Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Aisee hii ni ya zamani sijui hadi nitafute kwenye archives zangu... maana vingine vimeshapotea...

Ukiona mtu anakupiga chenga na anatafuta visababu ujuwe alikumbana na asiyoyatarajia. Kama yanavyomkumba Yericko kwenye hii mada.

Usione haya, iweke tu, ndio ukubwa huo.
 
Mohamed Said, kwa ukumbusho tu, majibu ya hii posti hapa chini bado yanasubiriwa, asante.
Nadhani sasa ni muda muafaka wa kufanya mathalani tathmini kidogo ya yaliyojiri na ikiwezekana kuwawezesha wengi wanaofuatillia huu mjadala kutafakari yaliyojitokeza na kujiuliza maswali kadhaa. Mengi ya haya maswali ni yale ambayo ninaamini majibu yake hayapatikani kirahisi ndani ya vitabu alivyoviandika Mohamed Said kuhusiana na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Hata hivyo nina ombi moja tu kwamba kuanzia sasa kama kuna hoja ama ufafanuzi unatakiwa kutolewa, utolewe kwa njia inayokubalika kwa lengo la kuelimishana lakini kama mtu hana hoja au jibu sahihi ingefaa sana akibakia msomaji tu.

Wanajamvi naomba kwanza tujaribu kujizuia na majibu ya dhihaka na kejeli tuweze angalau kudumisha amani, upendo, undugu na utanzania ambao tumejivunia kwa miaka mingi bila kubaguana kwa misingi aliyotuwekea Baba wa Taifa. Na pili naomba mimi niwe wa kwanza kumuuliza Mohamed Said maswali mawili matatu ambayo yanaleta utata katika maandiko yake ambayo, kama anavyodai ameyafanyia utafiti wa muda mrefu, sidhani kama atashindwa kuyajibu kwa ufasaha.. Mohamed Said, maswali yangu kwako ni haya;


  1. Baada ya TANU kuasisiwa, viongozi wake wengine wa juu, pasi Mwalimu Nyerere aliyechaguliwa kwa kishindo kuwa Raisi wake wa Kwanza, walikuwa ni akina nani, walipatikanaje (kuteuliwa au kupigiwa kura?) na kwa sifa zipi? Hapa nina maana ya Makamu Raisi, Katibu na msaidizi wake, Katibu Mwenezi kama alikuwapo, Mweka Hazina n.k Hapo naongelea iliyokuwa kama kamati kuu ya TANU baada ya kuzinduliwa kama iliwahi kuwepo.
  2. Kama viongozi hawa waliteuliwa, ni nani aliyewateua na kwa kuzingatia nini. Je, katiba ya TANU ilikuwa inasemaje na je ilifuatwa katika kuwateua?
  3. Kama viongozi hawa walichaguliwa, walipendekezwa na nani waweze kupigiwa kura? Je hawa wajumbe waliowachagua walipatikanaje? Je majina yao yanaweza kuwekwa wazi kwa wanaofuatilia mjadala huu?
  4. Mohamed Said, umedai kuwa TANU ilivyozidi kupanuka na kuenea sehemu mbali mbali, idadi ya viongozi Wakristo iliongezeka kwa kasi na kuanza kuwatia shaka wenzao wa Kiislaam...je hawa viongozi walipatikanaje? Je waliteuliwa au walichaguliwa kwa kupigiwa kura?... vyovyote vile je katiba ya TANU ilifuatwa?

Wanajamvi naamini haya maswali ya mwanzo ni muhimu sana katika kuangalia, kutafakari na kujiridhisha na timeline kuhusu baadhi ya Watanganyika walioshiriki karika harakati za kudai uhuru kutokuwa na imani na uongozi wa Mwalimu kabla ya uhuru. Baadaye tutaingia kwenye awamu ya pili nayo ni baada ya uhuru...kitu gani kilileta kutokuaminiana?
 
Mohamed Said, kwa ukumbusho tu, majibu ya hii posti hapa chini bado yanasubiriwa, asante.

Hata hayo huyajuwi? ustake kutuchekesha.

