Ucheleweshwaji wa Pasipoti: Changamoto na Maswali Yasiyojibiwa

Ucheleweshwaji wa Pasipoti: Changamoto na Maswali Yasiyojibiwa

www.immigration.go.tz



Kwa ufupi na uchache unatakiwa uwe na viambata vifuatavyo;-

1. Fomu ya maombi ya passport iliyojazwa na kusainiwa na wewe pamoja na wakili (unajaza online kisha unai print).

2. Barua yako ya kuomba passport (just a simple official letter).

3. Barua ya utambulisho toka serikali ya mtaa.

4. Nakala ya cheti chako cha kuzaliwa.

5. Nakala ya cheti cha kuzaliwa ya mzazi wako mmoja. (Kama hauna unapeleka kiapo yaani affidavit)

6. Namba yako ya NIDA au nakala ya kitambulisho cha NIDA kama unayo.

7. Uthibitisho wa safari (hizi zinatofautiana kulingana na madhumuni ya safari yako). Kwa wewe hapo unaweza kupeleka uthibitisho wa uwezo wa kujilipia gharama za safari, malazi, n.k (Bank statement yenye "mzigo" wa kutosha kufanya hayo).



Kwa uchache ni hayo hapo.



Gharama:

20,000/= (Unalipia wakati unajaza fomu online)

130,000/= (Unalipia benki mara baada ya kupeleka nyaraka zako uhamiaji na zikakaguliwa kuonekana ziko sahihi).



Jumla ni 150,000/=



Hapo sijahesabia gharama za wakili na "lojistiki" zingine ndogondogo.
Shukrani anko
 
Hii ndio bongo bana. Hakuna anaekemea huo ukiritimba, wote wanamuona mtoa mada zwazwa kwa kushindwa kutoa rushwa ahudumiwe haraka.

Bado tuna safari ndefu sana.
Umemsikia CDF alichosema? hao wakikaza watu wa Kigoma hamtopata passport, acha ibaki hivihivi, wanaharakati endeleeni na harakati zenu tu.
 
Nchi zenye rushwa ndio nzuri kufanikisha mambo yako, unadhani wazungu wangekuwa watu wa rushwa viza za Marekani si zingekuwa za kununuwa tu kama Brazil?
yeah sure.
Hivi brazil kuna maisha kweli?mpaka watu wananunua visa?
au watu wanakimbilia nini huko
 
Mnamo tarehe 23 Septemba 2024, nilikamilisha hatua ya kwanza ya maombi ya pasipoti ya kawaida kwa kujaza fomu namba 24ER-Y091-Q020 na kuwasilisha viambato vyote vya msingi na ziada kwa njia ya mtandao, kisha kulipa shilingi 20,000/- za Kitanzania kama ada ya huduma. Siku iliyofuata, tarehe 24 Septemba 2024, nilikamilisha taratibu zote ikiwa ni pamoja na kuambatanisha fomu na viambato vya msingi kama vile nakala ya cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Taifa (NIDA), kiapo cha mahakama cha mzazi mmoja, pamoja na barua ya maombi na kiambato cha ziada cha barua ya utambulisho kutoka serikalini ya mtaa.

Nilifuata taratibu zote kwa mujibu wa muongozo wa huduma ya pasipoti, ambapo baada ya ukaguzi wa fomu na viambato vyangu, nilijulishwa kuwa taarifa zangu zilikuwa kamili. Hivyo, niliendelea na hatua inayofuata ya kufanya mahojiano na Afisa Ernest Maganga. Baada ya mahojiano, nilifanya hatua ya kupiga picha na kufanya uthibitisho wa alama za vidole. Nilitarajia kuwa baada ya kumaliza taratibu zote, ningepokea pasipoti yangu katika kipindi cha siku 7 hadi 14 kama ilivyoelekezwa kwenye muongozo. Hata hivyo, nilijulishwa kuwa kulikuwa na changamoto za kiufundi, hivyo nikaelekezwa kurudi baada ya mwezi mmoja na wiki mbili, yaani tarehe 14 Novemba 2024.

Ilipofika tarehe 14 Novemba, nilifika ofisi za uhamiaji nikiwa na matumaini ya kupokea pasipoti yangu, lakini nilishangazwa na taarifa kwamba fomu yangu haikuchakatwa kwa sababu ya kipengele kimoja ambacho sikukamilisha, licha ya kuwa fomu ilikuwa imekaguliwa na mahojiano kufanyika mwezi mmoja na wiki mbili kabla. Baada ya kuelekezwa, nilikamilisha kipengele hicho kupitia mwanasheria wangu na kuirudisha tena fomu pamoja na viambato vyote ofisi za uhamiaji Kurasini. Nilijulishwa kwamba pasipoti yangu ingekamilika na kuwa tayari tarehe 22 Novemba 2024 na ningeenda posta, wizara ya mambo ya ndani kuichukua.

Ilipofika tarehe 21 Novemba 2024, nilipokea simu kutoka kwa namba 0784520840 iliyonijulisha kuwa pasipoti yangu bado haipo na kwamba nilipaswa kuleta matokeo yangu ya chuo pamoja na barua nilipojaribu Kuhoji alinikatia simu na toka hapo nikipiga simu haipokelewi. licha ya kuwa nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu, sikujulishwa kuhusu uhitaji wa taarifa hizo za ziada.

Maswali ya Kujiuliza:

1. Kwa nini taarifa za ziada na maboresho zilikuwa hazijafahamika miezi miwili nyuma, wakati nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mchakato wa mahojiano?kwani ingeweza kunisaidia kukamilisha mchakato wa maombi kwa wakati.

2. Kwa nini maafisa wa uhamiaji wanatupia lawama zote kwangu kwa makosa ambayo wao ndio waleyasababisha au kuyatengeneza? Ingawa niliwasilisha fomu na viambato vyote kwa usahihi, bado nashindwa kuelewa kwa nini nilikosa kupewa taarifa muhimu ambazo zingenisaidia kupunguza ucheleweshaji.

Kwa sababu ya ucheleweshaji huu wa pasipoti kwa miezi miwili, nilikosa ufadhili wa safari ya utalii wa nje baada ya mdhamini wangu kusitisha kwa kutozingatia kwangu muda (deadline). Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na ucheleweshaji wa pasipoti yangu, ambao ulileta athari kubwa katika mipango yangu ya safari.

Ushauri:

1. Kutengeneza Mfumo wa Ufuatiliaji wa Maombi: Mfumo huu uwape uwezo wateja kufuatilia hatua za uchakatwaji wa maombi yao ya pasipoti. Hii itasaidia kujua hali halisi ya ombi lao, nyaraka zilizokosekana, na maboresho yanayohitajika.

2. Masharti na Hatua Muhimu Ziwekwe Wazi na Kwa Wakati: Kueleza kwa uwazi taarifa zilizokosekana na maboresho yanayohitajika katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mahojiano.

3. TAKUKURU na Wadhibiti Ubora kafanye kazi yao.

Pole sana mkuu!

Picha ya haraka haraka ni kwamba uliwekewa mazingira ya wewe kujiongeza. Pamoja na sababu za kukosekana paspoti kutolewa bado kuna viashiria/mazingira ya wewe kunyoosha mkono.

Wewe usikate tamaa kwa sababu fursa ya ufadhili ushakosa basi endelea kufuatilia upate paspoti yako iwe tayari tu muda wowote Mungu anaweza kukufungulia mlango mwingine wa ufadhili.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Jiongeze bwashee, watu wanakula kwa urefu wa kamba zao.

Mimi nilipata passport yangu ndani ya siku 3 za kazi. Nilikamilisha mambo yote ya picha na finger print tarehe 14 August na tarehe 19 Aug nilienda kuchukua passport yangu.

Kwa nchi hii ukitaka kwenda kama ilivyoelekezwa utadoda mzee.

Soon utaambiwa ukaonyeshe kaburi la babu wa babu yako kudhihirisha utanzania wako.
 
Mnamo tarehe 23 Septemba 2024, nilikamilisha hatua ya kwanza ya maombi ya pasipoti ya kawaida kwa kujaza fomu namba 24ER-Y091-Q020 na kuwasilisha viambato vyote vya msingi na ziada kwa njia ya mtandao, kisha kulipa shilingi 20,000/- za Kitanzania kama ada ya huduma. Siku iliyofuata, tarehe 24 Septemba 2024, nilikamilisha taratibu zote ikiwa ni pamoja na kuambatanisha fomu na viambato vya msingi kama vile nakala ya cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Taifa (NIDA), kiapo cha mahakama cha mzazi mmoja, pamoja na barua ya maombi na kiambato cha ziada cha barua ya utambulisho kutoka serikalini ya mtaa.

