Uchaguzi Rais 2015: Utabiri Wa Mshindi Baina ya CCM na CHADEMA

Uchaguzi Rais 2015: Utabiri Wa Mshindi Baina ya CCM na CHADEMA

Thanks kwa uzi huu Mchambuzi.

Nategemea pia utarudi na takwimu zilizonyambulika zaidi kwenda Ki- Wilaya.
Kwa mfano sidhani kama ni sahihi kuupa Mkoa wote wa Mbeya CHADEMA, huku wilaya kama ILEJE na CHUNYA zikiwa nyuma sana katika harakati hizi za mageuzi.
Takwimu hizi hazina maana kwa sasa kwa sababu nchi yetu haitumii UZITO WA MAJIMBO [electoral votes] katika kumchagua mtendaji mkuu wa nchi. Takwimu za Wilaya zitatoa picha halisi ya kura tarajiwa za CHADEMA na CCM.
Naunga mkono hoja Mkuu; Kama umekuwa unafuatilia mjadala, kuna changamoto kubwa kitakwimu kwani wengi wanajenga hoja kwamba kutumia matokeo ya 2010 sio sahihi kwani yalichakachuliwa; ingawa nakubaliana kimsingi na hoja hii, lakini kuna ushahidi tosha kwamba kuna baadhi ya sehemu matokeo hayakuchakachuliwa, kwa mfano rejea bandiko langu namba 99 lenye majibu yangu kwa MC;

Kinachoendelea sasa ni ujenzi wa takwimu from raw data, tukianzia na idadi ya waliojiandikisha kupiga kura 2010, lakini zoezi hili linakabiliwa na changamoto kubwa sana, ingawaje tukujitahidi tunaweza kuvuka kisiki hiki kwa mafanikio, hasa tukiwa makini katika kuja na vigezo na pia kutumia cross data nyingine mbalimbali; lakini changamoto ni kubwa, na EMT alizungumzia hili hapo awali;
 
Igunga cuf walikuwa na mtaji wa kura 11,000 kwenye uchaguzi mdogo miezi 18 baadae waliangukia pua kwa kupata kura ef 2,kwa hiyo kutumia takwimu z miaka mitano kufanya tathmini ya nchi ni kujidanganya
 
mkuu Mchambuzi.
asante kwa hizi statistics. good stuff for thought.

binafsi sina sababu au reference yoyote ya kuzipinga,so nimezifanyia analysis ndogo kama ulivyoziwasilisha.

for the sake of this argument therefor:
1/assume that votes zote 18M ni kati ya vyama hivi viwili tu
2/assume kwamba kwenye ngome yake chama husika kina votes 75% na kingine 25%
2/assume that kwenye sadakalawe kila chama kina 50% ya votes

CCM watapata 9,319,624 (52%) huku CHADEMA wakipata 8,695,043 (48%).

this means that uchaguzi wa 2015 utaamuliwa kwa very small margins which will be largely tactical-based.

Umenena mambo ya msingi sana; nipo njiani kuweka takwimu fulani (sio matokeo ya 2010) yakiambatana na hoja kadhaa kama jitihada ya kupelekea mjadala kwenye hatua nyingine muhimu; Vinginevyo hoja yako ya 'small margin' inasimama, na ndio maana nimekuwa nikisema kwamba iwapo Chadema hawatafanikisha kubadili kanuni ya mshindi ni mshindi ambayo ilipitishwa na bunge ili kuzuia aibu kwa CCM zanzibar dhidi ya CUF, CCM kupata 50.01% ya kura 2015, Chadema kupata kwa mfano 49.99% maana yake CCM ni mshindi; na CCM kupata asilimia hii ni rahisi sana, hata ikimsimamisha Sofia Simba, itapitwa kwa uhalali na mchana kweupe;

Bila ya kufanyia kazi kanuni hii, Chadema wanaweza kujimaliza kisiasa baada ya 2015 kwa sababu zifuatazo:

Kuna uwezekano wa Serikali ya mseto baina ya CCM na Chadema 2015, kwani ni kweli, ushindi wa CCM au Chadema utakuwa sio landslide; CCM wakiwaalika Chadema kwenye ndoa kama ile ya CUF na CCM Zanzibar, Chadema sidhani kama watakubali kwani walishaweka msimamo kupinga utaratibu huo bungeni; Kukubali itakuwa ni kula matapishi yake yenyewe; Lakini kukataa serikali ya umoja wa kitaifa itapelekea CCM kutumia mwanya huo na kuja na propaganda kwamba Chadema imekataa ridhaa ya watanzania 49.99% kutokana na ubinafsi n.k, na CCM ikihoji "Ni Chama gani kinataka kuvunja amani, CCM au Chadema?" Majibu ya wengo of course yatakuwa Chadema, kwani itaonekana wanataka winner to take it all, wakati haikushinikiza mabadiliko ya kanuni ya mshindi ni mshindi;

Ni muhimu Chadema wafanyie kazi kanuni hii ndani ya mwaka mmoja na wasisubiri katiba mpya, watumie bunge kupitia hoja binafsi; Kuna uwezekano majibu ya serikali yakawa kwamba tusubiri katiba mpya, lakini hili litakuwa kosa kwani kanuni ile ilibadilishwa bungeni kwa malengo ya kisiasa, haikupitia a referendum au kupitia maoni ya umma au vyama vya siasa;
 
;
Kwanza hapo kwa Dar es salaam umekosea sana aisee, hakuna ngome yenye nguvu kwa ccm km hii, Dar es salaam ina wenyewe mkuu, wengine wote wakuja tu.
Unaweza kufafanua au kujadili hoja yako kidogo mkuu ili tukupate sawa sawa? maana juhudi kubwa humu sasahivi ni pamoja na kufikia a consensus kuhusu suala la ngome;
 
MIMI NAOMBA TU KUJUA.MATOKEO YA KURA HIZI NDIO MTA CONLUDE KUWA CCM/cdm Itashinda uchaguzi 2015??
Maana JF ina Member takribani 97,3000 hawa ni wachache , na hakuna kumbukumbu za uwiano wa mtawanyiko wao na uwakilishi wao wa Tanzania nzima. na wengi wao wanauwezo wa kuwa na access ya Internet na ni wasomi na asilimia kubwa wanapatikana mjini tuu na ndio wengi wao hawaipendi ccm, Ingawa ukweli ni wapiga kura wengi ambao wako vijijini ambao ndio wengi ni tegemeo kubwa la ccm kwenye kura na hawana elimu kubwa ,umeme na access ya internet na wengi sio member wa JF.Msisahau pia viongozi wote waandamizi wa serikalini na familia zao lazima waipe kura ccm kulinda maslahi yao.Niondeleeni mashaka ya hizi findings kuwa reliable information to predict the victory of any party in the furthcoming election (2015!!!
Pamoja na ugumu wa zoezi hili, inatakiwa bado tupambane kiuchambuzi kwani tusipofanya sisi atafanya nani? CCM au NEC au Dr. Bana? nadhani tukiamua kuwekeza katika hili (hasa muda na mawazo), tutajenga mjadala mzuri sana ambao utatusaidia sana kuelewa dynamics kuelekea 2015 ni zipi, na variables gani ni muhimu kwa vyama na wapiga kura; kama alivyotamka EMT awali, pia hii itapanua sana elimu yetu ya demokrasia ambayo alone is a good thing;

Vinginevyo tumekubaliana kwamba hatutatumia takwimu za 2010 kama ndio primary data, hizi zitatumika marginally kujenga hoja za hapa na pale, hasa kwenye matokeo ya majimbo ambako hoja ya uchakachuaji haina mashiko sana; Tunajaribu kutengeneza data from the ground up kwa kukuna vichwa vyetu, hasa kwa kuanzia na raw data ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura, na pia mawazo very useful kwa mfano ramani aliyotoa bongolander kwenye bandiko namba 43 la uzi huu; Tunajua pia kwamba idadi ya wapiga kura itaongezeka katika kipindi hiki kuelekea 2015, lakini na tuta treat this accordingly kwani mjadala huu ni matarajio ya wengi kwamba utabakia hai kwa muda mrefu;
 


Does it mean Zitto is the reason why Kikwete (62.98%) Won Kura Za Kigoma Kaskazini Dhidi ya Dr. Slaa (30.66%)? Wapo wanaojenga hoja ya uchakachuaji katika hili lakini iwapo hizo hotuba za kampeni zina mashiko, basi ni ushahidi mzuri kwamba sio kila sehemu CCM ilichakachua matokeo; Hata Kwa Mbowe pale Hai, JK alimshinda Dr. Slaa kwa almost 30% kama kwa Zitto, na hawa wawili waliingia uchaguzi ule wakiwa ni viongozi wakuu wa kitaifa wa Chadema;

Kwa mfano:

Dr. Slaa alimbwaga Kikwete kwenye majimbo sita, huku mengi yakiwa ni ya wabunge wapya, na watu ambao hawakuwa wanasikika katika anga za siasa hata kupitia uongozi katika idara mbalimbali za Chadema; Majimbo hayo na wabunge hao ni kama ifuatavyo:

  • Kiwia, Ilemela, Dr, Slaa alimshinda Kikwete kwa karibia 2%;
  • Machemli ukerewe, Dr. Slaa alimshinda Kikwete kwa karibia 2%;
  • Lema, Arusha, Dr. Slaa alimshinda Kikwete kwa karibia 16%;
  • Sugu, Mbeya Mjini, Dr. Slaa alimshinda Kikwete kwa karibia 13%;

Hii ni aibu kubwa wa Mbowe na Zitto;

Zitto na Mbowe walikuwa ni wakongwe wa siasa tayari hivyo katika majimbo yao, ilitarajiwa wangempatia ushindi Dr. Salaa dhidi ya Kikwete kama alivyofanya mkongwe mwenzao Ndesamburo Moshi Mjini ambapo Dr. Slaa alimshinda Kikwete kwa karibia 12%;

Halima Mdee Kawe alipunguza sana ushindi wa JK,kwani JK alimshinda Dr. Slaa kwa kama 3%;
Mnyika, Ubungo pia, alipunguza sana ushindi wa JK, kwani JK alimshinda Dr. Slaa kwa kama 5%;

Silinde kule Mbozi West alikuwa ni mgeni sana lakini Dr. Slaa lost by margin ndogo kuliko kwa Zitto na Mbowe kwani Mbozi West, JK won by 27%;

Rev. Msigwa Iringa Mjini, pia alikuwa mgeni, na JK alimshinda Dr. Slaa kwa only 10%;

What does this tell us?
1. sio kila sehemu kura zilichakachuliwa, hivyo tukiwa makini, tunaweza kutumia sehemu ya takwimu za 2010 kupata mwanga fulani;
2. ni suala la Zitto na Mbowe; Charity begins at home, sasa kama hawawezi ku deliver kwenye kura za Urais majimboni kwao, wao wana hoja gani ya nguvu kwamba wataweza mbio za Urais?

Mchambuzi, ni sawa kabisa unachosema, uchakachuaji upo lakini sio pekee unaowapa ushindi CCM bali mbinu na udhaifu wa kimkakati wa wapinzani wao, CCM wanagombana sana kwenye chaguzi za ndani (CCM) lakini ikija kwenye swala la chaguzi za nje wanashirikiana sana.

ZZK ni mbunge pekee wa kuchaguliwa aliyepatikana kutoka Chadema kwa mkoa wa kigoma, bahati nzuri sana wapinzani (NCCR) waliochukua majimbo mengine. Lakini kama ambavyo ZZK aliweza kumsupport kafulila mpaka akafanikiwa, na alivyozunguka TZ kuwakampenia wagombea ubunge wengine, angeweza ku-influence kura za mgombea wake wa urais katika jimbo lake angalau ziendane na idadi ya kura za mbunge.

