Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hakika Nyerere Yericko kaumia sana.
Abdulwahid aliishi na alikuwa rafiki mkubwa wa Nyerere.

Nyerere kaondoka nyumbani kwa Abdu Mtaa wa Stanley kwenda Musoma kumuoa Mama Maria.
Wameishi nyumba moja.

Mama yake Nyerere alikuwa shoga wa mama yake Abdu Bi Mluguru.
Wameishi kwa hisani kubwa sana hadi uhuru umepatikana.

Nyerere kakichukua chama mikononi mwa Abdu kwenye nyumba hiyo ofisi ya TANU ambayo
alijenga baba yake Abdu kati ya mwaka 1929 - 1933.

Hii ndiyo historia ya wazee wangu na ndiyo mazungumzo nikiyasikia wazee wangu wakizungumza.
Nakushauri hebu na wewe fanya utafiti lau mchache katika haya.

Ni kweli nimeumia sana, watanzania wameumia sana, walimwengu wameumia sana, Hii yote ni kutokana na upotoshaji mkubwa ulioufanya ndugu yangu!

Simulizi za mashirikiano ya Nyerere na Abdu wala hazina kasoro yoyote kwenye historia ya Uhuru, kasoro ni ile tu uliyoipandikiza wewe kwa Waislamu nchini.
 
Hahaha mkuu inasemekana semekana zimekuwa nyingi hana hoja naona anajikanyaga na hii nikutokana na hao anaowaandikia kutokuwa na uwezo wa kuhoji haya mambo kwa undani wao wanalishwa tu maneno

Naandika kama ninavyosema.
Endapo unahisi msemo unakukwaza nakushauri kupuuza sentensi hiyo na endelea na nyingine.

Lugha inafatana na utamaduni na mambo mengine.
 
Hakika hayo ni maoni yangu wala hukukosea.

Mohamed Said, hebu endelea kutoa elimu ya uraia watanzania wanakusoma.

Nimekuwa nikitamani sana kujua nini maana ya Mfumo Kristo, na kama ni kitu halisi lakini kwa bahati mbaya sijawahi kupata jibu zuri. Yupo mwanaJF anayeitwa Mkandara, aliwahi kuniambia kuwa ni mfumo uliotumiwa na serikali za kikoloni, kutawala kwa kupendelea ukristo na kubagua wasio wakristo. Bw Mkandara alionyesha wasiwasi kuwa bado chembechembe za mfumo kristo hadi sasa, japo hakuweza kutoa mifano. Niliwahi tena kuendesha mjadala kwenye thread moja humu na mwanaJF anayeitwa Ami (sina uhakika kama nimekumbuka jina vizuri), ambae nae alionyesha hisia za uwepo wa mabaki ya mfumo kristo, lakini hakuweza kunipa mifano stahiki.

Binafsi niko very interested kujua kama mfumo kristo ni kitu kinacho exist hadi leo, au leo tunashuhudia tu makovu yake? Interest yangu kwa kiasi fulani inatokana na kwamba mimi ni mwalimu katika mojawapo wa taasisi za juu za elimu Tz, na huwa najiuliza kwa nini hadi sasa (miaka 50 baada ya kuondoka wakoloni) bado ratio ya waislamu darasani ni ndogo sana ukilinganisha na wakristu? Mzee Mohamed Said, nimejaribu kusoma maandiko yako mengi humu JF, kwa bahati mbaya sijawahi kusoma maandiko yake mengine. Katika hayo niliyosoma sijapata kuona sharp evidences za uwepo wa mfumo kristo hadi leo, na namna unavyoathiri maendeleo ya waislamu kielimu.

