Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
hahahaha RAI + ROSTAM unategemea nini magamba bwana yanachakachua hadi kwenye blog hapo bado jambo leo habarileo and co
 
Kweli magamba wana mpango thabiti wa kuhakikisha waTZ wanabaki maskini. Hii itawasaidia sana kuhakikisha wanaendelea kubaki madarakani kwa kutumia hongo kama chakula.

Imeniuma sana. Imeniaminisha kuwa magamba hawatafanya mpango wowote wa maendeleo ya watu ikiwemo kuhakikisha usalalma wa chakula kwani wanajua kuwa mtaji wao kisiasa ni ujinga na umaskini(unaosabisha kukosa uhakika wa chakula) wa waTZ.

Narudia kusema, Imeniuma sana kuona waTZ wakipewa chakula tena cha mlo mmoja kwenye mkutano wa kampeni.
 
Wewe umedanganywa na ubwabwa ila wanaigunga hawadanganyiki na mlo wa siku moja na octoba 2 watakudhihirishia
mimi siwezi kubishana na mtu anayefikiri kwa kutumia ''masburi'' tusubiri hiyo octoba 2; ndio utajua kuwa peple's ni ccm.
 
kwa kuwa wapiga kura wa igunga ni wa mikoa jirani na tabora kama mlivyowachukua waje kwenye ufunguzi, basi mtashinda.
mimi siwezi kubishana na mtu anayefikiri kwa kutumia ''masburi'' tusubiri hiyo octoba 2; ndio utajua kuwa peple's ni ccm
 
Hoja ina mashiko, ni kweli kwamba "complacence" yaani ile hali ya kuona mambo yako shwari na hivyo kuamua kustarehe au kubweteka kwa kujiamini ni jambo la hatari. Hata bondia makini anapotamba kabla ya pambano huwa moyoni anajua kwamba akifanya masihara tu ameliwa, kwa hiyo umakini unahitajika, usimdharau adui.
 
CCM waliandaa wazingira ya ushindi tangu muda kwa kuwaandalia watanzania mazingira ya umaskini ili kwenye uchaguzi wawahadae watanzania kwa pilau/ubwabwa kwa vile hata mlo mmoja kwa kutwa ni mtihani, kugawa kofia na fulana(bila suruali au kaptula) bure, kuwabeba vizee, akinamama na watoto kwenye malori(ya kubebea mchanga) kuwapeleka kwenye mikutano ya kampeni kwa vile hata baiskeli hawana matarajio ya kununua. Kugawa chumvi na dagaa, kugawa visenti(sio kama vya Chenge). Hivyo kazi mnayo "magwanda" kuwang'oa "magamba". Nimeitoa kiwepesi ili kuua soo au mnasemaje?
 
Hii ya watu kurudisha kadi za vyama vya upinzani tulishaizoea. Inabidi watafute propaganda nyingine. This is a very old trick.
 
Mkuu,

Tunaposema haingwi mkono wewe pia usikosee kutuelewa, nani kakwambia bondia aingiapo ulingoni kupambana husema atapingwa japo ngumi moja, au unadhani hajui kuwa mpinzani wake atarusha makonde. Hivyo basi unaposikia 'ccm haiungwi mkono' wewe malizia na neno hili 'na watanzania wengi' kuliko kuanza kuwatishia watu yakwamba ..........watakuwa wajinga kumbe wewe ndiyo umefikiri ndani ya box. Soma picha kwenye post #6, utatafuta mpaka kwa tochi hukuti cdm inawarubuni watu kwa peremende ili wakawasikilize.

CCM haina ubavu wa kuitisha mkutano igunga au sehemu yoyote isijifiche nyuma ya ze comedi, tot, usafiri na ubwabwa wa kumwaga, usijaribu kujenga hofu kwa wapiganaji wako, wajasiri wataku fire friendly, ndugu jamaa na marafiki wakaishia kukuombea u-rip.
 
Mkuu ni kweli kuamini CCM haiungwi mkono ni ujinga, lakini kuiunga mkono CCM pia ni ujinga. Our part should remain to educate people that they may not support CCM period.

 
Uwingi wa watu ni ishara kuwa ccm watashinda kwa ushindi wa kimbunga ccm oyeeeee

Acha kuleta ndoto za mchana humu jamvini. Mbona ktk uchaguzi mkuu uliopita 2010 picha za mikutano ya CCM zilijaa wingi wa watu na mabango kibao nchi nzima na bado wakapigwa chini u rais, ila walichakachua tu. Hao watu wamelipwa pesa na chakula kisha wakaletwa mkutanoni kwa marori na mabasi, nakwambia Watanzania kama KAWA, pesa ya CCM wataila sana lakini kura hawataipa CCM ng'o. Yetu macho tu.
 
kila unapotokea uchaguzi mdogo najikuta namkumbuka Halima Mdee

yeye peke yake alizungumza kitu cha maana kuhusu hizi chaguzi ndogo...

alisema chaguzi ndogo zinapoteza muda na pesa nyingi

ni bora ukawekwa utaratibu wa chama kinachoshikilia jimbo hilo
kuchagua ni nani arithi jimbo......

hakuna anaesikiliza haya,but huu ndo ukweli mtupu....

hizi chaguzi ndogo its a waste of time and money.....

zipigwe marufuku......

nafikiri unakosea , kwa utaratibu tuliokuwa nao zaidi ya kuchagua chama, kuna kuchagua mtu, so hii hoja haikubaliki!
ili hoja hii ikubalike tufuate mtindo wa proportional representation , ndipo hoja hii itakapo kuwa na mshiko, na suala hili lilisha ongelewa na mzee mapesa , na pia jaji Bomani
 
suala la kuchukua mshindi wa pili ni kutafutia watu vifo mana watauana tu. Asikwambie mtu ubunge pesa ni tamu na haina kutoa majasho na ninavyowajua magamba kwa uchawi duuh watauana.
 
Huyo Halima Mdee mwenyewe ana jinsia gani, KE au ME. Kama KE mbona sijawahi kumuona na mpenzi hata siku moja na kama ME mbona hataki kuoa? Nikijibiwa ndiyo nitatoa mchango wangu.
<br />
<br />

Kwa kweli, mnnnh!
 
Wanajamii safari bado ni ndefu.Umaskini na ujinga wa Wananchi ndo Mtaji wa Chama fulani sikitaji.Ila nadhani siku zinahesabika ikiwa Vyama Mbadala vitajizatiti nakuoyesha nia ya kuwasaidia Watanzania kwa uhalisia wake.Mungu ibariki Tanzania.
 
HTML:
[HTML][HTML] [IMG]https://www.jamiiforums.com/template/JamiV1/default/misc/quote_icon.png[/IMG] By [B]King'asti[/B] [URL="https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/171593-halima-mdee-na-uchaguzi-wa-igunga.html#post2480953"][IMG]https://www.jamiiforums.com/template/JamiV1/default/buttons/viewpost-right.png[/IMG][/URL] 

 the  boss, sounds sensible lakini inategemea na sababu ya uchaguzi mdogo.  endapo ni kifo inawezekana kumpa 2nd runnerup wa uteuzi chamani.lakini  kama ni issues ambazo zilisababisha wapiga kura kukosa imani na chama,  ama mfumo mzima wa uchaguzi inaweza kutokuwa sawa sana kukwepa uchaguzi.  kumbuka kuwa sio wanachama wenzie mbunge pekee wanaompigia kura, bali  wanajimbo wote bila kujali sana itikadi zao za kisiasa wanaweza  kumchagua mbunge kwa sababu wanaona anaweza kuwaongoza na kutatua  matatizo yao sugu.
    well hapo unaongea kitu cha maana.....
tunaweza kutenganisha sababu..
mfano kama ni kifo basi apewe second runner up...
 
au ya chama kilichoshinda kwa asilimia labda sabini..wafanye uchaguzi wa chama
na atakeshinda
au vyovyote vile but sio hivi sasa.[QUOTE][/QUOTE]



mbona hueleweki kabisa yani apewe second runner up, sasa kwa nini hasipewe aliyekuwa first runner up?? hata huko Marekani hapewi second runner up! Lakini pia tunapoiga tunaangalia mambo mengi na si kila kinachofanywa na marekani na sisi tukiige. gharama ya uchaguzi ni ndogo sana ukilinganisha na gharama ya demokrasia inayolindwa hapo. hapo vinavyokuza gharama ni vyama vya siasa vyenyewe na serikali haipati hasara kubwa sana labda ikichakachuliwa na chama tawala, ingawa wao wamezoea kuchakachua hatazisingeenda huko zingeenda kwao tu.[QUOTE][/QUOTE]
 
Kama tatizo ni gharama, kwa nini msiweke sheria ya gharama ya matumizi kwenye uchaguzi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom