Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Siipendi CCM na viongozi wake. angalieni uongo wa gazeti la uhuru

Mkapa atikisa jimbo la Igunga


Friday, 09 September 2011 12:15 newsroom



apa .jpg



WAKATI ujio wa Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa, ukitikisa wilayani Igunga, vyama vya CHADEMA na CUF vimezidi kuingia kwenye mgogoro. Msafara wa Mkapa uliwasili wilayani hapa jana kwa njia ya barabara na kupata mapokezi makubwa, huku wananchi wakiacha shughuli zao na kujitokeza kumlaki.

Awali, Mkapa ambaye ujio wake umekuwa mwiba kwa wapinzani, alipokewa na viongozi wa CCM, wanachama na wananchi katika kijiji cha Makomero, nje kidogo ya Igunga. Baada ya kuwasili katika kijiji hicho, msafara wa Mkapa ulisimama kwa muda ili asalimiane na wana-CCM na wananchi waliojitokeza.

Mkapa aliwaeleza amekwenda Igunga kukamilisha kazi moja tu, ambayo ni ushindi kwa CCM. Mkapa atazindua kampeni za mgombea ubunge wa CCM, Dk. Peter Kafumu, kesho kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Rostam Aziz, aliyejiuzulu.

"Nimewasili Igunga na wana-Igunga kazi iliyopo mbele yetu ni moja, ni ushindi tu," alisema huku akishangiliwa. Alisema anaona fahari kubwa kufika Igunga kwa njia ya barabara, tena ya lami na kwamba, mara ya mwisho alipita ikiwa ya vumbi. "Nafarijika kufika hapa kwa kutumia barabara, haya ni maendeleo makubwa jamani," alisema.

Mkapa aliwaasa wananchi wa Igunga kujitokeza kwa wingi Oktoba 2, mwaka huu, kumpigia kura mgombea wa CCM, Dk. Kafumu. Alisema kwa kufanya hivyo, wananchi watakuwa wamechagua maendeleo na kuachana na wapinzani, ambao hawana sera. "Kuna mengi ya kuwaeleza tutakapokutana kwenye mikutano yetu ya kampeni, lakini mfahamu kuwa kura zote kwa Dk. Kafumu," alisema.

Baada ya kusalimiana na wana-CCM hao, msafara wa Mkapa uliingia mjini ukiongozwa na waendesha pikipiki na baiskeli, zilizopambwa kwa bendera za CCM. Msafara huo ulizunguka katika mitaa mbalimbali ya mjini wa Igunga na kuzidisha hofu kwa wapinzani, ambao wamekuwa wakimhofia kiongozi huyo mwenye historia nchini. Mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM utafanyika katika viwanja vya Kumbukumbu ya Samora, ambapo leo Mkapa atakuwa na shughuli mbalimbali za kichama.

CHADEMA, CUF ‘watoana roho'

Wakati kivumbi cha kampeni kikianza kutimka jimboni humu, vyama vya upinzani vinavyopambana na CCM, vimeanza kuingiwa na kiwewe huku CHADEMA kikiwasilisha malalamiko polisi ya kufanyiwa fujo na wafuasi wa CUF na kutaka hatua za haraka zichuliwe kabla hali haijawa mbaya.
Kupitia barua yenye kumbukumbu namba CDM/W/IG/UCH/VOL.5/2011, Katibu wa CHADEMA wilayani Igunga, Christopher Saye, aliiomba polisi kuichukulia hatua CUF kwa madai kitendo hicho kikirudiwa kinaweza kuvuruga amani.

CHADEMA imedai Jumanne iliyopita wafuasi wa CUF waliwafanyia fujo wakiwa katika harakati za kurejesha fomu za mgombea wao.
Walidai wakiwa katika msafara wa kurejesha fomu, magari ya CUF yaliyokuwa yameegeshwa jirani na ofisi za CHADEMA yalianza kupita katikati ya msafara wao.

Kutokana na madai hayo, juzi Msimamizi wa Uchaguzi huo, Magayane Protace, alilazimika kuwaita wawakilishi wa CHADEMA na CUF na kuwakemea kutokana na vurugu hizo.

Kwa upande wao, CUF wamedai shutuma zilizotolewa na CHADEMA kwamba CUF ndiyo waanzilishi wa vurugu ni za uongo na zenye lengo la kuupotosha umma.

Last Updated ( Friday, 09 September 2011 12:57 )
 
Kwa heshima aliyopata Mkapa kama Rais mstaafu haipendezi kuingia kwenye siasa za vyama, hizi si ndio kazi za kina Nape? Au ndio Nape keshaonesha failure tayari!?
 
teeeh teeehteeh! yangu macho,
ukiona mzinga wa nyuki halafu hawakufuati usidhani ni wapole au hawang'ati, ukiwachokoza utakiona,
ndo anachokifanya mkapa, anadhani hatujui mauchafu yake? kachokoza atakioba sasa!
 
ccm inagenge la wezi tupu, hakuna hata aliemsafi, woote si saafi , wadokozi na generally ni mafisadi kwelikweli
 
Angalau Mkapa atupe majibu ya maswali haya;
1.Je,aliyoyasema Rostam kuhusu CCM kuwa na siasa uchwara ni ya kweli?
2.Je,(kama jibu la kwanza ni HAPANA) CCM ipo tayari kumkemea Rostam na kujisafisha Igunga?
3.Je,(kama jibu la swali la kwanza ni NDIO) Mkapa anawathibitishiaje wanaigunga kwamba anachokifanya si sehemu ya siasa hizo uchwara?
 
