Aisee hii ni ya zamani sijui hadi nitafute kwenye archives zangu... maana vingine vimeshapotea...
Aisee hii ni ya zamani sijui hadi nitafute kwenye archives zangu... maana vingine vimeshapotea...
Nadhani sasa ni muda muafaka wa kufanya mathalani tathmini kidogo ya yaliyojiri na ikiwezekana kuwawezesha wengi wanaofuatillia huu mjadala kutafakari yaliyojitokeza na kujiuliza maswali kadhaa. Mengi ya haya maswali ni yale ambayo ninaamini majibu yake hayapatikani kirahisi ndani ya vitabu alivyoviandika Mohamed Said kuhusiana na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Hata hivyo nina ombi moja tu kwamba kuanzia sasa kama kuna hoja ama ufafanuzi unatakiwa kutolewa, utolewe kwa njia inayokubalika kwa lengo la kuelimishana lakini kama mtu hana hoja au jibu sahihi ingefaa sana akibakia msomaji tu.
Wanajamvi naomba kwanza tujaribu kujizuia na majibu ya dhihaka na kejeli tuweze angalau kudumisha amani, upendo, undugu na utanzania ambao tumejivunia kwa miaka mingi bila kubaguana kwa misingi aliyotuwekea Baba wa Taifa. Na pili naomba mimi niwe wa kwanza kumuuliza Mohamed Said maswali mawili matatu ambayo yanaleta utata katika maandiko yake ambayo, kama anavyodai ameyafanyia utafiti wa muda mrefu, sidhani kama atashindwa kuyajibu kwa ufasaha.. Mohamed Said, maswali yangu kwako ni haya;
- Baada ya TANU kuasisiwa, viongozi wake wengine wa juu, pasi Mwalimu Nyerere aliyechaguliwa kwa kishindo kuwa Raisi wake wa Kwanza, walikuwa ni akina nani, walipatikanaje (kuteuliwa au kupigiwa kura?) na kwa sifa zipi? Hapa nina maana ya Makamu Raisi, Katibu na msaidizi wake, Katibu Mwenezi kama alikuwapo, Mweka Hazina n.k Hapo naongelea iliyokuwa kama kamati kuu ya TANU baada ya kuzinduliwa kama iliwahi kuwepo.
- Kama viongozi hawa waliteuliwa, ni nani aliyewateua na kwa kuzingatia nini. Je, katiba ya TANU ilikuwa inasemaje na je ilifuatwa katika kuwateua?
- Kama viongozi hawa walichaguliwa, walipendekezwa na nani waweze kupigiwa kura? Je hawa wajumbe waliowachagua walipatikanaje? Je majina yao yanaweza kuwekwa wazi kwa wanaofuatilia mjadala huu?
- Mohamed Said, umedai kuwa TANU ilivyozidi kupanuka na kuenea sehemu mbali mbali, idadi ya viongozi Wakristo iliongezeka kwa kasi na kuanza kuwatia shaka wenzao wa Kiislaam...je hawa viongozi walipatikanaje? Je waliteuliwa au walichaguliwa kwa kupigiwa kura?... vyovyote vile je katiba ya TANU ilifuatwa?
Wanajamvi naamini haya maswali ya mwanzo ni muhimu sana katika kuangalia, kutafakari na kujiridhisha na timeline kuhusu baadhi ya Watanganyika walioshiriki karika harakati za kudai uhuru kutokuwa na imani na uongozi wa Mwalimu kabla ya uhuru. Baadaye tutaingia kwenye awamu ya pili nayo ni baada ya uhuru...kitu gani kilileta kutokuaminiana?
Mohamed Said, kwa ukumbusho tu, majibu ya hii posti hapa chini bado yanasubiriwa, asante.
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...Mohamed Said, kwa ukumbusho tu, majibu ya hii posti hapa chini bado yanasubiriwa, asante.
Katika biography ya Muhammad Ali "The Greatest" kuna kisa anahadithiafujo alizofanya Drew Bundini kwenye kupima uzito pambano na Sony ListonMiami Beach Florida 1964.Kweli Ali anasema nilimtuma Bundini tufanye "fujo" ya kupata "publicity" magazeti na TV zitutoe.Ali anasema Bundini kafanya vurugu iliyofurtu ada.Akajuta."Kweli tuliandikwa sana lakini tulipigwa faini na boxing board."Alipomuuliza Bundini akajibu, "Si ulisema tufanye fujo."Ali anamaliza mkasa huu kwa kusema kuwa toka siku ile alimuogopa Bundini.Sababu ni kuwa Bundini alikuwa mwehu.Ali anasema mtu mzima yoyote lazima amuogope mwendawazimu.
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...
Umesema vema ABDALLAH na siyo MwamnyanyiKilemba?
Naamini mpaka leo hii vazi lao la heshima wahehe ni kilemba na kanzu, hapo Chief Abdallah Mkwawa ndani ya Ihraam na Kilemba ananikumbusha Wasudan huyu.
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...
Mohamed hili ni kosa kubwa na nashangaa kwanini mtu wa uelewa wako anaweza kudhani ni jambo jema.
Kwa kadri nijuavyo uislam ni dini na ili uwe mwislam ni inakupasa kuisoma dini katika Korani, kusoma hadithi na kuzielewa sunna.Ndio maana katika Uislam wale waliobobea ni wasomaji wazuri sana hata kama wamezaliwa kutoka koo za mahalifa.
Notion ya kwamba baba anaitwa Mwinjuma na mama Mwanameka basi mtoto wao Mwanamtama atakuwa Mwislam ni upotofu mkubwa. Atakuwaje mwislam bila kusoma na kuielewa dini yake!
Matokeo ya haya ni kupata ''half baked'' scholars na kazi yao kubwa ni kupidisha mafunzo ili kukidhi haja zao.
Mfano ni Ilunga na wenzake wanaoamini kuwa ''kisasi'' ni neno linalosima lenyewe na hivyo kuropoka tu.
Matokeo ya haya ni kupata washabiki na si waumini.
Anyway hii ilikuwa off topic turudi kwenye mnakasha na hasa hoja za Mag3 na tathmini ya mnakasha.
Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,
Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!
Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,
Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!
Lakini muheshimiwa mwanakijiji mwandishi alisha sema anarudisha wazee wake walio ondelowa kwenye historia ya taifa letu, sasa aandike wengine ambao walisha ingizwa katika historia ama sio wazee wake ili iweje?KUna msemo wa kuwa unaweza kuwa "unatwanga maji kwenye kinu" au ni sawa "na kumpigia mbuzi gitaa". Kama watu wametusoma vya kutosha humu kuna mambo yako wazi kabisa kuhusu maandishi ya Bw. Mohammed Said. NIkiamua kujumlisha tu kwa ufupi ni kwamba:
1: Hakutaka kuandika kazi ya historia
Japo mara kwa mara ndugu yetu anapenda kuelezea maandishi yake kuwa ni kazi ya kihistoria ukweli ni kuwa - na tumefanikiwa kuuonesha mara kadhaa sasa - Bw. Said alitaka kuanzika simulizi (narrative) ya wazazi wake biila kujali USHAHIDI kihistoria. Sote katika utoto tumekaa na wazee wetu ambao wametusimulia mambo mengi - yawe ya uhuru au ya maisha ya kijijini - na yametupa mawazo fulani juu yetu sisi wenyewe. Kwa mfano, kuna watu ambao wanamchukia Nyerere kwa kuendesha kampeni ya Ujamaa Vijijini kwa sababu wazazi wao waliwasimulia jinsi hali ilivyokuwa mbaya. Wapo wengine ambao walijikuta wanamchukia Idi Amin kwa sababu wakati wanakua simulizi kubwa pale nyumbani lilikuwa ni chuki dhidi ya Idi Amin.
Sasa masimulizi hayo ya utotoni hata yakitoka kwa baba, babu, wajomba au shangazi hayawi historia kwa sababu wao wamesema. Yanakuwa historia kama yana ushahidi wa kihistoria. Bahati mbaya sana Bw. Said hajajali ushahidi wa kihistoria kwani ushahidi pekee ambao yeye kautumia ni ule wa kuthibitisha hoja yake. Kwa kufanya hivyo Bw. Said amefanya kosa kubwa sana katika uandishi wa historia - kuonesha historical bias. Sasa historical bias ni rahisi sana kuiona kwenye maandishi ya mtu.
Kitabu cha Bw. Said kinampa msomaji kile kinachojulikana kama revisionist history; yaani ameamua kutoka kwenye historia ilivyo na kuielea kwa misingi ya bias yake.
2. Bias kubwa ya Bw. Said naweza kusema inatokana na kile ambacho yeye anaamini ni nguvu yake - yaani wazee wake. Kwa kujaribu kuandika historia kwa kutumia wazee wake kama "the most reliable sources' na kushindwa kuwa huru kimawazo kusoma mawazo yanayopingana na wazee wake amejikuta anaandika historia kwa kutumia bias without any sense of objectivity. Kwa yeye anaamini hilo ni sawa kwa sababu "ni historia ya wazee wangu". Tatizo ni kuwa historia ya wazee wake haiwi historia kwa vile wamemsimulia yeye inakuwa historia kama inaangaliwa objectively. Hili ndio tatizo kubwa.
3. Kutokana na hayo mawili hapo juu maandishi ya Bw. Said yamejaa hisia zaidi kuliko ushahidi wa kihistoria. Hisia ambazo zinatokana na mapenzi ya mtoto kwa wazee wake, uchungu wa mjukuu kwa babu yake, na hisia ya fungamano la dini. Bw. Said ataamini yale yote anayoambbiwa na wazee wake bila kuyahoji kwani kuhoji ni kuwavunjia heshima, kuuliza ni kutokuwaamini. Mwanahistoria mzuri ni yule ambaye anahoji na kuuliza maswali. Bw. Said amekuwa mpokeaji wa majibu lakinibila kuuliza maswali wala kuwa tayari kutambua contradictions katika maelezo ya watu.
4. HIvyo Bw. Said kaandika kile nilichokipa jina la "histohisia" yaani historia inayoandikwa kutoka kwenye hisia. Bw. Said aliaminishwa toka utotoni kuwa wazee wake walionewa; pale mtaani alipokulia alizungukwa na watu ambao walimuaminisha kuwa Waislamu wameonewa na wazee wa Dar hususan wamefutwa katika historia. Aliambiwa adui aliyefanya hivi ni Julius Nyerere aliyekaribishwa na wazee wake na kufanyiwa kila aina ya ukarimu; akaambiwa kuwa alipoingia madarakani Nyerere aliwageuka Waislamu wa Dar na kuwatenga. Simulizi hili lilimgusa ndugu Said kiasi kwamba alijiapia mwenyewe kuwa akipata nafasi ya kuandika simulizi la wazee "wake" atafanya hivyo.
Maandishi yake basi na yeye mwenyewe ameshasema mara nyingi ni kutimiza ndoto ya kusimulia yaliyowakuta wazazi wake kwa kadiri walivyomwambia. Hakufanya juhudi zozote za kutaka kuhakikisha kama aliyoambiwa na wazee wake ni kweli na kama ni kweli basi kwa kiasi gani na je kuna maelezo mengine yanayoweza kuelezea aliyosimuliwa.
5. Kutokana na hilo la nne kwa makusudi kabisa na pasi ya kufikiria sana Bw. Said akaamua kufanya mambo mawili makubwa sana ambayo yanaharibu kabisa simulizi zake.
a. Kutosimulia wazee wengine ambao walishirikiana na wazee wake katika harakati za Uhuru pamoja na Baba wa Taifa. Na wazee hawa WOTE ni Wakristu. Kimsingi, Bw. Said amefanya exactly kile ambacho anamtuhumu Nyerere. Bw. Said anasema Nyerere aliacha historia iandikwe ikimuweka yeye kama 'peke yake' katika harakati za uhuru na kuwaacha wazee wa Kiislamu (hasemi wazee wengine); na yeye kwa makusudi ameamua kuandika historia ya wazee wa Kiislamu na kuwaacha wazee wengine! Lakini la kwake analihalalisha kuwa ni sawa kuandika 'historia' kwa kuangalia upande mmoja lakini ni makosa kwa waandishi wa historia ya Nyerere kuandika kwa upande mmoja!
b. Kutoka kwenye simulizi la historia aliyosimuliwa Bw. Said akaenda mbali zaidi na kuanza kuelezea kwa misingi ya kuonesha kuwa Wakristu nchini wananufaika na wamenufaika sana na uhuru kuliko Waislamu na hii imetokana na ukwlei kuwa Wakristu wamependelewa na Waislamu wametengwa. Simulizi lake basi limetoka kuwa la kihistoria na kuwa la kiharakati - sasa hili halina tatizo kabisa kama akisema awali kuwa ni suala la harakati.
6. Bw. Said amefanikiwa kupata wasikilizaji wengi na watu wengi wakimuamini kwa sababu wengi wa hawa hawana namna ya kujua mbinu anazotumia kujenga hoja. Ikumbukwe kuwa Bw. Said hajatumia mbinu za uandishi wa kihistoria ambao unaongozwa na historical method. Yeye kaandika kama alivyosmuliwa na alikusanya nyaraka na kuzipa tafsiri ya yeye anachoamini. Ukimsoma sana utaona ni jinsi gani anaandika kama ana uwezo wa kujua nia, hisia, na mawazo ya wahusika.
7. Kitabu chake maarufu kinachomzungumzia Abdul Sykes kwa kweli ni sehemu ndogo sana inahusiana na maisha ya Abdulwahid Sykes. NI kitabu ambacho kinaelezea kwa kirefu uwezo, ushawishi na uongozi wa Mwalimu Nyerere kati ya wazee wake Jijini Dar - Wakristu, Waislamu, Wahindi na Wapagani! Binafsi nilipokisoma kitabu hicho kwa kuangalia 'facts' peke yake nilikipenda mno kwani kinamuonesha Nyerere kwa mwanga mzuri sana. Ni pale tu Bw. Said anapoweka hisia zake ndipo unapoona utamu wa kitabu kufutika kwa sababu kwa kiasi kikubwa hisia zake hazina ushahidi wowote wa kuzithibitisha. Kwa mfano anaposema "ilisemwa" au "iliaminika" au "alidhaniwa" ni wazi kuwa hana namna yoyote ya kujua hisia hizo isipokuwa kwa kukisia - ndio maana naiita 'histohisia'.
Binafsi nashauri watu wote wanaopenda kujifunza tofauti ya historia na histohisia wakitafute kitabu hiki kwani kitawafundisha namna YA KUTOANDIKA HISTORIA.
MMM
Unaona kama umepata pakupumulia, wapi? ulijidai kuruka kwenda Iringa huko ukakutana na ma uppercut ya uhakika, ukaanza oooh, wewe hujui historia ya machifu, lakini ukaufyata hukuendelea, unakumbuka ulipojidai unamjuwa chifu wa huko ukaulizwa "Abdu Mkwawa?" ukabana kimya kama hukuona.
Nakuonea huruma sana kujitosa kwenye maji yaliyokuzidi kimo na kuogelea hujui. Naona wenzako wamekutupia tyubu ujivutevute, ukisha pata pumzi njoo na jingine.
Tunasubiri, ulisema ukimaliza la Mkwawa utakuja na la Abushiri, vipi? maji marefu? Naona la Mkwawa umeomba ukatafute data kama ulivyoomba kuleta klip ukaingia mitini wala huiongelei, nna uhakika na la Mkwawa limekuwa ni knockout ya ki Tyson (zile za raundi ya kwanza) kwako. Pole sana, lakini usikate tamaa, jitahidi ndio ukubwa huo.
Lakini muheshimiwa mwanakijiji mwandishi alisha sema anarudisha wazee wake walio ondelowa kwenye historia ya taifa letu, sasa aandike wengine ambao walisha ingizwa katika historia ama sio wazee wake ili iweje?
Mkuu Said umenichekesha sana, umenikumbusha mengi kuhusu Binadamu huyu ambaye alikuwa aogopi kusema ukweli aogopi DORA i.e Moh Ali! Jamaa huyu alikuwa mtu wa matani sana na alikuwa na mbinu nyingi za kuwahamasisha watu waje kuangalia mapambano yake na kumuongezea kipato, hakuwa na akili za kawaida yule: Kuna msemo wake ulio kuwa unawahacha wasikilizaji hoi - he goes " I'm so MEAN I can make MEDICINE SICK" hata sijuhi maneno alikuwa anayatoa wapi! "I ain't got no quarrel with them Viet Cong".
Back 2 the point, Ndugu SAID sijuhi ni watu wangapi wamekuelewa sentensi yako ya mwisho? Lakini mimi nimekuelewa sana.
Kwa Abushuri Bin Salim Bin Harith wa Pangani ndiyo hawezi kabisa.