Uchaguzi TLS ulikuwa kati ya Sheria na utulivu wa nchi

Uchaguzi TLS ulikuwa kati ya Sheria na utulivu wa nchi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kuna wakati watanzania wa kawaida wanashindwa kuchagua kipi Bora kati ya Sheria kwa upande mmoja na amani na utulivu kwa upande wa pili. Mh. Mwabukusi, Rais mteule wa TLS anahubiri Sheria Sheria Sheria Sheria mwanzo mwisho kwenye taifa ambalo watu wake wanajiona kuwa wako huru, Wana amani na utulivu. Mwabukusi anataka kuwaambia watanzania kuwa hapanaaa, hamko huru, hamna amani na hamna utulivu twendeni tukatafute amani na utulivu kupitia TLS.

Kwa maoni yangu mm amani na utulivu wetu hautokani na Sheria peke yake, bali ni pamoja na utamaduni, mazoea, uvumilivu, woga, sera, hulka ya watanzania na sheria. Kama ingekuwa ni sheria tu basi Kenya wangekuwa na amani na maendeleo zaidi kuliko sisi. Sheria iko hata DRC, Ethiopia, Somalia, Sudan na Ukraine.

Twendeni polepole na hiki kilichopo ambacho kinatuhakikishia kuimaliza Leo yetu na kutufikisha kesho na keshokuta kuliko watu wa Congo, Sudan, Somalia au Palestine na Israel. Present is known and secure.

Watu wetu Bado ni maskini sana kiuchumi na kielimu, hakuna sheria na demokrasia inayoweza kufua dafu 100% katikati ya watu maskini, wajinga na wenye njaa. Lazima tuinue elimu yao na kuondoa njaa zao kwanza kabla ya kuwaletea demokrasia na Sheria. (Abram Maslow's)
 
Kuna wakati watanzia wa kawaida wanashindwa kuchagua kipi Bora kati ya Sheria kwa upande mmoja na amani na utulivu kwa upande wa pili. Mh. Mwabukusi, rais mteule wa TLS anahubiri Sheria Sheria Sheria Sheria mwanzo mwisho kwenye taifa ambalo watu wake wanajiona kuwa wako huru, Wana amani na utulivu. Mwabukusi anataka kuwaambia watanzania kuwa hapanaaa, hamko huru, hamna amani na hamna utulivu twendeni tukatafute amani na utulivu kupitia TLS.

Kwa maoni yangu mm amani na utulivu wetu hautokani na Sheria peke yake, bali ni pamoja na utamaduni, mazoea, uvumilivu, woga, sera, hulka ya watanzania na sheria.

Twendeni polepole na hiki kilichopo ambacho kinatuhakikishia kuimaliza Leo yetu na kutufikisha kesho na keshokuta kuliko watu wa Congo, Sudan, somalia au Palestine na Israel. Present is known and secure.

Watu wetu Bado ni maskini sana kiuchumi na kielimu, hakuna sheria na demokrasia inayoweza kufua dafu 100% katikati ya watu maskini, wajinga na wenye njaa. Lazima tuinue elimu yao na kuondoa njaa zao kwanza kabla ya kuwaletea demokrasia na Sheria. (Abram Maslow's)
Haki je?
 
Vipi kuhusu "HAKI" ?
Haki kubwa kuliko zote ni haki ya kuishi. Tanzania haki hiyo ipo kubwa sana. Nchi kubwa kama China yenye watu robo ya Dunia huwezi kuiendesha kwa demokrasia. Mtawala wao anawajibika kuwapa watu wake haki ya kuishi, kula, kuvaa na kulala. Nchi kama DRC, Kenya, Rwanda, Sudan, Ethiopia, somalia, south Africa na hata Uganda na Rwanda wanatamani hali yetu hiihii na hivihivi tulivyo Leo, Mwabukusi anaweza kutamani kuwaletea watu kiasi kikubwa cha demokrasia ya kufikirika TU ambayo haipo duniani kote. Wale wenzangu tulioishi nchi za magharibi tunajua kuwa hata huko hakuna demokrasia pana mno kwenye mambo serious ya nchi. Vijana wengi hasa wanaume wamejaa magerezani, akina Snowden wanasakwa wauawe.

Tusichague Sheria na demokrasia dhidi ya amani na utulivu.
 
Kuna wakati watanzia wa kawaida wanashindwa kuchagua kipi Bora kati ya Sheria kwa upande mmoja na amani na utulivu kwa upande wa pili. Mh. Mwabukusi, Rais mteule wa TLS anahubiri Sheria Sheria Sheria Sheria mwanzo mwisho kwenye taifa ambalo watu wake wanajiona kuwa wako huru, Wana amani na utulivu. Mwabukusi anataka kuwaambia watanzania kuwa hapanaaa, hamko huru, hamna amani na hamna utulivu twendeni tukatafute amani na utulivu kupitia TLS.

Kwa maoni yangu mm amani na utulivu wetu hautokani na Sheria peke yake, bali ni pamoja na utamaduni, mazoea, uvumilivu, woga, sera, hulka ya watanzania na sheria.

Twendeni polepole na hiki kilichopo ambacho kinatuhakikishia kuimaliza Leo yetu na kutufikisha kesho na keshokuta kuliko watu wa Congo, Sudan, Somalia au Palestine na Israel. Present is known and secure.

Watu wetu Bado ni maskini sana kiuchumi na kielimu, hakuna sheria na demokrasia inayoweza kufua dafu 100% katikati ya watu maskini, wajinga na wenye njaa. Lazima tuinue elimu yao na kuondoa njaa zao kwanza kabla ya kuwaletea demokrasia na Sheria. (Abram Maslow's)
Sheria ni nini na utawala wa sheria ni nini?
Demokrasia ni nini na utawala wa kidemokrasia ni nini?
Utawala bora ni ule unaotegemea mifumo bora inayofuatwa, au hulka za kiongozi aliyeko na ubora wake?
Amani ni nini? Maendeleo ni nini?

Ni nini sababu za vita Congo, Sudan, Somalia au Palestine na Israel?
 
Katika kada ambazo hazina manufas kijamii,moja wapo ni sheria.
Hata huko ambako Sheria, haki na demokrasia vinahubiriwa wanawasigina wapalestine hadi tone lao la mwisho. Jamii yenyewe itawapuuza akina mwabukusi mchana kweupe akiangalia kwakuwa hakuna mbadala wa amani na utulivu kwa mtu na taifa. Watu wanataka wapande treni yao ya umeme kwenda kwa shangazi zao.
 
Sheria ni nini na utawala wa sheria ni nini?
Demokrasia ni nini na utawala wa kidemokrasia ni nini?
Utawala bora ni ule unaotegemea mifumo bora inayofuatwa, au hulka za kiongozi aliyeko na ubora wake?
Amani ni nini? Maendeleo ni nini?

Ni nini sababu za vita Congo, Sudan, Somalia au Palestine na Israel?
Tundu Lissu kanusurika kufa lakini hakuna mwananchi aliyeandamana kupinga kitendo hicho cha kinyama. Hii inaonuesha kuwa wananchi wanazo shida zao nyingine kabisa na zile anazosema lisu na wenzake. Mbowe alikuwa mahabusu kwa zaidi ya miezi 6 hivi, lakini hakuna mwananchi aliyemwagika barabarani kupinga kitendo hicho. Hii ni kionuesha kuwa kile anachotetea sio kile kinachowasokota wananchi.
 
Hata huko ambako Sheria, haki na demokrasia vinahubiriwa wanawasigina wapalestine hadi tone lao la mwisho. Jamii yenyewe itawapuuza akina mwabukusi mchana kweupe akiangalia kwakuwa hakuna mbadala wa amani na utulivu kwa mtu na taifa. Watu wanataka wapande treni yao ya umeme kwenda kwa shangazi zao.
Hueleweki, Kwa hiyo unataka nini hasa Hadi kufungua Uzi huu? Kwa hiyo hutaki kabisa kusikia utawala wa Sheria nchi hii?
 
