazuri tu au watu wabaya tu.

Sarah pallin na wenzake hawasemi Democtras wooote ni wabaya bali wanasema Obama kashindwa kuitoa Marekani kwenye anguko la uchumi kwa sera zake za kishoshalist. Nilitarajia kuona kampeni zilizojaa uchambuzi yakinifu badala yake kila chama kinajitahidi kupuliza "vuvuzela" lake la propaganda kama vile Igunga imezaliwa jana.

CCM imekuwa ikitawala Igunga kwa miaka yote tangu 1992, Imefanya kitu gani wanachojivunia ili wapewe tena ubunge wa jimbo la Igunga baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kutoka chama hicho hicho kujiuzulu. Hizi gharama tunazoingia watanzania kwa kufanya chaguzi mbili chini ya mwaka mmoja hazijasababishwa na CCM?

CDM,CUF na vyama vingine vimewekeza kiasi gani kwenye jimbo la Igunga hadi tuamini navyo pia havina tofauti na CCM? Wakati wote msimamo wangu ni kwamba siasa za kishabiki haziwezi kutufikisha popote. Take my word, leo hii Lowassa au Mwakyembe wakiamua kujiunga na CDM amini usiamini wtapokelewa kama mashujaa walioachana na Mafisadi. Kwani ilikuwaje kwa Mpendazoe na Shibuda?
 
................Taarifa za kutoka chini ya kapeti zinadai kuwa Ben kajilaumu kwanini ameenda huko...

Asijilaumu , mbona aliambiwa mapema anaenda kule kuvuna aibu akajifanya kichwa ngumu
 
Hizo ni baadhi ya picha ambazo zimepatikana leo katika uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM jimboni Igunga.
2.JPG

Rais Mstaafu Ndg Benjamini Mkapa akimnadi mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM Ndg Dr. Kafum.

3.jpg

Sehemu ya umati uliohudhuria mkutano huo.

5.JPG

Kama kawaida wasanii wa Original Komedi walikuwepo kusherekesha uinduzi huo.

9.jpg

Baadhi ya vijana wakirudisha kadi za CDM baada ya Mkapa kumwaga sumu.

11.jpg

Katibu mkuu Ndg Willson Mkama anaonekana akisisitza jambo katika uzinduzi huo. Awali ilidhaniwa asingehudhuria.

IMG_0310.JPG

Hapo awali ilidhaniwa Rostam asingehudhuria uzinduzi wa kampeni za kumtafuta mrithi wake, swali sijui siasa uchwara zilizomuondoa amezisamehe.

IMG_0312.JPG

Rostam na Mkama wakionekana wakifuatilia kwa umakini uzinduzi huo, siasa kazi kweli kweli.

IMG_0316.JPG

Bango hili mmmm utalisemea mwenyewe.

View attachment 36997

Haikueleweka mara moja kama na hii picha ilikuwa ni sehemu ya maandalizi ya uzinduzi wa kampeni za chama cha Mapinduzi (CCM) zilizozinduliwa rasmi jana.
 
kwa hili la Rostam Aziz kuzindua kampeni na Mkapa limethibitisha kuwa kweli ccm wanapenda siasa uchwara....wamevua gamba la RA na sasa wanalivaa wakati la chenge na wenzio magamba yao yamebana kiunoni. mchezo huu wa kuvua na kuvaa gamba una maanisha nini kwa ccm? au ndo namna ya kufikiri kwa kutumia masaburi?
 
Hizo ni baadhi ya picha ambazo zimepatikana leo katika uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM jimboni Igunga.
View attachment 36963

Rais Mstaafu Ndg Benjamini Mkapa akimnadi mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM Ndg Dr. Kafum.

View attachment 36965

Sehemu ya umati uliohudhuria mkutano huo.

View attachment 36966

Kama kawaida wasanii wa Original Komedi walikuwepo kusherekesha uinduzi huo.

View attachment 36967

Baadhi ya vijana wakirudisha kadi za CDM baada ya Mkapa kumwaga sumu.

View attachment 36968

Katibu mkuu Ndg Willson Mkama anaonekana akisisitza jambo katika uzinduzi huo. Awali ilidhaniwa asingehudhuria.

View attachment 36969

Hapo awali ilidhaniwa Rostam asingehudhuria uzinduzi wa kampeni za kumtafuta mrithi wake, swali sijui siasa uchwara zilizomuondoa amezisamehe.

