Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,306
Hongera kwa Biden. Vipi kuhusu madai ya kura kuibiwa, yana ukweli wowote?Biden rais USA, Trump hana chake tena, aendelee kwenda mahakamani tu.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera kwa Biden. Vipi kuhusu madai ya kura kuibiwa, yana ukweli wowote?Biden rais USA, Trump hana chake tena, aendelee kwenda mahakamani tu.
Mkuu sifikirii kama yana ukweli wowote kwa sababu Democrats waliwahimiza wanachama wao kupiga kura kutumia njia ya posta ambayo haiwafanyi kwenda kupiga kura siku ya uchaguzi na waliitikia hilo kutokana na ugojwa wa Corona. Trump yeye aliwahimiza wafuasi wake kwenda kupiga siku ya uchaguzi. Hata hivyo nampongeza sana kwa sababu sikutegemea kama Americans wengi wangempigia kura.Hongera kwa Biden. Vipi kuhusu madai ya kura kuibiwa, yana ukweli wowote?
Mkuu sifikirii kama yana ukweli wowote kwa sababu Democrats waliwahimiza wanachama wao kupiga kura kutumia njia ya posta ambayo haiwafanyi kwenda kupiga kura siku ya uchaguzi na waliitikia hilo kutokana na ugojwa wa Corona. Trump yeye aliwahimiza wafuasi wake kwenda kupiga siku ya uchaguzi. Hata hivyo nampongeza sana kwa sababu sikutegemea kama Americans wengi wangempigia kura.
Kinachonishangaza ni vile ambavyo amewaaminisha wengi kwamba anaweza kushindwa uchaguzi na kuendelea kukaa White House. Mpunga ambao ametumia kufungua kesi kwenye majimbo mbali mbali nalo ni la ajabu. Nategemea kumwona anaenda uhamishoni Russia, au Japan kama alivyosema hawezi kukaa USA kama akishindwa. Sioni kama atakimbilia Scotland kwenye golf course yake.
Asante mkuu. Video hapa chini toka kwa mashabiki wa Trump, inadai anayeongea ni mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Marekani. Ni yeye kweli au fiksi? Na kama ni yeye, nini mustakabal wa uchaguzi, mintarafu yale ayaongeayo:
![]()
Trey Trainor to Newsmax TV: Voter Fraud Is Taking Place
Chair of the Federal Election Commission Trey Trainor believes voter fraud is taking place in states still counting ballots.During a Friday appearance on Newsmax TV's "National Report," Trainor said locations not granting observers...www.newsmax.com
2020Trump akubali kushindwa tu, transparency ambayo wanaililia ni ipi? Hilo la kujaza form wakati kwenye hivyo vituo kumejaa cameras na waangalizi kibao haiwezekani kwa sababu watajaza hizo kura ngapi? Wizi wa kura huwezi kufanya namna hiyo. Kama wewe ni returning officer au poll clerk huwezi kufanya huo wizi kwa sababu ni wa kitoto. Uzuri moja USA wanatumia machine kuhesabu kura wakati nchi kama UK wanahesabu manually. (Kwenye machine kama isipohesabu ndio unaona hao poll clerks wanajaza nk.
Trump anaondoka madarakani kwa aibu!
https://www.dailymail.co.uk/news/ar...s-stage-17-minute-tirade.html#v-6485575615025
Naam, the Game is over. Wanajaribu tu kupunguza dozi ya maumivu kwani muda unavyozidi kwenda uchungu wa kushindwa nao hupungua! Wanaweza wakatangaza matokeo baadaye leo hii...Donald Trump is a one term president kwani hakuna mahakama inaweza kukubaliana na madai yake ya kipuuzi. Wamarekani hawawezi kurudia makosa waliyoyafanya 2016!NV, AZ,PA, GA, NC
Bandiko#9 tulieleza kuhusu idadi ya wapiga kura kwamba ilikuwa ya pande zote mbili, Repulican na Democrats.Hii ni kutokana na 'ushindani ' wa kirangi zaidi kuliko sera na kila upande ulijizatiti.
Katika majiji na miji kwenye watu wenye elimu Rais Trump amepoteza lakini maeneo ya wahafidhina na hasa vijijini huko imekuwa ngome . Rais Trump ana ushawishi katika maeneo hayo hata kama si wa kisera.
