Uchaguzi kwenye taasisi una kanuni na taratibu zake, Ni jambo nyeti. Huweza sambaratisha tasisi. Jee alichofanya Lissu ni sahihi?

Uchaguzi kwenye taasisi una kanuni na taratibu zake, Ni jambo nyeti. Huweza sambaratisha tasisi. Jee alichofanya Lissu ni sahihi?

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Uchaguzi wa viongozi wa vyama vya siasa na wale wa serikali una sheria, kanuni na taratibu zake ambazo zisipozingatiwa huweza kusababisha vurugu na kusambaratisha chama au nchi.

Kwa ujumla taratibu ziko hivi:

1. Siku na mwezi wa uchaguzi hujulikana mapema. Ni miaka mitano baada ya uchaguzi uliopita.

2. Siku au wiki chache kabla ya tarehe ya uchaguzi kwenye vyama vya siasa na serikali za mitaa fomu hutolewa kwa wale walio na nia ya kuwa wagombea. Watajaza fomu hizo na kuzirudisha kwenye mamlaka husika.

Mamlaka husika huzichakata fomu hizo na kwa wale watakaokubaliwa ndio watakaotangazwa na mamlaka kama "Watia nia" aka wangombea. Kwa uchaguzi mkuu wa serikali muda huu huwa mwezi mmoja au zaidi kidogo.

Huwezi tu mtu ukakurupuka kutoka huko ulikotokea, tena wakati wo wote na kujitangaza mwenyewe kuwa wewe ni mtia nia au mgombea wa kiti fulani kwenye chama chako.

Ingalikuwa hivyo basi tungalikuwa na maelfu ya watu wanaogombea kiti kimoja. Mtu yo yote anaruhusiwa na ni haki yake ya kutia nia, ie kujaza hiyo fomu ya kuomba kuwa mgombea kiti cho chote. cha kisiasa kwenye chama na serikali. Ni job application. Sasa ni kitu ambacho hakiwezekani (common sense) kwamba wapiga kura wakapelekewa maelfu ya majina kwa kila kiti wakayapigie kura. Lazima kuwe na mamlaka ya kuyapunguza (kuyakata) kubaki mawili hadi matano.

Kwani nani hapendi kuwa Raisi wa nchi au Mwenyekiti wa chama cha siasa?

3. Baada ya mamlaka husika kuchagua wagombea wa hivyo viti ndipo wagombea hao hupewa kipindi fulani cha kujitangaza, kufanya kampeni kwa wapiga kura. Kwa vyama vya siasa na s/mitaa kipindi hiki huwa ni kifupi tu cha siku au wiki chache tu kabla ya kupigiwa kura za uchaguzi.

Sasa hiki alichofanya Tundu Lissu ni sahihi kweli? Yeye ghafla kaitisha mkutano wa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama chake, kwenye ukumbi wa gharama kubwa wa Mlimani City na kujitangaza kwamba yeye ndiye mgombea wa kiti cha Mwenyekiti. Kafanya kampeni yake kwa wajumbe hao wa mkutano mkuu wa uchaguzi uliotangazwa na vyombo mbali mbali vya habari alivyo kuwa amevialika. Gharama zote: za usafiri, accommodation, perdiem, ukumbi etc kazilipa yeye kwa fedha alizochangiwa na akina Robert Amsterdam!

Mbaya zaidi katika kampeni yake hiyo kakivua nguo chama chake na Mwenyekiti wake wa sasa. Yaani kakitukana, kakifedhehesha mbele ya umma hadi umma hauna hamu nacho tena.

Kakisambaratisha vibaya, Kakitwanga na kukiacha mahututi. Yaani kumbe Mbowe alikuwa akikiendesha chama hicho kidikiteta? Maamuzi ya vikao mbali mbali ya chama tuliyokuwa tunaambiwa kumbe yalikuwa ni ya Mbowe pekee? Tundu Lissu kakichafua sana chama chake.

Sasa mtu unabaki unajiuliza: Itakuwaje kama mamlaka husika ya chama ikikata jina lake kuwa mgombea wa kiti hicho? Itakuwaje hata kama mamlaka ikapitisha jina lake kuwa mgombea lakini kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama akishindwa na Mbowe? Ataweza kubaki kwenye chama hicho kweli? Ndiyo maana kanuni na taratibu za kampeni za uchaguzi zinakataza kuchfuana. Sasa huyu anachafua hadi chama chake.

Mamlaka za chama zikiamua kumfukuza kwenye chama ataenda wapi? CCM au ACT kwani kuanzisha chama chake Jaji Mtungi hatakubali kwani anamfahamu busara zake.

