Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Well.. wapo wanaume watakaomchagua kama mke wake alivyomchagua hujaona wakipiga mavuvuzela na kushika mabango? Kama uko offended usimchague its as simple as that. Msamaha hupati.
Mzee Mwanakijiji, sidhani kama ni sahihi kuwahukumu watu wengi kwa kigezo cha kikundi kidogo cha washangiliaji au wabeba mabango walioandaliwa. Naomba ieleweke kwa wenzetu ambao hawakuwepo eneo la mkutano (waliokuwepo wote wanajua) kuna watu wengi sana walioletwa na CCM kwenye mkutano huo kwa majukumu mbalimbali, Hilo halikuwa siri kwani hata viongozi waandaaji walitutangazia hivyo pale mkutanoni, kuna watu maalum waliletwa kwa wingi wa mafuso ili kuja kushangilia tu, hawa walikuwa hawana haja ya kusikiliza kinachosemwa, wao ni kushangilia tu ili angalau mkutano uchangamke, wasipofanya hivyo, posho zao zitakuwa mashakani, tusiwalaumu. Ona mfano, wakati Mkapa anahutubia, aliona watu wako bored, ndipo akakatisha hotuba yake na kuanza kuimba "Wembe ni uleule" ambapo kumbe maskini alikuwa kausahau akawa anamung'unya ikabidi Cpt Komba aingilie Kati kumsaidia. Lakini pamoja na hayo yote, ilipofikia Kafumu kutaka watu wawe Kama Mkewe, ushangiliaji haukuwa na nguvu sana, hata yale mavuvuzela matatu yaliyoandaliwa pale uwanjani, ni moja tu ndio alijaribu kulipuliza lakini pia kwa bahati mbaya inaelekea hakumudu pumzi za kutosha kwani halikulia vizuri.
 
Yap, yamewakuta magamba. Wengi wa wananchi waliokwenda kwenye mkutano wa ufunguzi Chicm Igungwa walikusanywa. Vijana walikusanywa kutoka vijiji mbalimbali wakapewa uniform labda na posho. Ndo waliojaza mkutano.

Mbaya zaidi, wananchi wakaanza kuondoka. Sababu za kuondoka ni kuwa ccm haina jipya, Hao wananchi waliohojiwa na gazeti la mwananchi walisema ndio serikali inakusanya hela, mbona hakuna maendeleo??

Source: Mwananchi Paper, page 4.
 
Hoja ni kwamba wamchague na sio kama magwanda mnavyo potosha! Shame on you magwanda na magwanda yenu kama mgambo!
 
Ongeza na hizi picha:

View attachment 36990
Hii chupa ya Mwenyekiti Mbowe imejazwa nini? inafanana na wiski.
Nashawishika kusema kuwa chupa ya maji imetumika kuficha kilevi!

View attachment 36991
Hwa nao vipi? Wanamuiga mwenyekiti wao?
Hivi CDM hawawezi kufanya kampeni bila ulevi wa kupindukia? Matokeo yake ni kumwagia tindikali watu wasio na hatia.

WAKATI UMEFIKA KUKOMESHA HUU UHUNI NA KUWAADHIBU KWA KUWANYIMA KURA.
Teh teh teh teh...viroba kwa kwenda mbele
 
tooba taka kuwageuza wanaume wote wa igunga? na alaaniwe huyo
 
Ongeza na hizi picha:

View attachment 36990
Hii chupa ya Mwenyekiti Mbowe imejazwa nini? inafanana na wiski.
Nashawishika kusema kuwa chupa ya maji imetumika kuficha kilevi!

View attachment 36991
Hwa nao vipi? Wanamuiga mwenyekiti wao?
Hivi CDM hawawezi kufanya kampeni bila ulevi wa kupindukia? Matokeo yake ni kumwagia tindikali watu wasio na hatia.

WAKATI UMEFIKA KUKOMESHA HUU UHUNI NA KUWAADHIBU KWA KUWANYIMA KURA.
Pointi yako kwenye hizo picha ni nini?
 
Baada ya vyama viwili vinavyoongoza siasa za Tanzania chadema na ccm kufanya uzinduzi wa kampeni zake za ubunge huko igunga maoni mbalimbali yameanza kutolewa.Ni kweli vyama vyote vilizindua kampeni zake kwa kishindo huku vikijikusanyia maelfu ya watu.Tofauti kubwa ya vyama hivi ni kwamba chadema ilijikusanyia maelfu ya watu wakiongozwa na vijana wa igunga waliohudhuria kwa utashi wao wenyewe.Ccm ilijikusanyia maelfu ya watu waliokuja igunga kutoka wilaya mbalimbali za mkoa huo na hata nje ya mkoa.Kivutio kingine kwa ccm ni kuleta makundi ya wasanii wakiongozwa na TOT na Ze comedy ili kuvuta watu.Hii imethibitishwa na magazeti ya leo mfano gazeti la Mwananchi. Ukiyatazama yote yaliyoandikwa hapo juu utagundua ccm imeshindwa kuvunja rekodi ya chadema igunga.Ni suala la kusubiri na kuona kwani watakaopiga kura ni wakazi wa igunga na kamwe hawatasombwa na malori kutoka wilaya mbalimbali za jirani.Hii ndio tathmini yangu ya awali naomba Tujadili.
 
attachment.php

Makamanda pigeni kazi mpaka kielewe nyie ndiyo tegemeo letu...waacheni wavuana magamaba maana tumesikia wameanza na kuvuana damu kabisa...
 
