Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Hivi mtu anayetembea kifua wazi, mwanamke asiye hata na nguo za kuendea hospitali, sokoni akipewa kanga, fulana, kitambaa cha kichwani au kofia hivi vitu vinaashiria nini?

Nimewahi kuzunguka na kuwaangalia watu wakivitumia hivyo vitu katika siku za kawaida ambazo haziwatambulishi na ushabiki wa siasa bali kama vazi rasmi la kutokea. Kwa hiyo kwa mtu ambaye ni maskini kabisa kama ilivyo watanzania wengi wa vijijini ambako CCM hujitia inakubalika nguzo yake kubwa ni umaskini wa wa Watanzania na ugawaji wa vitu kama khanga, fulana, vitambaa vya kichwani na kofia ambazo hutolewa zawadi kwa wapiga kura na si kwa wanachama wake.

Tungependa waandishi wa habari wafanye uchunguzi kugundua hizi khanga na vitu vingine ambavyo hutolewa ikiwa ni pamoja na chakula vinaathiri kiasi gani mwenendo wa upigaji kura?

Bahati mbaya tuliyonayo ni kuwa PCCB na Tume ya Uchaguzi vyombo ambavyo vinawajibu wa kisheria kupiga vita rushwa katika uchaguzi ni kama idara maalum na zisizo halali za CCM
 
Asante Kigarama kwa kuwakumbusha wapenzi wenzako wa CHADEMA kwani ukisoma post za wengine humu ndani unahisi kuwa wanaishi katika ulimwengu wa kufikirika.

Ni kweli kuwa CHADEMA inaungwa mkono na vijana wengi lakini ni ukweli pia kuwa CCM bado inaungwa mkono na watu wengi wengine wakiwa ni vijana kama hawa wa CHADEMA. Unaweza ukajenga hoja kwa kuainisha sababu hasa zinazowavutia watu kuunga mkono chama kimoja na kuacha kingine.

Bahati nzuri nayaongea haya nikiwa sio mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpiga kura na hivyo navifuatilia vyama vyote kujua vinachosimamia.
 
Tatizo hapa ni watanzania kutojua tulipo, tunakoelekea na tunapopaswa kuelekea. Tufanye kazi ya kuelimisha umma, na lazima tujue kazi hiyo itakumbana na vikwazo vingi. Mwisho wa yote dhamira iwe ushindi. Inawezekana, kila anayeipenda nchi hii atimize wajibu wake.


Pesa za kuhonga wanazo lakini za kuleta maendeleo wanazitafuna wenyewe, hii ni aibu kwetu sisi Wananchi tunadanganywa na mlo 1 kwa kuuza haki yako. Watanzania hatuna njaa ya hivyo ya kugombaniana Chakula Njaa yetu ipo kwenye Maendeleo na Ajira, Still Magamba dont get it
 
Nawapa pole wale wote walioambiwa na kushangilia kama majuha, wenye akili tayari wameliona na sasa upinzani wanatakiwa kuliweka wazi kwa wananchi ili wamhukumu vilivyo maana waswahili walisema mdomo huumba na pia hubomoa mpaka hapo tayari Kafumu kajifumua mwenyewe.
 
Hao CCM badala ya kununua ambulance na kuboresha vituo vya afya wanaagiza magari ya maji ya kuwashaya bei mbaya ili kudhibiti upinzani! hebu angalia aibu tuliyoipata juzi kwenye ajali ya meli! Hata vifaa vya kujiokolea hakuna! Msafara wa RAIS WETU MPENDWA uana magari ya anasa ni balaa!
Ngoja sasa tusikie porijo za viongozi wetu juu ya hili! Maana ilipotokea ajali ya MV Bukoba tuliambiwa mengi mno! lakini baadaye kama kawaida Business as usual! Miaka 50 ya Uhhuru bado hata usafiri wa majini wa kueleweka hakuna! Looh1 Hebu wafike mahali waone aibu! Watanzania sasa ni wakati wa kufanya mabadiliko NO MORE POROJO!
 
kweli hii nchi imesha laaniwa muda mrefu kwa hiyo hakuna jinsi safari ni ndefu sana ya kukomboa nchi hii
 
kweli safari ndefu sana maana nchi hii kuna mengi sana angalia kwenye ubwabwa hapo juu hao watoto ndio wanatoa udenda juu ya punga hapo unategemea nini si rahisi na nirahisi kujinasua tukiwa serious
 
attachment.php

attachment.php


Yaani hizi picha mbili zimenichekesh mpaka basi, huu ndiyo haswaa uungwaji mkono wa CCM!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
kwani hujui kama wasukuma ukiwapa ubwabwa kama huo na maandazi umemaliza kula ni issue kanda ya ziwa, yaani wanapenda sana kula ndio shida yao kubwa na mlo ndio njia peekee ccm wanaisjua na wanaitumia hasa tabora uelewa wao bado ni mdogo sana.
 
ccm ccm ccm

attachment.php

Huu ni uzalilisahi wa wazi kabisa kwa WATU WA IGUNGA kuwahonga chakula!!! Jambo ambalo ni dhahiri hapa ni kwamba hii ndiyo style ya CCM kufanya kampeni. Hapa ni RUSHWA YA UBWABWA!! Bado kuna
Code:
[COLOR=#008000][B][I]RUSHWA YA PESA,VITENGE/KHANGA,T-SHIRT na KOFIA. 
[/I][/B][/COLOR]

Tunaomba TAKUKURU wafanye kazi yao. Ushauri kwa Wana-IGUNGA msikubali kuhongwa pilau/ubwabwa au khanga/vitenge au kofia/t-shirt! Haiwezekani CCM wanunue HAKI yenu ya kikatiba kwa vitu hivyo vyo muda. Je,CCM wanataka kuwaambia kuwa nyie hamna uwezo wa kula pilau/wali majumbani kwenu?Najua wana-Igunga ni wakulima hodari wa mpunga na mazao mengine.
Msikubali CCM kununua utu wenu kwa pilau.
 
Hii sio hoja ya kujadiliwa na watu wazima hapa, mrusha thread nenda facebook kwa watoto wenzako haraka, "If you have nothing say nothing"

We unayejiita MKUUWAKAYA nafikiri we ndio mtoto usiyeweza kujua hata nini unafanya...yani kutoa tu hiyo comment tayari umejadili...ungekuwa mtu mzima ungekaa kimya kabisa, ukue basi mana utoto wako wa facebook huku ndio hatuutaki kabisa, sawa bwana mdogo...!
 
Tatizo kubwa la wananchi wengi 'hawajitambua' na hata wakisaidiwa 'kujitambua' hawataki kujitambua,nawapa heko sana viongozi wa upinzani kwa kuwa na moyo wa kujituma,sasa ubwabwa wa mara moja unatoa kura?..naamini kazi ya siasa ya upinzani ni wito wa ajabu..
 
Jamani CCM tumewazoea hujibu hoja humu JF kwa matusi mazito na sio hoja zilizokwenda chuo. Wengi wao vilaza wametumwa na wanatekeleza kwa kukidhi njaa ambayo wameandaliwa na CCM ili watumike baadaye.
 
CCM waliandaa wazingira ya ushindi tangu muda kwa kuwaandalia watanzania mazingira ya umaskini ili kwenye uchaguzi wawahadae watanzania kwa pilau/ubwabwa kwa vile hata mlo mmoja kwa kutwa ni mtihani, kugawa kofia na fulana(bila suruali au kaptula) bure, kuwabeba vizee, akinamama na watoto kwenye malori(ya kubebea mchanga) kuwapeleka kwenye mikutano ya kampeni kwa vile hata baiskeli hawana matarajio ya kununua. Kugawa chumvi na dagaa, kugawa visenti(sio kama vya Chenge). Hivyo kazi mnayo "magwanda" kuwang'oa "magamba". Nimeitoa kiwepesi ili kuua soo au mnasemaje?

watanzania inatakiwa waamke, huu si wakati wa kuhongwa kwa chumvi na dagaa ambayo itawagharimu kwa miaka mitano.
Nakumbuka sana kuna wakati nilikuwa Maeneo ya Ngaramtoni, raia moja alimwuliza mbunge wa Arumeru Magharibi wa wakati ule Elisa Mollel, kuwa aliwaahidi kuwa ataleta maendeleo Ngaramtoni vipi mbona kimya ni miaka mitano inaisha? Elisa alimkemea kwa nguvu, akamwambia yule mpiga kura kuwa tena wewe usiulize kitu chochote, kwani kura yako nilikulipa!
 
kumbe kampeni zinaendana na chakula au ni sehemu ya shukran?/?
 
Kitendo cha CCM kumpeleka rais mstaafu wa awamu ya tatu Igunga kwaajili ya uzinduzi wa kampaini za uchaguzi mdogo unaotarajiwe kufanyika mapema mwezi ujao, kimetafsiriwa na wengi kuwa ni ushahidi tosha unaothihirisha ni kwa kiwango gani chama hicho hivi sasa kinavyokabiliwa na uhaba wa watu wenye mvuto katika jamii. Ni ukweli husiyo na shaka lolote ya kuwa machoni mwa watanzania wengi wa hali za kawaida Mkapa anahusihwa na kuporomoka kwa maadili katika jamii na mshikamano wa kitaifa. Sera zake zaq uchumi, ambazo nchi za magharibi zinamsifia, zimejenga ufa mkubwa kati ya wachache walionacho na wengi wa watanzania hoe hai. Aidha zimechochea uporaji mkubwa wa rasilimali ya taifa. Hivyo machoni mwa watu wengi rais mstaafu Mkapa ni kuhadi wa ubepari
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom