Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Hata mimi nimekusoma zaidi ya mara nne kwenye huu munakasha ukinitaja kwa jina kwenye maandiko yako na kunitolea mifano katika kujenga hoja zako dhidi ya Mohamed Said kama vile unajua fikra zangu au wewe una ruksa za kujua hisia za wengine.

Tatizo unapenda ukubwa sana ndugu yangu mimi nipo hapa kujifunza kwa yeyote ambaye ataleta kitu kipya na chenye mashiko.

Mimi ninachoandika kutoka kwako kinatokana na maandiko yako wala si kingine.
 

Wazee wako ni wa wapi, "Uswazi"?
 
Unajuwa huna la kujibu unatafuta pakutokea ukaona ni kwa Zomba, hata ukijibadili kama kinyonga haisaidii kitu.

Mie uzi uleule tu, mpaka ukweli uwaingie, mkiukubali mkiukataa hiyo ni shauri yenu, kinachotakiwa muujuwe tu.

Uko njema sana ZOMBA..

Uko makini sana na husahau kitu kichwani mwako..

nakubali zako HINTS..!
 
Mohamed Said,

Nikiwa napita Magomeni pale mtaa wa Ifunda kuna nyumba moja imepambwa na kuandikwa makumbusho ya Nyerere.

Unaweza kutupa historia yake.

Ritz,

Baada ya Nyerere kupokea barua kutoka kwa waajiri wake
wamishionari kuwa achague moja kati ya mawili.

Achague kazi ya ualimu au siasa Nyerere alipeleka barua ile
kwa Clement Mtamila aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri
Kuu ya TANU.

Kikao kilifanyika nyumbani kwa Mzee Mtamila Mtaa wa Kipata
na Sikukuu.

Uamuzi ukapita kuwa Nyerere ajiuzulu kazi aajiriwe na TANU.

Nyerere alipojiuzulu kazi alikaa kwa muda nyumbani kwa Abdu.
Kisha Mzee Rupia ndipo akamtafutia nyumba Magomeni.

Ndiyo hiyo nyumba uliyoiona sasa Makumbusho.
 
Mzee Mohamed,
Abdu kaanzisha TANU ipi? Ambayo haina KATIBA? Rais wa KWANZA wa TANU na wa mwisho wa TAA ni nani?
 
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU ni kitu gani hicho? Unaona umuhimu wa kutuletea KATIBA ya KWANZA ya TANU? Hivi vyeo na nyadhifa hizi unazitoa wapi Mohamed?
 
Mzee Mohamed,
Abdu kaanzisha TANU ipi? Ambayo haina KATIBA? Rais wa KWANZA wa TANU na wa mwisho wa TAA ni nani?

Ngoja aje na simulizi jingine... wakati swali liko wazi: Abdu alianzisha TANU lini? ..."ooh turudi kwa babu yake alipokuwa Msumbiji, halafu alipoenda Burma wakajadilianaa na mwisho... akaja hapa akamuingiza Nyerere kweney siasa mwaka 1954 halafu siku moja akamwambia Nyerere kwanini usianzishe TANU kwa niaba yangu; ukweli Abdul ndiyo alikuwa the king maker kwani alikuwa ndiyo the power behind the throne"...

Basi utamu kolea!
 
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU ni kitu gani hicho? Unaona umuhimu wa kutuletea KATIBA ya KWANZA ya TANU? Hivi vyeo na nyadhifa hizi unazitoa wapi Mohamed?
WC, Una haraka sana. Kwa nini usiniulize kwanza kabla ya kuniwekea dhana mbaya? Pokea jibu lako. Vyeo hivyo vilikuwapo. Rais wa TANU hakuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya chama.
 
Anaweza akaja kivingine pia. "Kasome kile kitabu changu" au zomba atakusaidia!
 
Last edited by a moderator:

MM,

Mimi siwezi nikabishana na wewe kuhusu mwanzo wa African Association
1929 na kuja kufikia kuundwa kwa TANU 1954. Hapa siwezi kubishana na wewe
kwa kuwa wewe unajenga hoja kwa jambo moja au mawili au kuzidi kidogo.

Mimi huko kuundwa kwa TANU wazee wangu wamekuishi maisha yao kuanzia 1929
hadi 1954 walipounda TANU. Katika maisha yao hayo ya siasa nimeandika kitabu
chenye kurasa takriban 400. Vipi katika hali kama hii nijiingize katika mjadala na
wewe?

Mtu ambae hukuwajua wazee wangu mpaka pale nilopowaeleza katika kitabu changu?

Endelea na kejeli lakini historia hii ya wazee wangu ipo na kama unapenda kuamini kuwa
Nyerere kaja Dar es Salaam na fikra ya kuunda TANU na akafanikiwa kuiunda peke yake
ni sawa kwangu.
 
WC, Una haraka sana. Kwa nini usiniulize kwanza kabla ya kuniwekea dhana mbaya? Pokea jibu lako. Vyeo hivyo vilikuwapo. Rais wa TANU hakuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya chama.
KATIBA ya KWANZA ya TANU iko wapi? Au vyeo hivi navyo ulisimuliwa?
 
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU ni kitu gani hicho? Unaona umuhimu wa kutuletea KATIBA ya KWANZA ya TANU? Hivi vyeo na nyadhifa hizi unazitoa wapi Mohamed?

WC,

Una haraka sana.
Kwa nini usiniulize kwanza kabla ya kuniwekea dhana mbaya?

Pokea jibu lako.

Vyeo hivyo vilikuwapo.
Rais wa TANU hakuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya chama.
 
KATIBA ya KWANZA ya TANU iko wapi? Au vyeo hivi navyo ulisimuliwa?

WC,

Umesema kweli nimesimuliwa.
Ama hilo la katiba hizo ziko wapi...

Labda swali hilo ulipeleke CCM au
Kivukoni College huenda wanazo
hizo katiba kwa maana wameandika historia
TANU.
 
Tatizo,wanavyosema U S DEPARTMENT OF STATE.
"Despite improvements in their political representation, Muslim leaders continued to complain that the number of Muslim students chosen to enroll in government-run schools was not equal to the number of Christians. Christian leaders continued to agree that the Muslim student population in institutions of higher learning was disproportionately low; however, they attributed this condition to historical circumstances (the legacy of colonial and early post-independence government policies that did not recognize the credentials of traditional Muslim schools) and low daily school attendance rates by Muslims, rather than discrimination. Many Christians and Muslims also attributed the educational disparity between Muslim and Christians to the disproportional emphasis that Islamic schools continued to place on religion at the expense of other academic subjects"
 
WC,

Umesema kweli nimesimuliwa.
Historia ya namna hii tuikubali tu yaishe. Wewe endelea kuwa "Authority" juu ya historia hii. Umesimuliwa peke yako hakuna namna ya kuzithibitisha simulizi hizi. Ulikosea sana kutotafuta KATIBA au miongozo ya AA, TAA, TANU na huenda hata katiba ya CCM haujapata kuiona!
 
Waliweza kuishi na vyama hivi bila KATIBA? Tunataka katiba ili tujue kwa uhakika vyama hivi vilianzishwa kwa madhumuni, imani na malengo gani.

Ni muhimu pia pale unapokataa kuwa AA na TAA havikuwa vyama vya starehe katiba zao ziwe ndio ushahidi sio kitabu chako cha mwaka 1998! Ambacho kimejaa simulizi tu za watu ambao karibu wote ni marehemu.
 

WC,

Sijakosea chochote kuhusu kuitafuta katiba kwa kuwa sikuwa na shughulinayo.

Nimekaa Maktaba ya CCM Dodoma na katika orodha ya vitu nilivyokwenda kuvisaka
katiba haikuwapo katika orodha yangu.

Kama wewe unaona ina umuhimu itafute utujuvye.

Mimi sihitaji ithbati ya simulizi za baba yangu kutoka kwa yoyote.
Itakuwa kichekesho kuwa mimi nisimuamini baba yangu nije nimsikilize mpita njia.

Hivi kwa nini historia hii inakushughulisheni kiasi hiki?
Si inatosha nyie mkaipuuza?

Hili vipi linakushindeni?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…