Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

Acha upambavu dogo.
uchawi upo me mwenyewe nishapoteza ndugu kwa huo uchawi (hawakuwa warengwa)

Kuhusu jini sijawahi liona, ila uchawi sio kuuonatu, mpaka kuubeba.

Ila malezi nayo yana changia, huwezi lelewa maisha ya mboga saba ukaujua uchawi, ila ungezaliwa uswahilini usingeongea hivi.
Uchawi ni nini na unajuaje huyo ndugu yako umempoteza kwa uchawi na si kitu kingine unachofikiri tu ni uchawi?
 
I have meets with this guys,they are so cool and humble "THIS IS CREATURES OF SPECIAL PRINCIPLES...DO YOU WISH TO SEE? ARE YOU CLEAN ENOUGH?,DO YOU WANT TO POSSESS ONE?I HAVE MANY I CAN GIVE YOU A LITTLE ONE.
English ya bongo... inaweza fanya ukatapika chakula umekula. Ongeeni kiswahili tu.

I have met these guys. THESE CREATURES HAVE SPECIFIC PRINCIPLES. Would you like to meet one of them face to face? Are you sanctified? I am possessed by many of them, and I can give one if you wish.
 
Wewe hata Demu Mzenji akikufanyia role play akijifanya jini utasema kuna jini hspi.

Kwa watoto wa enzi za Nyerere waliokulia kusikikiza RTD mtakumbuka kuna kipindi kimoja cha Mahoka jamaa alikuwa na wake wawili, wanamsumbua sana. Siku moja akajipanga na rafiki yake kujifanya kama kapandisha mashetani.

Wake zake wakaamini kapandisha mashetani kweli, mwisho akazidisha uongo akawa kaharibu.

Wewe unajuaje hujapigwa changa la macho kuoewa manjonjo kwa Mahoka?

Au unajuaje huyo demu hana matatizo ya akili ya multiple personality disorder?

Na sisi tutahakikishaje hayo mambo yalitokea kweli na hujatupatia chai tu hapa?
Bwana Kiranga.....

Uchawi upo na wachawi wapo.

Nimewashuhudia kwa macho yangu wanaingia ndani ya nyumba usiku saa nane!

Ukiwakurupua wanakimbia wanapotelea ukutani.

Hiyo nayo utanambia nimerukwa na akili?
 
Wewe hata Demu Mzenji akikufanyia role play akijifanya jini utasema kuna jini hspi.

Kwa watoto wa enzi za Nyerere waliokulia kusikikiza RTD mtakumbuka kuna kipindi kimoja cha Mahoka jamaa alikuwa na wake wawili, wanamsumbua sana. Siku moja akajipanga na rafiki yake kujifanya kama kapandisha mashetani.

Wake zake wakaamini kapandisha mashetani kweli, mwisho akazidisha uongo akawa kaharibu.

Wewe unajuaje hujapigwa changa la macho kuoewa manjonjo kwa Mahoka?

Au unajuaje huyo demu hana matatizo ya akili ya multiple personality disorder?

Na sisi tutahakikishaje hayo mambo yalitokea kweli na hujatupatia chai tu hapa?
Kuhakikisha huwezi labda na wewe upate demu mwenye majini na yakupende kama mimi ilivyonitokea nikatunukiwa mabikra wa kijini
 
Ndo maana ya kusema tembea uone umeishi dar maisha yako yote,utakuta.

Kama zambi wanatambua uchawi upo kwaiyo ukikamatwa wana mwita chief aje athibitishe maana chief lazima awe ni mchawi nae.

Ukikutwa ni mchawi wanakutoa uchawi afu unafungwa.

Kwa tulio zaliwa vijijini tunaelewa shughuri ya lamba lamba wakija kukamata wachawi watu wanavyo poteana.
 
Bwana Kiranga.....

Uchawi upo na wachawi wapo.

Nimewashuhudia kwa macho yangu wanaingia ndani ya nyumba usiku saa nane!

Ukiwakurupua wanakimbia wanapotelea ukutani.

Hiyo nayo utanambia nimerukwa na akili?
Kwanza kabisa nimeuliza uchawi ni nini.

Na utajuaje huu ni uchawi na si kitu kingine ambacho si uchawi ila hujakielewa tu.

Hujajibu.

Muandishi wa riwaya za kisayansi wa Kiingereza Arthur C. Clarke alikuwa na usemi wake mmoja naupenda sana.

Alisema " Any sufficiently advanced technology is indistinguishable from magic".

Yani hata watu kutoka Ulaya walivyokuja na mambo ya gramophone inayopiga muziki, mababu zetu wakaona muziki na sauti za watu zinatoka katika hiki kibox cha gramophone, waliona uchawi.

Hawa mababu zetu wangekuwepo leo wakaona ndege zinaruka, wangeona tunawasiliana kwa simu kutoka pande zote za dunia, wangeita huu ni uchawi.

Kumbe ni sayansi tu.

Hawa watu wa kutoka Ulaya walivyoweza kutabiri lini jua litapatwa (solar eclipse), kwa kujua sayansi tu, walionekana wachawi.

Sasa, uchawi ni nini na wewe unajuaje huu ni uchawi na si kitu kingine ambacho hukijui tu kama babu zetu walivyokuwa hawajui gramophone na jinsi ya kutabiri solar eclipse?
 
Kwanza kabisa nimeuliza uchawi ni nini.

Na utajuaje huu ni uchawi na si kitu kingine ambacho si uchawi ila hujakielewa tu.

Hujajibu.

Muandiahi wa riwaya za kisayansi wa Kiingereza Arthur C. Clarke alikuwa na usemi wake mmoja naupenda sana.

Alisema " Any sufficiently advanced technology is indistinguishable from magic".

Yani hata watu kutoka Ulaya walivy9kuja na mambo ya gramophone inayopiga muziki, mababu zetu wakaona muziki na sauti za watu zinatoka katika hiki kibox cha gramophone, waliona uchawi.

Hawa watu wa kutoka Ulaya walivyoweza kutabiri lini jua litapatwa (solar eclipse), kwq kujua sayansi tu, walionekana wachawi.

Sasa, uchawi ni nini na wewe unajuaje huu ni uchawi na si kitu kingine ambacho hukijui tu kama babu zetu walivyokuwa hawajui gramophone na jinsi ya kutabiri solar eclipse?
Wale watu niliowaona wakipitia ukutani nyakati za usiku waliwezaje kufanya hivyo?

Unasema huo sio uchawi? Ni nini?

Hebu tueleze, ni uwezo gani unaomuwezesha binadamu kupitia ukutani saa nane za usiku?

Physics? Ama?
 
Mmmh isije ikawa jini kaja kuweka mambo shwariiu[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Wale watu niliowaona wakipitia ukutani nyakati za usiku waliwazaje kufanya hivyo?

Unasema huo sio uchawi? Ni nini?

Hebu tueleze, ni uwezo gani unaomuwezesha binadamu kupitia ukutani saa nane za usiku?

Physics? Ama?
Unajuaje watu hao walikuwepo kweli na wewe huna matatizo ya akili tu au hujaona mauzauza kutokana na akili yako kukucheza shere tu?

Umehakiki vipi hizo habari zako?

Tunakuhakiki vipi wewe mwenyewe kwamba habari unazoleta hapa ni za kweli na si hadithi tu?

Hata mimi nilivyokuwa mdogo nilikuwa naona vitu gizani, lakini ule ulikuwa woga wa kitoto tu, nilivyokua nikawa sina woga huo nikaacha kuona hivyo vitu vya kufikirika.

Sasa unajuaje kwamba wewe hujaacha woga wa kitoto?
 
Kuna nadharia za ajabu sana Africa ambazo huwezi ziona dunia ya kwanza.
Uchawi ni nn.. Nani ambaye anaweza kutupa prove uchawi upo? Nani alimuona mchawi? Nani anaujua uchawi? Uchawi una nguvu gani?

Hayo Majini ni nini? Hakuna cha majini wala babu yake na majini?
Hizo ni drama za kufikirika.

Utasikia kuna majini. Ushawahi kuliona! Utasikia majini majini ni viumbe visivyoonekana kama hayaonekani umejuaje km yapo.
Majini na uchawi ni dhana za kufikilika
Lete prove hapa.

Hakuna cha majini wala uchawi
Unasumbuliwa na shibe
 
Kwa hiyo Mkuu unaweza kutuonesha oxygen, mionzi ya ki Electronic ya simu,satellite, vitamini vinavyopatikana kwenye vyakula n.k. Bila ya vifaa maalum huwezi, vile vile kwenye hayo mambo usiyoyaamini kuna vifaa au system imewekwa ili kuviona. Km wewe ni Mpagani pambana na akili yako mkuu hakuna wa kukuokoa huko ulipo
 
Unajuaje watu hao walikuwepo kweli na wewe huna matatizo ya akili tu au hujaona mauzauza kutokana na akili yako kukucheza shere tu?

Umehakiki vipi hizo habari zako?

Hata mimi nilivyokuwa mdogo nilikuwa naona vitu gizani, lakini ule ulikuwa woga wa kitoto tu, nilivyokua nikawa sina woga huo nikaacha kuona hivyo vitu vya kufikirika.

Sasa unajuaje kwamba wewe hujaacha woga wa kitoto?
Hahahaaaaa......

Haya, sawa!
 
Back
Top Bottom