Nilifikiri utakuja kusema Mshume ni jina la kubuniwa hakuwepo, wewe unataka tarehe, sijui nini kwa nini. Mohamed Said anakwambia alipoona kitabu cha kivukoni kimewaacha wazee wake na yeye anajuwa kuwa walipigania Uhuru akaamuwa kuandika historia na jinsi wazee wake walivyopigania uhuru. Sasa wewe kama unaona kuna mapungufu katika maandiko ya Mohamed Said kama alivyoona yeye mapungufu kwenye maandiko ya kivukoni hakuanza kuuliza uliza vitu visivyo na maana, aliingia kazini akaweeka mambo sawa kama ayajuavyo. Na leo hii unamjuwa Mashado Plantan ni nani, Mshume Kiate ni nani, Dossa Aziz ni na nani.

Jee, huoni kuwa utatenda wema na wewe badala ya kuja na kuuliza maswali yasiyo na maana ukaanza kuandika ukijuacho? Mwenzako ana kitabu sasa kina miaka 15 na bado kinauzika, na anaalikwa mialiko mbali mbali duniani kuelezea muono wake. Wewe Jee?

Hapo sasa.
 
Mohamed Said, kwa ukumbusho tu, majibu ya hii posti hapa chini bado yanasubiriwa, asante.
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...
 
Mag3 katika bandiko lako 2868 nayaangalia yafutayo na yatokanayo na kitabu, majibu na hoja za Mohamed Said.

1. Alichokiandika Mohamed ni kitu alichokuwa na majibu yake na utafiti ulilenga katika kukamilisha kile alichofikiri na si kile alichotafiti.

a) Ameonyesha bias ya uandishi kwa kuelekeza watu kuamini kile alichokusudia na si kile alichokitafiti
b) Aliandika katika mtazamo wa kushambulia ''attack'' kundi fulani la jamii na watu fulani si kutokana na hukumu ya historia bali kile alichodhani kuwa ima yeye au wazazi au ndugu zake hawakutendewa wema au walionewa.
c) Ameshindwa kuthibitisha maandiko yake kwa hoja za kitafiti,kukwepa maswali au hoja zinazoonekana kukinzana na a, b hapo juu.

Hoja: Endapo Mohamed alifanya utafiti asingeweza kuzama katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuzama katika TANU na kukwepa historia iliyoanzia karne nyingi. Mathalani, Mohamed hakueleza undani wa AA au TAA kwa kutambua kuwa hilo litaharibu historia nzima anayoidai, wala kulezea harakati nyingine nje ya Dar, mfano Mbiru na Wapare, vyama vya wafanyakazi n.k.

Mfano, angeandika kwa undani kuhusu AA na TAA ni dhahiri asingekuwa na hoja ya Nyerere kufundishwa siasa mwaka 1952 ili hali twajua kuwa alianza siasa miaka 6 kabla ya hapo tena katika uwakilishi wa jimbo kama Tabora.
Hilo peke yake lingetosha kupunguza nguvu za ziada anazompatia Abdul Sykes.

Ni kwasbabu ya kuonyesha bias, Mohamed amejikuta anaficha ukweli wa historia ya kweli.
Kwa vile lengo ni kushambulia kundi fulani, bwana Said ameacha makusudi mchango wa shirika la Maryknoll huku akiufahamu vema.

Kibaya zaidi ameenda mbali na kuudharau kwa kusema ni 'ticket' moja. Wakati akiudharau mchango huo Mohamed ameutukuza sana mchango wa ticket moja uliofanywa na wazee wake. Hapa ukweli upo wapi katika double standard kama hii.

Ili kukamilisha lengo alilokusudia,Mohamed amewaandika washiriki wa uhuru wasio katika kundi lake kwa dhalili ya hali ya juu. Amewataja kwa imani zao kama viambatanisho vya majina yao na kuacha mchango wao katika mapambano.

Katika hilo la bias, Mohamed ameandika kurusa za kutosha kuhusu Mwapachu kuliko alivyomwandika Mtamila aliyekuwepo kabla ya Mwapachu. Mo amemuelezea Mshume Kiyate kiasi kwamba Rais wa TAA Dr Vedastus Kyaruzi mchango wake hauonekani.

Kila mmoja alikuwa na mchango na si sahihi kuufanya mchango fulani bora kuliko mwingine hasa kwa kuangalia majina na viambatanisho vya imani zao. Hilo linaondoa hata hoja dhaifu iliyokuwepo.

Mohamed ameshindwa kuthibitisha madai yaliyomo ndani ya kitabu chake. Hata pale alipojaribu, MO alikwenda nje ya taratibu za utafiti na kanuni za asili za ''kisheria'' natural justice.

Mathalani, amelituhumu Kanisa kuhusika na mambo mengi maovu na mengi yaliyozuia harakati.
Ameshindwa kuthibitisha ushiriki wa kanisa, kinyume chake kunukuu habari za mtu mwingine ambaye kimsingi angekuwa chanzo cha utafiti wa ushahidi na si yeye kuwa ushahidi(sivalon).

Kwa vile uandishi wake ni katika misingi ya ''attack'' na siyo academic, Mohamed ameshindwa kutetea hoja zake kimantiki.
Mfano, hajaeleza kwanini ilipangwa njama ya kuondoa Nyerere katika uongozi wa TANU mara mbili wakati huo akiwa hana uongozi wa nchi au vyombo vya dola na akiwa chini ya baraza la wazee wa TANU waliokuwa wazee wake.

Moh ameshindwa kutetea hoja ni kwanini ukristo wake ulionekana kikwazo hata kabla ya kuingia madarakani na kwanini majaribio hayo yalipangwa. Pengine hapa alitaka kuficha hisia za udini ambazo ni sehemu ya malalamiko yake ya leo.

Mo ameshindwa kututhibitishia mkakati wa Nyerere kuumaliza Uislam na kuingiza ukristo ulianza lini na kwa mbinu gani.
Kinyume chake ametumia kifo cha EAMWS kumtupia lawama kama sehemu ya ukristo na kanisa.
Ameshindwa kututhibitishia ushiriki wa kanisa kwa ushahidi hivyo kubaki kuamini ndivyo ilikuwa.

Lakini pia ameshindwa kutetea hoja za EAMWS kwanini ilikufa huko kwingine na ni nani alihusika kuiua.
Kwa vile hoja yake haisimami yenyewe, Mo amewashirikisha baadhi ya waislam kama sehemu ya njama.

Iwe iwavyo mtu aliyekuwa na mtazamo tofauti na malengo ya MO huyo alikuwa kibaraka. Alikuwa kibaraka kama Amir Kweyamba aliyekuwa kachero wa serikali, lakini wale waliokula njama dhidi ya serikali walibaki kuwa waislam safi.

Mo ameupotosha umma mara nyingi katika hali ya kujenga hoja na pengine kuficha ukweli.
mfano, si kweli kuwa Nyerere alikuja Dar mwaka 1952, si kweli kuwa alionana kwa mara ya kwanza na Sykes mwaka 1952, si kweli kuwa viongozi wa TAA hawakumjua, si kweli kuwa alianza siasa mwaka 1952, si kweli aliandikiwa hotuba bila kujua alikwenda UNO kusema nini akiwa msomi mkubwa ndani ya TANU.

Ni katika upotoshaji huo, Mohamed ameacha kwa maksudi mchango uliotolewa na wazawa wengine wasio na imani kama yake. Amejikuta akikweza watu kwa majina ili kuficha majina yasiyompendeza.
Mfano, tunauthamini mchango wa Yusuf Ngozi lakini je, Yusuf alikuwa katika nafasi aliyokuwa nayo Dr Vedastus Kyaruz, Clement Mtamila, Stephen Mhando, Cecil Matola, Dunstan Omar na wengine ?

Mifano na hoja ni nyingi sana lakini kwa ufupi nimalizie kwa kusema, alichoandika Mohamed ni kutumia majina, nyakati na matukio ili kupata nafasi ya kushambulia sehemu ya jamii yetu kwa kudhalilisha na kudharau michango yao.
Hili limefanyika kwa kutumia majina kama Nyerere au kwa shambulizi la dini.

Amefanya hivyo kwa kuhadaa kuhusu utafiti kwasababu alijua kile alichokusudia kabla ya kuanza utafiti.
Mohamed amefanya hivyo ili kujenga uhalali wa kundi fulani juu ya umiliki wa nchi na kupitia hilo apenyeze madai yake ambayo mengi hayana uthibitisho kama kilivyo kitabu chake.

Sehemu kubwa ya maandiko yake yanatokana na ''third party'' na wengi aliowahoji ima walikuwa na duku duku au walieleza ukweli ambao Mo hapendi uwekwe hadharani. Ameshindwa kutuwekea shajara alizosoma na akitaka tuamini kile kilichomo ndani ya shajara. Kanuni za uandishi hasa wa kitafiti hazikubaliani na hilo.

Ili kuhakikisha kuwa jamii aliyokusudia kuieleza ina amini na haipati nafasi za kuhoji hoja zake, Mohamed ametumia sehemu kubwa ya utafiti wake na maandishi kujenga chuki, kuleta farki na uhasama.

Ametumia dhana kuhusu kile marehemu walichokifikiri hata kama hakuwahi kuwahoji na ameshindwa kuwahoji walio hai ili kupata upande wa pili.

Mo anafahamu kuwa sehemu rahisi sana ya kufikia malengo yake ni kutumia dini. Hili analifanya kwa njia ya ''sisi dhidi yao''

Ushahidi kuwa ameshindwa kutetea hoja zake,amepotosha, ameficha baadhi ya ukweli na ameshindwa kujibu hoja au maswali na pale alipojaribu alifanya hivyo kwa udhaifu, unatueleza kilichomo ndani ya mistari aliyoandika.
Na hapa ndipo taifa linapopaswa kutupia jicho.
 
Katika biography ya Muhammad Ali "The Greatest" kuna kisa anahadithiafujo alizofanya Drew Bundini kwenye kupima uzito pambano na Sony ListonMiami Beach Florida 1964.Kweli Ali anasema nilimtuma Bundini tufanye "fujo" ya kupata "publicity" magazeti na TV zitutoe.Ali anasema Bundini kafanya vurugu iliyofurtu ada.Akajuta."Kweli tuliandikwa sana lakini tulipigwa faini na boxing board."Alipomuuliza Bundini akajibu, "Si ulisema tufanye fujo."Ali anamaliza mkasa huu kwa kusema kuwa toka siku ile alimuogopa Bundini.Sababu ni kuwa Bundini alikuwa mwehu.Ali anasema mtu mzima yoyote lazima amuogope mwendawazimu.

Mkuu Said umenichekesha sana, umenikumbusha mengi kuhusu Binadamu huyu ambaye alikuwa aogopi kusema ukweli aogopi DORA i.e Moh Ali! Jamaa huyu alikuwa mtu wa matani sana na alikuwa na mbinu nyingi za kuwahamasisha watu waje kuangalia mapambano yake na kumuongezea kipato, hakuwa na akili za kawaida yule: Kuna msemo wake ulio kuwa unawahacha wasikilizaji hoi - he goes " I'm so MEAN I can make MEDICINE SICK" hata sijuhi maneno alikuwa anayatoa wapi! "I ain't got no quarrel with them Viet Cong".


Back 2 the point, Ndugu SAID sijuhi ni watu wangapi wamekuelewa sentensi yako ya mwisho? Lakini mimi nimekuelewa sana.
 
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...

Hoja au maswali yasiyo na mpango? kwani ni lazima ajibu kila upuuzi na ujinga anaoulizwa? kishasema kama anaona swali halina maana halijibu. Na wewe na wenzako wakuja, kama mnaona kuna mapungufu katika historia aliyoandika Mohamed Said, kwanini hamkai mkaandika kitabu chenu kwa muono wenu? Ulikuwa unamjuwa Tosiri kabla ya kumsoma Mohamed said? Ulikuwa unajuwa kuwa TANU ilibuniwa Burma kabla ya kumsoma Mohamed Said? Ulikuwa unajuwa kuwa Mwapachu alikuwa boss wake Nyerere katika chama huko Tabora?
 
Sweke,

Yeshakuwa ya kusutana?
Kwa mila za sie watu wa pwani huo ni mwiko.

Wanaume hatusutani.
 
Kilemba?

chief.jpg


Naamini mpaka leo hii vazi lao la heshima wahehe ni kilemba na kanzu, hapo Chief Abdallah Mkwawa ndani ya Ihraam na Kilemba ananikumbusha Wasudan huyu.

KhartoumAP0312_468x596.jpg
Umesema vema ABDALLAH na siyo Mwamnyanyi
 
Nilikuwa nina ka pendekezo kadogo. Kutokana na kuwepo kwa hoja nyingi ambazo Mohamed Said ameshindwa kuzijibu na urefu wa uzi huu ambao unaweza kuwafanya watu wengi wanaoanza kuangalia leo kutoziona hoja hizo, tujaribu kuzi compile hoja hizo ambazo hazijapata majibu halafu mkuu wetu Yericko Nyerere afanye utaratibu wa kuzibandika pale juu kwenye post yake. Kama hakuna space anaweza hata akaziweka kwenye word doc halafu akazi-attach kwenye post yake. Hizo hoja zikae pale juu ili ziwe kama zinamsuta huku na sisi tukiendelea kumkumbusha...

Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,

Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!
 
Mohamed hili ni kosa kubwa na nashangaa kwanini mtu wa uelewa wako anaweza kudhani ni jambo jema.

Kwa kadri nijuavyo uislam ni dini na ili uwe mwislam ni inakupasa kuisoma dini katika Korani, kusoma hadithi na kuzielewa sunna.Ndio maana katika Uislam wale waliobobea ni wasomaji wazuri sana hata kama wamezaliwa kutoka koo za mahalifa.

Notion ya kwamba baba anaitwa Mwinjuma na mama Mwanameka basi mtoto wao Mwanamtama atakuwa Mwislam ni upotofu mkubwa. Atakuwaje mwislam bila kusoma na kuielewa dini yake!

Matokeo ya haya ni kupata ''half baked'' scholars na kazi yao kubwa ni kupidisha mafunzo ili kukidhi haja zao.
Mfano ni Ilunga na wenzake wanaoamini kuwa ''kisasi'' ni neno linalosima lenyewe na hivyo kuropoka tu.
Matokeo ya haya ni kupata washabiki na si waumini.

Anyway hii ilikuwa off topic turudi kwenye mnakasha na hasa hoja za Mag3 na tathmini ya mnakasha.

Nguruvi3,

Wale Waislam ambao mnaowaandika humu wavivu hawana elimu, wavaa vipendo, watu wa kahawa tu, wavaa mateneti, watu wa ubwabwa tu, wana akili za madrasa watu wakulalamika hawataki kusoma unawaweka kundi gani.
 
Last edited by a moderator:
Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,

Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!

Unaona kama umepata pakupumulia, wapi? ulijidai kuruka kwenda Iringa huko ukakutana na ma uppercut ya uhakika, ukaanza oooh, wewe hujui historia ya machifu, lakini ukaufyata hukuendelea, unakumbuka ulipojidai unamjuwa chifu wa huko ukaulizwa "Abdu Mkwawa?" ukabana kimya kama hukuona.

Nakuonea huruma sana kujitosa kwenye maji yaliyokuzidi kimo na kuogelea hujui. Naona wenzako wamekutupia tyubu ujivutevute, ukisha pata pumzi njoo na jingine.

Tunasubiri, ulisema ukimaliza la Mkwawa utakuja na la Abushiri, vipi? maji marefu? Naona la Mkwawa umeomba ukatafute data kama ulivyoomba kuleta klip ukaingia mitini wala huiongelei, nna uhakika na la Mkwawa limekuwa ni knockout ya ki Tyson (zile za raundi ya kwanza) kwako. Pole sana, lakini usikate tamaa, jitahidi ndio ukubwa huo.
 
Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,

Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!

1) Usisahu kutuwekea na majina ya wale waasi walipewa msamaha na Nyerere na wengine wengi kupewa vyeo na mabalozi kama ulivyosema mwenyewe.

2) tuwekee na gari la kwanza la Nyerere uliosema kapewa na Mariale.

3) Utuwekee na kiasi cha pesa alichopewa Nyerere na Mariale kwenda UNO kama ulivyotuambia hapo mwanzo.
 
KUna msemo wa kuwa unaweza kuwa "unatwanga maji kwenye kinu" au ni sawa "na kumpigia mbuzi gitaa". Kama watu wametusoma vya kutosha humu kuna mambo yako wazi kabisa kuhusu maandishi ya Bw. Mohammed Said. NIkiamua kujumlisha tu kwa ufupi ni kwamba:

1: Hakutaka kuandika kazi ya historia

Japo mara kwa mara ndugu yetu anapenda kuelezea maandishi yake kuwa ni kazi ya kihistoria ukweli ni kuwa - na tumefanikiwa kuuonesha mara kadhaa sasa - Bw. Said alitaka kuanzika simulizi (narrative) ya wazazi wake biila kujali USHAHIDI kihistoria. Sote katika utoto tumekaa na wazee wetu ambao wametusimulia mambo mengi - yawe ya uhuru au ya maisha ya kijijini - na yametupa mawazo fulani juu yetu sisi wenyewe. Kwa mfano, kuna watu ambao wanamchukia Nyerere kwa kuendesha kampeni ya Ujamaa Vijijini kwa sababu wazazi wao waliwasimulia jinsi hali ilivyokuwa mbaya. Wapo wengine ambao walijikuta wanamchukia Idi Amin kwa sababu wakati wanakua simulizi kubwa pale nyumbani lilikuwa ni chuki dhidi ya Idi Amin.

Sasa masimulizi hayo ya utotoni hata yakitoka kwa baba, babu, wajomba au shangazi hayawi historia kwa sababu wao wamesema. Yanakuwa historia kama yana ushahidi wa kihistoria. Bahati mbaya sana Bw. Said hajajali ushahidi wa kihistoria kwani ushahidi pekee ambao yeye kautumia ni ule wa kuthibitisha hoja yake. Kwa kufanya hivyo Bw. Said amefanya kosa kubwa sana katika uandishi wa historia - kuonesha historical bias. Sasa historical bias ni rahisi sana kuiona kwenye maandishi ya mtu.

Kitabu cha Bw. Said kinampa msomaji kile kinachojulikana kama revisionist history; yaani ameamua kutoka kwenye historia ilivyo na kuielea kwa misingi ya bias yake.

2. Bias kubwa ya Bw. Said naweza kusema inatokana na kile ambacho yeye anaamini ni nguvu yake - yaani wazee wake. Kwa kujaribu kuandika historia kwa kutumia wazee wake kama "the most reliable sources' na kushindwa kuwa huru kimawazo kusoma mawazo yanayopingana na wazee wake amejikuta anaandika historia kwa kutumia bias without any sense of objectivity. Kwa yeye anaamini hilo ni sawa kwa sababu "ni historia ya wazee wangu". Tatizo ni kuwa historia ya wazee wake haiwi historia kwa vile wamemsimulia yeye inakuwa historia kama inaangaliwa objectively. Hili ndio tatizo kubwa.

3. Kutokana na hayo mawili hapo juu maandishi ya Bw. Said yamejaa hisia zaidi kuliko ushahidi wa kihistoria. Hisia ambazo zinatokana na mapenzi ya mtoto kwa wazee wake, uchungu wa mjukuu kwa babu yake, na hisia ya fungamano la dini. Bw. Said ataamini yale yote anayoambbiwa na wazee wake bila kuyahoji kwani kuhoji ni kuwavunjia heshima, kuuliza ni kutokuwaamini. Mwanahistoria mzuri ni yule ambaye anahoji na kuuliza maswali. Bw. Said amekuwa mpokeaji wa majibu lakinibila kuuliza maswali wala kuwa tayari kutambua contradictions katika maelezo ya watu.

4. HIvyo Bw. Said kaandika kile nilichokipa jina la "histohisia" yaani historia inayoandikwa kutoka kwenye hisia. Bw. Said aliaminishwa toka utotoni kuwa wazee wake walionewa; pale mtaani alipokulia alizungukwa na watu ambao walimuaminisha kuwa Waislamu wameonewa na wazee wa Dar hususan wamefutwa katika historia. Aliambiwa adui aliyefanya hivi ni Julius Nyerere aliyekaribishwa na wazee wake na kufanyiwa kila aina ya ukarimu; akaambiwa kuwa alipoingia madarakani Nyerere aliwageuka Waislamu wa Dar na kuwatenga. Simulizi hili lilimgusa ndugu Said kiasi kwamba alijiapia mwenyewe kuwa akipata nafasi ya kuandika simulizi la wazee "wake" atafanya hivyo.

Maandishi yake basi na yeye mwenyewe ameshasema mara nyingi ni kutimiza ndoto ya kusimulia yaliyowakuta wazazi wake kwa kadiri walivyomwambia. Hakufanya juhudi zozote za kutaka kuhakikisha kama aliyoambiwa na wazee wake ni kweli na kama ni kweli basi kwa kiasi gani na je kuna maelezo mengine yanayoweza kuelezea aliyosimuliwa.

5. Kutokana na hilo la nne kwa makusudi kabisa na pasi ya kufikiria sana Bw. Said akaamua kufanya mambo mawili makubwa sana ambayo yanaharibu kabisa simulizi zake.

a. Kutosimulia wazee wengine ambao walishirikiana na wazee wake katika harakati za Uhuru pamoja na Baba wa Taifa. Na wazee hawa WOTE ni Wakristu. Kimsingi, Bw. Said amefanya exactly kile ambacho anamtuhumu Nyerere. Bw. Said anasema Nyerere aliacha historia iandikwe ikimuweka yeye kama 'peke yake' katika harakati za uhuru na kuwaacha wazee wa Kiislamu (hasemi wazee wengine); na yeye kwa makusudi ameamua kuandika historia ya wazee wa Kiislamu na kuwaacha wazee wengine! Lakini la kwake analihalalisha kuwa ni sawa kuandika 'historia' kwa kuangalia upande mmoja lakini ni makosa kwa waandishi wa historia ya Nyerere kuandika kwa upande mmoja!

b. Kutoka kwenye simulizi la historia aliyosimuliwa Bw. Said akaenda mbali zaidi na kuanza kuelezea kwa misingi ya kuonesha kuwa Wakristu nchini wananufaika na wamenufaika sana na uhuru kuliko Waislamu na hii imetokana na ukwlei kuwa Wakristu wamependelewa na Waislamu wametengwa. Simulizi lake basi limetoka kuwa la kihistoria na kuwa la kiharakati - sasa hili halina tatizo kabisa kama akisema awali kuwa ni suala la harakati.

6. Bw. Said amefanikiwa kupata wasikilizaji wengi na watu wengi wakimuamini kwa sababu wengi wa hawa hawana namna ya kujua mbinu anazotumia kujenga hoja. Ikumbukwe kuwa Bw. Said hajatumia mbinu za uandishi wa kihistoria ambao unaongozwa na historical method. Yeye kaandika kama alivyosmuliwa na alikusanya nyaraka na kuzipa tafsiri ya yeye anachoamini. Ukimsoma sana utaona ni jinsi gani anaandika kama ana uwezo wa kujua nia, hisia, na mawazo ya wahusika.

7. Kitabu chake maarufu kinachomzungumzia Abdul Sykes kwa kweli ni sehemu ndogo sana inahusiana na maisha ya Abdulwahid Sykes. NI kitabu ambacho kinaelezea kwa kirefu uwezo, ushawishi na uongozi wa Mwalimu Nyerere kati ya wazee wake Jijini Dar - Wakristu, Waislamu, Wahindi na Wapagani! Binafsi nilipokisoma kitabu hicho kwa kuangalia 'facts' peke yake nilikipenda mno kwani kinamuonesha Nyerere kwa mwanga mzuri sana. Ni pale tu Bw. Said anapoweka hisia zake ndipo unapoona utamu wa kitabu kufutika kwa sababu kwa kiasi kikubwa hisia zake hazina ushahidi wowote wa kuzithibitisha. Kwa mfano anaposema "ilisemwa" au "iliaminika" au "alidhaniwa" ni wazi kuwa hana namna yoyote ya kujua hisia hizo isipokuwa kwa kukisia - ndio maana naiita 'histohisia'.

Binafsi nashauri watu wote wanaopenda kujifunza tofauti ya historia na histohisia wakitafute kitabu hiki kwani kitawafundisha namna YA KUTOANDIKA HISTORIA.

MMM
Lakini muheshimiwa mwanakijiji mwandishi alisha sema anarudisha wazee wake walio ondelowa kwenye historia ya taifa letu, sasa aandike wengine ambao walisha ingizwa katika historia ama sio wazee wake ili iweje?
 
Unaona kama umepata pakupumulia, wapi? ulijidai kuruka kwenda Iringa huko ukakutana na ma uppercut ya uhakika, ukaanza oooh, wewe hujui historia ya machifu, lakini ukaufyata hukuendelea, unakumbuka ulipojidai unamjuwa chifu wa huko ukaulizwa "Abdu Mkwawa?" ukabana kimya kama hukuona.

Nakuonea huruma sana kujitosa kwenye maji yaliyokuzidi kimo na kuogelea hujui. Naona wenzako wamekutupia tyubu ujivutevute, ukisha pata pumzi njoo na jingine.

Tunasubiri, ulisema ukimaliza la Mkwawa utakuja na la Abushiri, vipi? maji marefu? Naona la Mkwawa umeomba ukatafute data kama ulivyoomba kuleta klip ukaingia mitini wala huiongelei, nna uhakika na la Mkwawa limekuwa ni knockout ya ki Tyson (zile za raundi ya kwanza) kwako. Pole sana, lakini usikate tamaa, jitahidi ndio ukubwa huo.

Kwa Abushuri Bin Salim Bin Harith wa Pangani ndiyo hawezi kabisa.
 
Lakini muheshimiwa mwanakijiji mwandishi alisha sema anarudisha wazee wake walio ondelowa kwenye historia ya taifa letu, sasa aandike wengine ambao walisha ingizwa katika historia ama sio wazee wake ili iweje?

Kuwarudisha maanayake ni kuuwaunganisha na waliopo si kuwatenga tena!

Alichokifanya Mohamed Said hakina tofauti na anachokilalamikia!
 
Mkuu Said umenichekesha sana, umenikumbusha mengi kuhusu Binadamu huyu ambaye alikuwa aogopi kusema ukweli aogopi DORA i.e Moh Ali! Jamaa huyu alikuwa mtu wa matani sana na alikuwa na mbinu nyingi za kuwahamasisha watu waje kuangalia mapambano yake na kumuongezea kipato, hakuwa na akili za kawaida yule: Kuna msemo wake ulio kuwa unawahacha wasikilizaji hoi - he goes " I'm so MEAN I can make MEDICINE SICK" hata sijuhi maneno alikuwa anayatoa wapi! "I ain't got no quarrel with them Viet Cong".


Back 2 the point, Ndugu SAID sijuhi ni watu wangapi wamekuelewa sentensi yako ya mwisho? Lakini mimi nimekuelewa sana.

B,

Katika biographies zangu ninazozipenda na huzirudia kuzisoma baada ya muda ni hii ya
Muhammad Ali ''The Greatest My Own Story,'' ''Ghandi'' Robert Payne, ''Long Walk to
Freedom'' Nelson Mandela na ''Malcom X,'' Alex Hailey.

Ali alikuwa na kipaji cha kutunga mashairi ya papo kwa papo akakujibu swali kwa mashairi.
Hii akiwamaliza sana waandishi wa magazeti.

Nilifika Madison Square Garden, New York hapa ndipo 1971 Ali alipopigana na Joe Frazier katika
kile kilichoitwa ''Fight of the Century.''

Kuna picha kubwa sana ya Ali na Frazier ''in action'' pigano hili Ali alipigwa.

Huchoki kuitazama ile picha.
Ali good looking and at his best.

Kuna movie zake mbili moja kacheza mwenyewe ''The Greatest'' 1977 na nyingene kacheza
jina limenitoka la actor wake.

Unaweza kuzipata bure katika torrentz.
 
Kwa Abushuri Bin Salim Bin Harith wa Pangani ndiyo hawezi kabisa.

Mmeathiriwa na Mohamed Said,

Nilishasema juu ya mambo ya kichifu Mohamed Said hataniweza, anahitaji msaada wa haraka, na nikaongeza kuwa hata kama muumba amuongezee miaka 60 mingine mbele katika uhai wake, basi kwamambo yahusuyo uchifu na himaya zake afrika atabaki kuwa msikilizaji wangu tu!

Nasema tena upya kuwa historia ya Mkwavinyika Mwamuyinga haijui,

Hajui kwanini alijua kusoma na kuandika Kiarabu, eti anasema alizaliwa akiwa Muislamu????

Hivi pale Rungemba alipolala Mnyigumba baba yake mzazi wa Mkwavinyika Mnyigumba paliwahi kuwa na chembe la uislamu?

Mohamed Said nakujuza tu kuwa jina la Abdala kwa chifu Mkwawa alilipata akiwa tayari ni chifu na alilipata baada ya mahusiano mazuri na waarabu waliokuwa wakimuuzia nguo na vitu vingine, ndipo akajua kusoma na kuandika na akaiga kuswali kiarabu!

Walipokuja Wajerumani nao pia walimfundisha tamaduni zao za kusali na kusoma na kuandika,

Nenda pale Kalenga kuna maandishi mengi sana ya kijerumani,

Kumbuka Mkwawa Mnyigumba kwa dini alikuwa muamini wa DINI za ASILI/Jadi

Na maandishi ya Mkwawa yote ni mawasiliono ya barua kati yake na wajerumani

Na zaidi kuna mahali maalumu alipokuwa akisali kwa KIKRISTU (kijerumani)

Nakusihi na kukuonya Mohamed Said usijifungie kiudini tu, utasinyaa kwa kila jambo!
 
Back
Top Bottom