Uchaguzi 2020 Uchambuzi wa hotuba ya Lissu - Kawe

Uchaguzi 2020 Uchambuzi wa hotuba ya Lissu - Kawe

Leo nimefurahishwa Lissu kaongea huku ametulia tena kawa mpole, naona keshasoma upepo.

Katika hotuba yake naomba nichambue kidogo maelezo yake, kimsingi hayo aliyoyaelezea yaliwahi kutekelezwa na awamu zilizopita na yakashindikana, ni maneno yakuombea kura tu sio yakiutekelezaji.

1. Kuhusu fao la kujitoa, zipo changamoto za kiutendaji hasa uwezo wa mifuko yenyewe hivyo anaposema mtu ukipugwa tu ukachukue fedha zako. Labda angetueleza kiwango cha labour turnover kikoje, kama wanao acha kazi ni wengi kuliko wanao ajiriwa basi itakuwa pyramid financing, itafika sehemu ita collapse yenyewe. Kwanza tuangalie kwanini kijana afanyekazi miaka kumi halafu apoteze ajira yake na iwe mwisho wa tumaini lake kimaisha, tatizo ni nini? Kinacho mfanya asifanye kazi hadi uzeeni ni nini tunapaswa kuangalia "job security" ya watumishi wetu na sio kukimbilia kuwapa fedha ili wakafie mbele. Kabda ya kufikia huo uamuzi tunapaswa kuwa na labour data base kwanza tujue uwezo wa nguvukazi ya taifa.

2. Vitambulisho vya machinga, kule mbeya alisema atavifuta leo kasemea dosari zake hivyo naamini wazo lake la kuvifuta kaliondoa hivyo siwezi kuzungumzia kwani hajasema atafanya nini juu ya hilo

3. Kuhusu upunguzaji kodi, naona kaongea kienyeji sana labda mikutano ijayo atalitolea ufafanuzi, kasema importers wana kodi 15 yeye atazifuta ibaki moja, kwa kuwa kazitaja kwa idadi basi anazijua vizuri ni vyema akatuambia atafuta kodi zipi? Kwa uchache kuna import duty, exercise duty, vat, income tax etc. Hizi kodi zingine ni mfumo wa kimataifa chini ya WTO hiyo mifumo inafanana duniani sasa sijui anamaanisha Tanzania itajiondoa WTO, ipo mifumo ya SADC na EAC common customs kauli yake ni too skeleton na haijitoshelezi. Mfumo huu aliutumia Rais Mwinyi na ndio chanzo cha kuua viwanda vyetu vya ndani sasa anataka kuturudisha kulekule kwenye ruksa sio?

4. Kulipa fidia kwa maana ya kutibu vidonda, akumbuke kuna wahindi walinyanganywa nyumba zao wakati wa azimio la arusha nao watafidiwa? kuna makampuni ya Rockefeller na Mackenzie yalitaifishwa mashamba ya chai kahawa pareto je nayo yatafidiwa? vipi kuhusu bank ya Barclays UK ambayo ilitaifishishwa na kuanzishwa BOT nayo itafidiwa? Mgodi wa Geita Mine nao ataurudisha kwa Wajerumani? Ni vyema Chadema wakatafakari upana wa tatizo wanalotaka kulitengeneza.

5. Kuvutia wawekezaji, huu mfumo ndio alioutumia mzee wetu marehemu Mkapa, sote tunajua yaliyotupata na hatujasahau naomba usiturudishe huko, hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji tusidanganyane. Kwanza ukilegeza mfumo wa kodi hakuna mwekezaji atakuja wekeza labda wachimba mafuta gesi na dhahabu. Mambo amabayo yeye Lissu amekuwa akiyapiga vita tangu zamani huko ubelgiji wamempa nini? Kiujumla mawazo ya Lissu ni yakienyeji sana na yaliyopitwa na wakati.
Uchambuzi wako hauna mashiko.
 
Leo nimefurahishwa Lissu kaongea huku ametulia tena kawa mpole, naona keshasoma upepo.

Katika hotuba yake naomba nichambue kidogo maelezo yake, kimsingi hayo aliyoyaelezea yaliwahi kutekelezwa na awamu zilizopita na yakashindikana, ni maneno yakuombea kura tu sio yakiutekelezaji.

1. Kuhusu fao la kujitoa, zipo changamoto za kiutendaji hasa uwezo wa mifuko yenyewe hivyo anaposema mtu ukipugwa tu ukachukue fedha zako. Labda angetueleza kiwango cha labour turnover kikoje, kama wanao acha kazi ni wengi kuliko wanao ajiriwa basi itakuwa pyramid financing, itafika sehemu ita collapse yenyewe. Kwanza tuangalie kwanini kijana afanyekazi miaka kumi halafu apoteze ajira yake na iwe mwisho wa tumaini lake kimaisha, tatizo ni nini? Kinacho mfanya asifanye kazi hadi uzeeni ni nini tunapaswa kuangalia "job security" ya watumishi wetu na sio kukimbilia kuwapa fedha ili wakafie mbele. Kabda ya kufikia huo uamuzi tunapaswa kuwa na labour data base kwanza tujue uwezo wa nguvukazi ya taifa.