Kwa nini hakufuata busara za Msigwa? Alitakiwa kuondoka kwanza kwenye chama hicho ndipo ayaseme hayo aliyoyasema kwenye huo mkutano. Au angalifuata busara za Lowasa za kusubiri kuenguliwa na kufanya alichofanya.

Ngoja tusubiri. Ngoma inaweza kuwa tamu kuliko ile ya Lyatonga Mrema enzi zile alipokuwa NCCR - Mageuzi.
 
Kitendo cha Mbowe kuhodhi Madaraka kwa miaka 20 na bado haonyeshi dalili za kuachia ndicho kinachopelekea yote hayo.
Mbowe alitakiwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa kung'atuka kwa maslahi mapana ya chama.
Kahodhi madaraka kwa vipi wakati kila miaka mitano vikao halali vya chama vilikuwa vinamchagua kuwa mgombea wa kiti hicho na mkutano mkuu halali wa chama kupmpigia kura ya siri na kushinda. Tundu Lissu ni mmoja wa waliokuwa wanampigia kura hizo za ushindi. Hakuna aliyelalamika kuwa alikuwa anaiba kura wala kulikuwa na kura feki na kadhalika.
 
Inyeshe tu tujue panavuja wapi.

Mbowe alitakiwa kujifunza somo la kung'atuka kwa Nyerere muda mrefu sana.
Katiba yao haina time limit wala mambo ya kung'atuka. Take from me atakayeng'atushwa ni Tundu Lissu mwanaharakati na kibaraka wa mabeberu
 
When you discussed about politics I can see you as stupid just leave your life remember "POLITICS ITS A DIRTY GAME"
Ongea tu kiswahili, hiyo lugha nyingine huiwezi. Labda mwombe Erythrocyte akusaidie.
 
Kahodhi madaraka kwa vipi wakati kila miaka mitano vikao halali vya chama vilikuwa vinamchagua kuwa mgombea wa kiti hicho na mkutano mkuu halali wa chama kupmpigia kura ya siri na kushinda. Tundu Lissu ni mmoja wa waliokuwa wanampigia kura hizo za ushindi. Hakuna aliyelalamika kuwa alikuwa anaiba kura wala kulikuwa na kura feki na kadhalika.
Ni kweli walikuwa wanamuunga mkono, sasa wameshamchoka.

Muda umefika, Mbowe atumie busara kujiweka kando kunusuru chama.
Miaka yake 20 inatosha, aliyoyafanya yameonekana awaachie wengine waendeleze alipoishia.
 
Katiba yao haina time limit wala mambo ya kung'atuka. Take from me atakayeng'atushwa ni Tundu Lissu mwanaharakati na kibaraka wa mabeberu
Kufanya kitu sahihi si lazima ulazimishwe na katiba.

Hata Nyerere alivyong'atuka urais, hakulazimika kung'atuka kwa sababu ya katiba. Katiba ilikuwa inamruhusu aendelee urais.

Si hivyo tu, wananchi wengi walikuwa bado wanamtaka Nyerere awe rais. Lakini akakataa kuendelea, akang'atuka. Hakuendelea urais kwa kusema katiba inamruhusu.

Kwa nini?

Alifanya vile kwa busara zake tu. Aliona kawa rais muda mrefu zaidi si vizuri, aliona awaachie wengine waendeleze kazi.

Kwa hiyo hoja ya "katiba yao haina kung'atuka" ni hoja mufilisi.

Ama kukaa madarakani mtu mmoja muda mrefu ni kitu kibaya, ama kukaa madarakani mtu mmoja muda nrefu si kitu kibaya. Regardless ya katiba inasema nini.

Mimi mpaka sasa nipo kwa Mbowe aliyekaa kwenye uenyekiti muda mrefu bila ya kuwa na chochote cha maana cha kuonesha. Kwa Lissu sijafika kwa sababu sina nia ya kufanya hiki suala kiwe la ligi ya Mbowe na Lissu. Inawezekana kabisa Mbowe akatolewa na mtu mwingine kabisa ambaye hata si Lissu akaongoza chama. Kuna watu tofauti na Mbowe na Lissu watagombea uenyekiti, so in principle, this is not a strictly Mbowe vs. Lissu race.

Mbowe natakiwa ajiondoe mwenyewe wakati bado anaheshimiwa kabla hajaondolewa kama Nicolae Ceausescu kwa kuvunjiwa heshima zote.
 
Hahaha Lisu huyu hawezi kuivusha CHADEMA, analia lia sana.