Kuhusu mbowe umenifumbua macho, nitafanya kaufatiliaji kangu mwenyewe nijue inawezekana Vipi Jimbo la mbowe JK alipata kura zaidi ya Dr. Slaa; hapo nilikuwa sijapagundua ila nitafuatilia angalau kwa jamaa zangu wa huko watanipa mawazo yao.

Wakati matokeo yanatolewa sehemu mbalimbali jimbo la kigoma kaskazini nilikuwa nashangaa, tofauti inakuwa kubwa sana kati ya Kura za mgombea ubunge wa Chadema na mgombea urais wa chama chake. Ndio maana kwa chama kama chadema mwaka 2015 lazima wawe na team maalum na kubwa ambayo kazi yake ni kuzunguka mikoa mbalimbali kwa ajili ya kupiga kampeni za mgombea uraisi wa chama chao (of course na wabunge, lakini mgombea urais iwe kipaumbele), hawa miongoni mwao inabidi wawepo Viongozi wa juu wa chadema waachane na kugombea ubunge waki-support chama (kama kweli wana nia ya dhati ya mabadiliko). Kama swala ni human resources kwa sasa wanachama wenye uwezo ndani chama wako wengi, wachujwe na waandaliwe kwa ajili ya ubunge.

Kumbuka msimamo wa chadema na wananchi wengi ni kuwa Katiba mpya (kama kweli itapatikana kabla ya 2015) itamke kuwa mawaziri wasitokane na wabunge. Kwa hiyo asilimia flani ya Viongozi wa juu wa chama wajikite katika kampeni zinazomaanisha kushinda kiti cha uraisi na hivyo kuunda serikali.
 
Wakuu,

Nimeupenda mjadala huu. siasa za Tanzania zinabadirika sana. kuna rafiki yangu Diwani chama fulani aliniambia hivi'sism niwajanja.

hakasems mtaji wao ni pesa na propaganda chafu. nimi nimeliona hilo. Hila ninachojua M4C imekuwa mwiba kwao kwasababu inagusa watu wao-ignorant citizens. Ushauri wangu, kama nilivyoshauri pia kwenye threads zenye mlengo kama huu, nguvu yam4c izidishwe mara dufu kuelekea red na green no matter what kind of resistance you gone face.
Nadhani umuhimu wa M4C kwa chadema ni kutafuta kura za vijijini, huku wakizidi kulinda za mjini ambazo literally ni zao; Kwahiyo M4C needs to balance baina ya kutafuta kura za vijijini, na kulinda za mjini zisipotee; Moja ya Changamoto kubwa kwa Chadema katika hili ni kwamba Chama kimegeuka kuwa a Political Movement LATE; Ilitakiwa Chama kianze kama a political movement ili kujenga base ya uhakika, na baadae ndio kujikita zaidi kama Political party; TANU ilianza as a movement kwa muda mrefu (hasa kupitia TAA), na kilikuja kuwa chama cha siasa miaka michache tu kabla ya uhuru;

Umuhimu wa Movement ni kwamba watu wanakuwa loyal to the cause, ndio maana green parties kwa mfano katika nchi za wenzetu, they will always be loyal to the cause bila ya kujali siasa na propaganda kwani tayari wanajua wanataka nini - environmental sustainability; Chadema inataka nini in the long run? Bado wengi hatuna uhakika sana juu ya hilo, lakini in the short to medium term, tunajua lengo la Chadema ni kuiondoa CCM madarakani kutokana na ukweli kwamba CCM imeishiwa ubunifu wa kutatua matatizo ya wananchi; Lakini bado hatujajua kwa undani ubunifu wa Chadema ni upi, hasa ikizingatiwa kwamba Chadema wakiena Ikulu watakuwa wanatakeleza sera zile zile za uliberali, na ndio maana wahisani hawatokwi na jasho kujiuliza chama gani kitaenda ikulu, kikubwa ni vurugu zisitokee kwani zitaharibu interest zao kibiashara na kiuwekezaji; In the short to medium term, tunatarajia chadema ikulu ikitekeleza sera zile zile za CCM, tofauti ikiwa ni kwa ufanisi zaidi, hasa katika maeneo ya uwajibikaji, kuziba mianya ya rushwa, PENGINE KIDOGO utawala wa sheria na usimamizi mzuri wa rasilimali za taifa; nasema pengine kwa sababu hii itakuwa kazi ngumu; Vinginevyo, kuziba mianya ya rushwa, uwajibikaji na haya mengine hayatoshi kumletea maaisha bora mwanakijiji wa Tanzania;
 
MC,

Utakuwa umefanya jambo la maana sana kutupatia taarifa kuhusu nini kilitokea HAI; na kuhusu tofauti kubwa ya kura baina ya wabunge wa chadema na mgombea wao wa urais, katika mjadala wangu mwingine nilipata kuweka nadharia tete mbili kama njia ya kuamsha mjadala ili tukaribiane na jibu juu ya discrepancy hii; in general nilihoji, je, wapiga kura huwa na matarajio tofauti na mtu wanayemchangua kuwa mbunge wao tofauti na matarajio waliyo nayo kwa mgombea urais? Wananchi humpigia mgombea urais kura kwa msukumo gani? Je, kwa masuala yaliyo national zaidi? na ni yepi hayo? Na mbunge je, kwa masuala gani? masuala local zaidi? ni yepi hayo? kwa bahati mbaya mjadala ule haukuvutia wachangiaji wengi wenye hoja za maana;
 
Wakuu,

Kutokana na hoja za wachangiaji mbalimbali kama vile kutoka kwa bongolander, EMT, Zitto, Mimibaba, kwa kutaja wachache tu, kwamba tunahitaji a more realistic approach nimejaribu kutulia and dig out my brian ili kubaini njia nzuri ya kutufikisha tunapokusudia kufika; Nimefanikiwa angalau kukwangua ‘the surface' kwani hatua ya kuchimba shimo bado ipo mbali kidogo; Katika juhudi zangu mbalimbali, nikabaini kwamba matumizi ya takwimu za matokeo ya uchaguzi mkuu 2010 ni jambo lisilo epukika; However, sio takwimu za Urais kwani hizi zina mashaka ya uchakachuaji, bali takwimu za matokeo ya kura kwa wabunge, kwani licha ya mapungufu ya hapa na pale yaliyojitokeza maeneo kama Segera n.k, hizi kwa kiasi kikubwa takwimu za ubunge ni more reliable, na kama kuna tatizo la uchakachuaji, basi zitabadilika kwa Margin ndogo sana; Kabla sijaendelea, ni muhimu nikasema kwamba nimekuja na assumption moja muhimu that that should hold:

Ili kufanikiwa ushindi 2015, ni muhimu kwa Mgombea Urais wa Chadema akabebwa na Wabunge majimboni kwao kuliko kutumia mfumo wa sasa wa CCM ambao ulikuwa more effective chini ya Chama kimja na ambao kwa maajabu makubwa, bado unaendelea leo hii na kuigwa hata na Chadema na vyama vingine, yani - Mgombea Urais ndio mbeba Wabunge Majimboni; Iwapo this assumption holds, basi uchaguzi wa 2015, We should not expect a Discrepancy between kura za mbunge na Rais kama ilivyojitoeza 2010; Ni muhimu yaliyotokea kwa Zitto na Mbowe yasijirudie tena 2015 kwani bila ya hivyo, Chadema itakuwa na wakati mgumu wa kushinda kiti cha Urais;

Uchambuzi wangu wa takwimu za kura za wabunge 2010 umenipa picha ambayo sikuitarajia na ni tishio kwa Chadema tofauti na wengi wanavyodhania; Picha hii imenifanya nibadilishe kabisa mtazamo wangu juu ywa mikoa gani ni GREEN, BLUE na RED; Hoja za baadhi ya wachangiaji humu kwamba mkoa kama vile Dar-es-salaam sio BLUE bali GREEN, kumbe ni hoja yenye mashiko makubwa sana; Mbali ya Dar-e-salaam, Mkoa mwingine ambao wengi wetu hatukudhania ungekuwa GREEN au RED yani ARUSHA, pamoja na takwimu za marudio ya Uchaguzi wa Arumeru Mashariki mwaka huu (2012), bado Arusha sio BLUE bali ni GREEN; Sana sana ni RED, lakini BLUE? HAPANA; Nitajaribu kufafanua nimefikiaje findings hii kubwa na muhimu sana kwetu; Nitatumia mkoa wa Arusha kwa kuanzia na kuomba ridhaa yenu kama mnakubaliana na methodolofy niliyotumia ili kama tunafikia consensus, basi niendelee kwa mikoa iliyobakia ili tuweze kubaini wapi ni GREEN, wapi ni BLUE, wapi ni Sandakalawe;

Bongolander na wengine wachache walijadili hoja muhimu sana kwamba kura za mijini zio kigezo tosha kwamba Mkoa fulani ni ngome ya Chadema au CCM; Tutazame takwimu zifuatazo:

Kwa mujibu wa takwimu za Sensa za mwaka 2002, Arusha ina jumla ya watu 1,288,088; Hizi ni takwimu ya zamani, lakini kwa vile projections za population growth rate Tanzania zimeendelea kuwa takribani 3% kwa mwaka, ifikapo mwaka 2015, Arusha itakuwa na jumla ya wakazi karibia milioni 1.8; Nimepata takwimu hii kwa kuchukua 3% kwa mwaka (out of the 1.28 million population) mara miaka 13 i.e, na iwapo tutajumlishia ongezeko hili kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2015, tutapata takribani watu milioni 1.8 kama wakazi wa Arusha ifikapo 2015; Tofauti na matarajio ya wengi, kumbe Arusha ni mkoa muhimu sana kwani ukitazama jedwali kwenye bandiko namba moja la uzi huu, utaona kwamba Arusha haipo hata katika kumi bora in terms of idadi kubwa ya watu waliojiandikisha kupiga kura 2010, huku Arusha hiyo hiyo ikiwa sio tu kwamba ipo kwenye kumi bora, bali tano bora in terms of idadi ya watu miongoni mwa mikoa yote ya Tanzania;

This is a very important finding for vyama vyote vya siasa kwani takwimu za NEC zinaweza kuchuza, na kufanya vyama vya siasa viweke priority kwenye mikoa mingine na kupoteza ushindi; Finding hii emphasizes umuhimu wa chama kama Chadema kupitia m4c kuhakikisha kinajikita zaidi katika kuandikisha wapiga kura wapya badala ya kupoteza muda kugeuza wanachama wa CCM wahamie Chadema; Ukweli utaendelea kubakia kwamba – jumla ya wanachama wa CCM na Chadema haitafikia hata nusu ya jumla ya wapiga kura wa nchi nzima ifikapo 2015; Vinginevyo, mkoa kama Arusha utakuwa ni moja na mikoa muhimu sana kutupatia Rais mwaka 2015, hasa iwapo tuta acha kuchukulia takwimu za NEC juu ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura kama ndio takwimu mama; Ni muhimu kwa vyama vya upinzani kuhimiza wananchi wajiandikishe kupiga kura, na vyama hivi viweke malengo/targets kwa mizi sita/mwaka juu ya idadi ya wapiga kura wapya n.k, huku wakihakikisha wanalinda kura za wale wote wanaojiandikisha kuelekea 2015;

Takwimu nyingine muhimu kwa mkoa wa Arusha ni ile ya eligible voters ambayo EMT alijadili na kuniamsha kidogo juu ya umuhimu wa hili; Sasa naelewa kwanini EMT alijenga hoja kwamba Takwimu hii ni muhimu kuliko hata ile ya waliojiandikisha kupiga kura; Kwa mujibu wa findings zangu, 55% ya wakazi wa Arusha ni eligible voters, kwa maana kwamba wana umri kuanzia Miaka 15 na kuendelea (65+); tukumbuke kwamba watanzania wengi uanza kupiga kura wakiwa na umri wa miaka 15, licha ya sheria kutamka miaka 18; Kwa maana hii, ilipofika mwaka 2010, ambapo Arusha ilikuwa na idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura 723,874 kwa mujibu wa NEC, eligible voters ARUSHA walikuwa ni takriban 878,476 (nimepata takwimu hii kwa kutmia projections za 3% population growth per annum); Hii ina maana kwamba wakazi wa Arusha karibia 154,602 hawakujiandikisha kupiga kura 2010 licha ya kuwa eligible voters; Hii ni idadi kubwa sana, hasa ukizingatia kanuni ya sasa ya uchaguzi kwamba: MSHINDI NI MSHINDI;

Vile vile, kufikia Mwaka 2010, 41% ya eligible voters Arusha walikuwa na umri kati ya 15 na 39, huku 14% wakiwa na umri wa miaka 40 na kuendelea (65+); kwa maana hii, eligible voters chini ya miaka 40 walikuwa takribani 543,959, ambayo ni sawa na 75% ya idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura mkoani Arusha 2010, na eligible voters wenye umri wa miaka 40 na kuendelea (60+) walikuwa ni 185,742, ambayo ni sawa na 25% watu waliojiandikisha kupiga kura Mkoani Arusha; Kwahiyo, ifikapo 2015, karibia 75% ya wapiga kura watakuwa hawajavuka umri wa miaka 40; Takwimu hii inaendana na takwimu nyingine nyingi kwenye tafiti mbalimbali za ndani na nje ya nchi;

Tumalizie kwa kuangalia takwimu mbili za mwisho ambazo ni muhimu sana: Kwanza ni idadi ya watu kwa majimbo mkoani Arusha, na vile vile idadi ya watu katika majimbo ya CCM na Chadema;

Kati ya jumla ya majimbo SABA ya mkoa wa Arusha, CCM ina majimbo manne, na Chadema ina majimbo matatu; Tukianza na Majimbo ya CCM:

Wilaya Ya Monduli ambayo kiutawala imechanganywa na Longido, ina 15% ya total population ya mkoa wa Arusha; Ngorongoro ambayo pia ni Jimbo na wilaya, ina 11% ya total population ya Mkoa wa Arusha; Arumeru KIUTAWALA ni Wilaya, hivyo ina utata kidogo kwani ina majimbo mawili, huku kila chama (CCM na Chadema), kikishikilia jimbo moja; Nimejaribu kutatua utata huu kwa kufanya roundup/estimates; Arumeru kama wilaya ina takribani 42% ya wakazi wote wa Mkoa wa Arusha; Kwa vile jimbo moja la Arumeru (Arumeru Magharibi) ni la CCM huku lingine ni la Chadema, ili kurahisisha hesabu, tukigawanya 42% kwa majimbo mawili, ina maana kwamba kwa kukisia, Arumeru Mashariki na Magharibi kila moja ina takribani 21% ya jumla ya idadi ya wakazi wa mkoa mzima wa Arusha; Takwimu hii haipo mbali sana na ukweli kwani majimbo mawili ya Arumeru yote na karibia usawa in terms of maeneo ya urban, peri-urban and rural characteristics; Kwa maana hii, tukianza na majimbo ya CCM:

CCM inashikilia majimbo yenye karibia 47% ya wakazi wote wa Mkoa wa Arusha – Longido, Ngorongoro, Arumeru Magharibi na Monduli;
Na kwa Chadema:

Kwa maana hii, Chadema inashikilia Majimbo yenye karibia 53% ya wakazi wote wa Mkoa wa Arusha ambayo ni Arusha mjini, Karatu na Arumeru Magharibi; Swali linalofuatia ni Je, kwa maana hii Arusha ni Ngome ya uhakika ya Chadema?

Kwa mtazamo wa haraka haraka, hii inatosha ku conclude kwamba Arusha ni Ngome ya Chadema; Lakini picha hii inabadilika iwapo tutaangalia jumla ya idadi ya kura kwenye majimbo kwa CCM na Chadema;

Kwanza tutazame Jumla ya Kura za Ubunge katika Mkoa Mzima wa Arusha:

Kwa mujibu wa takwimu za NEC, jumla ya KURA zilizopigwa ngazi ya ubunge katika majimbo yote saba ya mkoa wa Arusha ni kura 368,128; takwimu hii ni inclusive na wapiga kura wapya katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki (2012), ambapo waliongezeka ingawa kwa idadi ndogo sana - kutoka 55,698 mwaka 2010 hadi 60,038 mwaka 2012;

Sasa ebu tutazame kila chama kilipata kura ngapi za ubunge mkoa mzima:

Tukianza na CCM, Jumla ya KURA ilikuwa ni 191,933 kati ya KURA 368,128 (sawa na 52%) ya kura za mkoa mzima wa Arusha, ngazi ya ubunge;

Kwa upande wa Chadema, jumla ya KURA ilikuwa ni 166,056 kati ya KURA 368,128 (sawa na 48%) ya kura za mkoa mzima wa Arusha ngazi, ya ubunge;

Swali linalofuatia ni je: ARUSHA NI NGOME YA CHADEMA?

Iwapo wengi wenu mnakubaliana na uchambuzi wangu, ARUSHA ni aidha GREEN au SANDAKALAWE;

Naombeni mawazo yenu juu ya methodology hii iwapo inafaa kutusaidia kubaini wapi ni GREEN, BLUE & RED, ili tuingia kwenye hatua zinazofuatia;

Pia naombeni mawazo yenu juu ya kigezo cha kutumia (in terms of percentage) kutaja kwamba hii au ile ni RED, BLUE au GREEN; Kuna wachangiaji wachache walikuja na namba hizo, lakini nadhani kigezo hiki kinaweza badilika, hasa kutokana na uchambuzi wangu huu;

Cc:jmushi1, blueray, companero, zitto, mwanamutapa, pasco, zenmoster, nguruvi3, jokakuu, jasusi, director, Africa-spring, for2015, MC, nasdaz, bongolander, EMT, kinenekejo, kagosaki, jujuman, gedeli, remmy; hawa ni wachangiaji ambao niliwasoma kabla ya kuingia mitamboni kuandaa bandiko hili; inawezekana wengine nimewasahau lakini haikuwa kwa nia mbaya;

Zitto, awali ulijenga hoja juu ya umuhimu wa kuja na scientific approach on this phenomenon, nimejaribu angalau to scratch the surface towards that end, nahitaji mawazo yenu katika kuboresha hili, ili tukifikia a consensus juu ya methodology, tutazame mikoa mingine kama Kigoma, Mwanza, n.k ambayo kwa mtazamo wa wengi, mikoa hii sio Green (CCM);

Nawasilisha;
 
Mchambuzi that is very interesting and insightful dig-out. Unajua suala la Arusha ni complicated kidogo, na sababu ni kuwa kuna factors nyingi sana zinaplay kwenye siasa za Arusha. Lakini generally unaweza kusema ARUSHA SI KIJANI, na sababu ni kuwa watu wa Arusha wana awareness kubwa sana ya mambo yanayoendelea nchini hasa ufusadi unaofanywa na wale walioko madarakani, kwa hiyo they are vigorously against. Wakazi wa Arusha ni watu ambao ni pro-wealth, kwa hiyo siku zote wanataka mtu ambaye atawasaidia kupata wealth, na watamchukia mtu ambaye ni fisadi na anayewafanya wawe maskini.

Lakini funny enough though kama huyo fisadi anawahonga na wanapata wealth, regardless of rangi yake anaweza kupata ushindi. I may be wrong on this, lakini kuna element fulani ya ukweli. A bit similar to Kilimanjaro. Huko huwezi kuwahonga watu kofia, kanga na pilau kushinda, kama kuhonga you have to do it big. This may not be intelligent observation, but for sure it is in play in Politics up there. Lakini vilevile ukiangalia utaona kuwa hata kielimu watu wa huko wamepiga hatua zaidi kuliko sehemu nyingine za Tanzania. Kwa hiyo candidate atakaye make sense on issues that are of concern to people watampigia kura huyo. Ukiangalia tangu tunze multiparty democracy watu wa Arusha ndio walikuwa wa kwanza kwanza kuembrace opposition party...kumbuka Makongoro Nyerere na Arusha mjini. Kwa sasa tunaweza kusema mwelekeo wa jumla wa Arusha ni blue.

Umeraise point moja nzuri sana kuhusiana na uwiano kati ya matokeo ya urais na ubunge. Hii imenikumbusha katika uchaguzi katika jimbo la Kenya. Pamoja na kuwa watu waliichukia sana CCM kutokana na ufisadi, hasa kutokana na mbunge wao Harrison Mwakyembe kuwagfahamisha first hand jinsi serikali inavyowahujumu watanzania, lakini CDM waliokuwa wanapresent kundi la kupinga ufisadi walikuwa na wakati mgumu kidogo, wapiga kura walimwambia wazi Dr Slaa kuwa tutakupa kura za urais lakini za ubunge tutampa Mwakyembe, Slaa alilazimika kumzika mgombea wake wa ubunge. In scenarios like this, it is hard to tell whether Kyela constituent is GREEN or BLUE, na hii si Kyela tu kuna majimbo mengi tu yana scenarios like this.

Kuna issue ya personalities ambayo ni kubwa na ina nguvu sana, ndio maana CCM hadi leo hawataki hata kidogo issue ya mgombea binafsi ifanye kazi licha ya kuwa halali kikatiba. Wabunge wengi ambao wako CCM kimaslahi na oppsition kiitikadi, wana uwezo wa kushinda ubunge without the backing of CCM, kama wakiwa independent candidates bila party affiliation.

Lakini factor hii kwa Zanzibar ni tofauti kabisa. Huko Zanzibar ukiitisha uchaguzi leo matokeo yanafanana kabisa na yale ya toka enzi za Sultan, Huko ni very clear kuwa ni Chama kinasimama na si mgombea. Kuna sehemu za pemba hata wakiweka jime limeandikwa CUF na mgombea wa CCM, jiwe litapigiwa kura, na Ungija kuna sehemu hata ukiwekwa mti umeandikwa CCM na mtu wa CUF mti unapigiwa kura. Huko ni rahisi sana kusema kuwa eneo hilo ni ngome ya chama fulani.

Kwa huku bara, CCM kuwa na wabunge wengi au madiwani wengi hakuna maana ya moja kwa moja wa wapiga kura wanakiunga mkono CCM, sababu kubwa ni personalities. Kwa sasa CDM as party wana momentums nzuri, that means kama wanweza ku-lure candidates wenye personality (including walioko CCM) wana easy ride ya kufanya sehemu kubwa ya ramaini ya uchaguzi iwe BLUE.

I still suspect kuwa si wazi sana kama CDM wanapata momemtum kutokana na kutangaza sera zao vizuri, ambazo ni tofauti na CCM, au kutokana na personality za wale walioko kwenye safu ya uongozi ya chama hicho.

Lakini kuchangia tu kutafuta approach inayofaa kujaribu kutabiri 2015 itakuwaje, tuangalie tabia za upigaji kura za watanzania na wasifu wa wapiga kura katika majimbo ambayo CCM, CDM na vyama vingine walikofanya vizuri

1. The more educated the people are, the blue they tend to lean. Ukiangalia mikoa ambayo CDM ilifanya vizuri, utaona kuwa ni mikoa yenye taasisi nyingi za elimu na watu wenye uelewa kiasi kuhusu siasa zetu. Kwa hiyo element ya elimu ni muhimu sana kwenye kudetermine kama mkoa, au jimbo ni BLUE au GREEN. Ukitaka kuangalia vizuri angalia kura zilizopigwa kwenye maeneo ya taasisi za elimu kama Chuo Kikuu unaweza kushangaa CCM inavyo-suffer.

2. Kiwango cha maendeleo ya kiuchumi- Ukiangalia maeneo ambayo watu wake wako bora zaidi kiuchumi unaweza kuona CCM inapata wakati mgumu kidogo na CDM wanapata urahisi kidogo, sababu sijui ni nini. Lakini vilevile hata baadhi ya sehemu ambazo ziko nyuma sana kiuchumi,(mfano Kigoma) watu ni anti-CCM sana, lakini hii haina maana kuwa ni blue, kwa hiyo factor hii inaenda pande zote mbili, integemea tu kampeni.

3. Lakini vile suala la demography- Hili umelieleza kiasi, lakini ukiangalia unaweza kuona watu wanaojua CCM imetoka wapi na ilifanya nini kwa nchi hii wanaimini sana. My grandparents are die hard supporters of CCM, mpaka leo huwezi kuwaambia kitu kuhusu CCM, wanaamini kuwa ilifanya kazi nzuri sana ila vijana wanaiharibu, wanatumai kuwa kikiongozwa vizuri kitabadilika na kuwa CCM wanayoifahamu. Kwa hiyo bado wanapigia kura CCM. Watu kama hao wamesambaa kila kona ya Tanzania, kwa hiyo most elderly are GREEN. Lakini wapiga kura wapya wengi ni pro CDM, kwa kuwa hawajui lolote kuhusu historia na hawajaona cha maana ilichofanya CCM. Ukiangalia wabunge kama yule wa wilaya ya mbeya mjini, utaona alishinda kutokana na demographic advantage.


Ukiangalia factor kama hizi unaweza kuona kuwa si rahisi kusema moja kwa moja mkoa huu ni blue, red, green au Islamist Naona kuna umuhimu wa kuangalia hata ripoti za sensa ili kujua hali ya population yetu kwa sasa tunaweza kupata insight ya kitakachotokea 2015.
 
Nimemaliza zoezi nililoanza na Arusha (rejea bandiko namba 109) na kubaini kwamba Chadema haina ngome hata moja Tanzania hata tukishusha criteria na ku-define ngome kama mkoa ambao chadema au CCM kimeshinda kura za ubunge hata kwa 55%; CCM kwa upande mwingine ina ngome chache, kwani hata tukiweka vigezo vya ngome kuwa 60-70% ya kura za wabunge kwa mkoa, CCM ina ngome kadhaa; Kwa ujumla wake, Chadema ina kazi kubwa sana bado ya kushinda popular votes uchaguzi wa mwaka 2015 kwani mikoa kadhaa ni GREEN huku mingine zaidi ikiwa ni RED leaning towards GREEN; Ningeweza kuwasilisha takwimu hizo humu lakini iwapo wadau watakubaliana na methodology yangu per post namba 109, kwani niliomba input and comment zao juu ya hili;

Key issue remains kwamba Chadema is running out of time kutengua kanuni ya mshindi ni mshindi kwani kama nilivyokwisha sema awali; Chini ya kanuni hii, hata Sophia Simba akisimamishwa na CCM dhidi ya Zitto, Lissu, Slaa etc, CCM kupata legit votes kwa 50.01% of votes ni rahisi sana, na hata Chadema ikipata 49.99%, kwa kanuni hii, CCM itakuwa ni mshindi; Kwa Chadema ushindi wake sana sana utakuwa ni uwezekano wa kualikwa na CCM kuunda GNU kama CCM na CUF Zanzibar; Changamoto kwa Chadema ni kwamba, wakikubali, watakuwa wamesaliti msimamo wao dhidi ya CCM na CUF, na hii itafungua mlango wa propaganda kutoka CCM etc kwamba Chadema wamekataa ridhaa ya watanzania 49.99% na ni chama chenye nia ya kuvunja amani; Chadema wakikubali kuunda GNU na CCM, its even worse kwani hoja yao bungeni dhidi ya ndoa baina ya CCM na CUF itajengewa propaganda na kuimaliza Chadema kisiasa;

Ni muhimu kwa Chadema na wapenzi wake kuweka focus kwenye kuvunja kanuni ya mshindi ni mshindi aidha kwa kupitia hoja binafsi bungeni, au maoni ya wananchi kwenye mchakato wa katiba, vinginevyo msishangae Chadema kumalizika kisiasa after 2015;
 
Bongolander,

Nakubaliana na hoja zako nyingi na za msingi sana kwenya bandiko namba 100 hapo juu; Ni kweli kwamba factors zinazo influence wapi ni green, blue, red ni pamoja na hizo tatu ulizojadili yani - Kiwango cha elimu kwenye population husika, Kiwango cha maendeleo/umaskini katika eneo husika, suala la demography characteristics, kama vile generational differences (youth vs elderly...), udini, lakini pia hapa ni muhimu tukaangalia ethnicity kwani hili nalo lipo sana;

Pamoja na jitihada kubwa ya Nyerere kuleta usawa katika Taifa, hata yeye aliwahi ku-admit kwamba hilo haliwezekani na akatolea mfano kwamba hata vidole vya mkono wake havilingani na kamwe havitolingana; baada ya Mwalimu kuondoka, lakini hasa kuuwawa kwa azimio la arusha, kumekuwa na sera za upendeleo ambazo zimeongeza regional imbalances (kimaendeleo), income inequality na inequality katika fursa za elimu na ajira; haya yamekuwa ni masuala ambayo chini kwa chini yanatumiwa na wanasiasa ili wapate support kutoka ukanda fulani au dini fulani; Tumeona madhara ya hili kwenye ngazi za ubunge na udiwani hasa vijijini, lakini hatupo mbali na madhara hayo kwenye ngazi ya urais;

Ningependa kusikia maoni yako juu ya hili: Je, pamoja na issues zote hizi, kwanini watanzania wengi, hasa vijijini wanachagua viongozi based on personalities kuliko issues?
 
