Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
The Boss,
Hilo haliwezekani Mkuu. Kumbuka kwamba tunapofanya uchaguzi Mkuu tunachagua Chama pamoja na Mgombea wake. Ndio maana kunakuwa na picha ya mgombea pamoja na chama kinachomdhamini. Hatuchagui chama alafu then chama kinamteua muwakilishi.

Hoja yako ingekuwa ya maana kama kwenye uchaguzi Mkuu wapiga kura wanachagua chama, then chama kinachoshinda kinamteua mtu kuwakilisha jimbo lake. Tuendelee kujadiliana.
 
the boss, sounds sensible lakini inategemea na sababu ya uchaguzi mdogo. endapo ni kifo inawezekana kumpa 2nd runnerup wa uteuzi chamani.lakini kama ni issues ambazo zilisababisha wapiga kura kukosa imani na chama, ama mfumo mzima wa uchaguzi inaweza kutokuwa sawa sana kukwepa uchaguzi. kumbuka kuwa sio wanachama wenzie mbunge pekee wanaompigia kura, bali wanajimbo wote bila kujali sana itikadi zao za kisiasa wanaweza kumchagua mbunge kwa sababu wanaona anaweza kuwaongoza na kutatua matatizo yao sugu.

well hapo unaongea kitu cha maana.....
tunaweza kutenganisha sababu..
mfano kama ni kifo basi apewe second runner up...

au ya chama kilichoshinda kwa asilimia labda sabini..wafanye uchaguzi wa chama
na atakeshinda apewe
au vyovyote vile but sio hivi sasa..
 
kila unapotokea uchaguzi mdogo najikuta namkumbuka Halima Mdee

yeye peke yake alizungumza kitu cha maana kuhusu hizi chaguzi ndogo...

alisema chaguzi ndogo zinapoteza muda na pesa nyingi

ni bora ukawekwa utaratibu wa chama kinachoshikilia jimbo hilo
kuchagua ni nani arithi jimbo......

hakuna anaesikiliza haya,but huu ndo ukweli mtupu....

hizi chaguzi ndogo its a waste of time and money.....

zipigwe marufuku......

majitu mengine bana eti Title HM na uchaguzi wa Igunga, kumbe hakuna lolote ambalo Mdee kazungumza kuhusu Igunga, no source no nini then unajiona ni GT masaburi thread
 
Acheni wale jamani, wanakazi kubwa ya kushangilia chama. Na nyie wa CDM mnaweza kwenda kula kama kwenye mikutano yenu hakuna msosi. Unajua kushindia karanga za kukaanga na miwa hamtaweza kutoa sauti. Ubwabwa ni muhimu.
 
Safari bado ni ndefu. Mungu ibariki Tanzania.
 
Gharama unazozizungumzia ndio gharama za Demokrasia na kwa kawaida hazina short cut. Ni lazima tuendelee hivyo hivyo kwani waliochagua mwanzo ni wananchi na kwamba kiongozi aliyechaguliwa kupitia uchaguzi nafasi hiyo haiwezi kuwa ya uteuzi ni lazima taratibu zifuatwe.

Binafsi namuamini mpambanaji huyo (Halima Mdee) lakini kama ni kweli alisema hivyo na si kwamba amenukuliwa vibaya, hapa naona alichemka!

Tujifunze mambo ya demokrasia toka kwa waliotufundisha mataifa makubwa. Aliyoyasema Halima Mdee ni sahihi kwa vile hata mataifa makubwa inapotokea jimbo la uchaguzi kuwa wazi wana utaratibu wa kuteua mtu wa kushikilia hadi uchaguzi utakapofikia muda wake ili kuongoa gharama za uchauzi.

Obama alipochaguliwa kuwa Rais wa Marekani, nafasi yake ya Useneta ilijazwa jimboni kwake kwa kuteuliwa mwakilishi mwingine hadi uchaguzi mwingine ulipowadia. So what is wrong?
 
Hii niliisikia tangu jana, lakini sikuweza kupata sababu yake. Jamaa yangu mmoja huko Igunga alinipigia simu kwamba wakati Mkapa alipokuwa anahutubia watu kwa makundi walikuwa wakiondoka mkutanoni. Leo hii nimesoma habari kama hiyo katika Mwananchi Uk wa 4 chini ya kifungu cha maneno 'Wengine waondoka":

Wakati Mkapa akiendelea kuhutubia, baadhi ya watu wakiwa kwenye makundi walianza kuondoka kwenye mkutano huo.

wengi waliohojiwa na Mwananchi Jumapili walisema hakuna jipya katika hotuba ya Mkapa na kuongeza kuwa, waliyokuwa wakiambiwa na wapinzani yalithibitishwa na Mkapa mwenyewe.

Walitoa mfano kuwa Mkapa alipoingia madarakani, makusanyo ya Serikali kwa mwezi yalikuwa Sh 28 bilioni, lakini hadi anaondoka, makusanyo hayo yalikuwa Sh 400 bilioni na kuongeza kuwa ni wazi Serikali ina fedha, lakini hazitumiki kwa shughuli za maendeleo.
 
Hapa aliongea pumba. Na raisi akifa, Nape anapewa nchi. Huu ni ujuha.
 
kwa hiyo unathibitisha kwamba kafumu alitumia maneno hayo
ila wapenzi wa cdm wanapotosha maaana? nawewe umeridhika
kabisa kwamba hii maneno ya "kufanya kama wife" yako poa! dah!

Hoja ni kwamba wamchague na sio kama magwanda mnavyo potosha! Shame on you magwanda na magwanda yenu kama mgambo!
 
majitu mengine bana eti Title HM na uchaguzi wa Igunga, kumbe hakuna lolote ambalo Mdee kazungumza kuhusu Igunga, no source no nini then unajiona ni GT masaburi thread

soma alichoandika candid scope uone wewe ulivyo masaburi
na upeo mdogo....
 
well hapo unaongea kitu cha maana.....
tunaweza kutenganisha sababu..
mfano kama ni kifo basi apewe second runner up...

au ya chama kilichoshinda kwa asilimia labda sabini..wafanye uchaguzi wa chama
na atakeshinda apewe
au vyovyote vile but sio hivi sasa..
kwa nini kwenye ubunge tu na sio udiwani,urais?
 
Lazima wananchi tuwakane wanafiki kama RA hadharani. Zile siasa uchwara za ccm zimebadilika? Huu ni unafiki mkubwa, ccm wameprove kuwa bila RA ccm haisimami.
 
Watu wengi wamekuja kuwaona ze comedy na TOT ya komba, lakini si kusikiliza sera za che nkapa
 
Bora ungesubiri uone kuliko kuleta tathmini njaa hapa.
 
kwa nini kwenye ubunge tu na sio udiwani,urais?

kwenye urais tayari sheria ipo
ambapo rais aikifa ghafla au akiondolewa wakati ameshamaliza nusu ya kipindi chake
makamu anakuwa rais mpaka uchaguzi ujao...

udiwani na ubunge bado tunahitaji sheria tofauti
 
Hapa aliongea pumba. Na raisi akifa, Nape anapewa nchi. Huu ni ujuha.

Perplex reasoning! The main theme/context is about "UCHAGUZI MDOGO" halafu unazungumzia Rais! Rais akifa (more clearly AKISHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE) automatically kuna Makamu wa Rais; ana take over. Kweli viumbe wazito.
 
democratic system mst follow democratic principles, no shortcut, halima mdee isn't perfect she can make mistakes.
Mkiogopa cost hata katiba mpya haitakuwa na uhalali kuliko ya zamani.
 
Nimeipenda ile picha yenye bango linalowataka CDM wapeleke fujo zao Arusha na Kilimanjaro. Wakamalizia...KURA HATUWAPI!

Saafi sana.
Tatizo lako huwezi kutofautisha Igunga na Arusha....Kikwete alipokuja mwaka jana kufanya kampeni pale kwenye uwanja wa sheikh Amri Abed, walipomaliza wasanii kutumbuiza watu walianza kuondoka ikabidi polisi waliokuwa magitini kuwazuia kutoka hata Kikwete alihutubia chini ya dakika 10, kwasababu watu walikuwa wanatoka....Arusha huwezi kutukusanya kwa wali na maharage labda pesa, kanga, kofia ,T-Shirt na wasanii na mbinu hizi tulichazijulia akikupa pesa chukua maana ni pesa yako akikupa t-shirt chukua utaenda kudekia au litakuwa vazi lashamba....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom