Vintage Mohamed Said!
Kitabu cha Mwakikagile hiki hapa.
Life in Tanganyika in The Fifties - Godfrey Mwakikagile - Google Books
Kitabu hiki ni mkusanyiko wa simulizi za watu walioishi Tanganyika katika miaka ya 50. Hiyo Appendix anayoizungumzia Shehe hapa ni kumbukumbu za Ally Sykes juu ya rafiki yake Peter Colmore. Hiyo plagiarism anayoizungumzia Mohamed Said iko wapi? Au anataka kutuambia ni yeye peke yake anayeruhusiwa kuongea na wakina Sykes? Au kilichomuuma ni huyu ndugu wa Abdulwahid anamkumbuka kwa mapenzi makubwa mmisheni aliyekuwa rafiki na mfanyabiashara mwenzake? Au wasiwasi ni kuwa tofauti na simulizi zake huu ni ushahidi kuwa wakina Sykes anaowazungumzia hawakuwa wadini?
Mohammed Said ni mchonganishi. Ni mtu mwenye pretensions of grandeur. Hana kingine zaidi ya hicho.
Amandla..........
FM,
Hapana hilo neno ''plagiarism'' unalitumia wewe.
Mimi nililikwepa.
Unaandika kwa hasira sijui kwa nini.
Maneno kama ''mmisheni'' yanaondoa utamu wa majibu yako.
Mimi siwezi kuumwa na chochote kwa kuwa hiyo Appendix
ni mimi niliyeandika.
Ilikuwa ni orbituary ya Peter Colmore ambae mimi nikimjua toka
wakati mimi ni kijana mdogo sana.
Ofisi na makao yake akiwa Dar es Salaam yalikuwa jirani na nyumbani
kwetu katika miaka ya mwanzo ya 1960.
Nikaja kukutananae ukubwani wakati naandika ''Under the Shadow of
British Colonialism...''
Nikimfanyia mahojiano nyumbani kwake Muthaiga au Muthaiga Club
Nairobi.
Kilichonisukuma kuandika ile taazia ni pale nilipoona taazia zilizochapwa
na magazeti ya Kenya hayakumtendea haki.
Orbituary hiyo iliyo kwenye Appendix ilichapwa na The East African.
Mhariri wa The East African, James Odindo alinipigia simu kuniuliza vipi
nilimjua Peter Colmore kwa kiasi kile.
Jibu langu nilimwambia alikuwa ni mzee wangu.
Ikiwa unajua staili yangu ya uandishi utanisikia humo nazungumza.
Sasa ukipenda pita ndani ya kitabu hicho cha Mwakikagile utanikuta.
Sina sababu ya kusema uongo.
Kwa kumaliza napenda kukufahamisha hii si mara ya kwanza kwa maandishi
yangu kutumiwa na waandishi wengine ndani ya kitabu.
Lakini kama nilivyosema katika Uislam hilo si kosa.
Hiyo hukumu juu yangu kuwa mimi napenda ''pretensions of grandeur''
hizo ni fikra zako na una haki nazo.