Nimefanya observation ndogo kwenye matokeo ya form four mwaka jana, nikajaribu kulinganisha ufaulu katika shule za serikali katika wilaya ya Morogoro vijijini (ambako wengi ni waislamu) na za wilaya ya Moshi vijijini (ambako wengi ni wakristo). Siwezi nikasema kuwa tofauti niliyoiona inatokana moja kwa moja na dini zao. Nilifikiria yapo mambo kama mazingira ya kufanyia kazi na kadhalika. Swala ambalo naomba Mzee Mohamed unisaidie, je ni kwa vipi serikali inaweza kufanya, bila upendeleo au bila kuwakandamiza wakristo, kuhakikisha ufaulu katika maeneo na shule zenye waislamu wengi sio tofauti na maeneo na shule zenye wakristo wengi?
Je, ni juhudi zipi ambazo waislamu wanaweza kuzifanya, wao kama wao, kuhakikisha watoto wao wanakuwa na ufaulu zaidi katika mitihani?
Tunaheshimu historia, lakini hatuwezi kuibadilisha, je leo tunaweza kurekebisha vipi yale ambayo yanaathiriwa hata sasa na historia, hususan ile ambayo ilibagua kundi fulani la watu, na hapa tukiongelea zaidi waislamu katika elimu?

Mimi ni mkristo, lakini nimeuliza maswali haya kwa sababu kama nilivyosema awali, ni mwalimu katika taasisi ya elimu ya juu, na siku moja niliwahi kukwaruzana na mwanafunzi wangu ambaye ni muislamu ambapo, japo niliona ni kutokana na utoto wake, lakini sina uhakika kama namna nilivyo handle suala lile ilikuwa sahihi hasa ukizingatia sina uelewa wa kutosha na hiki kinachoitwa mfumo kristo...
 
Ni kweli nimeumia sana, watanzania wameumia sana, walimwengu wameumia sana, Hii yote ni upotoshaji mkubwa ulioufanya ndugu yangu!

Simulizi za mashirikiano ya Nyerere na Abdu wala hazina kasoro yoyote kwenye historia ya Uhuru, kasoro ni ile tu uliyoipandikiza wewe kwa Waislamu nchini.

Watanzania gani walioumia?

Historia hii inapendwa sana na Watanzania wengi kitabu kinakwenda toleo la tatu.

Ulimwengu ndiyo huo kitabu kinasomwa kote.
Nitakuambia kitu.

Kila ninapokwenda basi nitaalikwa nuzungumze kuhusu historia hii.
Iwe ndani au nje ya nchi.

Nieleze nilichopotosha.
 
Nimekuwa nikitamani sana kujua nini maana ya Mfumo Kristo, na kama ni kitu halisi lakini kwa bahati mbaya sijawahi kupata jibu zuri. Yupo mwanaJF anayeitwa Mkandara, aliwahi kuniambia kuwa ni mfumo uliotumiwa na serikali za kikoloni, kutawala kwa kupendelea ukristo na kubagua wasio wakristo. Bw Mkandara alionyesha wasiwasi kuwa bado chembechembe za mfumo kristo hadi sasa, japo hakuweza kutoa mifano. Niliwahi tena kuendesha mjadala kwenye thread moja humu na mwanaJF anayeitwa Ami (sina uhakika kama nimekumbuka jina vizuri), ambae nae alionyesha hisia za uwepo wa mabaki ya mfumo kristo, lakini hakuweza kunipa mifano stahiki.

Binafsi niko very interested kujua kama mfumo kristo ni kitu kinacho exist hadi leo, au leo tunashuhudia tu makovu yake? Interest yangu kwa kiasi fulani inatokana na kwamba mimi ni mwalimu katika mojawapo wa taasisi za juu za elimu Tz, na huwa najiuliza kwa nini hadi sasa (miaka 50 baada ya kuondoka wakoloni) bado ratio ya waislamu darasani ni ndogo sana ukilinganisha na wakristu? Mzee Mohamed Said, nimejaribu kusoma maandiko yako mengi humu JF, kwa bahati mbaya sijawahi kusoma maandiko yake mengine. Katika hayo niliyosoma sijapata kuona sharp evidences za uwepo wa mfumo kristo hadi leo, na namna unavyoathiri maendeleo ya waislamu kielimu.

Nimefanya observation ndogo kwenye matokeo ya form four mwaka jana, nikajaribu kulinganisha ufaulu katika shule za serikali katika wilaya ya Morogoro vijijini (ambako wengi ni waislamu) na za wilaya ya Moshi vijijini (ambako wengi ni wakristo). Siwezi nikasema kuwa tofauti niliyoiona inatokana moja kwa moja na dini zao. Nilifikiria yapo mambo kama mazingira ya kufanyia kazi na kadhalika. Swala ambalo naomba Mzee Mohamed unisaidie, je ni kwa vipi serikali inaweza kufanya, bila upendeleo au bila kuwakandamiza wakristo, kuhakikisha ufaulu katika maeneo na shule zenye waislamu wengi sio tofauti na maeneo na shule zenye wakristo wengi?
Je, ni juhudi zipi ambazo waislamu wanaweza kuzifanya, wao kama wao, kuhakikisha watoto wao wanakuwa na ufaulu zaidi katika mitihani?
Tunaheshimu historia, lakini hatuwezi kuibadilisha, je leo tunaweza kurekebisha vipi yale ambayo yanayoathiriwa sasa na historia, hususan yale ambayo yalibagua kundi fulani la watu, ha hapa tukiongelea zaidi waislamu katika elimu?

Mimi ni mkristo, lakini nimeuliza maswali haya kwa sababu kama nilivyosema awali, ni mwalimu katika taasisi ya elimu ya juu, na siku moja niliwahi kukwaruzana na mwanafunzi wangu ambaye ni muislamu ambapo, japo niliona ni kutokana na utoto wake, lakini sina uhakika kama namna nilivyo handle suala lile ilikuwa sahihi hasa ukizingatia sina uelewa wa kutosha na hiki kinachoitwa mfumo kristo...

Kuna DVD za Ilunga Kapungu ni mashuhuri sana. Kazungumza kwa kirefu na kwa undani kuhusu mfumokristo.
Zinauzwa kwingi nchini.
 
Hilo swali lako ungemuuliza mzee wako nadhani angekujibu vizuri.
Ndio matatizo ya wafuasi wa Sultan Mangungu wa Bagamoyo, ukiwauliza maswali genuine wanabaki kuchekacheka tu/
 
Watu waliofilisika mawazo watajitambulisa kwa mambo mengi ya hovyo,ama udini ,au ukabila
 
ndugu mpemba mbishi, kwahiyo na shule za kiislam walimu wanaofundisha huko wanasema hata continuous assessment za watoto ni mbaya kiasi kwamba wakifanya mtihan wa taifa lazma wafeli tu, pendeni shule acheni maneno, mabinti wanafika miaka 16 mnataka waolewe ,taz pendekezo la waislam kwenye maoni ya katiba sasa mtasoma saangapi? kumbuka ukimwelimisha mama umeelimisha jamii. Ndugu zetu nyie hampendi shule, taz mashehe ndio wamekumbuka leo kuanzisha vyuo kuwasomesha mashehe ili wawe na elimu ya dini badala ya kujifunzia vichochoroni. Mimi nimesoma na waislam wao wenyewe wanakiri namna msivopenda shule., lakini pia tazama chuo kikuu cha kiislam pale morogoro kilivyojaa udini mpaka wakristu na hata waislam wenyewe wanaogopa kwenda kusoma, lakini angalia ST.AUGUSTINE, TUMAIN,ST JOSEPH, MAKUMIRA huko koote kuna waislam na wala hatubaguani. Huko utakuta walimu wakristo na waislam, lakini pale morogoro chuo kile hata mfagiaji lazma uwe muislam.QURAN imewataka msome na elimu DUNIA PIA.sasa serikali inatoa ruzuku kama ulivoonesha sababu wanaotibiwa pale BUGANDO, KULE KCMC, Na hospitali zoote za kikristu ni WATANZANIA WOOTE, lakini pia shule nyingi zilijengwa na wamisionari , hivi wakati waarabu wanafanya biashara ya utumwa wao walijua kujenga misikiti tu, sasa wakumlaumu nani? NYERERE Alitaifisha shule zilizokuwepo na zilikuwa za wakristo na kuamuru watoto wote wakasome, tatizo likaja waislam wakawa wanaogopa wakidhan watasilimishwa, taz kikwete, makamba, jaji othman na wengineo wengi wazai wao waliwapeleka shule hzo na leo ndo viongozi.PELEKENI WATOTO SHULE ,ACHENI KUKANDAMIZA WATOTO WA KIKE KWA KUWAOZESHA MAPEMA na NYIE WANAUME PENDENI SHULE BASI Elimu dunia na elim akhera...,.
 
Mwandishi wa uzi huu udini na kutojua historia ya zanzibar ndio ulokupelekea kuandika pumba zako soma kitabu kinachoitwa uhasidi wa marekani kwa mapinduzi ya zanzibar. Kilichotungwa na giorgio galinoshadjivayansi na abdulrahman babu ndio utajua ukweli wote otherwise u havo no right to question any thng about zanzibar

Mohamed Said inaonekana kila kitu kwake anakiangalia kwa mfumo wa waislam kunyanyaswa. Mbona hajamlaumu Nyerere kwa kutaifisha shule, hospitali, majengo, viwanda nk vya watu wengine? Je Nyerere alitaifisha shule za makanisa ili kuzuia maendeleo ya waislamu? Kama Mohamed anataka watu wamwone gwiji wa kutetea haki za watanzania, lazima afungue macho nje ya uislam aangalie matatizo ya watu wote na namna tunovyoweza kusonga mbele.
 
Nicho kiamini mm, nikwamba hakuna hata mkirsto mmoja atakae kubariana na hoja ya bw.Mohammed said. Kwakua ana tishia maslah yao kwenye Taifa hili. Hatakama aje na ushahidi gani watapinga2 kwani ukifuatilia kwa makini utagundua jinsigani anavyo wa jibu tena kwa heshma na taadhima. Labda ninavyoona mzee anatumia lugha ya balagha sana ktk kuwajibu lugha ambayo haibatikani kanisani. Chengine niwaambie ndugu zangu waislam tuschoke wala kuvunjika moyo ktk harakati hizi maana kwakweli zinaamsha hali ya kujitambua. Maana hata mm nilikua namuona Nyerere nimtu wa maana sana, ila tangu nisome kitabu chake mzee dah ! Sitaki hata kusikia tu jina la huyo mtu
 
Sawa mzee wangu nitazitafuta (ingawa sijui ni wapi)
Ila kama unachoweza kuongeza katika maswali nilouliza hapo juu nitashukuru pia...

Hapa Dar DVD hizo zinauzwa kwingi sana:

Msikiti wa Mtoro Kariakoo
Msikiti wa Ibadh Ilala
Msikiti Ngazija Mkwepu Street
Masjid Riadha, Moshi
Msikiti Mkubwa, Bondeni Arusha
Kwa Mazrui, Tanga
Takriban nchi nzima kwenye misikiti utazikuta bei ni kati ya shs 3000 - 5000

Sina cha kuongeza katika somo hilo.
Bingwa wake ni Sheikh Ilunga Kapungu
 
Nicho kiamini mm, nikwamba hakuna hata mkirsto mmoja atakae kubariana na hoja ya bw.Mohammed said. Kwakua ana tishia maslah yao kwenye Taifa hili. Hatakama aje na ushahidi gani watapinga2 kwani ukifuatilia kwa makini utagundua jinsigani anavyo wa jibu tena kwa heshma na taadhima. Labda ninavyoona mzee anatumia lugha ya balagha sana ktk kuwajibu lugha ambayo haibatikani kanisani. Chengine niwaambie ndugu zangu waislam tuschoke wala kuvunjika moyo ktk harakati hizi maana kwakweli zinaamsha hali ya kujitambua. Maana hata mm nilikua namuona Nyerere nimtu wa maana sana, ila tangu nisome kitabu chake mzee dah ! Sitaki hata kusikia tu jina la huyo mtu
Mchukie nyerere lakini pia jichukie wewe mwenyewe pia kwa kutopenda kujua ukweli na uongo.
 
Back
Top Bottom