Nilifuata taratibu zote kwa mujibu wa muongozo wa huduma ya pasipoti, ambapo baada ya ukaguzi wa fomu na viambato vyangu, nilijulishwa kuwa taarifa zangu zilikuwa kamili. Hivyo, niliendelea na hatua inayofuata ya kufanya mahojiano na Afisa Ernest Maganga. Baada ya mahojiano, nilifanya hatua ya kupiga picha na kufanya uthibitisho wa alama za vidole. Nilitarajia kuwa baada ya kumaliza taratibu zote, ningepokea pasipoti yangu katika kipindi cha siku 7 hadi 14 kama ilivyoelekezwa kwenye muongozo. Hata hivyo, nilijulishwa kuwa kulikuwa na changamoto za kiufundi, hivyo nikaelekezwa kurudi baada ya mwezi mmoja na wiki mbili, yaani tarehe 14 Novemba 2024.

Ilipofika tarehe 14 Novemba, nilifika ofisi za uhamiaji nikiwa na matumaini ya kupokea pasipoti yangu, lakini nilishangazwa na taarifa kwamba fomu yangu haikuchakatwa kwa sababu ya kipengele kimoja ambacho sikukamilisha, licha ya kuwa fomu ilikuwa imekaguliwa na mahojiano kufanyika mwezi mmoja na wiki mbili kabla. Baada ya kuelekezwa, nilikamilisha kipengele hicho kupitia mwanasheria wangu na kuirudisha tena fomu pamoja na viambato vyote ofisi za uhamiaji Kurasini. Nilijulishwa kwamba pasipoti yangu ingekamilika na kuwa tayari tarehe 22 Novemba 2024 na ningeenda posta, wizara ya mambo ya ndani kuichukua.

Ilipofika tarehe 21 Novemba 2024, nilipokea simu kutoka kwa namba 0784520840 iliyonijulisha kuwa pasipoti yangu bado haipo na kwamba nilipaswa kuleta matokeo yangu ya chuo pamoja na barua nilipojaribu Kuhoji alinikatia simu na toka hapo nikipiga simu haipokelewi. licha ya kuwa nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu, sikujulishwa kuhusu uhitaji wa taarifa hizo za ziada.

Maswali ya Kujiuliza:

1. Kwa nini taarifa za ziada na maboresho zilikuwa hazijafahamika miezi miwili nyuma, wakati nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mchakato wa mahojiano?kwani ingeweza kunisaidia kukamilisha mchakato wa maombi kwa wakati.

2. Kwa nini maafisa wa uhamiaji wanatupia lawama zote kwangu kwa makosa ambayo wao ndio waleyasababisha au kuyatengeneza? Ingawa niliwasilisha fomu na viambato vyote kwa usahihi, bado nashindwa kuelewa kwa nini nilikosa kupewa taarifa muhimu ambazo zingenisaidia kupunguza ucheleweshaji.

Kwa sababu ya ucheleweshaji huu wa pasipoti kwa miezi miwili, nilikosa ufadhili wa safari ya utalii wa nje baada ya mdhamini wangu kusitisha kwa kutozingatia kwangu muda (deadline). Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na ucheleweshaji wa pasipoti yangu, ambao ulileta athari kubwa katika mipango yangu ya safari.

Ushauri:

1. Kutengeneza Mfumo wa Ufuatiliaji wa Maombi: Mfumo huu uwape uwezo wateja kufuatilia hatua za uchakatwaji wa maombi yao ya pasipoti. Hii itasaidia kujua hali halisi ya ombi lao, nyaraka zilizokosekana, na maboresho yanayohitajika.

2. Masharti na Hatua Muhimu Ziwekwe Wazi na Kwa Wakati: Kueleza kwa uwazi taarifa zilizokosekana na maboresho yanayohitajika katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mahojiano.

3. TAKUKURU na Wadhibiti Ubora kafanye kazi yao.
Nchi imeoza hii,ngojea watakuja kujibu kwa mbwembwe,na utaambiwa unapotosha na kuleta taaruki
 
Mnamo tarehe 23 Septemba 2024, nilikamilisha hatua ya kwanza ya maombi ya pasipoti ya kawaida kwa kujaza fomu namba 24ER-Y091-Q020 na kuwasilisha viambato vyote vya msingi na ziada kwa njia ya mtandao, kisha kulipa shilingi 20,000/- za Kitanzania kama ada ya huduma. Siku iliyofuata, tarehe 24 Septemba 2024, nilikamilisha taratibu zote ikiwa ni pamoja na kuambatanisha fomu na viambato vya msingi kama vile nakala ya cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Taifa (NIDA), kiapo cha mahakama cha mzazi mmoja, pamoja na barua ya maombi na kiambato cha ziada cha barua ya utambulisho kutoka serikalini ya mtaa.

Nilifuata taratibu zote kwa mujibu wa muongozo wa huduma ya pasipoti, ambapo baada ya ukaguzi wa fomu na viambato vyangu, nilijulishwa kuwa taarifa zangu zilikuwa kamili. Hivyo, niliendelea na hatua inayofuata ya kufanya mahojiano na Afisa Ernest Maganga. Baada ya mahojiano, nilifanya hatua ya kupiga picha na kufanya uthibitisho wa alama za vidole. Nilitarajia kuwa baada ya kumaliza taratibu zote, ningepokea pasipoti yangu katika kipindi cha siku 7 hadi 14 kama ilivyoelekezwa kwenye muongozo. Hata hivyo, nilijulishwa kuwa kulikuwa na changamoto za kiufundi, hivyo nikaelekezwa kurudi baada ya mwezi mmoja na wiki mbili, yaani tarehe 14 Novemba 2024.

Ilipofika tarehe 14 Novemba, nilifika ofisi za uhamiaji nikiwa na matumaini ya kupokea pasipoti yangu, lakini nilishangazwa na taarifa kwamba fomu yangu haikuchakatwa kwa sababu ya kipengele kimoja ambacho sikukamilisha, licha ya kuwa fomu ilikuwa imekaguliwa na mahojiano kufanyika mwezi mmoja na wiki mbili kabla. Baada ya kuelekezwa, nilikamilisha kipengele hicho kupitia mwanasheria wangu na kuirudisha tena fomu pamoja na viambato vyote ofisi za uhamiaji Kurasini. Nilijulishwa kwamba pasipoti yangu ingekamilika na kuwa tayari tarehe 22 Novemba 2024 na ningeenda posta, wizara ya mambo ya ndani kuichukua.

Ilipofika tarehe 21 Novemba 2024, nilipokea simu kutoka kwa namba 0784520840 iliyonijulisha kuwa pasipoti yangu bado haipo na kwamba nilipaswa kuleta matokeo yangu ya chuo pamoja na barua nilipojaribu Kuhoji alinikatia simu na toka hapo nikipiga simu haipokelewi. licha ya kuwa nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu, sikujulishwa kuhusu uhitaji wa taarifa hizo za ziada.

Maswali ya Kujiuliza:

1. Kwa nini taarifa za ziada na maboresho zilikuwa hazijafahamika miezi miwili nyuma, wakati nikiwa katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mchakato wa mahojiano?kwani ingeweza kunisaidia kukamilisha mchakato wa maombi kwa wakati.

2. Kwa nini maafisa wa uhamiaji wanatupia lawama zote kwangu kwa makosa ambayo wao ndio waleyasababisha au kuyatengeneza? Ingawa niliwasilisha fomu na viambato vyote kwa usahihi, bado nashindwa kuelewa kwa nini nilikosa kupewa taarifa muhimu ambazo zingenisaidia kupunguza ucheleweshaji.

Kwa sababu ya ucheleweshaji huu wa pasipoti kwa miezi miwili, nilikosa ufadhili wa safari ya utalii wa nje baada ya mdhamini wangu kusitisha kwa kutozingatia kwangu muda (deadline). Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na ucheleweshaji wa pasipoti yangu, ambao ulileta athari kubwa katika mipango yangu ya safari.

Ushauri:

1. Kutengeneza Mfumo wa Ufuatiliaji wa Maombi: Mfumo huu uwape uwezo wateja kufuatilia hatua za uchakatwaji wa maombi yao ya pasipoti. Hii itasaidia kujua hali halisi ya ombi lao, nyaraka zilizokosekana, na maboresho yanayohitajika.

2. Masharti na Hatua Muhimu Ziwekwe Wazi na Kwa Wakati: Kueleza kwa uwazi taarifa zilizokosekana na maboresho yanayohitajika katika hatua ya ukaguzi wa fomu na mahojiano.

3. TAKUKURU na Wadhibiti Ubora kafanye kazi yao.
Pole sana!

Nilifikiri Uhamiaji wamebadilika kumbe bado ni business as usual! Safari bado ni ndefu!!!
 
Waliniomba matokeo ya Form Four nikawapa, nikapata Passport 21days
 
Back
Top Bottom