Uchebe kasaini kufundisha Singida black stars

Uchebe kasaini kufundisha Singida black stars

Nafasi ya 3 itasumbua sana msimu ujao Simba wajipange
Kwamba simba wao mmewazuia kusajili wachezaji wazuri wa kuwapa ubingwa? Bingwa wa NBC PL mwakani ni simba. Save hii .
Na hiyo nafasi ya 3 huenda ikakwapuliwa na Yanga .
 
Huyu kocha sitamsahau, aliitengeneza Simba Sc ikawa moto yenye vikosi viwili, nakumbuka ile super sub ya Miraj Athuman ilikuwa kazi ya Aussems...

Baadae yule gabachori akaanza wivu wake, anataka yeye ndie apendwe na kutukuzwa kama mungu mtu ndani ya klabu, akamfukuza uchebe bila kosa lolote huku kwa aibu hiyo kazi ya kumfukuza akimuachia dada yake asimamie yeye akakimbilia nje ya nchi.

Kutoka hapo ndio downfall ya Simba Sc ikaanza, kila siku ni kubadilisha makocha tu, timu hqina mbele wala nyuma uongozi haueleweki, sajili za hovyo.

Aliyebaki anafanya vizuri atlist ni Ahmed Ally pekee huku nae maneno mengi anayoongea yakigeuka uwongo kwasababu ya kutokuwepo kwa uwiano kati ya mdomo wake na vitendo uwanjani, maneno mazuri huku uwanjani mpira wa hovyo.
Wakuu mkiwa mnaongelea mpira mjitahidi kuwa na kumbukumbu basi.

Uchebe alifundisha Simba msimu wa 2018/2019 akafukuzwa mwezi August 2019.


Miraji Athuman alisajiliwa kutumika msimu wa 2019/2020 hivyo Uchebe alimtumia kwenye pre season tu huu super sub uliona kwenye pre season ?

Uchebe alifukuzwa August 2019 baada ya muda CEO aliteuliwa kuwa Senzo na Simba wakamteua Sven Vandenbroek kuwa kocha wa Simba kwa msimu wa 2019/2020.

Uchebe alifukuzwa Simba kwa sababu ya kushindwa kuirudisha timu Champions League kwa kutolewa na UD Songo na yeye alisema Target aliyopewa hakuifikia.

Babra alianza kazi Kama CEO msimu wa 2020/2021 na kocha pekee aliyesajiliwa na Barbra ni Didier Gomes Da Rosa.

Makocha aliofanya nao kazi Barbra ni Sven kwa muda mfupi , Gomes, Pablo, Zoran Maki na Robertinho kwa muda mfupi pia.

Tuoongelee mpira kwa uhalisia wake siyo kwa chuki zetu binafsi.
 
Kishingo pia alifanya kazi nzuri. Ndiye aliyeiondoa Simba kwenye utamaduni wa kupigwa hamsa 🪬 Uarabuni.
Kishingo hakuwahi kukutana na timu yoyote ya Uarabuni aliwaondoaje Simba kwenye hilo wakati hakukutana na waarabu ?
 
Uchebe ndio aliyeanzisha na kuasisi simba imara ya kimataifa. Ile mechi ya Simba Vs Nkana Ni bonge moja la mechi katika historia ya mpira wa Tanzania. Ndio mfumo wa kumtegemea Chama ulianzia hapo na mpaka leo simba bado wanamtegemea chama [emoji1787]
Hapana msimu huo mchezaji muhimu alikuwa Emanuel Okwi
 
Back
Top Bottom