Sio Uislam kama huu wa kwako.
His "wazee" told him so!
Mohamed, habari zako hazina uthibitisho hivyo haziaminiki! waambie wafuasi wako, mimi hapana.G,
Labda unaweza ukaelewa matatizo yaliyopita kuhusu kuandika historia ya
TANU.
Tafadhali soma hapa chini kipande hiki kutoka ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...'':
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] The first serious attempt to record the history of TANU was done by none other than Abdulwahid himself.
When TANU captured state power from the British in 1961 and was in the first phase of consolidating itself as a mass party, it is said that Abdulwahid was asked by Julius Nyerere, then Prime Minister of the country, to record the history of the struggle of the Africans of Tanganyika against the British.
This, in essence, was to be the history of TANU. To assist him in the research was the late Dr Wilbert Kleruu, recently returned from studies in the United States.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] Abdulwahid occupied his former office at the TANU headquarters; the one which he had occupied in the 1950s when he was TAA President.
Abdulwahid's personal files, dairies and his late father's papers dating back to the days of the formation of African Association in 1929 were made available to researchers for the first time as primary sources of information.
Abdulwahid's version, analysis, presentation of facts and interpretation of forces at play which led to the rise of nationalism were, however, not acceptable to the TANU leadership.
We shall see in the following pages reasons why Abdulwahid's version of history could not be allowed to flourish.
Abdulwahid abandoned the assignment after being convinced that the new leadership in TANU was not really interested in documenting an authenticated history of Tanganyika but was interested in merely creating a personality cult for President Nyerere.
Dr Kleruu went ahead with the research and completed the work.
This manuscript remains unpublished, at least in its original form and is nowhere to be found.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Mohamed, haya ni maoni yako wala haina taabu.
Lakini basi usiyafanye kama ukweli kwasababu huna proof ya hayo niliyokazia.
Hapa ndipo huwa nasema Mohamed kwani historia haikamiliki hadi uwekee watu maneno midomoni mwao!
Ukisoma hoja yake ya Warsha utaona tatizo la ku-generalize mambo lipo pale pale.
Anasema utafiti wa warsha ulionyesha connection kati ya church, Nyerere kuwamaliza vijana wa kiislam kielimu.
Hakuna detail za jinsi hilo lilivyofanyika.
Hapo ndipo anapokwepa swali la je, makakati wa Nyerere na kanisa kuuhujumu Uislam ulianza lini na kwa mbinu gani?
Na kwa vile Nyerere ''never mentioned patriots'' je bado unasimama na hoja yako kuwa Nyerere alipowaaaga wazee wa Dar es Salaam alisema hamjui Sykes! Hata kama hakumtaja kama patriots na alimtaja kwa ubaya hiyo haitoshi kuwa mentioned.
Je, umesoma vitabu alivyoandika Mwalimu Nyerere na kujirisha hakuwataja patriots. Hivi kuwataja ilibidi atamke majina yao wote au angeweza kutumia neno moja kuwaenzi wote. Neno wazee halitoshi. Je, angemtaja Sykes vipi watoto wa Ngozi na Kirlo nao wangesemaje kuhusu Nyerere.
Je, Maryknoll hawapaswi kuangikia katika kundi la Patriots
Hebu fafanua Patriots wanakuwaje tofauti na watu wengine.
Mohamed, utafiti wa Warsha haukutueleza mtazamo wa shule za awali, msingi na sekondari kwamba, kote huko mambo yalikuwa mazuri isipokuwa kuingia elimu ya juu.
Napo pia napata hoja ya kuuliza, Mohamed hivi unaweza kupata mwanafunzi wa chuo kikuu asiyefanya mtihani wa sekondari?
Siyo kusahihishiwa bali asiyefanya mtihani?
Mohamed, kuna utafiti mwingine uliowahi kufanywa kuhusu ellimu ya msingi na sekondari na nini matokeo ya utafiti.
Na tuwakumbushe wasomaji kuwa Mohamed anafanya self reference! halafu anasema ndio ukweli! real
mohamed, habari zako hazina uthibitisho hivyo haziaminiki! Waambie wafuasi wako, mimi hapana.
Ndugu yangu Zomba,Maandiko yako ni haya hapa "Hakukuwa na mkutano Camp David enzi za Menachem Begin" tazama tofauti na ulivyoandika sasa, nime bold.
Kwanza uliandika "Hakukuwa na mkutano Camp David enzi za Menachem Begin" halafu sasa unaandika "Mkutano uliokuwepo Camp David enzi za Menachem Begin ni baina ya Begin na Sadat"
Maandiko yako mwenyewe unayaruka? si useme ulikosea tu? usione vibaya, hakuna asiyekosea isipokuwa muumba wetu tu.
Humu tunapata ilm tu kwa njia ya kubadilishana maandiko na picha.
Mohamed, habari zako hazina uthibitisho hivyo haziaminiki! waambie wafuasi wako, mimi hapana.
Mkuu nguruvi3 alisema hiviG,
Labda unaweza ukaelewa matatizo yaliyopita kuhusu kuandika historia ya TANU.
Tafadhali soma hapa chini kipande hiki kutoka ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...'':
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] The first serious attempt to record the history of TANU was done by none other than Abdulwahid himself.
When TANU captured state power from the British in 1961 and was in the first phase of consolidating itself as a mass party, it is said that Abdulwahid was asked by Julius Nyerere, then Prime Minister of the country, to record the history of the struggle of the Africans of Tanganyika against the British.
This, in essence, was to be the history of TANU. To assist him in the research was the late Dr Wilbert Kleruu, recently returned from studies in the United States.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] Abdulwahid occupied his former office at the TANU headquarters; the one which he had occupied in the 1950s when he was TAA President.
Abdulwahid's personal files, dairies and his late father's papers dating back to the days of the formation of African Association in 1929 were made available to researchers for the first time as primary sources of information.
Abdulwahid's version, analysis, presentation of facts and interpretation of forces at play which led to the rise of nationalism were, however, not acceptable to the TANU leadership.
We shall see in the following pages reasons why Abdulwahid's version of history could not be allowed to flourish.
Abdulwahid abandoned the assignment after being convinced that the new leadership in TANU was not really interested in documenting an authenticated history of Tanganyika but was interested in merely creating a personality cult for President Nyerere.
Dr Kleruu went ahead with the research and completed the work.
This manuscript remains unpublished, at least in its original form and is nowhere to be found. [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Sasa mimi mambo kama haya ningeliyajua vipi kama nisingeelezwa na wazee wangu?
Haya yalitokea katika miaka ya mwanzo ya uhuru 1961/62.
Mwaka wa 1981 wakati CCM inaandika historia yake yakaja haya mengine tena hebu yasome:
This position was to assert itself years later when the Party was researching its history.
A research assistant by the name of Hassan Upeka, who happened to be one ofearliest recruits of TANU,
having joined the party directly from school in 1956,presented to the research panel, notes of an interview
he had with Abdulwahid many years back.
The research assistant was bluntly told that the intended book had nothing to do with Abdulwahid.
Ukipenda ninayo mengine mengi tu kuhusu mikasa kama hii ya kuandika historia kinyume na inavyotegemewa.
Unasemaje.
Nikuongeze taarifa au hizo zimetosha?
Na tuwakumbushe wasomaji kuwa Mohamed anafanya self reference! halafu anasema ndio ukweli! real
Mzee Mwanakijiji,
Na haya maswali yangu kuhusu historia ya Tanganyika naomba unisaidie.
1) Ofisi za Gavana Sir Donald Cameron zilikuwa wapi
2) Rais wa kwanza wa TAA alikuwa nani
3) Wakati wa TANU miaka ya 1950 kulikuwa na magazeti gani ya wananchi
4) Katibu Mwenezi wa TANU alikuwa nani mwaka 1958
5) TANU ilingia lini Mombasa.
6) Wanachama 20 wa mwanzo wa TANU na namba zao za kadi ukitoa namba moja ya kadi ya Nyerere hawa wengine 19
Tuanze na haya maswali machache kwanza ambayo siyafahamu.
MM,
Kwa kweli hili ni jambo nimelieleza kwa mnasaba wa majadiliano
yalivyokuwa yanaendelea.
Unaumizwa sana na habari ambazo wewe huzijui.
Hapana haja ya sie kunasa hapa.
Yapo mengine mengi ya kuzungumza.
Tuendelee Insha Allah.
Mkuu nguruvi3 alisema hivi
Na katika hali ya kushangaza kabisa, umediriki hata kutumia kitabu hichohicho kama uthibitisho wa ulichoandika katika kitabu hichohicho
Hivyo basi mzee saidi naweza kusema kuwa ulichoandika sio historia ila ni hisia zako binafsi juu ya ulivyotamani iwe,
Jambo baya zaidi ni kwamba umejaribu kutumia dini kutafuta uungwaji mkono wa hizo hisia zako binafsi,
Kwa sababu ulichoandika kinapotosha uma na kujenga uhasama wa kidini, ​HUO NI UCHOCHEZI.
Mjuvi wa histotia unashidwa kujibu maswali yangu lakini wewe unauliza maswali unajibiwa na Mohamed Said.Haya ni maswali ambayo unatakiwa kumuuliza Mohammed Said kwani yeye ni mtaalamu wa historia ya TAA na TANU. Binafsi naweza kuyajibu lakini pia haitokusaidia wewe mwenyewe. Nakushauri ufanye jambo moja kwani majibu ya maswali hayo karibu yote yako public - unaweza kufanya utafiti kidogo na kupata majibu.