2. Vitambulisho vya machinga, kule mbeya alisema atavifuta leo kasemea dosari zake hivyo naamini wazo lake la kuvifuta kaliondoa hivyo siwezi kuzungumzia kwani hajasema atafanya nini juu ya hilo

3. Kuhusu upunguzaji kodi, naona kaongea kienyeji sana labda mikutano ijayo atalitolea ufafanuzi, kasema importers wana kodi 15 yeye atazifuta ibaki moja, kwa kuwa kazitaja kwa idadi basi anazijua vizuri ni vyema akatuambia atafuta kodi zipi? Kwa uchache kuna import duty, exercise duty, vat, income tax etc. Hizi kodi zingine ni mfumo wa kimataifa chini ya WTO hiyo mifumo inafanana duniani sasa sijui anamaanisha Tanzania itajiondoa WTO, ipo mifumo ya SADC na EAC common customs kauli yake ni too skeleton na haijitoshelezi. Mfumo huu aliutumia Rais Mwinyi na ndio chanzo cha kuua viwanda vyetu vya ndani sasa anataka kuturudisha kulekule kwenye ruksa sio?

4. Kulipa fidia kwa maana ya kutibu vidonda, akumbuke kuna wahindi walinyanganywa nyumba zao wakati wa azimio la arusha nao watafidiwa? kuna makampuni ya Rockefeller na Mackenzie yalitaifishwa mashamba ya chai kahawa pareto je nayo yatafidiwa? vipi kuhusu bank ya Barclays UK ambayo ilitaifishishwa na kuanzishwa BOT nayo itafidiwa? Mgodi wa Geita Mine nao ataurudisha kwa Wajerumani? Ni vyema Chadema wakatafakari upana wa tatizo wanalotaka kulitengeneza.

5. Kuvutia wawekezaji, huu mfumo ndio alioutumia mzee wetu marehemu Mkapa, sote tunajua yaliyotupata na hatujasahau naomba usiturudishe huko, hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji tusidanganyane. Kwanza ukilegeza mfumo wa kodi hakuna mwekezaji atakuja wekeza labda wachimba mafuta gesi na dhahabu. Mambo amabayo yeye Lissu amekuwa akiyapiga vita tangu zamani huko ubelgiji wamempa nini? Kiujumla mawazo ya Lissu ni yakienyeji sana na yaliyopitwa na wakati.
Kwa ujumla wewe umechambua hotuba yake kienyeji hasa. Labda lengo lako lilikuwa tu kukosoa lakini huna uelewa wa kutosha kuhusu uliyoyasema. Labda kwa ufupi tu, ujue yafuatayo:

1) kabla ya awanu hii, mifuko ya hifadhi ya jamii, ilikuwa ikijiendesha na kutoa fao la kujitoa bila tatizo. Tatizo limekuja kutokana na serikali kukopa kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwenye mifuko hii na kisha kutokuwa tayari kulipa madeni. Awamu hii ilipoanza, haikutaka kutoa pesa kuilipa hii mifuko. Wakaamua kuweka sheria ya kuzuia fao la kujitoa, siyo kwa nia ya kumsaidia mfanyakazi bali ni kwa vile hakutaka serikali ilipe madeni kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Hii ni mbinu duni sana ya kukabiliana na deni.

2) Kuhusu kuwalipa fidia watu waliobomolewa nyumba, hili lipo wazi sana. Sielewi lina uhusiano gani na utaifishaji wa majengo ya wahindi mwaka 1967 wakati wa utekelezaji wa Azimio la Arusha. Kuwalipa waliobomolewa nyumba kupisha ujenzi wa barabara, ni haki ya walioathirika na ipo kwenye sheria zetu za nchi. Kila anayeondoshwa kwaajili ya kupisha mradi wowote ule, uwe wa serikali, mtu binafsi, kampuni au taasisi yoyote, anastahili fidia. Kutokuwalipa fidia, Rais Magufuli amevunja sheria. Rais badala ya kuwa mfano wa kufuata sheria, anakuwa mfano mbaya wa kukiuka sheria.

3) Kuvutia uwekezaji, nashangaa kusikia kuwa eti kukiwa na vivutio kwa wawekezaji, tutaangukia kwenye tatizo lile lililotokana na sera ya Rais Mkapa ya kuvutia wawekezaji. Ni tatizo gani? Msipende kudanganywa na Rais kuhusiana na uwekezaji, hasa kwenye sekta ya madini. Mambo mengi anayoongea Rais ameyaumba, hayana uhalisia. Rais Mkapa alifanya kazi kubwa sana, na alipata mafanikio makubwa sana, ambayo huyu wa sasa hawezi kufikia hata 25%.

Linganisha performance ya Rais Mkapa na huyu wa sasa kwenye:
1) FDI
2) Employment growth rate
3) Inflation control
4) GDP growth rate
5) Management systems installation

Katika hayo yote, huyu wa sasa hamfikii Rais Mkapa hata kwa 25%.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ujumla wewe umechambua hotuba yake kienyeji hasa. Labda lengo lako lilikuwa tu kukosoa lakini huna uelewa wa kutosha kuhusu uliyoyasema. Labda kwa ufupi tu, ujue yafuatayo:

1) kabla ya awanu hii, mifuko ya hifadhi ya jamii, ilikuwa ikijiendesha na kutoa fao la kujitoa bila tatizo. Tatizo limekuja kutokana na serikali kukopa kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwenye mifuko hii na kisha kutokuwa tayari kulipa madeni. Awamu hii ilipoanza, haikutaka kutoa pesa kuilipa hii mifuko. Wakaamua kuweka sheria ya kuzuia fao la kujitoa, siyo kwa nia ya kumsaidia mfanyakazi bali ni kwa vile hakutaka serikali ilipe madeni kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Hii ni mbinu duni sana ya kukabiliana na deni.

2) Kuhusu kuwalipa fidia watu waliobomolewa nyumba, hili lipo wazi sana. Sielewi lina uhusiano gani na utaifishaji wa majengo ya wahindi mwaka 1967 wakati wa utekelezaji wa Azimio la Arusha. Kuwalipa waliobomolewa nyumba kupisha ujenzi wa barabara, ni haki ya walioathirika na ipo kwenye sheria zetu za nchi. Kila anayeondoshwa kwaajili ya kupisha mradi wowote ule, uwe wa serikali, mtu binafsi, kampuni au taasisi yoyote, anastahili fidia. Kutokuwalipa fidia, Rais Magufuli amevunja sheria. Rais badala ya kuwa mfano wa kufuata sheria, anakuwa mfano mbaya wa kukiuka sheria.

3) Kuvutia uwekezaji, nashangaa kusikia kuwa eti kukiwa na vivutio kwa wawekezaji, tutaangukia kwenye tatizo lile lililotokana na sera ya Rais Mkapa ya kuvutia wawekezaji. Ni tatizo gani? Msipende kudanganywa na Rais kuhusiana na uwekezaji, hasa kwenye sekta ya madini. Mambo mengi anayoongea Rais ameyaumba, hayana uhalisia. Rais Mkapa alifanya kazi kubwa sana, na alipata mafanikio makubwa sana, ambayo huyu wa sasa hawezi kufikia hata 25%.

Linganisha performance ya Rais Mkapa na huyu wa sasa kwenye:
1) FDI
2) Employment growth rate
3) Inflation control
4) GDP growth rate
5) Management systems installation

Katika hayo yote, huyu wa sasa hamfikii Rais Mkapa hata kwa 25%.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo akina Lissu walimzushia maneno ya uongo kuwa kaingia mikataba ya unyonyaji?
 
Haya Mambo ya Lissu niya kawaida Sana hayamfanyi awe rais labda udiwani
 
Kabisa anaongozwa na mihemko,Lissu kaongelea fidia kwa wahanga wa serikali ya pombe
 
Huyu mtu alikuwa ughaibuni kwa miaka mitatu hajui muziki wa Magufuli. Ana generalise mambo, ati atafuta kodi 15 kwa wafanyabiashara halafu hazitaji. Wenziwe hata hawamwambii hao wafanyabiashara unaodhani ni mtaji wa kura, Magu alishakutana nao ana kwa ana tena wa nchi nzima na kumalizana nao juu ya kero zao mbalimbali.
Screenshot_2020-08-30-02-30-30-1-1.png
 
Kiukweli nchi hii haki haipo, mfano kwenye mifuko ya hifadhi za jamii hela zinaliwa sana, hivi wale waliofukuzwa kwa vyeti feki hela zao za hifadhi zimeenda wapi? Wizi mtupu.lissu akifanikiwa kushinda afuatilie hili
 
Huyu mtu alikuwa ughaibuni kwa miaka mitatu hajui muziki wa Magufuli. Ana generalise mambo, ati atafuta kodi 15 kwa wafanyabiashara halafu hazitaji. Wenziwe hata hawamwambii hao wafanyabiashara unaodhani ni mtaji wa kura, Magu alishakutana nao ana kwa ana tena wa nchi nzima na kumalizana nao juu ya kero zao mbalimbali.
View attachment 1552586
Mkuu wafanyabiashara moyoni hawamkubali magu kamwe, ni machoni tu
 
Haya Mambo ya Lissu niya kawaida Sana hayamfanyi awe rais labda udiwani
Kawaida kwako mkuu, kwa mifuko ya hifadhi ya jamii inatumika kudhoofisha wafanyakazi badala ya kuwaimarisha.serikali inachukua pesa zao kujengea miradi.hatari
 
Mkuu wafanyabiashara moyoni hawamkubali magu kamwe, ni machoni tu
Wewe wasema, Magufuli ndio mlezi wa chemba ya wafanya biashara inaliyoasidiwa na Mkapa, anakutana nao mara kwa mara na vinywa vyao vimejaa sifa za Magufuli.
 
Back
Top Bottom