Atakuwa pia anafarijika kuona miaka 50 ya uhuru ccm imetengeneza mgao mkali wa umeme nchi nzima na mwaka huu kwa kuvunja rekodi ya wanafunzi wa fm4 kufeli wengi toka tupate uhuru...kiitikio,TUNASONGA MBELE!!!
 
Baasi magamba kwishine. Maana jamaa anatisha sana au wamempaka enjoy face ili watu wasije kimbia mkutano!
 
Nipe tano (oooh - kwa lipi? sikupi), Hebu nikumbushe ... (Unajua mie nawaza Maisha mapya tu) - Hivii memtubutu nini vile? Na mmeweza nini na sasa mnasonga mbele kwa nini vile?

Wamethubutu kufisidi nchi, wameweza kuiba na kuwa maskinisha watanganyika bila kuchukuliwa hatua na wananchi na sasa wanasonga mbele kuwarithisha watoto wao uongozi wa kifisadi. Ni mtazamo wangu tu.
 
Watanzania wa kawaida na hasa wanaigunga wanakumbuka hoja mbili kila wanaposikia uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, kwanza tunafikiria juhudi za kujitakasa za Chama Cha Mapinduzi na pili tunakumbuka maneno ya kada maarufu wa chama cha mapinduzi ndugu na mpendwa wetu Rostamu Azizi aliyesema kuwa chama hiki kimebaki kuwa chama cha siasa uchwara kwa maana ya mjumuiko wa watu ambao kazi yao kubwa ni kuwachafua wengine.

Siku zote tumesikia ama kwa uwazi au kwa kificho juu ya tuhuma za mapacha watatu, mmoja amejitoa na wengine wawili bado. Swali na kitendawili ambacho lazima Mkapa akitegue leo au kesho wakati akizingua kampeni za CCM Igunga ni je Ufisadi CCM maana yake ilikuwa ni Rostamu pekee, je hoja ya Rostamu ya siasa uchwara, CCM inasemaje? vinginevyo hawataaminika na wanaigunga na watahesabika kama wameenda Igunga kufanya mchezo wa kuigiza.


Mkapa hata kama ni kada wa CCM chama hiki hakikumtendea haki na mimi kama mtanzania ambaye kodi yangu inamtunza Mkapa nasema kumuinua Rais mstaafu akafanye kampeni za ubunge ni kumdhalilisha, yeye saizi yake ni kumnadi Mgombea Urais. Hivi ikitokea CCM imeshindwa Igunga watasemaje? Mkapa atajisikiaje? najua wamemchukua kwa sababu ni mzoefu wa kushindwa rejea Temeke na Mrema. Mnapomdhoofisha lulu yenu nani atazunguka 2015 kumnadi mgombea wenu.

Mkapa asiye safi rohoni na machoni kwa Watanzania ushiriki wake Igunga nini tafsiri yake kwa Watanzania "Chama hiki hakina mtu safi anayeweza kumnadi mgombea wa CCM" Kwa nini si Salimu, Kwanini si Waryoba, Kwa nini si Anna Abdalah, Kwa nini si Nchimbi, Kwa nini si Sita? HAYA BWANA NAWAACHIA WENYEWE. Sijisikii amani Rais mstaafu kuingia mgogoro wa kupigana madongo ya kisiasa na vijana wa miaka 20 na hawatamuacha kabisa.

Ama kwangu mimi naona CCM imepanga kumumaliza Mkapa ili asiwe na mvuto au sauti katika mchakato wa kutafuta mgombea wao mwaka 2015. Kwa sababu kila akiinua shingo watamwambia na wewe yako tuliyasikia Igunga. Kama akishindwa watamwambia kaa pembeni wewe huwezi kumnadi mgombea wetu kwa hiyo usituchagulie

Usani wa CCM kwenye siasa ni kwamba wanataka wote wachafuke ili asiwepo wa kumnyooshea kidole mwenzake


VIVA uwazi na Ukweli
punde baada ya matokeo ya igunga yatakapo tangazwa kua CCM imepigwa chini huyu mkapa atagoma kuongelea hili swala kwa waandishi wa habari.Wanamzeeesha vibaya chinga.
 
Tukisema WAMESHINDWA KABLA HAWAJAANZA MNASEMA MAJUNGU, KWA KAULI MBIU YA KUFUMUA MTOTO WAO MNAWAOMBAJE KURA????? TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE
<br />
<br />
Narudia kusema tena hizo kaulimbiu za ccm ndo zinazozidi kudidimiza maisha yawa Tanzania
 
Haya ni majukumu ya lazima ya serikali yoyote ile inapokuwa madarakani sababu ndiyo yanayoendesha taifa. Sasa Mkapa anapodai kuwa barabara ya lami imetokana na CCM, kama bado akili zake zinafanya kazi alidhani serikali ipi ilitakiwa kujenga hiyo barabara?