[TABLE="width: 469, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD]MKOA[/TD]
[TD]IDADI YA WAPIGA KURA[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1[/TD]
[TD]ARUSHA[/TD]
[TD]723,874[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2[/TD]
[TD]DAR ES SALAAM
[/TD]
[TD]1,912,662[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3[/TD]
[TD]DODOMA
[/TD]
[TD]849,561[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4[/TD]
[TD]IRINGA
[/TD]
[TD]758,262[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5[/TD]
[TD]KAGERA
[/TD]
[TD]1,048,294[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]6[/TD]
[TD]KIGOMA
[/TD]
[TD]666,114[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]7
[/TD]
[TD]KILIMANJARO[/TD]
[TD]739,529[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]8
[/TD]
[TD]LINDI
[/TD]
[TD]450,620[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]9[/TD]
[TD]MANYARA
[/TD]
[TD]533,894[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]10[/TD]
[TD]MARA
[/TD]
[TD]752,906[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]11[/TD]
[TD]MBEYA
[/TD]
[TD]1,056,126[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]12
[/TD]
[TD]MOROGORO
[/TD]
[TD]988,113[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]13
[/TD]
[TD]MTWARA
[/TD]
[TD]658,220[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]14[/TD]
[TD]MWANZA
[/TD]
[TD]1,586,919[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]15[/TD]
[TD]PWANI
[/TD]
[TD]518,841[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]16[/TD]
[TD]RUKWA
[/TD]
[TD]489,289[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]17[/TD]
[TD]RUVUMA
[/TD]
[TD]607,920[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]18[/TD]
[TD]SHINYANGA
[/TD]
[TD]1,380,953[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]19
[/TD]
[TD]SINGIDA
[/TD]
[TD]545,074[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]20[/TD]
[TD]TABORA
[/TD]
[TD]840,014[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]21[/TD]
[TD]TANGA
[/TD]
[TD]891,942[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]22[/TD]
[TD]* ZANZIBAR
[/TD]
[TD]15,540[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD] JUMLA[/TD]
[TD]18,014,667[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


  • BLUE maana yake ni Ngome za uhakika za Chadema;
  • KIJANI maana yake Ngome za uhakika za CCM;
  • NYEKUNDU maana yake ni Mikoa ambayo hivi sasa ni 'Toss Up' au Sadakalawe;

Hivi kwa mgawanyo huo, hakuna uwezekano wa kuiga electoral college voting system ya Marekani?
 
Hivi kwa mgawanyo huo, hakuna uwezekano wa kuiga electoral college voting system ya Marekani?

Tungeweza kabisa lakini sidhani kama CCM watakubali kwani itakula zaidi kwao;
 
Bongolander,

Nakubaliana na hoja zako nyingi na za msingi sana kwenya bandiko namba 100 hapo juu; Ni kweli kwamba factors zinazo influence wapi ni green, blue, red ni pamoja na hizo tatu ulizojadili yani - Kiwango cha elimu kwenye population husika, Kiwango cha maendeleo/umaskini katika eneo husika, suala la demography characteristics, kama vile generational differences (youth vs elderly...), udini, lakini pia hapa ni muhimu tukaangalia ethnicity kwani hili nalo lipo sana;

Pamoja na jitihada kubwa ya Nyerere kuleta usawa katika Taifa, hata yeye aliwahi ku-admit kwamba hilo haliwezekani na akatolea mfano kwamba hata vidole vya mkono wake havilingani na kamwe havitolingana; baada ya Mwalimu kuondoka, lakini hasa kuuwawa kwa azimio la arusha, kumekuwa na sera za upendeleo ambazo zimeongeza regional imbalances (kimaendeleo), income inequality na inequality katika fursa za elimu na ajira; haya yamekuwa ni masuala ambayo chini kwa chini yanatumiwa na wanasiasa ili wapate support kutoka ukanda fulani au dini fulani; Tumeona madhara ya hili kwenye ngazi za ubunge na udiwani hasa vijijini, lakini hatupo mbali na madhara hayo kwenye ngazi ya urais;

Ningependa kusikia maoni yako juu ya hili: Je, pamoja na issues zote hizi, kwanini watanzania wengi, hasa vijijini wanachagua viongozi based on personalities kuliko issues?

Mchambuzi

Ukiangalia kwa undani utaona kuwa tatizo ni Stockholm syndrome kuna tatizo kubwa sana karibu katika kila pembe ya Tanzania. Sio kwenye siasa tu, ipo kwenye dini, michezo hata biashara. Bado captives hawajui kuwa wao ni wamoja, yaani victims, na adui yao au maadui wanaowagawa wao lengo lao ni moja tu, yaani kuwavuna.

Juhudi za Nyerere kuifanya Tanzania iwe nchi, na si collection of communities of people in Tanzania, sasa hivi zinafutwa kwa kasi sana, na hii ndio inaongeza Stockholm syndrome, which is of great benefit to corrupt politicians. Kwa hiyo la muhimu zaidi ni kuhakikisha kuwa watu wanatibiwa, yaani wawe na elimu ya kutosha kuhusu nchi yao, na kujua kuwa kumpa madaraka mwanasiasa anayewahonga ni kujimaskinisha zaidi, au kumuunga mkono mtu ambaye anataka kukugawa na mkristo, mwislamu au mpagani, basi ujue huyo hana maana, lakini bado watanzania wengi kidogo tuko mbali na hili, wengine wetu tunawathamini watu hao, kwa kununuliwa na pesa. Bado hatuwezi kujiangalia kama watanzania na kuangalia ni maswala gani yanatutatiza kama watanzania, we call ourselves Tanzanians, but the actual fact is we are trapped in a mindset of communities.
 
Back
Top Bottom