Alipewa TLS ikamshinda, hakufanya chochote, leo anaitaka CHADEMA bila Mbowe mtaja kusema humu humu kwamba anahujumiwa na Mbowe, lakini ukweli ni kwamba CHADEMA Lisu anaweza kelele tu lakini hawezi na hana uwezo kuendesha chadema.

CHADEMA siyo shule kwamba yeyote anaweza kuwa mwalimu mkuu, CHADEMA ni Tanzania, huwezo huo LISU hana jamani.
 
Uchaguzi wa viongozi wa vyama vya siasa na wale wa serikali una sheria, kanuni na taratibu zake ambazo zisipozingatiwa huweza kusababisha vurugu na kusambaratisha chama au nchi.

Kwa ujumla taratibu ziko hivi:

1. Siku na mwezi wa uchaguzi hujulikana mapema. Ni miaka mitano baada ya uchaguzi uliopita.

2. Siku au wiki chache kabla ya tarehe ya uchaguzi kwenye vyama vya siasa na serikali za mitaa fomu hutolewa kwa wale walio na nia ya kuwa wagombea. Watajaza fomu hizo na kuzirudisha kwenye mamlaka husika.

Mamlaka husika huzichakata fomu hizo na kwa wale watakaokubaliwa ndio watakaotangazwa na mamlaka kama "Watia nia" aka wangombea. Kwa uchaguzi mkuu wa serikali muda huu huwa mwezi mmoja au zaidi kidogo.

Huwezi tu mtu ukakurupuka kutoka huko ulikotokea, tena wakati wo wote na kujitangaza mwenyewe kuwa wewe ni mtia nia au mgombea wa kiti fulani kwenye chama chako.

Ingalikuwa hivyo basi tungalikuwa na maelfu ya watu wanaogombea kiti kimoja. Mtu yo yote anaruhusiwa na ni haki yake ya kutia nia, ie kujaza hiyo fomu ya kuomba kuwa mgombea kiti cho chote. cha kisiasa kwenye chama na serikali. Ni job application. Sasa ni kitu ambacho hakiwezekani (common sense) kwamba wapiga kura wakapelekewa maelfu ya majina kwa kila kiti wakayapigie kura. Lazima kuwe na mamlaka ya kuyapunguza (kuyakata) kubaki mawili hadi matano.

Kwani nani hapendi kuwa Raisi wa nchi au Mwenyekiti wa chama cha siasa?

3. Baada ya mamlaka husika kuchagua wagombea wa hivyo viti ndipo wagombea hao hupewa kipindi fulani cha kujitangaza, kufanya kampeni kwa wapiga kura. Kwa vyama vya siasa na s/mitaa kipindi hiki huwa ni kifupi tu cha siku au wiki chache tu kabla ya kupigiwa kura za uchaguzi.

Sasa hiki alichofanya Tundu Lissu ni sahihi kweli? Yeye ghafla kaitisha mkutano wa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama chake, kwenye ukumbi wa gharama kubwa wa Mlimani City na kujitangaza kwamba yeye ndiye mgombea wa kiti cha Mwenyekiti. Kafanya kampeni yake kwa wajumbe hao wa mkutano mkuu wa uchaguzi uliotangazwa na vyombo mbali mbali vya habari alivyo kuwa amevialika. Gharama zote: za usafiri, accommodation, perdiem, ukumbi etc kazilipa yeye kwa fedha alizochangiwa na akina Robert Amsterdam!

Mbaya zaidi katika kampeni yake hiyo kakivua nguo chama chake na Mwenyekiti wake wa sasa. Yaani kakitukana, kakifedhehesha mbele ya umma hadi umma hauna hamu nacho tena.

Kakisambaratisha vibaya, Kakitwanga na kukiacha mahututi. Yaani kumbe Mbowe alikuwa akikiendesha chama hicho kidikiteta? Maamuzi ya vikao mbali mbali ya chama tuliyokuwa tunaambiwa kumbe yalikuwa ni ya Mbowe pekee? Tundu Lissu kakichafua sana chama chake.

Sasa mtu unabaki unajiuliza: Itakuwaje kama mamlaka husika ya chama ikikata jina lake kuwa mgombea wa kiti hicho? Itakuwaje hata kama mamlaka ikapitisha jina lake kuwa mgombea lakini kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama akishindwa na Mbowe? Ataweza kubaki kwenye chama hicho kweli? Ndiyo maana kanuni na taratibu za kampeni za uchaguzi zinakataza kuchfuana. Sasa huyu anachafua hadi chama chake.

Mamlaka za chama zikiamua kumfukuza kwenye chama ataenda wapi? CCM au ACT kwani kuanzisha chama chake Jaji Mtungi hatakubali kwani anamfahamu busara zake.