Na mimi nashangaa hapa. Halafu toka uhuru ni wao tu waliokuwa madarakani, labda hapa katikati kama kulishawahi kuwapo na serikali ya chadema ama chama chochote kingine ndio angekuwa sahihi kusema ccm imefanikiwa kujenga barabara za km kadhaa ktk miaka kadhaa kulinganisha na serikali za vyama vingine. Kwa sasa mkapa anachoweza kulinganisha ni awamu tofauti za serikali ya ccm. Hivyo atakua sahihi kusema kwa mfano anajisifia mafanikio ya awamu yake kujenga barabara ya mwanza-dar wakati awamu ya kikwete haijafanya chochote
 
Pamoja na Tambo nyingi kwa Viongozi wa Chadema kwa kurusha makombora kwa CCM hakuna alie thubutu kugusa suala la Kagodaa kwenye uzinduzi wa kampeni Igunga. Hakugusia hata kidogo kashfa ya Kagoda! <br />
<br />
Watalamu wa mambo ya siasa wanasema Chadema hawana ushahidi juu ya Kagoda kama Ushahidi wa Msema kweli! Imekua vigumu kwa CDM kuongelea Kagoda tofauti na hapo nyuma kwani suala la Kagoda kwa sasa halitakiwi porojo za kisiasa kinachotakiwa ni Ushidi uwe kama ule wa Msemakweli au Zaidi! <br />
<br />
Suala la Kagoda linaipunguzia Chadema kuaminiwa kwani hawana ukweli wake.
<br />
<br />
Kazi ya Nape hiyo lakini Marwa tumia akili kwani wakati wa kuchezea watz umekwisha! Cdm ni sayari nyingine kama ni timu ya mpira ni sawa na Barcelona kwani Cdm ina viungo kumi uwanjani!
 
Atakuwa pia anafarijika kuona miaka 50 ya uhuru ccm imetengeneza mgao mkali wa umeme nchi nzima na mwaka huu kwa kuvunja rekodi ya wanafunzi wa fm4 kufeli wengi toka tupate uhuru...kiitikio,TUNASONGA MBELE!!!

Imebidi nicheke tu hii post yako. Hasa hapo kwenye kiitikio, mambo ya wimbo wa katikati nini hahahahaha
 
<br />
<br />
Watalamu wa mambo ya siasa wanasema Chadema hawana ushahidi juu ya Kagoda kama Ushahidi wa Msema kweli! Imekua vigumu kwa CDM kuongelea Kagoda tofauti na hapo nyuma kwani suala la Kagoda kwa sasa halitakiwi porojo za kisiasa kinachotakiwa ni Ushidi uwe kama ule wa Msemakweli au Zaidi! <br />
<br />
Suala la Kagoda linaipunguzia Chadema kuaminiwa kwani hawana ukweli wake.
<br />
<br />
Kweli cdM Balaa, kazi ya polisi wafanye wao!
 
duh katika haya masaa mawili tu wangemaliza kila kitu bado siku zote hizo Marwa ngojea muziki ndio umeanza kupigwa
 
Pamoja na Tambo nyingi kwa Viongozi wa Chadema kwa kurusha makombora kwa CCM hakuna alie thubutu kugusa suala la Kagodaa kwenye uzinduzi wa kampeni Igunga. Hakugusia hata kidogo kashfa ya Kagoda!

Watalamu wa mambo ya siasa wanasema Chadema hawana ushahidi juu ya Kagoda kama Ushahidi wa Msema kweli! Imekua vigumu kwa CDM kuongelea Kagoda tofauti na hapo nyuma kwani suala la Kagoda kwa sasa halitakiwi porojo za kisiasa kinachotakiwa ni Ushidi uwe kama ule wa Msemakweli au Zaidi!

Suala la Kagoda linaipunguzia Chadema kuaminiwa kwani hawana ukweli wake.

Masaburi sort of thinking!! just a waste ....
 
Mghaka tunaomba muulize swali Lingine kwa Mkapa,Msekwa alisema chama kimechafuka kinanuka,kinahitaji watu waadilifu jee tayari hawo watu wamepatikana
Malecela ,Makamu mwenyekiti wa CCM wa zamani alisema utawala wa sasa hivi wa CCM ni shaghalabaghala jee sasa umetengamaa
Waziri mkuu wa Zamani Msuya alisema CCM imepoteza dira ina watu wasioaminika je hiyo hali imebadirika
Waziri mkuu wa Zamani Lowassa alisema serikali ya CCM haina uthubutu jee sasa hivi inathubutu
Mwenyekiti wa CCM shinyanga alisema CCm kinaongozwa na makundi jee makundi yameisha
Waziri mkuu Pinda alisema kuna watu vimbelembele akichombezewa na Nape kada maarufu eti kuna mbio za kugombea uraisi 2015 kwamba zina vuruga chama jee mbio hizo zimekoma Mghaka usikose kutujuvya akikupa majibu tafadhali
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom