Uchawi gani umetumika kuiba hela zangu kwenye kibubu?

Uchawi gani umetumika kuiba hela zangu kwenye kibubu?

Formula ya kibubu ipo hivi Mkuu

unaenda kwa Fundi anakitengeneza upo hapo hapo unaondoka nacho, vile ambavyo unakuta kishatengenezwa Tayari ni Ugonjwa wa Moyo Mkuu, vibubu vingi ni autopilot
Wala si kweli, kama huamini tengeneza kibubu chako kwa kuangalia alafu jikoroge uweke noti uishi na washika koroshei wataiba zooooote
 
Nimevunja kibubu muda huu, kibubu nilichodunduliza 20% ya kila nilicho kipata kwa miezi nane (nilianza pasaka) nimekuta shilingi 4'500/ kweli? Dah
Kuna mwanangu aliwahi kukutwa na hilo jambo,basi tokea siku hyo naviogopa kinyama hivyo vibubu kwani nilikuwa na mpango wa kusave
 
Jana nlimuona stranger dirishani kwako anaingia na kibubu inawezekana amechukua chako amekuachia cha buku 4 jero

Ndio itakua ivo mana nlimuona anatoka anakibeba kama kizito (sikutaka kukwambia sababu aliingia na kibubu akatoka nacho)
 
Kudadeki, kwenye huu Uzi ndio nimepata majibu ya kibubu changu namie

Kuna mwaka fulani wakati ndio naanza maisha, niliwahi kuishi kigogo basi baada ya kupata ahueni ya maisha nikaenda kukaa mbezi baada ya kupiga deal la bumkubaa

Sasa nilipofika Mbezi na kufanya Tathmini ya maisha nikaona kulipa Kodi mbona itakuja itakuwa utata badae me nimezoea Kodi zangu za 30k

Wakati naishi kigogo niliwahi kuona Mzee fulani hivi anauza vibubu kwake, hivo nikapanga siku ya kwenda na nikanunua kimoja Kwa ajili ya kukusanya pesa ya kulipa Kodi

Basi kweli bana, nikawa najitahidi kila siku lazima niweke hela kuanzia 2000 kuendelea, nikafanya hivo Kwa miezi 2 mfululizo bila kusimama ata siku 1, nilipanga ikifika miez 3 ndio nivunje nitoe hela ya Kodi

ila bahati mbaya kabla ya kufika miez 3 nikawa nimepata msiba, nikaona nivunje tu kibubu ili nitumie ile pesa kama nauli ya kwenda Mkoa, ilikuwa imefika kama siku 78 hivi

Ohoooo si nikakitoa bana ili nichukue mafao, kudadeki baada ya kuvunja nakuta 6500, na hapo tangu nihamie hayo makazi mapya nilikuwa sijawahi kupeleka mshkaji wala Manzi

Ikabidi nikae tu niegemee ukuta maana sina nauli wala sina tumaini la kulipa Kodi, nikawaza na kuwazua kama steringi wa kihindi ila haikunisaidia chochote

Dahh sikuwahi kupata majibu ya hela yangu ilienda wapi hadi leo kwenye Uzi huu ndio nimepata Mwanga kuwa huenda ni kweli hivi vibubu waga vimefungwa Visimbuzi
 
Kuna mfanyakazi mwenzangu aliniambia ukinunua Kibubu , shurti uweke sindano mpya ,zile za kushona nguo kwa mikono,unaitanguliza ndani kabla ya kuanza kuweka pesa,hapo no mwanga atafaulu kuiba,hii nyingine niliona insta msanii Esha nae yalimtokea km yako,akashauriwa bora atumie kopo la rungu spray kubwa lililoisha unatoboa chini tundu dogo thn unaendelea kuhifadhi pesa zako
 
Mkuu upo dunia ipi?? Watu siku hizi hawaweki hela kwenye vibubu vyakununua labla ungekua umetengeneza mwenyewe

Saiv chuma ulete zimehamishiwa huko
 
Kwani kipato chako ni kiasi gani? Isijekua unalalamika wakati kwa wiki unaingiza jero
 
Mzee wa kawetele kona ya Mkoa na Mbalizi wacha wakupige bhana umezidi kutufokea...
 
Back
Top Bottom