Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Ni wazi wala haihita msaaada wa kumbukumbu kwamba kuna kitu yaitwa JEURI YA PESA. sina ushahidi wa wazi kwamba huyu amekula ngapi ila ushahidi wa matukio upo wazi. ukiangalia picha utagundua utagundua mambo matatu.

1. MAJUKWAA.

 
Mzee wa Rula nimeangalia vizuri picha zote ndani yake kuna baadhi ya watu ninakaa nao Mwananyamala nadhani walienda na tot
 

umemwabia vema wengewenge. tatzo ni wanasiasa maslahi binafsi na sio maslahi umma.
 
Kama ameoa wana Igunga waote atapita, Kama ameoa mkewe tu anakura 2, yake na mkewe. Amejidhalilisha, ameoa watoto wake wa kiume na wakike pia, poleniiiiiiii watoto wakeeeeeeeeeeeee
 

Mkuu hii ndio kawaida ya CCM,na si mara ya kwanza kwa viongozi wa CCM kufanya hivyo....kumbuka JK aliwapigia kampeni Mramba na Lowasa wakati wakiwa na tuhuma nyingi na nyingine zipo mahakamani...na kauli yake ilikuwa ni kuwa hawa ni majembe ya kale yasiyoishiwa makali....hili la Rostam ni dharau kwa watanzania kutuambia kuwa sisi hatujui kuchambua mambo,kuelewa yanayoendelea na ni wajinga fulani ambao hatuwezi kuchambua mambo.....lakini pia ni kuonesha namna CCM isivyojali hisia za watanzania wengi,Rostam analalamikiwa na umma wa watanzania na ni wazi ana matatizo mengi sana...cha ajabu CCM wanatia pamba masikioni mwao na kumtumia kuwahadaa watanzania,wanaacha kuangalia maslahi ya umma sasa wanatazama maslahi ya chama zaidi....lakini ushindi waja muda si mrefu...
 
@Bado hatujasahau ya Mramba ambaye serikali ya JK ilimfikisha mahakamani kwa makosa ya ufisadi, Uchaguzi mkuu ulipofika bado JK alimpitisha kugombea ubunge na kisha kwenda kumpigia kampeni ili ashinde kule Rombo, lakini watu wa Rombo wakashtukia utapeli huo wakaamua kuipiga chini CCM na kuamua kuichagua Chadema, na ndivyo wanaigunga watakavyofanya tu kwa kuipiga chini CCM mazima na kuamua kuichagua Chadema. @Tunakumbuka mambo ya Jairo, JK anamsimisha kazi kwa mwezi mmoja kwa kuwa Jairo ni mchafu, kisha anamrudishwa kazini kwa kuwa uchunguzi wake umeonesha ni msafi kabisa, asubuhi Jairo anapokelewa ofisini kwa mbwembwe halafu jioni ya siku hiyohiyo JK anamsimamisha kazi tena kwa kuwa Jairo bado ni mchafu!! @Hizo ndio za siasa za CCM inayoongozwa na JK, Ni mambo ya kisanii kwenda mbele tu. Utendaji wake ndani ya Serikali & chama ni kama tamthilia. Sijui issue ya Rostam itakuwa ni episode ya ngapi kwenye tamthilia ya JK? Lets wait&watch the cinema....
 

Cdm vs Ok, thats funny!!
Kwamba Ok ni maarufu kuliko Cdm.
Mjue adui yako na pambana naye siyo kutafutiza visababu, hakuna sheria imevunjwa kwa kuwatumia wasanii, kama Cdm wangeona itawasaidia wangeweza kuwatumia tena walizindua kabla ya Ccm.
Nakumbuka tulifungwa 3-0 utotoni, kumbe wenzetu golikipa wao alivaa gloves na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya kushindwa. Tukaendeleza visababu vya kipuuzi kama hivyo na tukaendelea kufungwa mpaka kitimu chenyewe kikafa. Stori kama zinafanana hivi...
 
Sema ww una shida bnafsi na Zitto...kwani umeona walioko Igunga ni wana ccm?
 

Kaka haya maneno yako yana walakini mkubwa sana, kwa anayeelewa kusoma kwa maarifa hawezi kukuamini hata punje. Kwanza Intnal banks zipo nyingi sana; Kosa la kwanza hukusema hiyo bank kwa kuwa unaogopa hapa JF tuna wana benki hizo wengi sana, ; Pili hizo 3 billion ni utashi wa mtu kuzitoa ama kuziingiza na napenda kukuweka wazi wamba katapila la ujenzi linanunuliwa kwa zaidi ya milioni 800 ambapo kwa makandarasi wakubwa hiyo billion 3 ni pea nut tu, ; Tatu mkuu, umesema una ushahidi na kwa nini sasa huumwagi kwa kuwa hakuna anayekujua humu kwa kuwa wewe mwenyewe hujiamini, na mwisho; siku ingine usijaze JF kwa propoganda za kipuuzi mjinga wewe...
 
pia ukichunguza kwa makini utawakuta vijana wengine hawafurahishwi na kinachoendelea hapo, wameuchuna na kuwashangaa wajinga walivyopandwa na mbwembwe, kumbe hawajui ubaya wa ccm.