HAKI YA KUISHI: YUPO WAPI DAUDI MWANGOSI, AKWELINA, BEN SAANANE, AZORY GWANDA, MWIJABE WA WIZARA YA FEDHA N.K.....?

IPO WAPI TANGANYIKA? WATU MILIONI 60 WANATAWALIWA NA KUIBIWA NA WATU MILIONI MOJA!!!!!

GO MWAMBUSI, GOOOOO.....TUNAITAKA TANGANYIKA YETU.
 
Hueleweki, Kwa hiyo unataka nini hasa Hadi kufungua Uzi huu? Kwa hiyo hutaki kabisa kusikia utawala wa Sheria nchi hii?
Jamaa kaja kwa kukamia mno (ubaya ubwela), anakuja kupambana, anakuja kuwanyoosha, anakuja Sheria inatawala
 
HAKI YA KUISHI: YUPO WAPI DAUDI MWANGOSI, AKWELINA, BEN SAANANE, AZORY GWANDA, MWIJABE WA WIZARA YA FEDHA N.K.....?

IPO WAPI TANGANYIKA? WATU MILIONI 60 WANATAWALIWA NA KUIBIWA NA WATU MILIONI MOJA!!!!!

GO MWAMBUSI, GOOOOO.....TUNAITAKA TANGANYIKA YETU.
Mbona hata Trump alinusurika kufa, wewe unajua nani hao walitaka kumuua? Kule kwao mbona homeless wako wengi sana lakini serikali inasaidia homeless wa Tanzania na Ukraine? Kakaaaa!! sheria haiwezi kwenda peke yake na kuyaacha nyuma maendeleo na uchumi wa watu. Kuna watu walikuwa wanapinga ujenzi wa bwawa la mwl Nyerere, si ndiyo? Kuna watu wanapinga Kila kitu hata kuwasogeza watu Ngorongoro ili utalii ushamili si ndiyo? Kuna watu waliponga royal tour si ndiyo? Kuna watu waliponga upanuzi wa barabara kimara si ndiyo? Kuna watu hawataki kujengwe bomba la mafuta kutoka Uganda, si ndiyo? . Nchi itakwenda vipi?
 
Vipi kuhusu "HAKI" ?
Haki na wajibu kaka. Wanaolipa Kodi tz ni 10% ya watanzania wote. Nchi zilizoendelea huwezi kukuta watu wengi mitaani siku za kazi, lakini hapa kwetu mitaa yetu imefurika watu siku zote za wiki kwa mwaka mzima. Ni haki gani wanastahili kupiganiwa kwa nguvu zote na mwabukusi? Hapa kwetu ni sukuma liende Bora liende. Wale wamasai waliokuwa wameletwa Ngorongoro na wakoloni sio hawa wa sasa. Hawa wa sasa ng'ombe haziwatoshi Tena badala yake wanakula wanyamapori, ugali, ndizi, wali, wanauza pembe za ndovu, ni wanasiasa na wanajenga nyumba za matofali ya block. Ni watanzania sawa na watanzania wengine TU ambao wanapaswa kukaa mbali na mbuga zetu kama wengine TU.
 
Haki na wajibu kaka. Wanaolipa Kodi tz ni 10% ya watanzania wote. Nchi zilizoendelea huwezi kukuta watu wengi mitaani siku za kazi, lakini hapa kwetu mitaa yetu imefurika watu siku zote za wiki kwa mwaka mzima. Ni haki gani wanastahili kupiganiwa kwa nguvu zote na mwabukusi? Hapa kwetu ni sukuma liende Bora liende. Wale wamasai waliokuwa wameletwa Ngorongoro na wakoloni sio hawa wa sasa. Hawa wa sasa ng'ombe haziwatoshi Tena badala yake wanakula wanyamapori, ugali, ndizi, wali, wanauza pembe za ndovu, ni wanasiasa na wanajenga nyumba za matofali ya block. Ni watanzania sawa na watanzania wengine TU ambao wanapaswa kukaa mbali na mbuga zetu kama wengine TU.
Haki haihusiani na ulipaji kodi, hata hivyo kila raia nchi hii analipa kodi. Raia wote wananunua au kutumia sukari, chumvi na mafuta.
 
