Uchaguzi wa Spika huenda usifanyike, kesi ya Mbatia juu ya ukiukwaji wa Katiba katika kupatikana Spika mpya inaanza kusikilizwa

Huwa napenda sana unavyotetea hoja na kuambatanisha na threads zako. Naishangaa serikali kwanini haikuajiri ukapambane na kina Kibwatala. Maana hakika sijaona mpinzani wako kwenye ujuvi wa sheria....
 
Bunge tulilonalo ni batili na ni bunge lisilo na uwakilishi wenye maamuzi ya wananchi kumbe tunaweza kusema bunge hili ni la KIJINGA tu.na kamwe haliwezi kusimamia serikali na hata wao CCM wanajua vzr sana hilo jambo.serikali ijue kwamba takribani asilimia 80 ya watanzania wenye akili timamu walishaacha zamani sana kusikiliza bunge la KIJINGA kama tulilonalo.HAKI IKITENDEKA KWENYE SUALA LA UWAKILISHI BUNGENI WANANCHI WATASIKILIZA BUNGE MAANA WATAJUA KABISA KUWA WABUNGE WANAOWAKILISHA MAWAZO YAO WAPO BUNGENI.BUNGE HILI HALINA UWAKILISHI HUO LIMEJAA TU WAPUUZI WANAOKULA HELA ZA WATU MASKINI.
 
Katiba inasemaje.Nadhani Mbatia ana hoja,sio zuzu kama akina Mbowe.Anyway ngoje niangalie Katiba inasemaje kuhusu hili,I will come back.
Ukipitia kwenye posts zangu zingine, utaona nimeweka vifungu vya katiba, na post ya mwisho (b4 this) nikaweka kanuni ya bunge!
 
Yh

Kanuni ya kujiuzulu iko wazi barua inapelekwa kwa katibu wa bunge
Katiba haisemi barua inasema taarifa! Sasa kama barua na taarifa ni kitu kile kile, then well and good, na ndo maana nikasema hapo zitatafutwa loopholses zozote!
 
Katiba haisemi barua inasema taarifa! Sasa kama barua na taarifa ni kitu kile kile, then well and good, na ndo maana nikasema hapo zitatafutwa loopholses zozote!
Kuna kanuni za kudumu za bunge zinaelezea hivyo
 
Soma katiba sura ya 148 (1) kisha unganisha na (c), ile (1) inaainisha kuwa kujiuzulu kufanyike kwa kuandika barua kwa mkono wake mwenyewe na kuweka sahihi yake. Kipengere (c) kinaainisha hiyo barua ipelekwe bungeni!! Ndugai hakufanya hivyo na nadhani hakufanya hivyo kwa makusudi kabisa!! Sasa hivi ataungwa mkono na makundi ya Chenge na wenzake waliopigwa chini kwenye mchakato wa uspika ndani ya ccm!!
 
Kusoma wengi wanajua, tatizo ni kuelewa kilichokusudiwa. Kuna mambo mawili yaliyokosewa:

1) Spika anayejiuzulu atalitaarifu Bunge

2) Kuna watu ambao hawaruhusiwi kugombea nafasi ya spika wakiwa bado kwenye nafasi zao, naibubspika ni mmojawapo.
Katiba iko wazi, spika anaejiuzulu, ataritaarifu bunge kwa barua original, na hatakiwi kutoa taarifa ya kujiuzulu kwenye chama chake kwanza , sharti aanze kwanza kutaarifu bunge KWABARUA ORIGINAL SIO COPY[emoji134][emoji23][emoji23]
 
Which means, of course, kwamba Mjuzulu JYN anaweza kufuata utaratibu wa kujiuzulu (unaomfaa mshtaki & mlalamikaji) even mwaka 2025, na Mheshimiwa Mbatia akaridhika tu!
Au kishafanya,, maana katiba haibanishi kwamba lazima mtangaziwe[emoji23]
 
Hivi kuna haja hata ya kufanya huo uchaguzi wa Supika?

Harafu eti wabunge wa CCM watapigishwa kura za ndio au hapana kuchagua jina moja la mgombea wao. Mambo ya kijima kweli haya
 
Katibu wa bunge alikiri kupokea barua ya kujiuzulu spika na ataisoma siku ya kwanza mbele ya bunge then patakua na uchaguzi wa spika, kuelekea siku hiyo ndiposa Naibu spika atajiuzulu na kuwa rasmi mgombea wa nafasi ya spika
 
Katiba haisemi barua inasema taarifa! Sasa kama barua na taarifa ni kitu kile kile, then well and good, na ndo maana nikasema hapo zitatafutwa loopholses zozote!
Katiba inasema vyote viwili sura 148(1) inasema barua iandikwe na isaniniwe kwa mkono wa mhusika. Baadaye kipengele (c) inasema hiyo taarifa (iliyo katika barua) ipelekwe bungeni!! Ndugai hakufanya hivyo!!
 
Vipi kama kesi ikisikilizwa na ikaonekana katiba ilikiukwa namna Spika alivyojiuzulu? Maana unaaza kutoa majibu kabla hata kesi haijasikilizwa.

Ndivyo mahakama za JF zilivyo. Hata kesi ya Ayatollah Mbowe ilishamalizika siku nyingi sana hapa JF!
 
Katibu wa bunge alikiri kupokea barua ya kujiuzulu spika na ataisoma siku ya kwanza mbele ya bunge then patakua na uchaguzi wa spika, kuelekea siku hiyo ndiposa Naibu spika atajiuzulu na kuwa rasmi mgombea wa nafasi ya spika
Alikiri kupokea barua ya katibu mkuu wa ccm (ambaye hahusiki kabisa katika mchakato wa spika kujiuzulu). Alikiri pia kupokea nakala ya barua ya Ndugai!!
 
Kupata tiketi ya chama haina maana utakapokuwa spika utaendelea kuwa mtumwa wa chama. Ukishakuwa spika unawajibika kwa bunge na kwa nchi, siyo kwa chama ndo maana unapigiwa kura na wabunge wa vyama vyote.........jaribu kuelewa.
 
Soma muktadha/context vizuri. Anaposema TAARIFA HIYO YA KUJIUDHURU ana-refer taarifa iliyoandikwa na kuwekwa sahihi kwa mkono wa spika!! Lazima hi hk kifungu cha 149 (1) c kisomwe chote kwa pamoja ili kupata muktadha vizuri!!
 
Hivi kuna haja hata ya kufanya huo uchaguzi wa Supika?

Harafu eti wabunge wa CCM watapigishwa kura za ndio au hapana kuchagua jina moja la mgombea wao. Mambo ya kijima kweli haya
Mkuu Consultant, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kilichofanyika katika uteuzi wa Dr. Tulia Akson ni utaratibu tuu ndani ya CCM. Baada ya utaratibu wa CCM kufuatwa, kila chama kitaleta mgombea wake aliyepatikana kwa mujibu wa taratibu za vyama na kumleta Bungeni ambapo sasa kanuni za Bunge kumchagua Spika lazima zifuatwe na Spika kuchaguliwa na hivyo Spika kuapa mbele ya Bunge na kuwa amepatikana kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.
Japo baada ya uteuzi wa CCM, huyo ndiye Spika, kinachofanyika ni maigizo tuu ya kukamilisha tuu taratibu za uchaguzi wa Spika wa Bunge kwa mujibu wa sheria na kanuni.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…