Uchaguzi wa Spika huenda usifanyike, kesi ya Mbatia juu ya ukiukwaji wa Katiba katika kupatikana Spika mpya inaanza kusikilizwa

Still wata-fasta track ili kutolea uamuzi hilo pingamizi hili hatimae wapate fursa ya ku-deal na kesi ya msingi!
 
Hakuna shughuli zozote za nchi hii zinategemea bunge hilo bunge kibogoyo, labda kama ni kufuata formalities tu. Lakini kila kitu huwa kinafanywa na serikali, hilo bunge ni rubber stamp tu.
Ndo hizo hizo formalities mzee! Na kwavile hapa tunazungumzia bunge, hizo shughuli za nchi ni zile zinazoendelea bungeni na sio pengine popote!!

Kwahiyo bunge liwe kibogoyo au vinginevyo, ni LAZIMA waendeshe shughuli zao hivyo hivyo! Ni ukweli mchungu ambao hatuna budi kuumeza kuliko kujipa matumaini fake!
 
Kama kweli katiba ilikiukwa juu ya kupatikana spika basi Mahakama kuu itende haki na uchaguzi wa spika usifanyike. Mahakama iwe huru na kufanya kazi yake.View attachment 2094670
Ndugai anatumika kuwapotosha Wananchi wasiosoma katikati ya mistari.Mtindo huu unaanza kuzoeleka sasa,alianza Profesa wa uchumi.Unajiuzulu halafu unarejea kwa sababu utaratibu wa kujiuzulu ulikiukwa!Ukimalizika uchaguzi wa spika unafuata uchaguzi wa Naibu Spika baada ya utaratibu wa uteuzi wa mgombea spika umekiukwa.

Bila Katiba mpya Watanzania tumekwisha.
 

Sasa kama kama ni shughuli za kupiga porojo wakati hazina impact yoyote, hata likisimama kuna shida gani?
 
Muhimili wa mahakama ulishajifia kitambo sana hapa TZ.

Usitegee chochote cha maana kutoka kwa jaji atakayehusika na kesi hii ys kikatiba.
Kesi za kikatiba,nakumbuka Mtikila alikuwa anashinda Sana,halafu kinachofuata ni hakuna.Ni Sawa na kushinda mechi ya fainali,halafu kombe linarudi tena ofisini Kwa waandaaji wa mchezo
 
Sijui kama muhimili wa Mahakama unaweza kuuingilia muhimili wa Bunge ambalo linatunga Sheria ila Mahakama izitumie
 
Kama kweli katiba ilikiukwa juu ya kupatikana spika basi Mahakama kuu itende haki na uchaguzi wa spika usifanyike. Mahakama iwe huru na kufanya kazi yake.View attachment 2094670
Uchaguzi wa Spika utafanyika kwa sababu kesi aliyopeleka mahakamani Mh. Mbatia , ni ya kumtaka Spika aliyepita ajiuzulu kkwa utaratibu. Mh, Mbatia si kwamba anahitaji Spika aliyepita arudi madarakani, hapana bali anamtaka ajiuzulu kwa kufuata utaratibu kama ambavyo Mh. Mbatia anavyodhani kuwa ni sahihi. Sasa hapa kuna hoja gani ya kuzuia uchaguzi usifanyike?

Mh. Mbatia hajapeleka mahakamani shauri la kuzuia uchaguzi wa Spika usifanyike na hivyo uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa.
 

Which means, of course, kwamba Mjuzulu JYN anaweza kufuata utaratibu wa kujiuzulu (unaomfaa mshtaki & mlalamikaji) even mwaka 2025, na Mheshimiwa Mbatia akaridhika tu!
 
Kwa hiyo mahakama watajenga hoja kwamba hawawezi kuingilia maswala ya mhimili mwingine, siyo? vipi swala la kuvunja katiba.....
 
Spika atachaguliwa kama kawaida, matokeo ya mahakama yatakuwa kinyume na matarajio ya Mbatia...mwisho wa siku hakuna kitachoharibika...

Tusijisahau sana kwamba sisi ni Waafrika na tuna namna yetu simple tu ya kuhandle issues zetu 😁
 
Vipi kama kesi ikisikilizwa na ikaonekana katiba ilikiukwa namna Spika alivyojiuzulu? Maana unaaza kutoa majibu kabla hata kesi haijasikilizwa.
Haiwezi kutokea. Kwasabb Kwa kufanya hivyo mahakama itakuwa imemchafua rais wa nchi na mwenyekiti wa chama Cha mapinduzi taifa kwa "kubariki" mchakato batili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…