Haki kubwa kuliko zote ni haki ya kuishi. Tanzania haki hiyo ipo kubwa sana. Nchi kubwa kama China yenye watu robo ya Dunia huwezi kuiendesha kwa demokrasia. Mtawala wao anawajibika kuwapa watu wake haki ya kuishi, kula, kuvaa na kulala. Nchi kama DRC, Kenya, Rwanda, Sudan, Ethiopia, somalia, south Africa na hata Uganda na Rwanda wanatamani hali yetu hiihii na hivihivi tulivyo Leo, Mwabukusi anaweza kutamani kuwaletea watu kiasi kikubwa cha demokrasia ya kufikirika TU ambayo haipo duniani kote. Wale wenzangu tulioishi nchi za magharibi tunajua kuwa hata huko hakuna demokrasia pana mno kwenye mambo serious ya nchi. Vijana wengi hasa wanaume wamejaa magerezani, akina Snowden wanasakwa wauawe.

Tusichague Sheria na demokrasia dhidi ya amani na utulivu.
Vipi kuhusu demokrasia ya tume huru ya uchaguzi na uchaguzi huru na wa haki?
 
Haki kubwa kuliko zote ni haki ya kuishi. Tanzania haki hiyo ipo kubwa sana. Nchi kubwa kama China yenye watu robo ya Dunia huwezi kuiendesha kwa demokrasia. Mtawala wao anawajibika kuwapa watu wake haki ya kuishi, kula, kuvaa na kulala. Nchi kama DRC, Kenya, Rwanda, Sudan, Ethiopia, somalia, south Africa na hata Uganda na Rwanda wanatamani hali yetu hiihii na hivihivi tulivyo Leo, Mwabukusi anaweza kutamani kuwaletea watu kiasi kikubwa cha demokrasia ya kufikirika TU ambayo haipo duniani kote. Wale wenzangu tulioishi nchi za magharibi tunajua kuwa hata huko hakuna demokrasia pana mno kwenye mambo serious ya nchi. Vijana wengi hasa wanaume wamejaa magerezani, akina Snowden wanasakwa wauawe.

Tusichague Sheria na demokrasia dhidi ya amani na utulivu.
Kwani Sheria haileti amani kati ya mtenda na mtendewa?
 
Haki haihusiani na ulipaji kodi, hata hivyo kila raia nchi hii analipa kodi. Raia wote wananunua au kutumia sukari, chumvi na mafuta.
Ni nani atalinda haki akiwa na njaa? Hakimu ana njaa, mtunga Sheria ana njaa, polisi ana njaa na mhalifu ana njaa. Bila wajibu wa kufanyakazi na kulipa Kodi kutimizwa kwanza hakuna haki itakayolindwa. Sheria namba Moja ambayo TLS inatakiwa kulinda kwa nguvu zake zote ni ni kuhakikisha kuwa Kila mtu anafanyakazi , analipa Kodi na anaekula Kodi hiyo anahukumiwa opasavyo, nothing less nothing more than this.
 
M
Kwani Sheria haileti amani kati ya mtenda na mtendewa?
wenye njaa ataachaje kuiba hata kama anajua kufanya hivyo ni kinyume na Sheria? Anaeumwa je?;asiyekuwa na ada je? asiyekuwa na pakulala je? Asiyekuwa na nauli je?. TLS lazima ivae viatu vya wananchi na sio viatu vya wanasheria na wanasiasa wanaotafuta madaraka. Maana sisi sote tunajua kuwa hata aingie nani madarakani kama watu hawafanyikazi, wanakwepa Kodi, na masoko yamehodhiwa na mabeberu na uchumi wa Dunia unaendeshwa na IMF, WB hakuna atakachofanya zaidi ya kubadilisha wapigaji TU.
 
Back
Top Bottom