Kila mara Trump amekataa kuwalaani '' proud boys au KKK na makundi mengine ya kibaguzi''
Trump anajua makundi hayo ni sehemu kubwa ya wapiga kura wake hasa vijini wanaoona nchi ''inabadilika''
Kwa upande wa Democrat's, VC Biden si msemaji mzuri kama watangulizi wake akina Obama na Clinton au hata wapinzani wakatika wa kutafuta mgombe kama akina Sanders, Butegig n.k.
Hata hivyo Biden ana Charisma tu Biden na hilo limesaidia sana kupunguza kura za Trump huko vijijini.
Katika mazingira ya kawaida Dems wangetoa kipigo kikali kwa Trump na kukamilisha uchaguzi kama wangeshinda Florida na North Carolina.
Florida walipoteza na North Carolina bado matokeo lakini inagemea sana kwa Trump.
Uchaguzi ukabaki katika states za Arizona, Georgia, Nevada, na commonwealth of Pennsylvania
Hapa panatoa njia kwa Trump ikiwa atashinda commonwealth.
Trump alitegemea atashinda Georgia na Arizona na kufikia idadi ya wajumbe 270. Mambo yamebailika
Georgia ambayo Republican (red state) imegeuza kibao na Biden anaelekea kushinda kama ilivyo Nevada na Arizona. Commonwealth (PA) hali ni nzuri sana kwa Biden kwani akishinda PA , mchezo umekwisha.
Kwa hesabu zozote uchaguzi umekwisha na Biden atakuwa Rais ajaye.
Rais Trump hataki kukubali matokeo na kusingizia kuna wizi n.k.
Hoja hizo alijenga hata kabla ya kura kupigwa.
Anachokifanya Trump ni kukwepa lawama ili aonekane amekuwa Rais wa kipindi kimoja kwa sababu ya wizi.
Trumpa ajilaumu mwenyewe. Kwanza, alikataza wapiga kura wake wasitumie 'vote by mail' bali waende vituoni. Katika mazingira ya sasa hilo limechangia sana kupunguza kura lakini pia limetoa fursa sana kwa wapiga kura hasa wa Democrats.
Kauli ya losers andsucker' inamtafuna. Katika eneo kama Georgia ambalo tofauti ya kura ni ndogo sana, hata zile za jeshi zimekwenda kwa Biden.
Trump amekwenda mahakamani, ukweli unabaki kuwa matokeo ya Arizona na Nevada yakitangazwa kukamilika Bidena atakuwa Rais wa Marekani bila kutegemea Commonwealth of PA.
Georgia peke na Nevada au Arizona zinatosha kumfanya Biden awe Rais.
Milango yote imefungwa na anachokifanya Trump ni kutafuta dirisha la kutokea salama.
Trump ni 1 term president na anakuwa 5 katika mlolongo huo.
Game over
Tusemezane
Bado ulikuwa na imani na Trumpet? Ahame nchi chacha si aliahidi?Breaking News: It is over! It is now President-Elect Joseph Robinette Biden!







Hivi unayo habari kuwa Trump ana pacha wake Tanzania? Wapenzi wa hawa mapacha wako upande moja na mpaka sasa nashindwa kuelewa imekuwakuwaje ukamchagua moja na kumwacha mwenzake. Kumbuka birds of a feather flock (fly) together! Wenzako wengi walikuwa upande wa Trump...je umepotea njia?Bado ulikuwa na imani na Trumpet? Ahame nchi chacha si aliahidi?
Wenzangu wakina nani? Wacha kamba mkuu mapacha wake atakuwa huyo balozi aliyemleta na JFI sidhani kama Biden atamwacha salama.Hivi unayo habari kuwa Trump ana pacha wake Tanzania? Wapenzi wa hawa mapacha wako upande moja na mpaka sasa nashindwa kuelewa imekuwakuwaje ukamchagua moja na kumwacha mwenzake. Kumbuka birds of a feather flock (fly) together! Wenzako wengi walikuwa upande wa Trump...je umepotea njia?
Nakuapia kwamba kama ingekuwa ni Tanzania, Trump angeweza kupata ushindi hata wa asilimia 99% na hakuna mbunge wa upinzani angetangazwa kashinda na Biden angeiota tu Ikulu.Wenzangu wakina nani? Wacha kamba mkuu mapacha wake atakuwa huyo balozi aliyemleta na JFI sidhani kama Biden atamwacha salama.
What's your point?Nakuapia kwamba kama ingekuwa ni Tanzania, Trump angeweza kupata ushindi hata wa asilimia 99% na hakuna mbunge wa upinzani angetangazwa kashinda na Biden angeiota tu Ikulu.
