Uchambuzi maalumu: Uzi wa Padri kulawiti watoto Vs Sheikh kulawiti watoto

Uchambuzi maalumu: Uzi wa Padri kulawiti watoto Vs Sheikh kulawiti watoto

Kuzimu kweupee mashetani wote mko nao uraiani
Hadi nyumbani kwenye MaTv wapo tena kwa nyimbo za siku hizi kama wanao wanasikiliza bongoFleva ,movies na baadhi ya vipindi vya runinga aningiza ujinga kwa kiasi kikubwa na uwezokano mkubwa wa kuathirika kutokana na anavyoviona na kuvisikia humo.
 
Hadi nyumbani kwenye MaTv wapo tena kwa nyimbo za siku hizi kama wanao wanasikiliza bongoFleva ,movies na baadhi ya vipindi vya runinga aningiza ujinga kwa kiasi kikubwa na uwezokano mkubwa wa kuathirika kutokana na anavyoviona na kuvisikia humo.
Kupitia simu, Tanakilishi na Tv jamaa wamemaliza Game.
Haachwi mtoto Wala mzee wote ndani.
 
Habari za muda huu wana Jf..

Baada ya kuibuka hivi karibuni matukio ya viongozi wa dini kulawiti na kupitia michango ya wadau mbalimbali humu kuna mambo nimeona muhimu kugusia.

Inapaswa kutambua kuwa kwa zama hizi suala la malezi na maadili linapitia wakati mgumu mno maana kila sehemu usalama mdogo na ukija kwenye miziki ,muvi na mitandao ya kijamii uovu unahamasiswa kwa kiasi kikubwa mara kama kuingiliana kinyume na maumbile,mapenzi ya jinsia moja ,Uzinzi nk kwa kiwango kikubwa hivyo wakati huu umakini katika malezi unahitajika sana.

Wiki za karibuni kuliibuka matukio ya Padri kulawiti vilevile kumewahi kuripotiwa matukio ya Shekhe kulawiti inasikitisha sana watu wanaacha kujadili njia bora za kukomesha na kuepukana na haya mambo na kuanza kukashifiana na kutukana na kuzuka vita za kidini wakati matukio hayo yapo katika jamii na binafsi nina amini hakuna dini inayoruhusu hayo mambo kabisa.

Japo vita za maneno zipo kwa watu wa pande zote ila kwa uchunguzi wangu baada ya kupitia nyuzi zote kwa umakini nimeona kuna utofauti mkubwa katika nyuzi zinazohusu Shekhe na Padri kulawiti mifano huu chini.View attachment 2379870
Na

View attachment 2379880
Mara nyingi nyuzi zinahusu upande mmoja naona mara nyingi unashambuliwa kiasi ambacho uadilifu unakosekana mfano juzi ulianzishwa huu uzi wa Shekhe kulawiti mtoto wa miaka tisa kimara Bonyokwa mtu alianzisha tu bila kutaja majina na chanzo ghafla bila watu kuhoji kama taarifa za kweli au la na kufanya uchunguzi kisha kujadili kistaarabu matokeo yake ikawa tofauti naona uzi umefutwa tokea siku ile sababu nahisi ni taarifa ilikuwa ya uongoView attachment 2379900

Hapa imhotep alionyaView attachment 2379903

Maoni Yangu Binafsi View attachment 2379905
Sikubaliani na naomi ya mrangi hapo juu kwani naamini hata mashuleni kuna uhuni mwingi kwa wale tuliosomea shule za kata tutakuwa mashidi maana kule kumezidi lakini hatuwezi kufikia hitimisho la kufuta shule na kutopeleka watoto wetu shule bali katika swala hili ninachokipendeza wazazi wawe wafuatiliaji wa kina kuhusu watoto wao kila siku pamoja kuchunguza na kuwapeleka sehemu bora bila kusahau mamlaka husika kuandaa mikakati bora ya kuziuia na kupunguza matukio kama hayo.

Mimi mwenyewe niliwahi kutoa pendekezo nyumbani kuwapigia marufuku ndugu zangu madrassa fulani walivyokuwa wanasoma niliona uhuni mwingi maana ilikuwa inaruhusu hata watu wa mtaani waje chuo kwa ajili ya kitengo cha madufu sasa hata wengine wahuni walikuwa wanakuja kwa malengo tofauti na nikaona mabadiliko mara wakati wa kwenda chuo kujiremba sana nikatoa tamko kama wanataka kweli kusoma waende madrassa ya kisunni msikiti ninaoswali ambao hakuna kuchanganyika Kati ya wanaume na wanawake ,uhuni ,hata ostazi hawezi kuona sura ya mwanafunzi wa kike na maOstaz wa hapo huwa wanafuatiliwa mienendo yao.

#UziUnaendelea
Kuna tatizo kubwa la maadili sasa hivi. Watu tunazembea sana katika dini au kuipuuzia kabisa.

Kuna wengine wanaweza kusema kama sababu ni kuzembea katika dini, inakuwaje kuna "masheikh" wanafanya haya na ndio viongozi wa hiyo dini. Bado hoja yangu iko pale pale, ni kuzembea katika dini na kufanya tunachokitaka sisi badala ya kufuata Dini inavyotaka.

Hao "masheikh" badala ya kufuata dini wao wanafuata matamanio ya nafsi zao kama vile watu wengine wengi katika jamii zetu sasa hivi.

Haya matatizo yanatokana na watu kuacha kushika dini kama ilivyo, kuzipuuza Sharia za Allah au kuzifuata kwa matamanio. Na baadhi ya watu, wanaoyafanya matatizo haya, ambao watu wanawadhania ni viongozi wa kiislam kiuhalisia hawako hivyo. Bali ni wahuni ambao hawana elimu kabisa ya Dini lakini wamevikwa "vilemba" vya Uongozi wa Dini. Au Wengine wana elimu lakini hawajashika Dini (hawafuati), wako mbali na mwenendo wa Mtume na ni watu wanaofuata matamanio yao. Badala ya kufuata Dini wao wanafuata mkumbo na kusombwa na upepo wa watu wajinga waliojaa katika jamii.

Uislam unakataza mambo machafu yanayofanyika katika jamii zetu, tena unayakataza vikali mno. Hivyo watu kuuhusisha Uislam na machafu haya, kwa sababu eti baadhi ya watu wanaoyafanya wana sura ya dini, ni dhulma. Kwa kuwa haya mambo hayapo katika Uislam na yanapigwa vita na kupingwa vikali, basi wanaoyafanya wanayatoa nje ya Uislam. Haya machafu hayajaletwa na Uislam.

Machafu haya (ya zinaa na liwati) yanapigiwa chapuo katika jamii kupitia miziki, mafilamu, vyombo vya habari na watu wengine wanaoyatangaza wazi. Na baadhi ya wahuni wanayabeba katika jamii bila kujali, na inapotokea yakapingwa baadhi ya watu hao watayatetea kwa nguvu kwamba yaachwe yafanywe, tusiwahukumu, na wakatazaji wanakejeliwa. Ndio matokeo yake haya yanatokea ya watoto kuharibiwa na baadhi ya watu kutoka jamii hiyo hiyo ya wahuni ambao baadhi yao (hao wahuni) wamejificha katika Dini, halafu baada ya kutokea hayo madhara baadhi ya watu hao hao katika jamii na wajinga wengine wanaopinga Dini wanalaumu Dini eti ndio zimesababisha.

Solution ni matendo haya machafu yapingwe vikali kwa watoto na wakubwa na watu wahimizwe kurudi katika Dini kwa kusoma Elimu (Dini) ya sawa sawa (Qur'an na Sunnah juu ya ufahamu wa Salaf) na kuufuata na wala sio kuhimizwa kuikimbia Dini (Uislam). Na watu wahuni wasipewe nafasi ya kuvaa "vilemba" vya usheikh.

Mwisho niseme haya mambo ya watoto kubakwa na kulawitiwa yanaonesha ishara ya kuharibika kwa jamii zetu.

Mchango wangu ndio huo. Mapungufu yoyote ya uandishi na mtiririko wa hoja ni katika upungufu wangu wa kibinadamu. Ukamilifu na Ujuzi wote ni wa Allah.

Allah atunusuru sisi na vizazi vyetu kutokana na machafu haya na athari zake.
 
Kuna mfululizo wa Khutba za Ijumaa zenye anuani "Kutahadhari Dhidi ya Janga la Ushoga na Usagaji" zilizotolewa na Khatwiyb Ustaadh Abuu 'Abdillaah Fahad 'Abdallaah Hanneyn (Allah Amhifadhi). Kuna faida kubwa mno humo. Nawanasihi mkaitafute msikilize. Nimesikiliza khutba ya Ijumaa moja natafuta zengine.
 
Mmetoa maoni mazuri sana suala la maadili siku hiz halizingatiwi pia tusipende kuhukumu imanizetu Kwa makosa ya mtu mmoja mmoja
 
Ni uzi mzuri wenye mlengo mzuri lakini utaharibiwa na wafia dini walioachana na matumizi ya fikra zao.........kwao uchambuzi unaanza baada ya kutazama mlengo wa kuegemea
 
Hadi nyumbani kwenye MaTv wapo tena kwa nyimbo za siku hizi kama wanao wanasikiliza bongoFleva ,movies na baadhi ya vipindi vya runinga aningiza ujinga kwa kiasi kikubwa na uwezokano mkubwa wa kuathirika kutokana na anavyoviona na kuvisikia humo.
Kabisa hii ni kweli
 
Yaani wakuu hii boat imeshaenda...

Waliopaswa kupambana na haya ni wakina Nyerere na Sokoine huko au wazee kwenye miaka ya 80 na early 90s uko...Now it's too late.

Maadili yameshamomonyoka, Tarajieni kuendelea zaidi.

Labda mfikirie namna ya Kucope, lakini hii meli imeshaondoa nanga..Kizazi kimeshaharibika na hamna chochote yeyote anaweza kufanya saivi.

Tena tarajieni mambo kuwa mabaya zaidi ya haya kadri muda unavyoenda..
Hatuna cha kufanya, ni kama Movie tunaangalia, Huwezi kubadilisha stori ya Movie unayoangalia kwenye Tv.

Chakufanya Labda ni kusali mwisho wako uwe mzuri na watoto wako wasiingie huko.

I'm being a realist.
 
Yaani wakuu hii boat imeshaenda...

Waliopaswa kupambana na haya ni wakina Nyerere na Sokoine huko au wazee kwenye miaka ya 80 na early 90s uko...Now it's too late.

Maadili yameshamomonyoka, Tarajieni kuendelea zaidi.

Labda mfikirie namna ya Kucope, lakini hii meli imeshaondoa nanga..Kizazi kimeshaharibika na hamna chochote yeyote anaweza kufanya saivi.

Tena tarajieni mambo kuwa mabaya zaidi ya haya kadri muda unavyoenda..
Hatuna cha kufanya, ni kama Movie tunaangalia, Huwezi kubadilisha stori ya Movie unayoangalia kwenye Tv.

Chakufanya Labda ni kusali mwisho wako uwe mzuri na watoto wako wasiingie huko.

I'm being a realist.
Kweli kabisa kila siku zinavyeonda maadili yanazidi ubaya unazidi kuongezeka hilo halina ubishi ila jambo lisilowezekana lote haliachwi lote kuna vitu vinawezekanika kufanywa kupunguza mambo haya nyumbani ,mashuleni ,mtaani nk
 
Pia Waislam tukumbushane juu ya Jihad ya kupambana na Nafsi na matamanio yake kisha Jihad dhidi ya Shaitwan. Jihad hizi mbili tutaendelea kupigana katika maisha yetu yote. Kuanza na Jihad ya Nafsi kupambana na matamanio. Siku zote nafsi ni yenye kuamuru maovu (Qur'an 12:53)

1666197715175.png

Kisha kupambana na Shaitwani;

1666198098797.png


Hakika Shet'ani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui. Kwani yeye analiita kundi lake liwe katika watu wa Motoni.
(Qur'an 35:6)

Na Shaitwan hutumia Shahawaat (matamanio) na ukimshinda hapo atatumia shubuhat (mambo yenye kutatanisha mfano linakujia jambo ukitazama kama ni dini vile kumbe sio dini au kama zuri vile kumbe sio zuri) na hii inahitaji mno Elimu na njia hii Shaitwan huitumia sana kuwapoteza wale walioshika dini ambao wanaweza kushinda shahawaat ila hawana Elimu.

Tumejisahau sana na Jihad hizi mbili ambazo tunatakiwa kupigana katika maisha yetu yote.

Na Allah anajua zaidi.
 
Mange kule kwenye App yake kuna section anaita za kuzimu. Sijui huwa anaonyesha nini huko ila naamini kule kuna wachungaji,mashekhe,wababa,wamama,mabinti kwa vijana wanashinda wanaangalia hivyo vitu. Kama kweli unataka Mungu aokoe kizazi chako acha kabisa kushabikia matendo yote ambayo ni machukizo kwa Mungu ikiwa pamoja na kuangalia picha au maudhui yasiyofaaa.
 
Kuna mfululizo wa Khutba za Ijumaa zenye anuani "Kutahadhari Dhidi ya Janga la Ushoga na Usagaji" zilizotolewa na Khatwiyb Ustaadh Abuu 'Abdillaah Fahad 'Abdallaah Hanneyn (Allah Amhifadhi). Kuna faida kubwa mno humo. Nawanasihi mkaitafute msikilize. Nimesikiliza khutba ya Ijumaa moja natafuta zengine.
Muda mrefu sijapita kwenye grupu la msikitini wa mtaani kwangu hapa nimepita sasa nimeona wametuma hiyo khutba ngoja nizifuatilie.
IMG_20221019_204703.jpg
 
Inatakiwa wote Wakristo na Waislamu waungane waandamane kupinga hivi vitendo.
 
Inatakiwa wote Wakristo na Waislamu waungane waandamane kupinga hivi vitendo.
Tatizo mawazo mgando ,watu mambo ya kidini wamefanya kama ushabiki wa Simba na Yanga kuombeana mabaya na kuyafurahia kila kukicha.
 
Huu uzi umeshika sehemu nyingi sio katika kipengele hiko bali kitu chochote humu itokee imefanywa na muislamu ,nchi yenye Waislamu wengi ,au kiwe kina husiana na Uislamu lazima lawama itakwenda kwenye Uislamu pasipo na haki bila kujali kama Uislamu unakataza au la ..

Tofauti ikiwa upande wa pili hakuna shida....hapo ni kukosa uadilifu kabisa.
 
  • Nzuri
Reactions: Tui
Huu uzi umeshika sehemu nyingi sio katika kipengele hiko bali kitu chochote humu itokee imefanywa na muislamu ,nchi yenye Waislamu wengi ,au kiwe kina husiana na Uislamu lazima lawama itakwenda kwenye Uislamu pasipo na haki bila kujali kama Uislamu unakataza au la ..

Tofauti ikiwa upande wa pili hakuna shida....hapo ni kukosa uadilifu kabisa.

Ttzo uislamu umejaa unafiki mwingi,nakujiona ni dini perfect kumbe namo wahuni kibao.
 
Back
Top Bottom