..Inahitajika kwanza kuujua uzuri wa vyama vingine ndipo watakapoweza kuuchukia kwa vitendo ubaya wa CCM, fahamu kuwa wengi wenye mashaka na uwezo na umakini wa vyama pinzani wata-opt kuendelea na Zimwi Walijualo, CCM,...
 
Nimewahi kuona Mbwa akitapika then huwa anakula matapishi yake ila sijawahi kuona binadamu mwenye akili timamu akitapika na kula matapishi yake pengine hapa ndio naona sasa jamaa anakula matapishi yake..
 
Masanja noma! Yaani watu walihudhuria kwa wingi kisa masanjaboy 'entertainer'. Wanaigunga wamevutiwa na wasanii wa ze komedy wala sio ushabiki wa ccm.
 
Kweli Jeuri ya Pesa yaweza fanya jambo, hasa kwa jamii ya Ki-Kwetu ambayo fedha kwao ni zaidi ya maisha. hatuna ushahidi wa nani kampanini nani, ila kuna ushahidi wa matukio ambao unahitaji macho tu.. ukiangalia picha za uzinduzi huu utagundua mambo kama matatu makubwa.

1. MAJUKWAA


View attachment 36981
Jukwaa hili ni gharama sana, kuliunda na kulipack pale lilipo, si chini ya paund 7,218 (kama mil16 zaktz). nadhani wahandisi wabobezi tunajua hilo. ama ametoa mtu mmoja au chama kimegharimia, ila tunajua ni fedha toka ardhi ya Tanzania, na ni fedha ya wananchi wa TZ. na hii inafanyika tu kwa uchaguzi wa jimbo moja tu kati ya majimbo 348 ya uchguzi nchi nzima. INATISHA. NADHANI chama HIKI chawaza kuwa ni cha wafujaji wa mali..




JUKWAA LA HILI: Jukwaa la kizalendo, linalo jazia hisia ya uhalisia wa mkutano, wananchi, na matumizi halali ya mali za uma. sidhani kama viongozi wote wa CHAMA HIKI wangechanga nadhani wangeunda jukwaa kubwa sana, but why, kwanini kutumia mali nyingi kwa tukio la siku moja. mie kwangu nashawishika kufikiri kwamba huo ni moyo wa kizalendo zaidi. kwa nchi yangu.
2: MKUTANONI.

View attachment 36983
Wakazi hawa, maskini ya Mungu, mbali na kuvishwa kofia, tshirt, hadi kupewa vuvuzela za njano, ila bado wanaonekana wana tafakari nzito. wana umakini wa kupima kila jambo na kila neno, hawako kwa kudanganywa. nadhani wana jua wanachokifanya. sikubahatika kusikia hotuba iliyotolewa, ila wananchi wanaonekana hawajaridhika na yaliyotamkwa.

View attachment 36984
Wananchi wa Chama Hilki wanaonyesha uhai wa hisia juu ya chama HIKI. kwa hisia moja, tendo moja na hamasiko moja, nadhani CHAMA HIKI kinajua kinachofanya kwa watu. nadhani pia chama hiki kinaelewa nini wananchi wanahitaji ndio mana wako tayari kuonyesha hisia zao kwa chama chao. sisi tunasema, mwanamke bora ni yule mwenye uwezo wa kuonyesha hisia zake kwa wazi kwa mwanamme ampendaye"..

MIE SI MWANASIASA KIIVYO SANA.. NAANGALIA TU.. NAPITAPITA
 
rostam akae akijua leo hii kapewa nafasi feki ya uanachama safi hadi akaombwa akisaidie chama katka kampen.baada tu ya kampen hiz uchwara zinazofanywa na chama chenye siasa uchwara,basi chama kitarudia kumtambua yeye kama gamba na ataendelea kuwa gamba hadi 2015 ambapo atavikwa vazi la uanachama safi ili aombwe kuchangia kampen."AKILI MKICHWA".
Mi nadhani ukishakuwa mwanachama wa chama cha magamba chenye siasa uchwara upeo wa kufikiri unapungua na unakuwa huwezi kutambua haya.
 
Unajisikia vibaya! I know. Lakini mkuu do again your calculations, the opposite might be true. Kwamba Ccm haters wanaweza kuwa converted na kuwa Ccm lovers just to have something in common with their favourite commedians. Love that huh...

