Uchaguzi kwenye taasisi una kanuni na taratibu zake, Ni jambo nyeti. Huweza sambaratisha tasisi. Jee alichofanya Lissu ni sahihi?

Taasisi kubwa kama CCM, CDM, ACT. Viongozi huwa hawachaguliwi ila wanaandaliwa, Nadhani Lisu amenusa harufu fulani kuwa yeye ahuyoko miongoni mwa Watu wanao andaliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama kwa hiyo anataka kutumia Force. Hii itamgharimu sana wala hiyo vita hataiweza. Pamoja na mapungufu yote aliyonayo Mbowe Lisu bado alipaswa amuheshimu Mbowe hata kwa unafiki, mbona amefanya hivyo kwa Mda mrefu, Lisu anajua madudu yote anayo yafanya Mbowe ndani ya Chama na yeye alikuwa anayamezea sasa iweje sasa akurupuke tu huko aliko toka na kuanza kumshutu mwenyekiti wake na viongozi wenzake hilo siyo sawa, kiongozi ni pamoja na kuwa na Roho ya uvumilivu na ustahimilivu bila kuchoka. Uwenyekiti wa taasisi kubwa hizo nilizozitaja, uongozi wake auji vup, vup tu unakuja kwa mipango ya mda mrefu. Tazama uongozi wa Magufuli, Haukuweza kudumu kwa mda Mrefu kwakuwa CCM walikuwa wamemuandaa Membe ndiye awe kiongozi lakini upepo ukabadilika katikati ya vikao ikabidi wamteue, Magufuli tazama jinsi alivyo tawala na kukanyaga kanyaga. Kwahiyo Lisu ajaribu kujituliza kwanza na wala asihame Chama kwasabu chama bado kinamuhitaji ila Mbowe tu na genge lake ndiyo hawamtaki kwa ajili ya mstakabali wa Maslahi yao, na kwakuwa hajajipanga na wenzake wameshajipanga yeye awe mpole tu.
 
Naona Sasa mmeamua ila upepo unawakataa
 
Alilishambuliaje chama?
 
Katiba yao haina time limit wala mambo ya kung'atuka. Take from me atakayeng'atushwa ni Tundu Lissu mwanaharakati na kibaraka wa mabeberu

Kibaraka wa mabeberu ni wewe na CCM yake.
 

Acha majungu. Lissu ndio alifanya watu wakaanza kufuatilia chaguzi za TLS mpaka Leo. Pamoja kwamba zilikuwa zinafanyika huko nyuma. Hilo tu ni impact.
 
Kwani Mwl alitawala miaka mingapi ?.
Alitawala miaka 24, lakini baba yako akifanya makosa na kujifunza kwamba alifanya vibaya unatakiwa ujifunze kwake usirudie makosa. Usitumie makosa yake kutaka kurudia makisa na wewe.
 
Haahaa juzi anasema Nyerere alikuwa eti ni mtumishi wa umma ndo maana alngatuka, nilishangaa Sana, kwani kiongozi wa chama sio wa umma?
Mbowe anavyozidi kuongea ndiyo anavyozidi kudhihirisha kuwa ana elimu ndogo.

Ule.msemo wa "Kaa kimya ili watu wasijue ujinga wako" unamhusu sana Mbowe.

Hili jambo la ujinga wa Mbowe lilikuwa linafichika kirahisi wakati anaisema serikali na CCM, kwani hapo huhitaji elimu kubwa kuisema CCM. Huhitaji mambo mengi ya nuance. Hata mjinga anaweza kusema tu "Katiba mpyaa, tume huruu, peopleees, power" akaonekana ana akili.

Lakini, ukija kwenye issue kama kutetea kukaa kwenye uenyekiti muda mrefu kwenye nchi ambayo Nyerere kashaweka somo na standard, mpaka tumejifunza neno "kung'atuka", Mbowe ameshindwa kujenga hoja za kimantiki kwa nini yeye abaki. Kasema, kawafokea watu, halafu baada ya kusema kwa mihemuko kaja Lissu kapanga maneno vizuri, kwa hoja, kabla.Lissu hajatangaza kugombea uenyekiti mimi nikasema hapa mbona Mbowe kaongea pumba halafu Lissu ndiye kaongea vizuri?
 
Hivi elimu ndogo ni hadi kiwango gani?
 
Ni kweli walikuwa wanamuunga mkono, sasa wameshamchoka.
Kumchoka kunaoneshwa kwenye sanduku la kura. Ukikionesha kwa mtindo aliofanya Lissu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu kwa chama na mwenyekiti wake. It is insubordination to Mr Freeman Mbowe. Hili halikubaliki, hatua kali za kinidhamu zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya Tundu Lissu.
Bw. Kiranga, jaribu kutofautisha Nyerere wa kabla ya uhuru na yule Nyerere wa baada ya uhuru.

Nyerere wa kabla ya uhuru aliacha kazi yake ya umma kama mwalimu wa sekondari huko Pugu, na kwenda kujiunga na chama cha siasa cha TAA ambacho baadaye kiliitwa TANU na yeye akawa mwenyekiti wake. Lengo la TANU lilikuwa ni kuung'oa utawala wa Muingereza ili Tanganyika ipate uhuru. Aliacha mshahara wake mzuri wa ualimu. Kazi ya uenyekiti wa TANU haukuwa na mshahara wo wote. Ilikuwa ni kazi ya kujitolea. Kazi hiyo ilitegemea michango ya matajiri wa wakati huo hususani akina Sykes na baba yake na Freeman Aikel Mbowe ambao walikuwa wanaharakati wa mbio hizo za kuleta uhuru. Hivyo katika mbio hizo huwezi ukaweka muda wa ukomo wa uongozi wala mambo ya kung'atuka.