Kwa nini hakufuata busara za Msigwa? Alitakiwa kuondoka kwanza kwenye chama hicho ndipo ayaseme hayo aliyoyasema kwenye huo mkutano. Au angalifuata busara za Lowasa za kusubiri kuenguliwa na kufanya alichofanya.

Ngoja tusubiri. Ngoma inaweza kuwa tamu kuliko ile ya Lyatonga Mrema enzi zile alipokuwa NCCR - Mageuzi.
Kweli CHADEMA ni chama kikubwa,imara na chenye nguvu na mshikamano mkubwa sana Tanganyika.. Yaani mpaka leo bado mijadala zinaendelea baada tu ya TAL kutangaza nia ya kugombea uenyekiti siku tatu zilizopita
Viva CHADEMA! Viva forever📌🤣💪🏿❤❤❤
 
Kufanya kitu sahihi si lazima ulazimishwe na katiba.

Hata Nyerere alivyong'atuka urais, hakulazimika kung'atuka kwa sababu ya katiba. Katiba ilikuwa inamruhusu aendelee urais.

Si hivyo tu, wananchi wengi walikuwa bado wanamtaka Nyerere awe rais. Lakini akakataa kuendelea, akang'atuka. Hakuendelea urais kwa kusema katiba inamruhusu.

Kwa nini?

Alifanya vile kwa busara zake tu. Aliona kawa rais muda mrefu zaidi si vizuri, aliona awaachie wengine waendeleze kazi.

Kwa hiyo hoja ya "katiba yao haina kung'atuka" ni hoja mufilisi.

Ama kukaa madarakani mtu mmoja muda mrefu ni kitu kibaya, ama kukaa madarakani mtu mmoja muda nrefu si kitu kibaya. Regardless ya katiba inasema nini.

Mimi mpaka sasa nipo kwa Mbowe aliyekaa kwenye uenyekiti muda mrefu bila ya kuwa na chochote cha maana cha kuonesha. Kwa Lissu sijafika kwa sababu sina nia ya kufanya hiki suala kiwe la ligi ya Mbowe na Lissu. Inawezekana kabisa Mbowe akatolewa na mtu mwingine kabisa ambaye hata si Lissu akaongoza chama. Kuna watu tofauti na Mbowe na Lissu watagombea uenyekiti, so in principle, this is not a strictly Mbowe vs. Lissu race.

Mbowe natakiwa ajiondoe mwenyewe wakati bado anaheshimiwa kabla hajaondolewa kama Nicolae Ceausescu kwa kuvunjiwa heshima zote.
Kwani Mwl alitawala miaka mingapi ?.
 
Uchaguzi wa viongozi wa vyama vya siasa na wale wa serikali una sheria, kanuni na taratibu zake ambazo zisipozingatiwa huweza kusababisha vurugu na kusambaratisha chama au nchi.

Kwa ujumla taratibu ziko hivi:

1. Siku na mwezi wa uchaguzi hujulikana mapema. Ni miaka mitano baada ya uchaguzi uliopita.

2. Siku au wiki chache kabla ya tarehe ya uchaguzi kwenye vyama vya siasa na serikali za mitaa fomu hutolewa kwa wale walio na nia ya kuwa wagombea. Watajaza fomu hizo na kuzirudisha kwenye mamlaka husika.

Mamlaka husika huzichakata fomu hizo na kwa wale watakaokubaliwa ndio watakaotangazwa na mamlaka kama "Watia nia" aka wangombea. Kwa uchaguzi mkuu wa serikali muda huu huwa mwezi mmoja au zaidi kidogo.

Huwezi tu mtu ukakurupuka kutoka huko ulikotokea, tena wakati wo wote na kujitangaza mwenyewe kuwa wewe ni mtia nia au mgombea wa kiti fulani kwenye chama chako.

Ingalikuwa hivyo basi tungalikuwa na maelfu ya watu wanaogombea kiti kimoja. Mtu yo yote anaruhusiwa na ni haki yake ya kutia nia, ie kujaza hiyo fomu ya kuomba kuwa mgombea kiti cho chote. cha kisiasa kwenye chama na serikali. Ni job application. Sasa ni kitu ambacho hakiwezekani (common sense) kwamba wapiga kura wakapelekewa maelfu ya majina kwa kila kiti wakayapigie kura. Lazima kuwe na mamlaka ya kuyapunguza (kuyakata) kubaki mawili hadi matano.

Kwani nani hapendi kuwa Raisi wa nchi au Mwenyekiti wa chama cha siasa?

