Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Tatizo ni kuweka kitu kinachowatisha watu ''tunapigania dini''. Mohamed ameweka tuhuma dhdi ya kanisa makusudi kabisa ili ima mtu awe mwislam au awe kafir. Ili kuwa mwislam unapaswa kumeza kila unachoambiwa. Ukitaka kutoka katika Uislam kama BAKWATA hoji jambo kinyume na lengo tarajiwa.Kusema ukweli binafsi nasikitika kuona vijana wa Kiislamu ambao wana nia njema kwelii na wanataka kujua sana wanaamini habari za Mohammed Said bila kuzihoji. Wanaamini si kwa sabbau wanajua ni kweli bali kwa sababu mzee anaonekana anautetea Uislamu na hivyo kumuuliza au kumkatalia kunawafanya wajihisi kama hawautendei haki Uislamu. Hii si sahihi kwa sababu ni mbinu ya 'sympathy' ambayo kwa kweli kwenye ukweli haina nafasi.
Maandishi ya mzee Said yanahitaji kuangaliwa kwa mwanga wa kisomi tu; hoja zake hata zingetolewa na mpagani bado zingeangaliwa kisomi. Ni jukumu la mtu yeyote mwenye akili kuuliza maswali mbele ya mtu anayetoa madai. Lengo si kumdhalilisha mtoa hoja bali kumsaidia mtoa hoja kuelezea vizuri hoja zake, kuzisahihisha na hata kuzitetea vizuri. Binafsi naamini Waislamu na hasa wale mashabiki wa Bw. Said waanze kumuuliza maswali ya akili ili kuupata ukweli vizuri.
Kwa jinsi mjadala ulivyo na yanavyozuka tuyajuayo na tusiyoyajua, jinsi watu wanavyo flip flop position na kutengeneza conducieve environment, kuna vijana wengi wa kiislam watasoma makala za Mohamed kwa jicho tofauti kabisa na awali.
Wengine watakuwa chumbani ima wakiugulia maumivu ya kupigwa changa au wakilaani upotoshwaji n.k.
Hii ni changamoto kwa wanahabari hasa wale wachanga. Pitieni uzi huu na nyingine chagueni yale mnaona yana walakini, fanyieni tafiti kidogo kujiridhisha na majibu yaliyo wazi kabisa, waiteni wahusika wayatetee.
Kwa mwandishi makini Mohamed can hardly speak for 20 minute!
Kwanza hana uwezo wa kutetea hoja zake na hoja zake hazisimami zenyewe bila 'self quotation''.
Kitu kizuri sana, hoja zake zina ji contradict na akipelekwa kwenye kona hatoki! flat!