Pre GE2025 Uchaguzi wa CHADEMA umedhihirisha Lissu ni Mwanaharakati Mbowe ni Mwanasiasa

Pre GE2025 Uchaguzi wa CHADEMA umedhihirisha Lissu ni Mwanaharakati Mbowe ni Mwanasiasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mwamba tuvushe
1000211802.jpg
 
Wajumbe Wana wasiwasi kuhusu uwezo wa Tundu Lissu kuongoza Chadema kama mwenyekiti, na kuna sababu kadhaa zinazoweza kuungwa mkono na mtazamo huu:
1. Historia ya Kiongozi
- Uzoefu wa Kisiasa: Ingawa Lissu ana uzoefu kama mwanasheria na mbunge, kukosekana kwa uzoefu wa moja kwa moja katika uongozi wa chama kikubwa kunaweza kumfanya asionekane kuwa na uwezo wa kutosha kuongoza chama katika mazingira magumu ya kisiasa.

2. Mgawanyiko na Mizozo
- Mgawanyiko wa Chama: Lissu anaweza kuwa na maono tofauti na wanachama wengine. Hali hii inaweza kuleta mgawanyiko na kuathiri umoja wa chama, jambo muhimu katika kuongoza chama kikubwa.

3. Uwezo wa Kujenga Ushirikiano
- Mahusiano na Wafuasi: Uwezo wa Lissu kujenga na kudumisha mahusiano mazuri na wanachama ni muhimu. Ikiwa hatashirikiana vizuri na wanachama, kuna hatari ya kupoteza uaminifu na ushirikiano wa ndani.

4. Athari za Kisheria
- Mizozo ya Kisheria: Tundu Lissu amekuwa katika mizozo ya kisheria na serikali, ambayo inaweza kuathiri hadhi ya chama na uwezo wake wa kuongoza. Hali hii inaweza kuleta changamoto zaidi katika uongozi.

5. Mtazamo wa Kisiasa
- Msimamo Mkali: Lissu anaweza kuwa na mitazamo ambayo ni makali au yanayopingana na sera za chama. Hii inaweza kumfanya asikubalike na wanachama wengine, na hivyo kuathiri uwezo wake wa kuongoza.

Hitimisho
Kwa mantiki hii, kuna sababu za msingi za kutokubaliana na wazo la kumchagua Lissu kuwa mwenyekiti wa Chadema.

Ni muhimu kwa wajumbe wa chama kuzingatia uwezo wa kiongozi kuleta umoja, kujenga ushirikiano, na kukabiliana na changamoto za kisiasa.
Uamuzi wa kuchagua mwenyekiti unahitaji uelewa mzuri wa uwezo wa kiongozi kuongoza chama katika mazingira magumu.
 
Mbowe: Siondoki kwasabb nimetumia fedha zangu nyingi sana ktk chama hiki

Mbowe: Mimi Sina njaa, nina vitega uchumi mpk nje huko, lkn wengine ni wabangaizaji tu.

Kauli hizi za Mbowe, ndiyo unamsifia kuwa anajenga taasisi???
Mamluki yke yanajikeshesh hku kumpamba..yn akifany kosa la kujikuta chama ni yeye tu anafaa kuw chea asibinue domo kutak katiba wkt udikteta ameuvaa
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Huenda siku za cdm kuendelea kuwa top ktk siasa za Tz zimeisha. Tusubiri tuone
 
Kwa wanaofuatilia Uchaguzi huu watakubaliana na mimi kwamba ukimsikiliza Mbowe unaona picha ya Mwanasiasa imara na Kiongozi na ukimsikiliza Lissu unaona Picha ya ya Mwanaharakati aliyekomaa ila Mwanasiasa dhaifu sana.

Ukiangalia kwa undani zaidi utaona Hotuba nyingi za Lissu zinaiumiza sana CHADEMA kama Taasisi na Viongozi wenzake, nyingi ya Hotuba za Lissu zinalenga kumjenga yeye Binafsi wakati za Mbowe zinalenga sana kujenga Umoja wa kitaasisi,hapa sizungumzii wapambe wao.

Ukiangalia kwa mbali zaidi utaona Kampeni za Lissu zinalenga watu wa Mitandaoni na wananchi wa nje ambao wengi wao siyo wapiga kura wakati Kampeni za Mbowe zinalenga Wanachadema ambao ni wapiga kura.