3. Baada ya mamlaka husika kuchagua wagombea wa hivyo viti ndipo wagombea hao hupewa kipindi fulani cha kujitangaza, kufanya kampeni kwa wapiga kura. Kwa vyama vya siasa na s/mitaa kipindi hiki huwa ni kifupi tu cha siku au wiki chache tu kabla ya kupigiwa kura za uchaguzi.

Sasa hiki alichofanya Tundu Lissu ni sahihi kweli? Yeye ghafla kaitisha mkutano wa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama chake, kwenye ukumbi wa gharama kubwa wa Mlimani City na kujitangaza kwamba yeye ndiye mgombea wa kiti cha Mwenyekiti. Kafanya kampeni yake kwa wajumbe hao wa mkutano mkuu wa uchaguzi uliotangazwa na vyombo mbali mbali vya habari alivyo kuwa amevialika. Gharama zote: za usafiri, accommodation, perdiem, ukumbi etc kazilipa yeye kwa fedha alizochangiwa na akina Robert Amsterdam!

Mbaya zaidi katika kampeni yake hiyo kakivua nguo chama chake na Mwenyekiti wake wa sasa. Yaani kakitukana, kakifedhehesha mbele ya umma hadi umma hauna hamu nacho tena.

Kakisambaratisha vibaya, Kakitwanga na kukiacha mahututi. Yaani kumbe Mbowe alikuwa akikiendesha chama hicho kidikiteta? Maamuzi ya vikao mbali mbali ya chama tuliyokuwa tunaambiwa kumbe yalikuwa ni ya Mbowe pekee? Tundu Lissu kakichafua sana chama chake.

Sasa mtu unabaki unajiuliza: Itakuwaje kama mamlaka husika ya chama ikikata jina lake kuwa mgombea wa kiti hicho? Itakuwaje hata kama mamlaka ikapitisha jina lake kuwa mgombea lakini kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama akishindwa na Mbowe? Ataweza kubaki kwenye chama hicho kweli? Ndiyo maana kanuni na taratibu za kampeni za uchaguzi zinakataza kuchfuana. Sasa huyu anachafua hadi chama chake.

Mamlaka za chama zikiamua kumfukuza kwenye chama ataenda wapi? CCM au ACT kwani kuanzisha chama chake Jaji Mtungi hatakubali kwani anamfahamu busara zake.

Kwa nini hakufuata busara za Msigwa? Alitakiwa kuondoka kwanza kwenye chama hicho ndipo ayaseme hayo aliyoyasema kwenye huo mkutano. Au angalifuata busara za Lowasa za kusubiri kuenguliwa na kufanya alichofanya.

Ngoja tusubiri. Ngoma inaweza kuwa tamu kuliko ile ya Lyatonga Mrema enzi zile alipokuwa NCCR - Mageuzi.

Tunaomba utusaidie huo utaratibu ulioanisha upo kwenye Katiba au Sheria ipi ili tupate rejea
 
Kuna uwezekano Mbowe mwenyewe amempa baraka Lissu ya kutangaza nia.

Hilo la Lissu kuonekana kama anakosoa chama na uongozi wa sasa ni muhimu sana. Hata JPM na CCM kwa ujumla walifanya hivyo 2015.

Hapa majuzi tu Kamala Haris alifanya kosa kama hilo la kuogopa kumkosoa bosi wake kwenye uchaguzi wa Marekani, aliulizwa ni kitu gani atafanya cha tofauti na Joe Biden, akasema hakuna atakachofanya cha tofauti. Alisema hivyo kwa kutotaka kumkosoa bosi wake. Kosa kubwa.

Lazima uoneshe tofauti yako na waliopo sasa ili kuwapa sababu watu ya kukuchagua. Kama hauna cha tofauti utakachokifanya kwanini watu wakupigie kura? Si afadhali waendelee na huyohuyo aliyepo?
 
Wengi sisi ni wapenzi na washabiki wa Lissu, lakini kitendo chake cha kukisema chama hadharani si afya, kitendo cha kumshambuklia kiongozi wa taasisi hadharani si afya.

Lissu kashakosa maadili na nafikiri kaamua bila kufuata kanuni kwamba liwalo na liwe - kaamua kuisambaratisha CDM na msije mkashamgaa akasaidiwa na Msajili kumwomdoa Mbowe kama walivyofanya kwa NSSR Mageuzi. Mbatia aliondolewa kihuni kwa usaidizi wa Msajili.

CDM inatakiwa kiwa makini sana kwenye jambo hili vinginevyo tayari CCM itapenda kuweka mkono wake kumalizia kazi aliyoianzisha Lissu.

SI dhambi kutangaza nia lakini fuata taratibu basi na si kutangaza vita.
 
Back
Top Bottom