Siku moja Nyerere akiwa ndani ya msafara wake wa mapikipiki akienda Gerezani kufungua mradi wa viwanda vidogo vidogo, msafawa wake uliingia Mtaa wa Sikukuu ukawa unaelekea mitaa ya Kiungani.
Nyerere akiwa ndani ya benzi lake alikuwa akitupa macho huku na huku akiangalia mitaa yake aliyokuwa akiikanyanga kwa miguu enzi za kudai uhuru.
Bila shaka msafara ulipopita Kipata na Sikukuu Nyerere aliiangalia nyumba ya Mzee Mtamila, msafara ulipoingia Sikukuu na na Kirk kuna shaka alinyoosha shingo yake kuangalia nyumba aliyoijua sana, nyumbani kwa Abdulwahid Sykes na mama yake Bi Mluguru.
Hapa jicho la Nyerere likagongana na sura ya Bi Mluguru aliyekuwa amejipanga mstari pamoja na wananchi wengine kuangalia msafara wa Nyerere.
Alipotambua kuwa yule mama aliyesimama alikuwa Bi Mluguru, Nyerere aliamua gari yake isimame na kwa ghafla dereva wake alisimamisha gari.
Nyerere alitoka nje ya gari akamwendea Bi Mluguru kumwamkia.
Mapikipiki yalisimama madereva wamepigwa na butwaa.
Wanaangalia nyuma wanamuona Nyerere anazungumza na mama mmoja mtu mzima.
Haraka walinzi wakawa wamemzunguka Nyerere na Bi Mluguru.
Kwa hakika kitendo kile kilikuwa cha kushangaza.
Nyerere alipoondoka na msafara wake nyuma aliacha gumzo kubwa.
Ilikuwa miaka michache baada ya kifo cha Abdulwahid.
Walioijua historia ya Nyerere na marehemu Abdulwahid Sykes kitendo kile cha kiungwana cha Nyerere hakikuwashangaza.
Tabu walipata wale waliokuwa hawaijui vyema historia ya Nyerere alipofika Dar es Salaam...
Ilikuwa miaka michache baada ya kifo cha Abdulwahid.
Kaka Mohamed Saidi nashukuru sana kwa majibu yako mazuri na ya kusisimua kuhusu Al Marhum Sheikh Kassim Bin Jumaa Imamu wa Msikiti Wa Mtoro!
Kama ulivyoahidi naomba utujuze na hayo mengine nanukuu tena:
Jee, Almarhum Shekh Mohamed Ali Burhi aliyekuwa katibu Mkuu wa Bakwata nini kilisababisha ajiuzulu Ukatibu Mkuu? na Jee, Al marhum Tewa Saidi Tewa alifariki lini? maana mara ya mwisho kumuona Mpigania uhuru huyu ilikuwa mwaka 1991 ktk ukumbi wa Nkrumah Chuo kikuu dar ktk harakati za kuleta mabadiliko Bakwata!
Jee, Mohamed, ktk vitabu vyako umewakumbuka wapigania uhuru wetu wa huku Moshi kama akina Mzee Yusuf Olotu, Osman Farah, Mariam baiskeli, Mama Halima Selengia (bado yu hai), Liwali Musa Mwinyijanga na wengine? hawa Wazee ni watu muhimu sana hasa kwa huku Moshi walishiriki kikamilifu ktk kuchangishana fedha Misikitini na fedha hizo kupewa Tanu ili ijiimarishe! lakini wote wamesahaulika na hakuna mtu anaewakumbuka hata kwa dua!
Natanguliza Shukrani kwa muda unaotumia kutushibisha na historia sahihi Alla akujaze kila la kheri!
Mohamed Said,
Unaweza kutuelezea nini kipi haswa kilichokusukuma mpaka ukaamua kuanza utafiti mwishowe ukaandika hicho kitabu chako.
R,
Dharau kwa Waswahili...vibaraza, gahawa nk. nk.
Somo linasomeshwa la historia ''Government and Politics in East
Africa.''
Anaelezwa Nyerere mwanzo hadi mwisho vipi alikuta TAA chama
cha starehe akakigeuza cha siasa...
Nikasema njia ya kukomesha yote haya ni mimi kuandika historia ya
wazee wangu.
Kianzio nilikuwanacho cha babu yangu kisha Abdu Sykes na TANU.
Ndipo nilipoanza utafiti wangu pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Publisher wa kwanza nilipomuonyesha ule mswada wangu akanambia
wewe haya yote umepata wapi?
Akanambia unajua kama hii kazi ni nzito sana kijana?
Lakini aliogopa kuchapa kitabu changu.
Oxford nikawapa wakanambia kazi nzuri sana lakini sisi tunafanya biashara
na serikali ya Tanzania.
Kitabu chako kitatuponza.
Miaka inapita kila publisher haitaki kazi wanaogopa...