Uchambuzi: Shirika la ujasusi la Uisraeli Mossad

Uchambuzi: Shirika la ujasusi la Uisraeli Mossad

Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 6
“BRING EICHMANN DEAD OR ALIVE!”
Mwandishi anasema kuwa mwaka 1957 walipokea ujumbe kutoka Frankfurt kuwa mjerumani mmoja aliyeheshimika sana Dr Fritz Bauer alitaka kutoa taarifa nyeti kwa Mossad.Fritz alikuwa mjerumani mwenye asili ya Israel ambaye aliwekwa kwenye kambi za mateso kabla ya kutoroka,baadae akawa mpinzani mkubwa wa sera za chama cha Nazi
Huyu dr Fritz alirejea Ujerumani baada ya anguko la Hitler na alikuwa msitari wa mbele katika kuhakikisha wote walioshiriki wanafikishwa mbele ya sharia,hata hivo hakuridhishwa na jinsi mamlaka za ujerumani zilivoshughulikia swala zima.
Sasa basi huyu Dr Frits alikuwa na taarifa nyeti,ambayo aliiwasilisha Mossad kuhusu bwana Eichmann,bwana Eichman alikuwa mchinjaji na muuaji maarufu wakati wa Hitler,na baada ya anguko la Hitler alikimbilia Argentina.Ni kwamba baada ya Hitler kujiua Israel ilianzisha operesheni ya siri sana kwa lengo la kulipiza kisasi kwa wahusika wote walioshiriki kuwaua wayahudi wenzao.Na wengi wa wafuasi wa Nazi walikimbilia Argentina wakabadili majina na mfumo mzima wa maisha.Hivo basi bwana Frits alitoa taarifa za sehemu anakoishi Eichman kufuatia kujulishwa nab inti yake ambaye alikuwa anaishi huko sasa Mossad wakaanzisha rasmi operesheni ya kumkamata na kumrejesha Eichman nchini kwao akiwa hai au mfu.Mossad walianza operesheni hii kutafuta hasa kama kweli Eichman alikuwa bado anaishi baada ya upepelezi wa muda mrefu waligundua kitongoji ambacho alikuwa anaishi akiwa na jina lingine na utambulisho tofauti kabisa ambao ilikuwa sio rahisi kugundulika
Sasa basi Mossad walimpa kazi jasusi mmoja aliyeitwa Ahoron alikuwa kijana mdogo mwenye akili nyingi,alifika Argentina katika jiji la Buenos Aires,hapa aliweza kupata taarifa za sehemu bwana Eichman alikokuwa anaishi,na jina jipya alilojibadilisha alikuwa anaitwa Ricardo Klement,baada ya kufika mtaa walikoelekezwa walikuta nyumba ikiwa haina mtu ni gofu,hapa ilibidi sasa wao Mossad waende kwenye wakala wa kupeleka vifurushi wakatengeneza zawadi ya na kumtaka wakala awasilishe kwa muhusika,hii kampuni ya uwakala ikaanza kazi ya kutafuta makazi ya Bwana Eichman (Ricardo) na baada ya siku mbili wakafanikiwa kupapata na kumkabidhi mzigo wake,wakati wote agenti wa siri wa Mossad alikuwa nyuma kumfuatilia yule wakala wa kusambaza zawadi.Sasa baada ya kupata nyumbani kwa bwana Ricardo yule Jasusi alifika hapo kesho yake akiwa amevalia suti ya kimarekani ambako alijitambulisha kama mfanyabiashara kutoka kampuni moja kutoka USA na wanataka kuwekeza kiwanda hapo,hivo wanataka kununua eneo lote hilo kwa matumizi yao,wakati akijieleza alikuwa na camera ndogo ambayo haikuonekana akawa anapiga picha mbalimbali maeneo hayo,yule jirani akajibu kuwa hawatauza ila ngoja aongee na familia yake kesho yake angetoa majibu.Bwana Ahoron Jasus wa Mossad alirejea alikofikia na kwa kutumia uzoefu wake aliingiza zile picha kwenye mfumo wa masjila ya mji wa Buenos Aires ambako ilionyesha kuwa ni eneo binafsi mali ya Ms.Vera Liebl de Eichmann,huu ubini ukawa moja ya kielelezo muhimu kuwa mwenye nyumba ni ndugu na Ricardo mtu wanayemtafuta>Baadae walikuja kugundua kuwa Vera ni mke wa Eichman ingawa walishaachana kitambo ila kwa tamaduni za Argentina bado mke ataendelea kutumia ubini wa mumewe.
Mwandishi anasema kuwa baada ya kugundua makazi haya ilitumwa timu ya watu 12,ili kumkamata na ilipendekezwa akamatwe na apelekwe Israel akiwa hai yaani alikuwa na dhamani kubwa akiwa hai kuliko akiwa mfu.Mossad wana tabia ya kuingia kwenye nchi nyingine kijasusi na mar azote hutokea nchi jirani…huwa na paspoti za mataifa mengine ili kuficha utambulisho wao,na huingia kama watalii au wawekezaji.Sasa hawa watu 12 wote waliingia Argentina kila mmoja kutoka sehemu tofauti na wakiwa na paspoti tofauti,walipofika Argentina walikutana na kutengeneza NGOME na kugawana majukumu ya namna bora ya kumteka Eichman..Sasa basi Mossad wakaweka mtego na ikatokea bahati nzuri kulikuwa na maadhimisho ya kitaofa nchini Argentina ambako Serikali ya Israel ilikuwa inawakilishwa na waziri wake wa Elimu,hii ilikuwa fursa kubwa kwa Mossad hivo wakaazimia kuwa waziri asafiri na ndege binafsi,hili jambo lilifanywa bila waziri kujulishwa msingi wake,kuanzia rubani hadi wahudumu wa ndege walichaguliwa na Mossad na wengi walikuwa majasusi.Kule nchini Argentina kile kikosi cha watu kumi na mbili kiliendelea na mipango na walikodisha apartment ambayo iliwekewa mfumo wote wa ulinzi na uokozi,ikiwepo hadi handaki la kutoroka ikitokea polisi wa Argentina wamegundua kuhusu mpango kabla
Sasa mpango kamili ukawa kama ifuatavyo siku ya kutekwa Eichman angekamatwa akiwa anaingia nyumbani kwake,Mossad walikodisha gari mbili moja ya kumteka na moja kwa ajili ya ulinzi,ile ya kumteka ingeegeshwa nje kidogo ya nyumbani kwa Eichman alafu ingefanywa kama vile imeharibika na moja ya Mossad angeingia chini kama anaitengeneza(Kumbuka walishamfuatilia Eichman kwa muda mrefu na walikuwa wanajua muda wa kuingia nyumbani jioni)siku ya tukio walipanga kumsubiri hadi saa mbili kamili usiku awe amefika na ikatokea kuwa hajatokea basi waondoke,wale jamaa wakasubiri hadi saa mbili na robo Eichman alikuwa hajatokea,wakaongeza dakika kumi Zaidi wakiwa katika kukata tamaa ghafla wakaona basi limeshusha abiria kumbe ni Eichman sasa yule jasusi aliyepangwa akamsemesha Eichman alipogeuza shingo akarukiwa chapu na kuingizwa kwenye gari wakamtaka atii sharia bila shuruti…gari zikaondoka mwendo wa kasi hadi kwenye ile Apartment…baada ya kumgagua kwa kina wakajiridhisha kwa kina kuwa ndie muhusika wao..baadae alihojiwa majina yake,na namba yake ya Nazi,namba ya kiatu etc,bwana Eichman alitoa ushirikiano mkubwa kujibu maswali yote.Eichmann alieleza yote baada ya kugundua kuwa ametiwa nguvuni na watu ambao alikuwa amewatoroka kwa miaka mingi,alieleza jinsi alivojibadilisha majina na kupata Uraia wa Argentina na jinsi ambavo chama cha Nazi kilikuwa kinawaunga mkono kupitia taasisi zao za siri,alifikiri kuwa sasa angemalizia maisha yaliyobaki kwa Amani
Sasa ikatokea kitu ambacho hakikutarajiwa ile sherehe iilikuwa ifanyike May 10 ikasogezwa mbele hadi Mei 19,hivo walilazimika kukaa na mteka kwa siku tisa jambo ambalo ni hatari sana.Kiongozi wa hii operesheni akalazimika kuwaelekeza wale majasusi waliomshikilia Eichman kuwa ikatokea wakakamatwa na polisi basi wajitambulishe kwa utambilisho rasmi kuwa wao ni Waisrael wamemkamata mtuhumiwa namba moja wa Nazi(kumbuka hawa majasusi walikuwa na utambulisho tofauti tofauti)..pia ikatengeneza document feki inayoonyesha kuwa Eichman amekiri makossa yake na ameomba kupelekwa Israel ili akashtakiwe mahakamani
I, the undersigned Adolf Eichmann, of my own free will hereby declare: now that my real identity has been discovered, I recognize that there is no further use in trying to evade the course of justice. I agree to be taken to Israel and stand trial before a qualified tribunal. It is understood that I shall be given the assistance of an advocate and that I shall be permitted to lay before the court, without travesty of the facts, an account of the last years of my service in Germany, so that a truthful description of those events may be passed on to the future generations.I am making this declaration of my own accord. Nothing has been promised to me and I have not been threatened. My desire is to find inner peace at last. As I am unable to remember all the details,and may become confused when stating the facts, I ask that the relevant documents and testimonies be placed at my disposal to help me in my efforts to establish the truth. Adolf Eichmann, Buenos Aires,May 1960.
This declaration, of course, had no legal validity.
Mei 20 ndege ilipangwa kuondoka,hivo Mossad walimvalisha Eichman kama muhudumu wa ndege na wakatengeneza ripoti feki ya kitabibu kuwa muhudumu ameugua na yupo hoi kwenye kiti cha kubebea wagonjwa.Eichman aliingizwa uwanjani kwa utaratibu huo(Mossad walikuwa wanatembea na kila kitu ikiwepo mtambo maalum wa kutengeneza kila aina ya nyaraka iliyohitajika ikiwepo vitambulisho,pamoja na pasi mbalimbali).Mwaka 1961 Eichman alifikishwa kortini kujibu tuhuma zake mahakama ilimkuta na hatia na alihukumiwa kunyongwa hadi kufa,haya ndio maneno yake ya mwisho
: “We’ll meet again …I have lived,believing in God …I obeyed the laws of war and was loyal to my flag …”
Mkuu huyo fashisti alipewa pombe akalewa chakari wakati akipitishwa uwanja wa ndege, hii alitupatia the Bold
 
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Mishal Nissim
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 7


Where is Yoselle


Mwandishi anasema kuwa Yossele Schuchmacher, alikuwa mtoto wa miaka nane ambaye alitoweka katika mazingira tatanishi,baadae ilikuja kujulikana kuwa alikuwa ametekwa na babu yake mwenye itikadi kali ya Ordhodox,sasa kukawa na mgogoro ambao ulikuwa kutoka ngazi ya kitamilia hadi kufikia kutishia kugawa Taifa,ilifika mahali hofu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ikawa inanunukia..mjadala ukawa wa kitaifa hadi kwenye bunge lao maarufu kama KNESSET.


Kufuatia mgogoro kukua ilibidi waziri mkuu aombe msaada wa Mossad kutafuta wapi mtoto aliko,Mossad wakaanzisha operesheni waliyoita Operation Tiger Cub.
Huyu babu yake Yoselle alikuwa pande la mtu ambaye alipigana vita ya pili ya Dunia na alikuwa amepoteza jicho moja vitani pamoja na kucha kadhaa,alikuwa mtu mwenye msimamo usioyumba,aliamini mjukuu wake alikuwa mtoto mzuri isipokuwa alizaliwa na wazazi wabaya...wasiokuwa na imani.


Mossad walikubali hii kazi ingawa ni nje ya majukumu yao,sasa ndani ya Mossad kuna idara ya ulinzi wa ndani inaitwa Shabak au kifupi Shin ilikuwa chini ya Jasusi Mbobezi Isser Harel,huyu jamaa alikuwa ameshiriki operesheni nyingi sana na hakuwahi kumshirikisha mkewe,ila kazi hii ya kipolisi aliamua kumjulisha mkewe kuwa Taifa lipo hatarini kumeguka kutokana na utata wa kutoweka kwa mtoto
Sasa basi Jasusi Isser Harel akaanzisha team ya watu 40 wabobevu na raia waliojitolea wengi wakiwa dhehebu la Orthodox ambako walikuwa na msimamo wa wastani na waliolewa hatari ya dhehebu lao kuhusishwa.Jitihada kubwa ilifanyika kwa kutumia ubandia ndani ya ardhi ya Israeli na nje ya mipaka ikiwepo UK,Ufaransa,Italia,USA etc kote huko hawakufua dafu.
Mwandishi anasema ilibidi Shabak wawaingize mawakala ndani ya kanisa Orthodox walijifanya wafia dini na wenye msimamo mkali...wakala mmoja wa kike alipenya na aliaminika ni mfia dini ambaye viongozi walimwamini na kumpeleka London kwa mafunzo zaidi,hapa London alitakiwa kufikia kwa yule babu wa Yossele ambaye wakati huo alikuwa anaishi London akiendelea na kazi za dini yake.Jitihada hizi zilisaidia kupatikana kwa taarifa ambazo zilikuja kusaidia kupatikana kwa mtoto,Mossad waligundua kuwa yule babu alimtoa mtoto kwa mama mmoja ambaye alimbadilisha majina na tarehe za kuzaliwa ili kuficha kabisa utambulisho.Ikatokea huyu mama akawa anafuatiliwa akiwa kwenye rada akaweka tangazo kwenye magazeti ya Ufaransa kuwa anauza nyumba yake iliyoko USA,Mosaad wakajibu haraka kuwa wanataka kuinunua...mama bila kujua ni mtego akakubali kufanya biashara na wanapanga siku ya kukutana jijini Paris,mnunuzi ambaye ni Mosad alijitambulisha kama raia wa Ufaransa,wakafika kwenye hotel moja kubwa hapo hotelini yule Mnunuzi akasema wakili wake amechelewa kufika na ameomba wamfuate ofisini..bila hiyana mama akakubali walipofika ofisini kwa Wakili kumbe ni safe house ambayo Mossad waliandaa kwa ajili ya kufanya mahojiano na watu mbalimbali kwenye hii operesheni......Mossad wakiwa wamemteka Mama kule nchini Israel walimshikilia mtoto wake hivo mama na mtoto wakawa wanahojiwa kwa wakati mmoja
Hii ni mbinu ambayo hutumika kumlainisha target hasa kama ni mtu ambaye ni mgumu kufunguka...kwa huyu mama hii mbinu ilifeli,nguvu pia ikafeli...baadae Bwana Isser Harel akabadili mbinu hii ilikuwa siku ya kumi mama na mtoto wakiwa wameshikiliwa katika nchi mbili tofauti lakini mama hakufungua mdomo
Hivo basi ikalazimu sasa Bwana Isser akiri kuwa yeye ni afisa wa Mossad na wanamtafuta Yosele kwa ajili ya usalama wa Taifa na sio kwamba wapo kinyume na dini,haya maneno malaini yakaanza kumwingia huyu mama .Mama alikiri kumtorosha mtoto akiwa kwenye mavazi ya kike kwa sababu za kiimani..na alikuwa amemficha New York akiwa na majina mengine,mara moja Mossad waliwasiliana na wakala wao ambaye aliomba kibali cha FBI,FBI waligoma hapo ndio Isser Harel akampigia simu bwana Robert Kennedy ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa USA akamtaka mara moja atoe kibali haraka sana,ndani ya masaa machache FBI walifika wakiwa na Mossad anbako walimkuta mtoto kwenye eneo waliloelekezwa na yule mama,na siku hiyo hiyo wakamrejesha kwa wazazi wake nchini Israel...
Hii operesheni ilichukua miaka miwili..na iliendelea kufanya Mossad ipendwe na raia na hadi leo ni miongoni mwa mashirika ya siri ambayo yanapendwa na raia wake wa kawaida
 
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Mishal Nissim
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 7


Where is Yoselle


Mwandishi anasema kuwa Yossele Schuchmacher, alikuwa mtoto wa miaka nane ambaye alitoweka katika mazingira tatanishi,baadae ilikuja kujulikana kuwa alikuwa ametekwa na babu yake mwenye itikadi kali ya Ordhodox,sasa kukawa na mgogoro ambao ulikuwa kutoka ngazi ya kitamilia hadi kufikia kutishia kugawa Taifa,ilifika mahali hofu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ikawa inanunukia..mjadala ukawa wa kitaifa hadi kwenye bunge lao maarufu kama KNESSET.


Kufuatia mgogoro kukua ilibidi waziri mkuu aombe msaada wa Mossad kutafuta wapi mtoto aliko,Mossad wakaanzisha operesheni waliyoita Operation Tiger Cub.
Huyu babu yake Yoselle alikuwa pande la mtu ambaye alipigana vita ya pili ya Dunia na alikuwa amepoteza jicho moja vitani pamoja na kucha kadhaa,alikuwa mtu mwenye msimamo usioyumba,aliamini mjukuu wake alikuwa mtoto mzuri isipokuwa alizaliwa na wazazi wabaya...wasiokuwa na imani.


Mossad walikubali hii kazi ingawa ni nje ya majukumu yao,sasa ndani ya Mossad kuna idara ya ulinzi wa ndani inaitwa Shabak au kifupi Shin ilikuwa chini ya Jasusi Mbobezi Isser Harel,huyu jamaa alikuwa ameshiriki operesheni nyingi sana na hakuwahi kumshirikisha mkewe,ila kazi hii ya kipolisi aliamua kumjulisha mkewe kuwa Taifa lipo hatarini kumeguka kutokana na utata wa kutoweka kwa mtoto
Sasa basi Jasusi Isser Harel akaanzisha team ya watu 40 wabobevu na raia waliojitolea wengi wakiwa dhehebu la Orthodox ambako walikuwa na msimamo wa wastani na waliolewa hatari ya dhehebu lao kuhusishwa.Jitihada kubwa ilifanyika kwa kutumia ubandia ndani ya ardhi ya Israeli na nje ya mipaka ikiwepo UK,Ufaransa,Italia,USA etc kote huko hawakufua dafu.
Mwandishi anasema ilibidi Shabak wawaingize mawakala ndani ya kanisa Orthodox walijifanya wafia dini na wenye msimamo mkali...wakala mmoja wa kike alipenya na aliaminika ni mfia dini ambaye viongozi walimwamini na kumpeleka London kwa mafunzo zaidi,hapa London alitakiwa kufikia kwa yule babu wa Yossele ambaye wakati huo alikuwa anaishi London akiendelea na kazi za dini yake.Jitihada hizi zilisaidia kupatikana kwa taarifa ambazo zilikuja kusaidia kupatikana kwa mtoto,Mossad waligundua kuwa yule babu alimtoa mtoto kwa mama mmoja ambaye alimbadilisha majina na tarehe za kuzaliwa ili kuficha kabisa utambulisho.Ikatokea huyu mama akawa anafuatiliwa akiwa kwenye rada akaweka tangazo kwenye magazeti ya Ufaransa kuwa anauza nyumba yake iliyoko USA,Mosaad wakajibu haraka kuwa wanataka kuinunua...mama bila kujua ni mtego akakubali kufanya biashara na wanapanga siku ya kukutana jijini Paris,mnunuzi ambaye ni Mosad alijitambulisha kama raia wa Ufaransa,wakafika kwenye hotel moja kubwa hapo hotelini yule Mnunuzi akasema wakili wake amechelewa kufika na ameomba wamfuate ofisini..bila hiyana mama akakubali walipofika ofisini kwa Wakili kumbe ni safe house ambayo Mossad waliandaa kwa ajili ya kufanya mahojiano na watu mbalimbali kwenye hii operesheni......Mossad wakiwa wamemteka Mama kule nchini Israel walimshikilia mtoto wake hivo mama na mtoto wakawa wanahojiwa kwa wakati mmoja
Hii ni mbinu ambayo hutumika kumlainisha target hasa kama ni mtu ambaye ni mgumu kufunguka...kwa huyu mama hii mbinu ilifeli,nguvu pia ikafeli...baadae Bwana Isser Harel akabadili mbinu hii ilikuwa siku ya kumi mama na mtoto wakiwa wameshikiliwa katika nchi mbili tofauti lakini mama hakufungua mdomo
Hivo basi ikalazimu sasa Bwana Isser akiri kuwa yeye ni afisa wa Mossad na wanamtafuta Yosele kwa ajili ya usalama wa Taifa na sio kwamba wapo kinyume na dini,haya maneno malaini yakaanza kumwingia huyu mama .Mama alikiri kumtorosha mtoto akiwa kwenye mavazi ya kike kwa sababu za kiimani..na alikuwa amemficha New York akiwa na majina mengine,mara moja Mossad waliwasiliana na wakala wao ambaye aliomba kibali cha FBI,FBI waligoma hapo ndio Isser Harel akampigia simu bwana Robert Kennedy ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa USA akamtaka mara moja atoe kibali haraka sana,ndani ya masaa machache FBI walifika wakiwa na Mossad anbako walimkuta mtoto kwenye eneo waliloelekezwa na yule mama,na siku hiyo hiyo wakamrejesha kwa wazazi wake nchini Israel...
Hii operesheni ilichukua miaka miwili..na iliendelea kufanya Mossad ipendwe na raia na hadi leo ni miongoni mwa mashirika ya siri ambayo yanapendwa na raia wake wa kawaida
Daaah asee
 
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Mishal Nissim
Mchambuzi.Nanyaro EJ


Chapter 8


NAZI HERO AT THE SERVICE OF THEMOSSAD


Mwandishi anasema kuwa wiki mbili tangu Yosele apatikane,ambayo ni mwaka 1962 Misiri ilizindua makombora yaliyoushangaza ulimwengu,kombota lilikuwa na ukubwa wa 175maili na 375, Rais wa Misri Abdul Naser alijigamba kuwa wana uwezo wa kumpiga yoyote,kuanzia kusini hadi kaskazini.Katika ulimwengu wa kijajusi hii ilikuwa taarifa nyeti ba Israel waliogopa zaidi kwa kuwa sasa wangeweza kushambuliwa sehemu yoyote.
Mossad wakaanzisha operesheni ya kutambua kiwango cha uwezo wa kijeshi wa misri na kutambua wapi wanapata teknolojia,baada ya miezi miwili waligundua kuwa Misri wanauziwa teknolojia na Ujerumani hasa waliokuwa wanachama wa Nazi!.Hadi wakati huu yaani 1963 Misri walikuwa wameajiri wanasayansi zaidi ya 300 kutoka Ujerumani ambao walishaanza ku asemble ndege za kivita .Mossad wakaenda hatua moja mbele,kwenye uchunguzi wao waligundua kuwa kuna Bwana Mmoja Mjerumani anaishi Madrid Spain na ambaye ndio alikuwa kitovu kwa maana ya fedha zilikuwa zinapitia kwake,wakamfuata ofisini kwake ambayo ilikuwa ni kampuni ya Injinia,wakajitambulisha na kumjulisha kuwa wamemkata Eichman na yeye akibisha atakamatwa Mossad wakampa ofa ya maisha (Uhai)na fedha nyingi..jamaa hakuwa na la kufanya


Ujerumani na Misiri zilianzisha kile majasusi wanaita front companies..hizi ni kampuni zinazoliwa chini ya umiliki wa shirika la ujasusi kwa lengo maalum,sasa miongoni mwa hizi kampuni ni pamoja na Meco,Intra-Handel,” “Patwag,” and “Linda”—ambazo zilipewa kandarasi ya kuuza vifaa mbalimbali kwa ajili ya miradi tajwa.


Mwandishi anasema kuwa ndani ya Mossad iliaminika kuwa Ujerumani ilikuwa inaisadia Misri kama mpango wa kulipiza kisasi kwa Wazayuni.Sasa kukawa na sintofahamu kubwa maana Ujerumani ilikuwa mshirika wa karibu wa Serikali ya Israel illikuwa imetoa mkopo wa usd500mil(ilikuwa pesa nyingi sana mwaka 1962 na hata leo 2020 ni pesa nyingi)na pia Ujerumani ilikuwa unafadhili mradi wa Silaha wa Negev uliomilikiwa na Israel,Chancelor wa Ujerumani na Waziri mkuu walikuwa na urafiki binafsi,kufuatia utata huu Mossad wakaamua kufanya mauaji bila kumshirikisha Waziri mkuu,haya yalikuwa mauaji ya kitaalam yalihusisha watu wachache sana ndani ya Mossad,sasa basi
Novemba 27, Bwana Hannelore Wende, ambaye alikuwa katibu katika kiwanda 333 alipokea email kutoka kwa wakili Jijini Humburg aliyemjua alipofungua kumbe ilikuwa kirusi kikalipuka na kuunguza ofisi yote na waliokuwepo hawakufa ila walipofuka na kuwa viziwi wote miili ikiwa na majeraha makubwa
siku iliyofuata bahasha kubwa iliyokuwa na imeandikwa vitabu ilipokelewa ofisini hapo hapo ilipofunguliwa ikalipuka na kuua watu watano na wengine wengi kujeruhiwa,ziliendelea kupokelewa barua na mizigo iliyokuwa na milipuko,wanasayansi waliingia upepo maana maisha yao yalikuwa hatarini...wengi walipokea simu za vitisho pamoja na familia zao,hii ilipelekea wengi kuacha kazi kwa hofu hapa ndio Mossad walikuwa wanapataka...baadhi walianza kujisalimisha kwa Mossad kama njia ya kuokoa maisha! Kwa mkwara huu Mosaad walipata Wajerumani wengi ambao waligeuka kuwa Sleeping agents
 
Asante sana mkuu,ukipata muda ulete muendezo.
 
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Sehemu ya 9

OUR MAN IN DAMASCUS

Mwandishi anaanza kwa barua hii ….Mpenzi Mke wangu Nadia,nakuandikia haya maneno machache nikitarajia kuwa utabaki salama,naomba unisamehe na jitahidi kumsomesha mtoto wetu apate elimu bora,Mpenzi wangu Nadia kama itakupendeza unaweza kuolewa tena na mwanamume utakayempenda wewe,ili watoto wetu wawe na malezi ya Baba,nakuomba sana usiomboleze juu yangu wala usitazame ya nyuma,bali songa mbele.Niombee kwa mola.Wako Elie
Hii ni barua ilifika ofisi za Mosad Mei 1965,kutoka kwa jasusi bobevu la wakati wote Elie Cohen,aliandika barua hii dakika chache kabla ya kunyongwa Jijini Damascuss akiwa na mikono inayotetemeka…kwenye kifo hakuna jasusi
Maisha ya usiri wa hali ya juu ya Elie Cohen yalianza na kudumu kwa miaka Zaidi ya 20.Huyu jamaa alikuwa mzayuni aliyekulia nchini Misiri,ambako alifanya kazi ya ujasusi akafanikiwa kupenya kwenye vyombo vya ulinzi na usalama ambako aliajiriwa
Kufuatia Syria kuanza kuwa adui wa Israel Mossad waliagiza Uniti 131 kuanza operesheni maalum yenye lengo la kujua na kutambua mipango yote ya Syria,ambayo ilianza harakati za kutaka eneo la Golan Heightes pamoja na kugawa maji ya mto Jordan,chanzo muhimu cha maji kwa nchi ya Wazayuni hivo Elie Cohen alipewa jukumu hili zito,kabla ya kupewa kazi hii alifanyiwa mafunzo maalum ikiwepo,jinsi ya kuwa na kumbukumbu bila usaidizi
Somo la mwisho kwa huyu Elie Cohen ilikuwa kupewa passport ya Misiri akatakiwa aseme kuwa yeye ni Mmisiri aende Jerusalem kwa siku kumi,ndani ya hizo siku kumi atengeneze mtandao wake,marafiki,alipaswa aongee kifaransa na kiarabu tu,na kuwa ajitambulishe kama mtalii kutoka Misri amekuja kutembea.Alipaswa asijulikane kwa utambulisho wake halisi na ahakikishe kuwa hakuna mtu anamstukia wala kumfuatilia.Alihitimu vizuri baada ya siku kumi kisha ikafuatiwa na kufunzwa masomo Fulani ya Kurani takatifu…baada ya haya alipaswa kusafiri kwenda nchi Fulani nje ambako alipaswa aishi kama Mwislamu na ategeneze mtandao wake,sasa basi huyu Elie Cohan alibadilishwa jina na akaitwa Kamal Amin Tabet,mama yake mzazi ataitwa Saida Ibrahim na alikuwa na dada ambao wametangulia mbele ya haki,walizaliwa Beirut nchini Lebanon na alipokuwa na miaka mitatu wazazi wake walihamia Alexandria nchini Misiri.Wazazi wake wote wawili ni kutoka nchini Syria,Mjomba wako alihamia nchini Argentina 1946 na mwaka mmoja baadae 1947 mjomba aliwakaribisha wazazi wako nchini Argentina ambako walipata fursa ya kufungua kiwanda kidogo cha ushonaji,hata hivo kilifilisika na baba kufariki kutokana na stress za maisha,miezi sita baadae mama yako alifariki kwa msongo wa mawazo,hivo mjomba wako aliendelea kukulea.Baadae ulipata kazi kwenye shirika moja la usafirishaji kisha ukajiajiri baadae sana na ukafanikiwa.
Mwandishi anasema kuwa Bwana Elie Cohen aliporejea nyumbani kwake alimwambia mkewe kuwa amepata kazi kwenye kamouni binafsi inayofanya kazi na wizara ya mambo ya nje na hivo wamemwajiri na atakuwa anasafiri ulaya mara kwa mara na wakati mwingine kukaa huko kwa muda…hii Kamba mke alielewa maana sasa maisha yalikuwa yanabadilika na mumewe angelipwa fedha za kutosha….
Mto Jordan ndio uti wa mgongo wa Taifa la Israel,bila mto Jordan Israel haiwezi kuishi
Mwaka 1961 Elie Cohel alisafiri akiwa na passport yake halisi kwenda Zurich ambako alipokelewa na mtu ambaye alimpatia passpot ingine ya nchi ya Ulaya ikiwa na viza ya nchi ya Chile na Argentina.Siku iliyofuata alisafiri tena kwenda Argentina na alipewa anuani ya mahali pa kufikia,alipofika alipokelewa na kupewa utambulisho mpya sasa wa Kamali
Miezi mitatu baadae Elie alikuwa amejifunza Spanish,na alikuwa analijua kila kichochoro cha Jiji la Buenos Aires,na aliishi kama raia kutoka Uarabuni.Hapa alipaswa sasa kuanza kutembelea migahawa na vijiwe ambavo waarabu walipendelea,na kutakiwa kutengeneza marafiki na mtandao mkubwa kwa kadri awezavyo.Hii ilikuwa rahisi maana Mossad walimjaza hela za kutosha hivo alikuwa analipa bill na kutoa mchango wa fedha sana kwa jamii ya watu kutoka uarabuni,yaani alijifanya mwarabu hasa
Mossad walimfungulia kampuni ambayo yeye ndio alikuwa mkurugenzi,na kupitia kampuni hii akaanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kusaidia jamii ya waarabu.Kufuatia kujiamini kwake,ucheshi na ukarimu wake haikuchukua muda akajikuta mtu muhimu sana kwenye jamii ya waarabu,na aliaminika sana.Bwana Elie aka Kamali alikuwa mtu mwenye akili nyingi sana,mbele ya macho ya Wasyria walioishi Argentina alionekana kama shujaa na mzalendo,siku moja alifika Ubalozi wa Syria nchini Argentina ambako alishatengeneza mtadao wake na kuomba apewe barua ya utambulisho ili arejee nchini kwao ambako anaipenda sana maana hakumjua mtu yoyote.Ubalozi haukusita wala kuwa na wasiwasi nae,akaandikiwa barua za utambulisho kwenye vyombo mbalimbali nchini Syria
Mwisho wa mwaka 1961 Elie aka Kamali alipanda ndege kwenda Zurich kisha Munich,ambako alikutana na Mossad wakampa tiketi na passpot ya Israel ili arejee kwanza nchini kwao kwa muda mfupi.Kipindi hii alikitumia kusoma saana kuhusu silaha za Syria,jeshi lake,mfumo wake wa mawasiliano jeshini etc.Alirejea Zurich kisha kupanda ndege ya kwenda Damascuss
Wakati anafika Damascuss uhusiano na Israel ulikuwa tete sana
Sasa basi Elie Cohen alipewa kila aina ya vifaa kuanzia redio maalum,hadi vidonge vya kujiua ikibidi kufanya hivo.Alifanikiwa kuingia nchini huko kwa msaada wa rushwa,kwa kuwa alitaka kujulikana mapema aliamua kutafuta apatmenti nzuri jirani na makao makuu ya jeshi la Syria,aliamini akiishi eneo hili atakuwa salama na hakuna mtu atakuja kukagua apartment iliyo jirani na makao makuu ya jeshi.Sasa zile barua za utambulisho alizopewa nchini Argentina alizitumia vizuri sana,ndani ya muda mfupi alikuwa ameweza kupenya kwenye chama tawala,ambako alitoa msaada wa fedha,na kwa maofisa kadhaa wenye ushawishi serikali…alionekana kijana mwenye mafanikio makubwa na anayependa nchi yake na watu wake,aliendelea kutoa misaada kwa watu maskini katika jiji la Damascus.Wakati akiendelea kujipenyeza ndani ya serikali alitumia pia muda huo kuseti mitambo yake,alifunga transmita iliyoingilia mawasiliano ya jeshi na kuyapeleka nchini Israel makao makuu ya Mossad,mitambo hii aliifunga kwenye moja ya vyumba katika apartment yake aliyokuwa ameinunua,hapo jirani na makao makuu ya jeshi la Syria
Mwandishi anasema kuwa ilitokea kama ngekewa mwaka 1963 yule jamaa aliyekuwa amewambdikia barua za utambulisho bwana Kamali nchini Argentina,alikuja kuteuliwa Waziri wa Ulinzi wa Syria,huyu alikuwa rafiki binafsi wa Kamali,ndio kusema sasa mossad walikuwa na mtu ndani kabisa ya yaani inner circle of power.Kamali akaanza kutengeneza sherehe na hafla mbalimbali nyumbani kwake,na kuwaalika majenerali wa jeshi pamoja mawaziri,,unaambiwa hapo nyumbani kwake magari ya kifahari ya wakubwa na wafanyabiashara maarufu yalikuwa hayakauki..alifuata ile falsafa ya magharibi …kuwa mweke rafiki yako karibu nawe ila adui yako mweke karibu Zaidi….Kamali alikuwa anawanunulia hadi zawadi za gharama kubwa.Kamali akawa mtu ndani ya Syria na akaanza kukaribishwa kwenye vikao vikubwa vya chama tawala kisha baadae akawa miongoni mwa watu wanaotoa ushauri kuhusu mambo ya uchumi ndani ya serikali
Kwa kuwa alikuwa ndani ya serikali alipata taarifa zote za kijeshi ambazo alizipeleka Israel kwa njia ya Transmita maalum,yaani kila siku alirusha transmita kupeleka taarifa sahihi.Kamali alifanikiwa kuaminisha jeshini kuwa anaichukia Israel kwenye mazungumzo yake,hii ilifanya aaminiwe na majeneral wakawa wanamtembeza kwenye kambi mbalimbali za kijeshi hata zile ambazo hakuna raia anaruhusiwa kufika…yaani Syria wakawa wanamwachia fisi bucha……
Pamoja na Udhaifu wa Syria lakini walingamua kuwa kuna jinsi taarifa zao zinavuja,walijua sasa wanauzwa,ila nani anawauza? Waligundua kuwa tangu mwaka 1964 kila uamuzi uliofanywa na Syria usiku au mchana ulikuwa unatumwa kwa lugha ya kiarabu nchini Israel,sasa wakaagiza shirika lao la siri Mukhabarat liingie kazini.Syria walijikuta wapo uchi mbele ya Wazayuni,hata uamuzi uliofanywa na watu watatu bado Wazayuni waliupata.Walihangaika kutafuta hii transmita kwa miezi sita bila mafanikio ila sasa walitambua tu kuwa kuna transmita swali likawa itakuwa wapi?
Syria walilazimika kuzima mitambo yote jeshini nchin nzima ili kutafuta hii transmita,ofisa aliyekuwa zamu aligundua mawimbi ambako walianza kutafuta yanarushwa kutoka wapi.Kabla ya kufika haya mawimbi na transmita vilizima ghafla ikawa kazi tena,,ila angalau walikisia eneo ambalo ni nyumba ya bwana Kamal,ofisa alishindwa kukubali kuwa bwana Kamali ambaye alitarajiwa kuteuliwa waziri kwenye baraza lijalo angeweza kuwa jasusi.Jioni ya siku hiyo ile transmita iliendelea na sasa waliamua kuvamia jengo la kifahari la bwana Kamali…katika hali ya kutoamini macho yao walimkuta bwana Kamali akiwa anafanya kazi yake ya kupeleka taarifa,akiwa na vifaa vyake,vifaa vya kila aina…yalikuwa maajabu hakuna aliyeamini,milionare,rafiki wa Rais,rafiki wa chama,mtu makini mwenye upendo anawezaje kuwa msaliti?ilikuwa ngumu kuamini lakini ushahidi ulikuwa wazi…ilibidi hata Rais aje amhoji,Rais wa Syria wakati huo alinukuliwa akisema alipomwangalia kwa makini akiwa selo aligundua kuwa huyu sio mwarabu bali ni Mzayuni…alishinndwa kutaja hata sura ya kwanza ya kurani…..
Taarifa za kukamatwa kwa Bwana Kamali,tajiri zilienea kama moto wa kifuu na hakuna aliyeamini
Akiwa kizuizini Kamali alipata kila aina ya mateso yampasayo Msaliti,aliteswa na kichapo cha kila aina hapa Duniani,alingolewa kucha,baada ya mateso makali alikiri kuwa hakuwa Kamali Tabet bali aliitwa Elie Cohen,haraka sana Damascuss ilitangaza kumkata jasusi wa Kizayuni.Watu 400 walihojiwa na 70 walikutwa na kesi ya kujibu,kitu cha ajabu ni kuwa robo tatu ya wanasiasa wa chama tawala cha Syria walikutwa walikuwa watu wa karibu sana na Elie,wapelelezi walishindwa kuwataja au kuwahoji kwa kuwa nchi ingepasuka vipande vipande
Serikali ya Israel iliamua kujaribu kumsaidia Elie hivo waliajiri wakili bora na maarufu kutoka Ufaransa kwa niaba ya familia.Wakili anasema alipofika tu Damascuss aligundua ameshashindwa tayari.Mamlaka za Syria zilihofia kuwa akiruhusiwa kupewa wakili ataeleza kila kitu mahakani hivo iliamuliwa kuwa hakuna mtu yoyote kuruhusiwa kumwona wala huduma ya wakili.Bwana Elie alipelekwa kwenye mahakama ya kijeshi ambako hakuruhusiwa kujitetea wala kusema chochote,alipoomba kuwa anahitaji wakili jaji akamjibu kuwa“You don’t need a defender.All the corrupt press is on your side, and all the enemies of the revolution are your defenders.” Huyu Jaji ambaye kabla alikuwa rafiki wa karibu wa Elie alikuwa Jenerali wa jeshi.Hii ndio kesi pekee ambayo Jaji alikuwa ndio yeye Mwendesha mashtaka,ndio yeye mjibu mashtaka,ndio yeye mlalamikaji na ndio jaji.Moja ya kichekesho kwenyen hili shauri ilikuwa swali ambalo Jaji alimwuliza mshtakiwa..(kimsingi walifahamiana sana na jaji alikuwa na hofu) akamwuliza unamfahamu jaji akataja jina lake..yeye Elie akamjibu hapana simwoni hapa chumbani…..
Jitihada kadhaa za Israel ikiwepo kutoa madawa pamoja na teknolojia ya kilimo,vyenye gharama ya mamilioni ya dola vilikataliwa….Israel ikatoa ofa ya pili ya kuwaachia majasusi 11 wa Syria waliokuwa wameshikiliwa nayo ikakataliwa…..mwisho Israel ikwatumia viongozi wakubwa akiwepo Pope Paul VI Mwanafalsafa wa Uingireza Bertrand Russell;Malikia wa Ubeligiji,wabunge 21 wa Uingereza na watu wengine wengi lakini haikufua dafu….walikataliwa
Mwisho alinyongwa na kabla ya kunyongwa alipewa fursa ya kuandika barua kwa famila yake.Ndiyo ile barua mwanzoni kabisa.Kifo chake cha kunyongwa kilirushwa mubashara kwenye TV zote za Syria
Hadi leo ndani ya Mossad Elie Cohen ni moja ya watu mashuhuri kabisa na wanaamini kuwa alikufa kifo ambacho wakala makini huwa wanakufa.
 
WAKUU WA MOSSAD

Reuven Shiloah, 1949–53
Isser Harel, 1953–63
Meir Amit, 1963–68
Zvi Zamir, 1968–73
Yitzhak Hofi, 1973–82
Nahum Admoni, 1982–89
Shabtai Shavit, 1989–96
Danny Yatom, 1996–98
Efraim Halevy, 1998–2002
Meir Dagan, 2002–2011
Tamir Pardo, 2011–2016
Yossi Cohen, 2016–present


Kwa kumbukumbu zangu Ariel Sharon hakuwahi kuwa mkuu wa mossad, au hata kufanya kazi mossad.
 
Back
Top Bottom