Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Yericko Nyerere; Nakwambia ya kwamba huyu Mohamed Said huyu ninaweza kusema ya kwamba ni janga kwa nyakati hii tuliyonayo. Nakuomba achana naye kabisaaaa!

Janga hulijuwi wewe, tulikuwa nalo kwa miaka 25 ya mwanzo ya Uhuru, mpaka tulipanga foleni kupata mlo wa siku, utafikiri tuko kwenye "concentration camp" au jela (fikiria waliokuwa jela bila hatia walikuwaje) tulikuwa tunavaa mabaki ya matairi ya magari (makatambuga). Jiulize nani alikuwa janga hilo?
 
Nyerere realized very early on that equal access to education among Christians and Muslims would bring national unity and cohesion. Inversely, he recognized the potential dangers of religious discord resulting from imbalances in that area. Equal opportunities in matters of employment and participation in national affairs for Muslim and Christian Tanzanians were the direct result of equal education opportunities.

Soon after independence Nyerere initiated a legislation which was passed in 1962, compelling missionary schools to admit students of all denominations and faiths. In 1969 all non-state schools (the majority of which belonged to Christian missions) were taken over and made state schools. Seminaries were the only ones spared-
 
Nyerere realized very early on that equal access to education among Christians and Muslims would bring national unity and cohesion. Inversely, he recognized the potential dangers of religious discord resulting from imbalances in that area. Equal opportunities in matters of employment and participation in national affairs for Muslim and Christian Tanzanians were the direct result of equal education opportunities.

Soon after independence Nyerere initiated a legislation which was passed in 1962, compelling missionary schools to admit students of all denominations and faiths. In 1969 all non-state schools (the majority of which belonged to Christian missions) were taken over and made state schools. Seminaries were the only ones spared-

Jipatie elimu ya bure:


1. Kuendeleza mfumo wa kibaguzi katika elimu kama ulivyoachwa na wakoloni. Wakoloni wa kijerumani ndio walioanzisha mfumo wa kuwabagua Waislamu katika elimu baada ya kushinikizwa na makanisa. Ushahidi wa mashinikizo hayo unaweza kupatikana katika rejea zifuatazo: Cameroon and Dodd 1970:56, Kurtz1972:19, Smith 1963:16. Hatimaye kutokana na mashinikizo hayo serikali ilikubali kufaya yafuatayo:-


i. Kuwafukuza kazi Waislamu waliokuwa serikalini na kuwaingiza Wakristo (Tazama Cameroon and Dodd1970: 25, 56, pia Roland 1970:205)


ii. Kuzipa shule za wamisheni msaada wa kifedha kutoka kodi za wananchi huku wakizibagua zile za Waislamu (Tazama Roland: 1970: 205,na Cameroon and Dodd 1970:50)


iii. Kuweka mpango mkakati wa kuwabagua na kuwahujumu Waislamu na Uislamu wao. Tazama Roland 1970:205, Kurtz 1972:29. Cameroon and Dodd 1970:114


iv. Kujenga hoja kwamba Waislamu kwa asili yao si watu wa kuendelea na kuwa ni wavivu. Tazama E.B Castle 1966:37 ambaye anasema, " Islam hinders progressive attitude to change in society and a community that accepts Islam is less likely to advance in social welfare and education", Yaani Uislamu ni kikwazo cha fikra za maendeleo na mabadiliko katika jamii, na kwamba jamii ikiukubali Uislamu haiwezi kamwe kupiga hatua za katika ustawi wa na elimu. Pia Abel Ishumi 1980:208 anasema, "From the beginning Muslims were opposed to western type formal education", Kwamba Waislamu walipinga elimu. Pia Abel Ishumi 1981:43, "Muslims believe highly in fatalism" Kwamba Waislamu wanabweteka na kuamini kwao kuwa mambo yameshakadiriwa.


2. Kuhujumu taasisi za Waislamu na kuweka viongozi mamluki. Baada ya uhuru Serikali ya Tanzania imekuwa na muelekeo wa kuziandama taasisi zinazoonekana kuwa na mipango madhubuti ya kuwakomboa Waislamu kuondokana na ujinga na umaskini. Rejea Bergan 1981:26 na Sivalon 1992:3 kuhusu kuvunjwa kwa EAMWS na kuanzishwa kwa BAKWATA. Pia soma Anuur na. 13 la Agosti 1992 juu ya taarifa ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ya kuitaka Serikali kuifuta EAMWS. Pia tazama Njozi 2000:31. "Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania kuhusu kadhia ya kuvamiwa kwa Msikiti wa Mwembechai na hatimaye kuuliwa kwa Waislamu.