Zitto hawezi kuhudhuria kwasababu ya tofauti zao na Mbowe. Unajua Zitto huwa hapendi kupelekwa pelekwa kama Mkokoteni. Sasa bila yeye sijui mtashinda vipi uchaguzi?
wewe ndiyo msemaji wa Zitto?
 
Jamani RA hakuacha Ubunge kwa kuchukia gutter politics ila walimtega Lowasa na Chenge ili wapate pa kupumulia lakini wakakuta ma mvi an ngozi ngumu kuliko gamba anapasua tu na wao wakawa wamesha mtoa kafara RA. JK na CCM kwa pamoja mkakati wao umeshindwa kabla hawaajaanza .Ndiyo maana unamuona Rostam yuko hapa anakula matapishi yake this is typical CCM maana huwezi kuwa mmember wao wa juu hata wa chini kabla hujawa kichaa.
Mkuu ulisikia alipokuwa anaoongea Rostam Aziz....inaonyesha amelazimishwa kwashinikizo furani...
 
kwa hiyo jamaa anatuambia "alitokewa" na mke wake,yaelekea huyu kafumu ni mfipa.kwa wafipa mume huiacha familia yake na kuolewa na mwanamke.sioni kama ana kosa lolote as far as kafumu sio mtu wa tabora.(niko tayari kusahihishwa)
 
Hivi CCM hawana vijana wanapowatimua kina nepi kwenye kampeni na kujaza wazee watavunaje kundi la wapiga kura vijana ambao ndio wengi, hapo ndipo CDM inapowapiga bao.
attachment.php
 
Nape aibu yako au Rostam? Ndugu yangu ningekua wewe ningeachana na gutter politics ili kulinda utu na heshima! think twice..
 
Angalieni kauli za Chenkapa akimsifia matonya kwa safari zake za kuombaomba (ikiwepo kuomba suti)

MWENYEKITI mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa amezindua kampeni za chama hicho jana katika uchaguzi mdogo wa Igunga na kuwataka wananchi kumchagua mgombea wa chama hicho na kuwakanyagakanyaga wapinzani.

Akizungumza huku akijibu vijembe vya wapinzani hasa Chadema kwa kuainisha maendeleo yaliyofanyika Igunga na Tanzania kwa ujumla, Mkapa alisema kauli za wapinzani kuwa tangu Uhuru hakujafanyika kitu ni kufuru na hawawatendei haki waasisi wa Taifa.

Alifafanua kuwa asingesemea suala la vyama hivyo kukebehi maendeleo yaliyofikiwa kwakuwa wanajidhalilisha wenyewe, lakini amelazimika kulizungumzia kwa kuwa wanadhalilisha nchi.

Kabla ya kumtambulisha mgombea wa CCM katika uchaguzi huo, Dk. Peter Kafumu kuhutubia wananchi hao, Mkapa alianza kujibu hoja zinazoelekezwa kwake na kwa Rais Jakaya Kikwete kuhusu safari za nje, sera ya ubinafsishaji, elimu, afya na maji.

*Safari za nje za Rais Kikwete
Mkapa alisema Rais Kikwete anakwenda nje kutafuta masoko ya bidhaa za Tanzania na kutafuta mitaji, ujuzi na utaalamu ili nchi ibadili rasilimali zake kuwa utajiri wa wananchi wake wakati vyama vya upinzani na vyenyewe vikienda nje ya nchi, lakini kutafuta ruzuku za vyama kwa ajili ya maandamano.

"Ukimpata atakayekuja na mtaji, utaalamu wapate stahili zao na sisi wenye rasilimali zetu tupate stahili yetu," alisema.

*Sera ya ubinafsishaji
Mkapa alisema Serikali ilikuwa na uchumi wa Dola ambao karibu kila kitu mpaka bucha vilikuwa vikimilikiwa na Serikali lakini wananchi walikuwa wamefungwa mikono.

"Tukasema hapana, tufungue mikono wananchi wajiletee maendeleo," alisema Mkapa na kuongeza kuwa katika sera ya ubinafsishaji, kati ya mashirika karibu 300 yaliyobinafsishwa, sera hiyo inaweza kulaaniwa kwa kushindwa kwa mashirika mawili tu; Shirika la Reli (TRC) na Shirika la Ndege (ATC).

*Elimu, afya na maji
Mkapa alisema yeye alipokuwa akienda shule, alikwenda akiwa peku na alilazimika kulala njiani tofauti na sasa ambako shule ziko nyingi na wanafunzi si tu, hawaendi shule peku, bali wanakwenda na baiskeli.

*Rostam amuombea kura Dk.Kafumu
Naye Rostam alipopewa nafasi ya kuwasalimu wananchi hao, alisema amekwenda katika kampeni hizo kwa shughuli moja ya kumuombea kura Dk. Kafumu.

Source: Habari Leo aka Udaku
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom