Maswali haya ya Nguruv3 yamenivutia, sijaona majibu yake. baada ya mihangaiko ya nimejaribu kupitia sijaona majibu.
By Nguruvi3
1. Nyerere alikuja kwa mara ya kwanza lini Dar kama ulivyoulizwa?
2. Akienda UNO baada ya kuchangiwa fedha na wazee wako safari yake ilianzia wapi?
3.Halafu ulishaulizwa EAMWS ilianzia wapi na kwanini huko ilikoanzia haipo kwa sasa?
4.Unapozungumzia umoja wa waislam, ni upi huo kati ya Sunni, Shia, Bohora, Ismailia n.k.?
Nini kinashindikana kurudisha umoja huo?
5.Umeulizwa, mlezi wa iliyokuwa EAMWS alikuwa Agakhan, vipi mbona yeye anarudi na kujenga chuo kikuu kingine katika serikali ile ile iliyoua EAMWS 1968?
6.Ushahidi wa kanisa kushinikiza kifo cha EAMWS ni upi?Tusaidiane kumkumbusha Mohamed
sijibu kila kitu.Kubwa ni kuwa siko katika ushindani kwa hiyo hujibu lile lenye tija.
Nikiona swali halina maana huwa sijibu.
Siko humu kushinda mjadala
Siku zote Mohamed ameandika kuhusu tuhuma dhidi ya kanisa na Nyerere. Hilo halina tatizo kama basi ushahidi upo wa kuthibitika. Mathalani amekuwa anadai kuwa kanisa limeua EAMWS bila ushahidi wowote.
Hivi karibuni amekuwa akijaza watu fikra za kuwa bila wazee wake Nyerere asingekwenda UNO.
Tunawashukuru sana wazee wake kwa mchango huo.
Baada ya ukweli kuanza kudhihiri Mohamed amekubali kuwa John Rupia ni mmoja wa watu waliotoa mchango katika harakati za uhuru ikiwa ni pamoja na kuchangia gharama za usafiri wa Nyerere kwenda UNO
Mohamed sasa anakiri kuwa kuna wafuasi wa kanisa waliOchangia ticket (yeye anasema mara moja).
Mohamed aliujua ukweli huu kwasababu alishawahi kusema kuwa amekwenda New York na kukutana nao(ushahidi upo JF)
Kwasababu tu ngano hii ililenga katika kuwadhalilisha baadhi ya watu waliochangia uhuru wa nchi hii, Mohamed hakutHubutu kuandika mchango wa ticket moja wa shirika la Marknoll.
Ameuficha kwasababu ukitoka hadharani atakuwa ameondoa maana halisi ya historia aliyokusudia na siyo iliyokuwepo.
Kitendo cha kuendelea kulaani kanisa huku akijua hilo si kweli na badala yake kuficha ukweli ni unafiki na ulaghai.
Ameupumbaza umma unaotembea na majenereta kusikiliza hotuba zake huku akiwa na siri moyoni.
Hii maana yake ni nini! Maana yake ni kuwa hata zile shajara, makabrasha na mafaili aliyoyaona peke yake kwa akina Sykes huenda kuna mambo mengine hakutaka kuyaweka hadharani kama alivyoficha hili la shirika la Maknoll.
Ni Mohamed huyo huyo ameficha ukweli wa lini Nyerere alifika Dar es Salaam, ameficha ukweli wa kwanini sheikh Amir alitimuliwa, ameficha ukweli kwanini kulikuwa na jaribio la kumuondoa Nyerere mara 2 kabla ya uhuru.
Mohamed ameficha ukweli kwanini EAMWS ilikufa huko ilikoanzia, ilianza lini na washirika wake walikuwa nani.
Pamoja na kuficha ukweli, bado amekuwa kinara wa kubambikia marehemu maneno. Ameshindwa kuthibitisha lini Nyerere alisema hataki historia ya Kleruu na Sykes. Ameshindwa kuthibitisha ushiriki wa kanisa katika kuua EAMWS.
Mohamed kwa kutumia vibaya kalamu yake ameupotosha umma kuwa Nyerere alianza siasa baada ya kuonana na Abdul Sykes, kushonewa suruali kariakoo na kufundishwa kula chapati! Ney! imethibitika ni uzushi uliobobea, Nyerere alianza siasa akiwa Makerere, amevaa mavazi kuanzia Musoma, Makerere, Tabora, Scotland na hakuwahi kutembea na vibwenda
MO hakuwahi kumhoji Nyerere achilia mbali kuomba appointment ya kumuona. Alichobaki kutuambia ni maneno ya Marehemu Prof Othman ambayo pia hakumlizia Nyerere alimjibu nini.
Alichobaki ni kutueleza kuhusu Nyerere kutoa picha na kumuonyesha Malima baila kutuambia Malima alijibu nini.
Mohamed akamsingizia Malima kuwa ndiye aliyeanzisha namba za mitihani. Tulipotaka ushahidi hoja hiyo kaiondoa katika agenda zake! sasa kimyaa! Ulikuwa uzushi tu usio na thibitisho.
Mzee Said anatuambia Nyerere asingefanikiwa kwasababu alikuwa mkristo na hawakukubalika Dar es Salaam.
Tunaushahidi kuwa viongozi wa kisiasa kama Clement Mtamila na Vedastus Kyaruzi walikubaliwa kuongoza chama cha kisiasa ndani ya mji ule ule unaosemekana Nyerere asingeweza.
Mohamed anasahau kuwa Nyerere alikuwa katibau wa AA Tabora mji uliokuwa na Waislam wengi na msisimko wa siasa za nchi yetu naykati hizo.
Mohamed amemsingizia Nyerere kuwa alisema hamjui Abdul Sykes katika hotuba ya kuaga wazee.
Hotuba imewekwa, Mohamed yule yule aliyenukuu hotuba ya Nyerere anataka uthibitisho wa hotuba ile ile aliyonukuu eti kwa audio.
Sijui alinukuu misukule au nini!
Flip flop zote ni kutapa tapa kwasababu hana pa kutokea na taratibu ngano inajichuja na mashudu yanaelea.
Mohamed hakuwahi kumhoji Abdul Sykes kwasababu alikuwa na umri wa miaka 16, na haionekani kama alikuwa tofauti kimtazamo na fikra. Anachosimulia ni third part story ndio maana huchagua nini cha kujibu na mara nyingi hukwama.
Nyerere akifika Dar kwa mara ya kwanza Mohamed hajazaliwa na alipokutana na Sykes Mohamed alikuwa kichanga, kushuhudia kuwa Nyerere alishonewa suruali ni dharau sana, kumsingizia na kumwekea maneno mdomoni ni dhihaka kubwa lakini Kuupotosha umma ni ukosefu wa maadili ya kiroho '' moral authority''.
Usikimbie Mohamed, tupo hapa kuusaidia umma kukuelewa wewe na lengo lako kwa amani na usatwi wa taifa hili.