3. Kuhodhi mfumo wote wa elimu nchini. Tangu kuondoka kwa Mkoloni Wakristo wamekuwa kama mabaki ya wakoloni na ukoloni. Ukiondoa shule za msingi na sekondari za Kata, huko katika shule za sekondari za Serikali, vyuo vya kati na vyuo vikuu wanafunzi na wafanyakazi ni Wakristo kwa zaidi ya asilimia 80. Siku hizi katika shule za Kata wanafunzi Waislamu wameanza kuonekana. Katika taasisi za elimu mfano T.I.E, TEA, NECTA, Bodi ya Mikopo, I.A.E na vyuo vyote nchini, uongozi umekuwa ni mali ya Wakristo. Huko mwanzo walidai kwamba hamna Muislamu mwenye elimu ya kutosha kuongoza. Kwa siku za hivi karibuni madai yao kwa wale Waislamu wachache waliofanikiwa kupata elimu ni kuwa hawafai kwa vile wana, "udini". Aidha katika Wizara ya Elimu (MOEVT) tangu Wizara hiyo kuundwa uongozi umekuwa mali ya Wakristo kwa zaidi ya asilimia 90. Nafasi kama ya Kamishina wa Elimu haijawahi hata kuwa na Kaimu Muislamu na wala haitarajiwi chini ya Mfumochristo. Nafasi za wakurugenzi nazo zimemilikiwa na Wakristo. Mfumokristo umejikita barabara. Uongozi wa Shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu nao umemilikiwa vilivyo. Nafasi za Maafisa elimu Wilaya na Mikoa na wakaguzi wakuu wa elimu wa Kanda kwa zaidi ya asilimia 85 zinaendelea kuwa miliki ya hawa Wakristo.

4. Kukataa kutunga sera za kuondoa upendeleo wa Wakristo katika elimu na kuendeleza ulaghai dhidi ya wananchi wasiokuwa Wakristo. Mara baada ya uhuru ilielezwa na viongozi wetu akiwemo Mwl. Nyerere kuwa serikali itachukua hatua kuondoa mpango ulioasisiwa na Wakoloni wa kuwabagua Waislamu. (tazama A. Jumbe 1994:123, Court 1976 na Nyerere in Hansard Desemba 10, 1962). Badala yake hatua zilizochukuliwa hazikulenga kuondoa tatizo la ubaguzi wa kidini katika elimu nchini na kuwaondoa pia katika ajira na madaraka.Mfano wa hatua hizo ni pamoja na:

i. Kufuta ada shule za msingi na sekondari miaka ya 1960/70.

ii. Kuweka kikomo cha elimu ya msingi kuwa miaka 7 bila kusita.

iii. Kuondoa mitihani ya darasa la 4 na 5. iv. Kuanzishwa kwa mpango wa UPE.

v. Kujenga shule za msingi za bweni kwa watoto wa wafugaji na wavuvi wanaoishi kwa kuhamahama

vi. Kutaifisha shule za binafsi zilizokuwa chini ya mashirika ya dini na watu binafsi. Mpango huu haukuhusisha seminari za Wakristo.

vii. Kupeleka wanafunzi sekondari kwa kigezo cha KUCHAGULIWA badala ya KUFAULU kulikoendana na kuyafanya matokeo ya mtihani wa darasa la saba kuwa ni siri.

viii. Kuanzishwa utaratibu wa "quota system" ambapo kila mkoa ulipangiwa idadi ya wanafunzi watakaochaguliwa kwenda sekondari.

ix. Kuweka utaratibu mgumu wa kuanzisha na kuendesha shule binafsi chini ya sheria ya elimu ya mwaka 1978, hivyo watu wote kulazimika kusoma katika shule chache za sekondari za Serikali

x. Kuanzishwa kwa shule maalum za vipaji katika miaka ya tisini mfano: Kibaha, Kilakala, Ilboru, n.k.

xi. Kutoa upendeleo maalum (Affirmative Action) kwa watoto wa kike kuingia sekondari na vyuo. Aidha kuwepo pia kwa mipango ya kuwasomesha watoto wa kike kutoka familia maskini.

xii. Ujenzi wa Shule za Sekondari za Kata. Sera hizi zote pamoja na nyinginezo hazikusaidia kuondoa uwiano mbaya au ubaguzi wa elimu kwa Waislamu. Tuangalie mfano michache ifuatayo: Ni ukweli usiopingika kwamba UPE awamu ya kwanza iliyosukumwa na UNESCO na awamu ya pili iliyosukumwa na Malengo ya Milenia (MDGs) na Mpango wa Elimu kwa wote (EFA) zimesaidia kuwahakikishia watoto wengi wa Kiislamu elimu hiyo ya msingi. Lakini sera hii ilikuja katika kipindi ambacho elimu ya msingi haikuwezi tena kumpatia mtu ajira katika sekta rasmi na hata ile ya binafsi.

Ikumbukwe kwamba katika kipindi hicho cha miaka ya 60 hadi 2000 nafasi za masomo ya sekondari ziliendelea kuwa haba. Wakati wote huu watoto wa Kikristo ndiyo walioendelea kufaidika na elimu ya sekondari. Masomo hayo ya sekondari hatimaye yaliwapatia fursa za kuingia vyuo vikuu na hivyo kuwa katika nafasi za kuajiriwa serikalini, kuteuliwa katika vyeo na nyadhifa mbalimbali huku Waislamu waliowaacha shule za msingi wakiambulia ajira za usafi na utarishi.

Naam, Mfumokristo umefanikiwa kuwafanya Wakristo kuwa warithi wa wazungu wakoloni na kuwaacha Waislamu katika hadhi lie ile waliokuwa nayo wakati wa ukoloni. Aidha kutaifishwa kwa shule hakujasaidia Waislamu kupata elimu ya sekondari kama inavyodaiwa kuwa Nyerere alitaifisha shule ili Waislamu wasome.

Kama tulivyoona awali kuwa tangu wakati wa Mjerumani serikali ya kikoloni ilikuwa ikitoa pesa kusaidia ujenzi na uendeshaji wa shule za Wakristo ni dhahiri kuwa shule hizi zilikuwa zimeshalemazwa na pesa za serikali kwa kipindi cha miaka 55, tangu mwaka 1914 hadi mwaka 1969 zilipotaifishwa. Tazama maandiko ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maskofu Katoliki (TEC) Fr Robinson, D.W 1965:14 kwamba, "The Church is now totally dependent on State aid for the administration of these schools. If this aid were withdrawn the church will be forced to close its schools"

Yaani, Kwa sasa Kanisa limekuwa tegemezi kabisa kwa serikali katika kutoa pesa za kuendesha shule zake na ikiwa serikali itasita kutoa fedha kwa shule hizi basi Kanisa litalazimika kuzifunga. Ni dhahiri basi kwamba hatua aliyochukua Julius Nyerere ilikuwa na malengo makuu ya kuziokoa shule za Kanisa kufungwa kwa sababu ingekuwa jambo la kiroja kwa serikali ya Tanzania kuendelea kutoa pesa za kuendesha shule za Kanisa kwa wakati ule, na pili kuhakikisha kwamba malengo ya shule zile ya kuwasomesha Wakristo yanaendelea kutekelezwa kwa kutumia pesa za umma.

Kimsingi kilichobadilika ni jina la mmiliki tu uongozi na malengo ya shule yalibaki vile vile. Ndiyo maana hakuna mtu yoyote aliyethubutu au atakayethubutu kudai eti kwamba ukienda katika shule zilizotaifishwa mfano, Pugu, Minaki, Tambaza, Zanaki, Jangwani, Kibasila, Ilboru, Weruweru, Tosamaganga, Msalato, Umbwe, Ndanda n.k, utakuta idadi ya kuridhisha ya wanafunzi Waislamu wanaosoma huko. Lakini hata katika shule za sekondari chache mpya ambazo serikali ilijenga au kujengewa mwishoni mwa miaka ya 70, kama vile: Kibiti, Ruvu, Karatu, Bagamoyo n.k , kote walimu, wafanyakazi na wanafunzi ni Wakristo kwa zaidi ya asilimia 80.

Watoto wachache wa Kiislamu wanaosoma huko huonekana kama wakimbizi wanaosaidiwa katika nchi ya ughaibuni. Kuhusu kuingia sekondari kwa kigezo cha kuchaguliwa na mpango wa quota system, watendaji Wakristo waliojazana katika mfumo wa elimu nchini wamekuwa wakihakikisha kwamba Waislamu hawasomi kutokana mbinu zifuatazo:-

i. Kufanya matokeo ya darasa la saba kuwa ni siri hivyo kuweza kuibadili nafasi walizoshinda Waislamu na kuwapa wengine. Tazama ushahidi mzito uliotolewa na Njozi mwaka 2000; katika kitabu cha Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania uk. wa 62 -70. Hapa vijana wa Kiislamu waliofaulu darasa la saba walinyimwa nafasi kuingia sekondari na wale waliofaulu kidato cha nne walinyimwa kuingia kidato cha tano. Kazi hii ya kuwakwamisha vijana wa Kiislamu ilifanywa vyema na mawakala wa Mfumokristo waliojazana katika mfumo wote wa elimu nchini.

ii. Kuhamisha wanafunzi Wakristo kutoka maeneo yenye ushindani mkubwa kwenda Mikoa iliyokuwa na alama ndogo za kuchaguliwa kama Pwani, Dar, Lindi, Mtwara na Tanga ambayo pia ni maeneo ya Waislamu . Tazama Malekela 1983 in "Access to secondary education in Sub- Sahara Africa"

iii. Huko nyuma kabla ya wanafunzi kupangiwa shule za sekondari namba zao za mtihani ziliambatanishwa na majina ili kujua nani Mkristo apendelewe na nani siyo awachwe iv. Kuhakikisha kwamba viongozi na watendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) wote ni Wakristo. Aidha kwa asilimia kubwa kabisa watungaji wa mitihani na wasahihishaji pia ni dini hiyo hiyo. Tazama kitabu cha Miaka Thelathini ya NECTA, 2004 au www.necta.ca.tz

 
Hivi kweli kuna Great Thinker hapa JF ambae hajaona uchochezi wa Mohamed Said NILIOUTHIBITSHA katika UZI huu na anahita kuonyeshwa zaidi kwa kidole?
 
nyerere was ahead of his time,ndio maana it was easy to shrug off wazee wa dar-because of him,wewe zomba badala ya kucheza bao una thump keyboard
As president of Tanzania from 1961 to 1985--and even afterwards--Nyerere continued to challenge the church until his demise in 1999. He often had the opportunity of speaking to church leaders and the laity and told them that the church had to serve the whole person, mentally, spiritually, and physically. Furthermore, he said that church had to serve people beyond the church. For instance, schools, hospitals, and income generating projects would not only benefit churches and Christians but also non-believers. This was a means of witnessing the Word of God to unbelievers
 
Last edited by a moderator:
kikwete huyo BOSTON University
"The political unity and religious tolerance that we pride ourselves in did not come by accident. It is a product of deliberate action and the vision of leaders of Tanzania from the founding president, the late Mwalimu Julius Nyerere, to the present. (&#8230😉 Thanks to the remarkable foresight of our founding president Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, specific actions were taken to engender tolerance in matters of faith and manage potential cracks to our country. These categories can be classified into four categories: equitable policies, institutional innovations, political messages, and legal constitutional provisions"
 
Tumeaga wote na tumerudi wote.

Mag3, unaposema usitujazie server kwani JF ni mali yako halafu usipende kuwasema wanabodi wa JF kwa niaba yao wewe jisimamie peke yake yako hakuna member yeyote alikutuma unatumia maneno eti sisi JF. JF tunaita ngano.

JF kuna members zaidi ya laki moja huna mamlaka ya kuwasemea jenga hoja zako na kundi lako la kina Yericko.

Halafu hapa hatupo kwenye chumba cha mtihani kama unaijua historia andika watu wakusome siyo kujifungia na chumbani kuleta maswali ya chekechea.

Wafuatiliaji ndiyo wanapima mambo siyo wewe, hebu andika tukusome na wewe siyo kujificha nyuma ya laptop huku unatoa kejeli na matusi, au JF kwako ndiyo umefika.

JF kuna fikra nyingi kuna wasomi makini, kuna wasomi wapuuzi, kuna watu wanaheshimika kwa michango yao, kuna kundi la wajinga pia, kuna kundi la kutukana pia. Wewe mimi na members wengine ni sehemu tu ya JF.

Tarudi tena kujibizana na wewe ambaye unajifanya rais wa JF.

mkuu umenisemea mimi, yaani nliyotaka kusema yoote umemwambia, kwanza yeriko alishindwa kujiweka wazi kama alivyofanya ms lakn pia yeye na kundi lake wamekuwa hawa hawana hoja za kuweza kimridhisha mtu mwenye akili zake amini kiwa ms ni mchochez, mdini nk. Mbaya zaidi lugha zake ni za mtu aliyekata tamaa baada ya kuona uzito wa kukubalika hoja yake, halafu tumemwomba atuahidi kama atatoa kitabu kama alivyofanya ms. Ili tuamini hoja yake lakin hatujapata chochote zaidi ya ubishi na kejeli.
 
Last edited by a moderator:
nyerere_with_people2.jpg
 
Hivi kweli kuna Great Thinker hapa JF ambae hajaona uchochezi wa Mohamed Said NILIOUTHIBITSHA katika UZI huu na anahita kuonyeshwa zaidi kwa kidole?

napia hauko mwenye akili timamu anaeweza kukubaliana na wewe kwa hoja zako dhaifu kuwa mohamed said ni mchochezi kwani yeye ameongea kila kitu kwa ushahidi ili kuipa nguvu hoja yako ilitakiwa utoe vielelezo ya kubatilisha ushahidi wake lakini hujafanya hivyo, hebu toa vielelezo vya kupinga ushahidi alioutoa ili tukuunge mkono coz naona unatafuta kuungwa mkono kwa nguvu
 
Back
Top Bottom