Natabiri Matokeo hapa Lissu anaenda kuangukia Pua vibaya sana kwenye Uchaguzi wa Chama kama hatabadili Strategy zake na hadhira yake ya Kampeni,Mods msifute hii thread pls.
Lissu labda ashinde Njaaa
 
Usikose kuja kuyanena hayo kwenye mdahalo japokuwa hadi sasa bado hujazibitisha kushiriki

Kifupi MBOWE miaka 21 imemtosha kwa kuwa muda wake haupo naye busara asubuli hilo sanduku la kura litakavyomuumbua

Atashindwa kwa kura ambazo hata ukiiba hawezi kushinda

Mark maneno haya 80% ndio ushindi wa LISSU trh 21
 
Mbowe: Siondoki kwasabb nimetumia fedha zangu nyingi sana ktk chama hiki

Mbowe: Mimi Sina njaa, nina vitega uchumi mpk nje huko, lkn wengine ni wabangaizaji tu.

Kauli hizi za Mbowe, ndiyo unamsifia kuwa anajenga taasisi???
Kuna uongo Gani hapo?
 
Badilisheni mada! Sikilizeni hii maneno sasa
 

Attachments

  • VID-20241228-WA0044.mp4
    23.2 MB
Hahaha Team Lisu kama Team Wema, kelele kila kona.

Mbowe yeye katulia anapiga kampeni kimya kimya tu, Kura itaamua mshindi.

Team Lisu hamuoni aibu kupiga kelele hovyo hovo kiasi hiki?
 
Kwa uchache maandishi.
Lisu bado si mwanasiasa ila mwanaharakati.

LIsu bado hana uwezo wa kuongoza chama cha siasa kama mwenyekiti

Lisu ni mzuri akiwa chini ya uangalizi na akiwa anapangiwa nini cha kufanya na kipi si cha kufanya hasa yale mambo makubwa.

Mbowe ni mzuri sana kwenye uongozi na kiongozi.
 
Kwa uchache maandishi.
Lisu bado si mwanasiasa ila mwanaharakati.

LIsu bado hana uwezo wa kuongoza chama cha siasa kama mwenyekiti

Lisu ni mzuri akiwa chini ya uangalizi na akiwa anapangiwa nini cha kufanya na kipi si cha kufanya hasa yale mambo makubwa.

Mbowe ni mzuri sana kwenye uongozi na kiongozi.
1000211802.jpg
 
Tulipo hatuitaji Mwanasiasa Bali Kiongozi asiyefata script na kuleta Sanaa na hadaa za kishamba.
Matokeo ya kuleta siasa na kukwepa uwajibikaji ndio chanzo Cha hapa tulipo.
 
Katika muktadha wa uchaguzi wa mwenyekiti wa Chadema Taifa, wajumbe wa mkutano mkuu wanakabiliwa na maamuzi muhimu yanayoweza kuathiri mustakabali wa chama hiki.

Hivi karibuni, kumekuwa na mjadala mzito kuhusu aina ya kiongozi anayefaa kuongoza chama katika kipindi hiki cha changamoto. Wajumbe wanahitaji mgombea ambaye ni mwasiasa, si mwanaharakati, ili kuweza kuimarisha siasa za chama na kukabiliana na matatizo ya kisiasa yanayolikabili taifa.

Wakati wa uchaguzi huu, ni muhimu kuelewa tofauti kati ya mwanasiasa na mwanaharakati. Mwanasiasa anajitahidi kutafuta mbinu na mikakati ya kisiasa inayoweza kuleta mabadiliko chanya katika jamii, huku akitafuta njia za kushirikiana na wadau mbalimbali katika uwanja wa siasa.

Kwa upande mwingine, mwanaharakati anajikita zaidi katika harakati za ukombozi, akilenga kuleta mabadiliko kupitia mapambano ya moja kwa moja dhidi ya mfumo uliopo. Hii ni tofauti kubwa ambayo wajumbe wa mkutano wanapaswa kuzingatia katika uchaguzi wao.

Tukichunguza majina mawili yanayojitokeza katika uchaguzi huu, Tundu Lissu na Freeman Mbowe, ni wazi kwamba kila mmoja anawakilisha aina tofauti ya uongozi. Lissu amejijengea sifa ya kuwa mwanaharakati mwenye msimamo thabiti katika masuala ya haki za binadamu na demokrasia.

Hata hivyo, siasa za mwanaharakati mara nyingi zinaweza kuonekana kama za kukabiliana na mfumo, badala ya kujaribu kuujenga na kuuboresha. Wakati huu, wanachama wa Chadema wanahitaji mtu ambaye anaweza kuhamasisha umoja na ushirikiano, si mtu anayepigana vita vya kisiasa pekee.

Katika upande wa Mbowe, yeye anajulikana kama mwanasiasa mwenye uzoefu wa muda mrefu katika siasa za Tanzania. Mbowe anajua jinsi ya kuendesha siasa na kuujenga chama katika mazingira magumu. Kuweka kando tofauti za kisiasa, Mbowe anaweza kuwa kiongozi ambaye anaweza kuleta umoja na kuelekeza chama katika njia sahihi ya kisiasa. Katika wakati wa mgawanyiko na changamoto za kisiasa, ni muhimu kuwa na kiongozi ambaye anaweza kuleta ushirikiano na kuelekeza juhudi za chama katika kujenga mustakabali bora.

Wajumbe wa mkutano mkuu wanapaswa kuelewa kwamba wakati huu wa uchaguzi, siasa zinazohitajika ni zile zinazoweza kuleta maendeleo kwa chama na kwa jamii nzima. Wanachama wanahitaji siasa zinazoweza kuleta mafanikio na siasa ambazo zinaweza kuimarisha ushawishi wa chama katika jamii. Kiongozi anayejikita katika siasa atakuwa na uwezo wa kujenga na kudumisha uhusiano mzuri na wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na jamii kwa ujumla.

Aidha, ni muhimu kufahamu kwamba siasa si tu kuhusu kushinda uchaguzi, bali pia ni kuhusu kujenga mazingira bora ya kuishi na kufanya kazi. Wanachama wanahitaji kiongozi ambaye ataweza kuangalia maslahi ya chama kwa ujumla, badala ya kujikita katika masuala binafsi au ya kikundi fulani. Mbowe, akiwa na uzoefu wa kisiasa, anaweza kuwa na uwezo wa kujenga mazingira hayo na kuimarisha nafasi ya chama katika siasa za nchi.

Katika hali hii, wajumbe wa mkutano wanapaswa kuzingatia umuhimu wa kuwa na kiongozi ambaye ataweza kuhimiza siasa za maendeleo, badala ya siasa za ukombozi pekee.

Wanachama wanahitaji mtu ambaye ataweza kubuni mikakati ya kisiasa itakayowezesha chama kuendelea kuwa na mvuto katika jamii na kuongeza ushawishi wake katika masuala ya kitaifa. Hii itasaidia Chadema kuwa na nafasi imara katika siasa za Tanzania na kuweza kushiriki katika maamuzi yanayohusu mustakabali wa nchi.

Kwa kumalizia, wajumbe wa mkutano mkuu wa Chadema wanahitaji kufikiria kwa makini kuhusu uchaguzi wa mwenyekiti. Wanahitaji kiongozi ambaye ni mwasiasa, sio mwanaharakati, ili kuweza kuimarisha siasa za chama na kukabiliana na changamoto za kisiasa.


Wakati huu, Mbowe anaonekana kuwa na uwezo wa kuleta mabadiliko chanya na kujenga umoja katika chama, wakati Lissu anahitaji kuzingatia zaidi harakati za ukombozi. Chaguo sahihi litasaidia Chadema kuendelea kuimarika na kuwa na sauti yenye nguvu katika siasa za Tanzania.
Chadema inahitaji uongozi wenye HYBRID yaani mwansiasa mwenye sura zote mbili kulingana na mazingira ya kisiasa ya sasa na muktadha wa mapambano mapya yaliyopo. mwana siasa aliye na uanaharakati sehemu kadhaa na mwanadiplomasia mazingira kadhaa. hapo rangi mbili hazina budi kutumika. CCM imebadili maxingira ya siasa zake. inahitaji vyote viwili kuiendea.
 
Lissu anaweza kuongoza iwapo tu atakuwa karibu sana na Mbowe kumshauri na kumshirikisha kwenye mambo mengi kama Mzee wa Chadema kwa muktadha ya siasa za nchi hii. Na pia asimame na siasa za ndani kuwaleta pamoja wanachama na kutowatumikia sauti ya watanzania ambao wanaweza kuigeuka chadema na kuitelekeza au kuendesha uanaharakati kwa mgongo wake. Hapo ndipo penye Paradox
 
Back
Top Bottom