Hakika unachokisema ndio sahihi kuwa CCM kwa sasa ndio wako kazini kuakikisha wale wote wnaoichukia CCM wageuke kuwa waumini wazuri wa CCM.Na hilo limekuwa hivyo ukizingatia hata humu ndani ya JF watu wamekuwa na chuki ya dhahili juu ya CCM el maalufu humu jamvini kama wanamagamba..

Sipendezwi na siasa za kuona kuwa hakuna watu wazuri ndani ya CCM,na kuwa ni lazima kila jambo sasa liwe ni upinzani tuu,no hiyo siyo sahihi,ili Nchi iende kwenye mstari tunawaitaji wote chama tawala na vyama upinzani,leo hii CCM wakiwa upinzani chadema wakawa chama madaraka CCM wataonekana wa maana kwa mujibu wa mapungufu ambayo CDM watayaonyesha na uhitaji wa matakwa ya umma.

Lakini kinachoendelea sasa haters wamekuwa mbele hata kwa mambo ambayo ni kwa faida ya Taifa na sio ya Chama.Ndio CCM wanamadudu yao lakini sio kuwa sasa kila jambo watu watengeneze chuki isiyo na msingi.Tutashindwa kutofautisha tofauti hiko wapi,itafikia hatua wananchi wataamua ni heri ya zimwi likujualo alikuli likakwisha.

Yani ili kwa lugha nyepesi ni afadhari ya kubaki na CCM hii ya sasa kuliko kuchagua chama ambacho ujui kesho itakuwaje.Na hili swala itabidi wana JF ambao baadhi yao wana mapenzi na chama cha CDM, watumie uchaguzi mdogo wa Igunga kubadilika na kuwa na mikakati [strategies] humu ndani za kisayansi na sio kuwa na ushabiki wa kupinga na kumwaga matusi kwa kila kitu,vinginevyo tunakokwenda uenda wakatengeneza aina ya usindikizaji wa kudumu na kuanza kupoteza credit kwa kada ya waelewa kusupport movement yao.

Ebu tuwe wazi humu ndani wapenzi wa JF ni wangapi wanachama au wapenzi wa CCM uwa wanalusha madongo ya kuwakejeri wanaCDM humu ndani ukiachia FF ambae anajulikana kwa misimamo yake ambayo imeegemea kuchallange zaidi na kujenga mjadala uweze kuleta tofauti ya mawazo lakini hayuko kukejeri kiivyo.

Binafsi nimeshaweka msimamo wangu wazi Tanzania Mbele, kwangu Nchi kwanza vyama baadae,hivyo ni ukiwa mwana CDM kwangu poa,ukiwa CCM mwake,ukiwa CUF kama kawaida,hivyo kila mmoja atizame kuwa kwa zama hizi tuanze kujenga uungwana wa vitendo na maneno kwa kuwa fito wanazopigania CDM,CCM au CUF ni kwa ajili ya ujenzi wa Nchi inayoitwa Tanzania.

Vyama hivi vishindane kwa HOJA kumjenga MPIGA KURA NA KUKUSANYA WAPENZI NA WANACHAMA WA KUWAUNGA MKONO.Ni vyema pia CDM waanze kutoa elimu ya kwa wapenzi na wanachama wao jinsi ya kuwa na muonekano [behave] ambao unabeba sura ya kichama kwa kila mmoja ambao kwa jumuiko lao ndio tunapata taswira ya kundi ambalo ndio chama kwa ujumla wake.

Tukiendelea kuona matusi ya kuwakebehi wana magamba kuliko mikakati ya kuibua mapungufu na changamoto za kuwafungua masikio yao Wananchi kuwa UPINZANI una sababu zote za kuaminika hakika itakuwa ni hadithi na malalamiko yasiyoisha wanaiba kura na maneno kadha wa kadha yasiyo na tija na ufanisi.

Ukiwaangalia CCM uwa wanabolonga kwelikweli,lakini ninachowakubali wakigundua kosa lao hakika CCM uwa ni wepesi sana kujirekebisha kimya kimya tena chini kwa chini ikibidi hata kwa kukopi mbinu ya adui wao lakini wao cha msingi wa win mapenzi yao kwa wananchi wao.Kwa sasa wameeanza kuwa na ustaarabu wa kauri hata kwa viongozi wao,ambao walio wengi walikuwa na busara.CDM viongozi wana ustaarabu wa matumizi ya maneno lakini wapenzi wake na wanachama wamekuwa na lugha za matusi na kejeri kwa wingi sana na kwa mfano mkubwa ni ndani ya JF.

Please tunawategemea CDM,kuleta changamoto kwa CCM na CUF ambao ni vyama tawala,kwa mambo haya tufika kweli mpaka CDM kuwa chama tawala uko tunakokwenda.Kwenye Red ni hakika hesabu mpya zinatakiwa
 

Unakereka kweli, i can imagine.
Lakini kuwa mkweli, kinachokukera hapo ni huo mstari wa mwisho.
Acha kuzungukazunguka mkuu, just hit to the point...
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…