Nyerere wa baada ya uhuru alichaguliwa kwenye utumishi wa umma kwenye ngazi ya uraisi wa nchi na amiri jeshi mkuu. Pia aliendelea kuchaguliwa na chama chake cha TANU kilichoitwa baadaye CCM kama mwenyekiti wake. Katiba na sheria za nchi na zile za TANU hazikuwa na kipengele cha ukomo wa kugombea nafasi hizo. Baada ya kushika nafasi hizo kwa miaka takribani 25 mfululizo, busara yake ikamuongoza kung'atuka na kuweka utaratibu wa kikatiba wa ukomo wa miaka 10 kwenye vyeo hivyo serikalini na kwenye chama chake cha CCM.

Lengo kuu la vyama vya siasa vya upinzani kama CHADEMA ni kuung'oa madarakari utawala wa CCM, kama ilivyokuwa lengo kuu la TANU kabla ya uhuru ie kuung'oa utawala wa Muingereza. Mbio au harakati zote za vyama vya upinzani ni hilo. Uongozi wake ni wa kujitolea. Uendeshaji wake unategemea michango ya wanachama wake. Utumishi wao hauna mishahara, tofauti na wengi wanavyofikiria. Inashangaza hadi watu wanararuana na wakati mwingine kuuana kugombea vyeo kwenye vyama hivyo? Jee sababu ni kwenda kudokoa au kuiba hiyo michango ya wanachama ya kuendeshea chama chao? Freeman Aikel Mbowe alizaliwa siku ya uhuru wa Tanganyika. Baba yake alikuwa kati ya wanaharakati waliochangia kwa hali na mali kumng'oa Muingereza. Hivyo uanaharakati huo wa Mbowe ni wa kuzaliwa na kulelewa nao.

Kipindi cha kampeni ni kipindi hatari sana. Ni kipindi cha kubomoana. Busara na taratibu zinawatakq wagombea wabomoane kwa staha. Ndiyo maana kwa kuzingatia athari zake, kipindi hicho hupangiwa siku au wiki chache tu kabla ya uchaguzi wenyewe. Ratiba lazima izingatiwe. Huwezi ukaanza kufanya kampeni kabla ya filimbi ya kuanza kampeni aka kubomoana haijapulizwa. Tundu Lissu kaanza kabla ya filimbi haijapulizwa. Tarehe ya uchaguzi wala bado haijapangwa. Inawezekana ikawa hata mwezi wa nne mwakani. Sasa ataendelea kubomoa kwa miezi yote hiyo kabla ya uchaguzi? Hadi siku ya uchaguzi si atakuwa amebomoa kila kitu?

Mwaka 2020 NEC TANZANIA yenyewe haikukata jina la Lissu kugombea urais sembuse hao viongozi wa CHADEMA ambao ni vibaraka wa CCM! Unaota ndoto mbaya sana, Amka!
NEC hupokea majina kutoka kwa vyama vya siasa, jina moja kwa kila chama kilicho na usajili kamili. Tundu Lissu hakupeleka jina lake mwenyewe huko NEC. Angalifanya hivyo halingalipokelewa. NEC haina ya kukata majina yaliyowakilishwa na vyama hali vya siasa.

Tunaomba utusaidie huo utaratibu ulioanisha upo kwenye Katiba au Sheria ipi ili tupate rejea
Kwa upande wa vyama vya siasa kasome katiba, kanuni na taratibu za kila chama ambazo huwa zimepitiwa na kukubaliwa na msajili wa vyama vya siasa kwa niaba ya serikali. Hizi zisipofuatwa msajili ana mamlaka ya kuwaadhibu wahusika.

Kwa upande wa uchanguzi wa serikali kasome katiba ya nchi, sheria na kanuni za uchaguzi

Sasa kwani kuna mtanzania ambaye halijui hilo? Chadema kwa upande wa Tanzania bara kwa sasa ndiyo chama cha upinzani chenye wanachama na washabiki wengi na kimeenea kote. Na aliyewezesha hili kutokea ni Freeman Mbowe kwa kuwapokea Edward Lowasa na Sumaye kwenye uchaguzi mkuu wa 2015.

Hivyo mitifuano ye yote kwenye vyama hivi viwili (CCM na CHADEMA) vinaweza kuleta athari kwa mtanzania yeyote, mwanachama na asiye mwanachama hususani kutekana na kuuana kwa sababu za kisiasa. Na kwa kiasi kikubwa vyama hivi vinaendeshwakwa pesa ya kodi zetu kupitia ruzuku ya serikali.

Huko tunakoelekea Tundu Lissu anaweza kuiua CHADEMA na kuiacha Tanzania bara kuelea kwenye utawala wa chama kimoja, kitu ambacho hakipendezi.
 
Ni kweli walikuwa wanamuunga mkono, sasa wameshamchoka.
Kumchoka kunaoneshwa kwenye sanduku la kura. Ukikionesha kwa mtindo aliofanya Lissu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu kwa chama na mwenyekiti wake. It is insubordination to Mr Freeman Mbowe. Hili halikubaliki, hatua kali za kinidhamu zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya Tundu Lissu.
 
Kama lengo kuu la chama cha siasa cha upinzani ni kuung'oa utawala madarakani kama unavyosema, Mbowe anatakiwa kujiuzulu uenyekiti kwa sababu ameshindwa kutimiza lengo hilo over and over again.
 
Kama lengo kuu la chama cha siasa cha upinzani ni kuung'oa utawala madarakani kama unavyosema, Mbowe anatakiwa kujiuzulu uenyekiti kwa sababu ameshindwa kutimiza lengo hilo over and over again.
Ukipewa wewe unaweza kutekeleza,ulichoandika hapa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…