View attachment 36970

Rostam na Mkama wakionekana wakifuatilia kwa umakini uzinduzi huo, siasa kazi kweli kweli.

View attachment 36971

Bango hili mmmm utalisemea mwenyewe.
Hapo kwenye meza kuu wazee wanaonyesha sura za watu waliokata tamaa.
 
@It is very contradiction for Nape & Rostam kuwepo pamoja Igunga kwenye kampeni za CCM, Kifupi kunawachanganya wanaCCM & wananchi wakawaida (undecided voters). Katika hili kunawapa nguvu & nafasi kubwa sana CHADEMA kushinda uchaguzi huu. @Sote tunajua sababu zilizopelekea kurudiwa uchaguzi Igunga, ni kujiuzuru kwa Rostam Aziz kwa madai ameamua kuachana na siasa uchwara za CCM (Siasa za kuvuana magamba zinazopigiwa debe na Nape). Viongozi wa juu wa CCM (wakiongozwa na Nape & Kamati kuu) walijitamba kuwa huo ulikuwa ni mwanzo wa mwitikio wa siasa za uvuaji magamba, na kuonya kuwa wale waliobakia (EL&EC) wafuate nyayo za Rostam kwa kuachia ngazi mara moja!! Sasa leo vipi tena Rostam anakuwa mpiga debe wa CCM Igunga. Ndio kusema siasa uchwara zimekwisha au siasa za kuvuana magamba ulikuwa ni usanii wa Ze comedy? @Ama kweli CCM haitabiriki na wala haiminiki, katika hali hii, nitashangaa sana kama kuna mwanaCCM atakwenda kukipigia kura chama chake, Labda kama anamatatizo ya akili. Lets wait&watch the cinema...
 
Ni unafiki na uthibitisho kuwa ccm inamtumia rostam kama ambavyo yeye anaitumia ccm kufisadi rasilimali za taifa.Katika hali ya kawaida kwa mtu aliyedai kuwa hataki kuwa sehemu ya 'gutter politics' na leo anakuwa sehemu yake haiingii akilini.Lazima uwe ni mtu usiyejiamini na mwenye hofu kuweza kufanya kitendo alichokifanya rostam.Swali la kujiuliza ni kwa nini hajiamini kama kweli kujiuzuru kwake hakutokani na 'kujivua gamba'kama alivotaka tuamini?CCM kama chama ambacho kinapiga kampeni kupata jimbo la mbunge wa chama chake aliyejiuzuru kwa shinikizo la chama kwa dhana ya kwamba matendo yake yamekipotezea chama mvuto!Kwa nini mtu yuleyule aje kupiga kampeni ya kusaidia chama ambacho anadaiwa kukipunguzia mvuto?Kujumuika kwake na viongozi wa kitaifa wa chama hakupunguzi tena mvuto kwa chama?Uelewa wa wananchi wengi bado ni kikwazo cha kufikia Tanzania tunayoitaka.Fikiria mwananchi ambaye anahudhuria kampeni ya ccm igunga na kushabikia kwa mbwembwe ccm huku akiwa na ama kofia na/au fulana za njano na kijani.Hivi anakumbuka hata kwa nini uchaguzi unafanyika Igunga na si sehemu nyingine kwa sasa?
 
Sad to say, but idadi ya mbumbumbu Tanzania haitopungua...!!! <img src="/images/styles/JamiiForums/smilies/sad.gif" border="0" alt="" title="Sad" smilieid="270" class="inlineimg" />
<br />
<br />
Mkuu mbona hii comment yako haiendani kabisa na thread ya hapo juu.
 
Wana jamvi habari ya Igunga ngoja tuwaachie wanaigunga wenyewe, mimi nimeangalia hizo picha za bwana MICHUZI, umati uliohudhuria wakati wa uzindzi wa kampeni za ccm pia ulikuwa mkubwa , ila sijajua hao watu kama waliwafuata akina masanja na hao wengine, ila mimi kilichonishangaza sana ni msululu mrefu wa hao mbumbumbu mara mukama, wasira, ben, msekwa tena huyu juzi tu alikiponda chama chake sasa sijajua amenda kufanya nini tena kule, mi naona mzee Malecela kwa sehemu ndio pekee mwenye nafuu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom