Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ritz,

Hebu soma hapo chini jibu lako lipo hapo labda kama utataka ziada:

When the Tanganyika African Association (TAA), TANU's predecessor, held a secret meeting to collect donations to send Germano Pacha to Dar es Salaam to attend the TANU founding conference in 1954, the highest contribution, which was twenty shillings, came from my grandfather, Salum Abdallah.

Germano Pacha was then TAA's Provincial Secretary Western Province.

That meeting was attended by the notables of Tabora including school teachers, Abubakar Mwilima, Harub Said and George Magembe.

These men came to play very important roles during the struggle.

However, my grandfather fell out with President Julius Nyerere, as many were to do, and was detained by the government soon after independence under the 1962 Preventive Detention Act.


Shekh M. Said,

Hapo kwenye Red! umenikumbusha Sheikh maarufu sana huyu miaka ya 80! jee, bado yuko hai? si alikuwa Serikalini miaka ya nyuma?
 
Makoye,

Serikali ina hofu ya kumjua nani anambagua nani.
Waislam tumelieleza tatizo hili miaka mingi...

Bado tunapuuzwa.

mohamed, tuacheni ushabiki! mkuu, hawa watu wote wanabaguana kwa sasa, tujiulize, mbona hii haikutokea kabla ya miaka ya kuanzia 1980?
 
Shekh M. Said,

Hapo kwenye Red! umenikumbusha Sheikh maarufu sana huyu miaka ya 80! jee, bado yuko hai? si alikuwa Serikalini miaka ya nyuma?

Bi. Z,

Sheikh Mwilima amefariki miaka mingi sasa inazidi 15 na zaidi.

Sheikh Mwilima alipambana na Nyerere katika Halmashauri Kuu
ya CCM.

Alitaka kujua vipi Waislam wako nyuma katika nyanja zote na
akamwomba mwenyekiti alitazame tatizo hili kama alivyolitazama
tatizo la Wabarbaig, Wahadzabe na wanawake.

Amenihadithia mwenyewe.

Anasema ukumbi mzima ulikuwa kimyaaaaaa...
Wajumbe wanasikiliza mwenyekiti Nyerere atajibu nini.

Kwa kama dakika moja mbili...

Sheikh Abubakar Mwilima na Nyerere walitazamana kama majogoo
wanaotaka kupigana.

Nyerere akaahirisha kikao....
 
Bi. Z,

Sheikh Mwilima amefariki miaka mingi sasa inazidi 15 na zaidi.

Sheikh Mwilima alipambana na Nyerere katika Halmashauri Kuu
ya CCM.

Alitaka kujua vipi Waislam wako nyuma katika nyanja zote na
akamwomba mwenyekiti alitazame tatizo hili kama alivyolitazama
tatizo la Wabarbaig, Wahadzabe na wanawake.

Amenihadithia mwenyewe.

Anasema ukumbi mzima ulikuwa kimyaaaaaa...
Wajumbe wanasikiliza mwenyekiti Nyerere atajibu nini.

Kwa kama dakika moja mbili...

Sheikh Abubakar Mwilima na Nyerere walitazamana kama majogoo
wanaotaka kupigana.

Nyerere akaahirisha kikao....
Mara ya mwisho nilimuona hakiwa na Huthoman Matata kwenye munakasha wa Quran and Sciance miaka mingi imepita.
 
mohamed, tuacheni ushabiki! mkuu, hawa watu wote wanabaguana kwa sasa, tujiulize, mbona hii haikutokea kabla ya miaka ya kuanzia 1980?

Makoye,

Baada ya Nyerere kuivunja EAMWS na kuundwa BAKWATA Waislam wakawa
kama wamepwelewa.

Umma ulihangaika sana na jinsi ya kuiangusha BAKWATA lakini ikawa tabu
kwa kuwa serikali iliipa BAKWATA ulinzi kamili.

Ilipofika 1980 ilifanyika semina Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam iliyotayarishwa
na wanafunzi wa Kiislam wa Mlimani (MSAUD).

Hapo ndipo ilipoamuliwa vijana wa Kiislam waingie BAKWATA kutoa uongozi.
Vilevile kulikuwa na ''underground movement'' ikiitwa Warsha.

Hii ilifanya kazi kubwa sana kuwaamsha Waislam kuhusu dhulma.

Jambo la kwanza waliofanya vijana kutoka MSAUD ilikuwa kwanza kuwaeleza
Waislam kuwa ipo dhulma nchini.

Hapo ndipo pakawa mwanzo wa Waislam kuanza kujitazama upya...

Ni kisa kirefu hapa hapatoshi lakini kuanzia hapo hali ikaanza kubadilika.
 
Bi. Z,

Sheikh Mwilima amefariki miaka mingi sasa inazidi 15 na zaidi.

Sheikh Mwilima alipambana na Nyerere katika Halmashauri Kuu
ya CCM.

Alitaka kujua vipi Waislam wako nyuma katika nyanja zote na
akamwomba mwenyekiti alitazame tatizo hili kama alivyolitazama
tatizo la Wabarbaig, Wahadzabe na wanawake.

Amenihadithia mwenyewe.

Anasema ukumbi mzima ulikuwa kimyaaaaaa...
Wajumbe wanasikiliza mwenyekiti Nyerere atajibu nini.

Kwa kama dakika moja mbili...

Sheikh Abubakar Mwilima na Nyerere walitazamana kama majogoo
wanaotaka kupigana.

Nyerere akaahirisha kikao....

Mohamed hebu watendee haki watu wanaotufuatilia hapa,

Hivi Mwalimu aahirishe kikao baada ya swali hilo la Abubakar Mwilima?

Je ni kweli Mwalimu hakujibu kitu akabaki kumtazama tu Mwilima kama usemavyo majogoo watazamanavyo?
 
Nawashukuru Mods kwakuifanya kuwa thread maalumu, hilo litasaidia watanzania wengi kuujua uongo na uchonganishi wa huyu ndugu yetu Mohamed Said
 
Bi. Z,

Sheikh Mwilima amefariki miaka mingi sasa inazidi 15 na zaidi.

Sheikh Mwilima alipambana na Nyerere katika Halmashauri Kuu
ya CCM.

Alitaka kujua vipi Waislam wako nyuma katika nyanja zote na
akamwomba mwenyekiti alitazame tatizo hili kama alivyolitazama
tatizo la Wabarbaig, Wahadzabe na wanawake.

Amenihadithia mwenyewe.

Anasema ukumbi mzima ulikuwa kimyaaaaaa...
Wajumbe wanasikiliza mwenyekiti Nyerere atajibu nini.

Kwa kama dakika moja mbili...

Sheikh Abubakar Mwilima na Nyerere walitazamana kama majogoo
wanaotaka kupigana.

Nyerere akaahirisha kikao....

sasa hizi porojo,,, wote waliokuambia sasa marehemu! hakuna hata mmoja tunayeweza kumuuliza.
 
Naona Uislam unazungumzwa sana humu.
'
Sijui kwa nini, Ritz , zomba , Boko haram na wengine,hebu kutaneni na huyu jamaa, www.faithfreedom.org !
'
Naona mnataka kwenda kweny mjadala wa kutaka kupaka matope imani zingine zionekane zinatetea uhalifu.
'
Kwanini msizungumzie historia bila kupaka matope imani zingine?

Imani ndio nini? sisi Waislaam tuna nguzo za imaan. Jee wewe?
 
Zomba, huna hoja hapa, unapiga makelele kama mtoto tu, ona aibu, mtu mzima wa umri wako hata kama elimu ilikupita kando bado unanafasi ya kutumia uzoefu kujadiri hoja na sio ushabiki huu wa kipumbavu.

"lekebisha" basi ili tuanze kujadili mada kwa mujadala ulio fasaha. Usione haya wala yale.
 
Mbona umesahau na vita vilivyotokea Angola, Msumbiji, Eritrea, Norhern Ireland, Spain, Srilanka, Vita vikuu ya Kwanza na vya pili, Vietnam, nk! bila shaka hizi pia ni nchi za Kiislam!!!!!
Na hata Mgalatia Hitler alipowaua Mamilioni ya Wayahudi bila shaka hao nao walikuwa..........!
zubeda, naomba mkumbushe na Biafra!
 
Last edited by a moderator:
Mohamed hebu watendee haki watu wanaotufuatilia hapa,

Hivi Mwalimu aahirishe kikao baada ya swali hilo la Abubakar Mwilima?

Je ni kweli Mwalimu hakujibu kitu akabaki kumtazama tu Mwilima kama usemavyo majogoo watazamanavyo?

Wewe si utuletee alivyojibu!
 
Nawashukuru Mods kwakuifanya kuwa thread maalumu, hilo litasaidia watanzania wengi kuujua uongo na uchonganishi wa huyu ndugu yetu Mohamed Said

Pia watapata kumjuwa Abdu Sykes, Kleist Sykes (senior), Iddi Mafongo, Mshume Kiate, Tosiri, Mashado Plantan< Mama Mluguru.

Udhalim wa Nyerere na Kanisa Katoliki.
 
WC,

Tuhuma za udini na kuwa Nyerere hakuiasisi TANU ilimuathiri
sana Prof. Haroub Othman.

Akamwendea Nyerere na kutaka kujua yeye anasemaje.

Prof. Othman alimwambia Nyerere ni lazima aandike maisha
yake ili ukweli uwe wazi, vinginevyo historia yake itachafuka
.

Mimi nimeyasema haya wazi Nyerere akiwa hai.

Nimeyaandika haya toka 1988 wakati naandika na Africa Events.

Badala ya kunijibu magazeti yakawa yanakusanywa na kutiwa moto.

1998 ndipo nikatoa kitabu.
Sasa niko na nyie humu kwa jambo lile lile.

Nyinyi hamuwezi tena narudia hamuwezi.
Yote niliyosema ni kweli.

Mohamed Said sijui mpaka lini utaendelea kupotosha ukweli kuhusu hili jambo, Nilishakueleza hili mjadala ule wa 2010/2011) na ukakiri huku ukiendelea kusisitiza eti msukumo mwingine ulitokana na hadithi zako. Haya narudia tena kukuelezea historia ya wazo la uandishi wa biografia ya Nyerere lilikujaje: This is an extract kutoka gazeti lile lile lilochapisha makala zako kwa wiki tatu mfululizo - The East African, October 26, 1999.



"Tanzania's founder president and father of the nation , the late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, died before his autobiography could begin.
Prof. Ahmed Mohiddin, a former academician, told the East African that three people himself, Prof Haroub Othman, now live in Liberia, and former ambassador Ferdinand Ruhinda one of mwalimu's confidants had earlier approached the late Mwalimu to seek his consent.

He had initially agreed, on that and Prof Othman was to meet him in August 12, 1999 so that we could work on strategy on how we were going to do it. I think he knew his disease was fatal.

Prof Mohiddin who describes Mwalimu as the last revolutionary, said it is sad that he departed without it.

Ambassador Ruhinda said in Dar, "We were going to sit with him whenever he had time, and write his own words and then he would go through the manuscript and correct it because we wanted it to be his own work. It is just bad that he departed before the project could take off"

He added "Actually we were just going to assist him to write, but not for us to write for him; there are so many books that have been written about him that we wanted one from himself.

The three writers who had worked on a framework for the Nyerere Autograph now have daunting task ahead. "We will have to reorganize ourselves and the work. But it will never be the same again."

Bahati mbaya na Prof Othman akafariki pia.

Mzee Mohamed ni upotoshaji wa namna hii unaofanya baadhi ya members humu na watanzania kiujumla waone kwamba wewe una nia ovu, unataka kufitinisha jamii na kuleta mitafaruku isiyo na tija kwa "histohisia" , na lengo lako si jema hata kidogo. Unawezaje kuendelea kudanganya jamii mchana kweupee namna hiiii and not once Mohamed, not once. Sasa utaaminikaje na haya si mambo ya 1960's au enzi za African Association sijui 1930's. Kama nakumbuka vizuri MMM, Nguruvi na Mag3 walikubana utuambie kama umewahi kuwahoji Prof. Mohiddin na Ruhinda kuhusu uwepo wa hadithi zako kwenye maandalizi ya hiyo biographia jibu lake hujatoa mpaka leo. Halafu bila haya eti unasema yote uliyosema ni kweli!!!!
 
Mohamed Said sijui mpaka lini utaendelea kupotosha ukweli kuhusu hili jambo, Nilishakueleza hili mjadala ule wa 2010/2011) na ukakiri huku ukiendelea kusisitiza eti msukumo mwingine ulitokana na hadithi zako. Haya narudia tena kukuelezea historia ya wazo la uandishi wa biografia ya Nyerere lilikujaje: This is an extract kutoka gazeti lile lile lilochapisha makala zako kwa wiki tatu mfululizo - The East African, October 26, 1999.




Bahati mbaya na Prof Othman akafariki pia.

Mzee Mohamed ni upotoshaji wa namna hii unaofanya baadhi ya members humu na watanzania kiujumla waone kwamba wewe una nia ovu, unataka kufitinisha jamii na kuleta mitafaruku isiyo na tija kwa "histohisia" , na lengo lako si jema hata kidogo. Unawezaje kuendelea kudanganya jamii mchana kweupee namna hiiii and not once Mohamed, not once. Sasa utaaminikaje na haya si mambo ya 1960's au enzi za African Association sijui 1930's. Kama nakumbuka vizuri MMM, Nguruvi na Mag3 walikubana utuambie kama umewahi kuwahoji Prof. Mohiddin na Ruhinda kuhusu uwepo wa hadithi zako kwenye maandalizi ya hiyo biographia jibu lake hujatoa mpaka leo. Halafu bila haya eti unasema yote uliyosema ni kweli!!!!
Ndio maana sisi wengine tunamwambia mchochezi Mohamed Said aache kujaza kurasa za JF na ngano na kujinukuu mwenyewe, ajibu maswali anayoulizwa lakini akiamua kuwa muongo ajue kutunza kumbukumbu.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Said tafadhali uwe mkweli basi. Hoja yako nzima dhidi ya Baba wa Taifa imejengwa kwenye nadharia kuwa Nyerere alikuwa na chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu na alifanya kila awezalo kuukandamiza Uislamu (dhulma). Umewaaminisha mashabiki wako kuwa Nyerere alikuwa mtumishi wa kanisa akitumikia kuujandamiza Uislamu na hawa wamekuamini. Sasa unageuka na kusema kuwa hilo siyo tatizo? Kuwa sasa tatizo ni historia?

Nyerere alisema nini dhidi ya Uislamu, Waislamu au Mtume Mohammed kiasi cha kumfanya awe adui wa Waislamu? Au alitoa agizo gani lililowalenga Waislamu pekee yao na kutishia dini na ibada yao?

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Betrayal of Ideals
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] On 5 th November, 1985, before he stepped down as president, Nyerere delivered an emotional speech to elders of Dar es Salaam. Most of them were former members of TANU-the townsman who supported Nyerere during the struggle for independence[1] Nyerere acknowledged the role of Muslims in those difficult days. Nyerere told his audience that the imbalances between Muslims and Christians which his government had inherited from the British were rectified under his rule:
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] ''And they (Muslims) gave us chance through our education policies, to correct the imbalances which we have done. I am now in the happy position of sometimes not knowing whether a new member of Parliament, a Minister, or a Principal Secretary in our government ministries, is a Muslim or a Christian or neither unless their first name happens to give it away. And even that is not a sure guide in Tanzania, for we have Christians with Muslim names, Muslims with Christian names. This religious tolerance and freedom is your creation; what I have done is to speak up for those values on your behalf.'' [2]

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] The speech was a farce. The truth is that three decades after independence Muslim are not better off than they were under colonialism. Sivalon has revealed that the Church has been able to create its own lobby which controls 75% of the seats in the parliament. Among these seats 70% are held by Catholics and the rest are divided among Muslims and Christian denominations.[3][/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1] See footnote no.19.
[2] Daily News, 6 th November, 1985

[3] Sivalon, op.cit. p. 49.

Hivi nina hitaji mie kusherehesha hii yaani kutia maelezo?


Brother MS.......maandishi uliyotoa hapo juu hayajibu maswali uliyoulizwa.......rudia kusoma swali la MMKJJ....

Kusema ukweli binafsi nasikitika kuona vijana wa Kiislamu ambao wana nia njema kwelii na wanataka kujua sana wanaamini habari za Mohammed Said bila kuzihoji. Wanaamini si kwa sabbau wanajua ni kweli bali kwa sababu mzee anaonekana anautetea Uislamu na hivyo kumuuliza au kumkatalia kunawafanya wajihisi kama hawautendei haki Uislamu. Hii si sahihi kwa sababu ni mbinu ya 'sympathy' ambayo kwa kweli kwenye ukweli haina nafasi.

Maandishi ya mzee Said yanahitaji kuangaliwa kwa mwanga wa kisomi tu; hoja zake hata zingetolewa na mpagani bado zingeangaliwa kisomi. Ni jukumu la mtu yeyote mwenye akili kuuliza maswali mbele ya mtu anayetoa madai. Lengo si kumdhalilisha mtoa hoja bali kumsaidia mtoa hoja kuelezea vizuri hoja zake, kuzisahihisha na hata kuzitetea vizuri. Binafsi naamini Waislamu na hasa wale mashabiki wa Bw. Said waanze kumuuliza maswali ya akili ili kuupata ukweli vizuri.

....na huo ndio MTEGO wa Brother MS...... uliowanasa vijana wengi....
 
Mohamed Said anatoa hoja based on some very wrong premise ambayo ni hatari katika ustawi wa taifa letu. Kwamba eti "waislamu ambao hawajafanikiwa ni kutokana na dhulma ya mfumo kristo na wakristo waliofanikiwa basi ni kutokana na kupendelewa na mfumo kristo. Hii ni premise ya aibu kabisa and makes u fail hata kabla safari haijaanza. Lakini ndugu yetu huyu na mashabiki wake kwao huo ndiyo ukweli. Je ni vipi kwa waislamu waliofanikiwa na wakristo walioshindwa na kukata tamaa?????????

Turudi nyuma kidogo, Mohamed katika kujenga hoja zake juu ya mfumo kristo amebase zaidi D'salaam kitu ambacho ni cha ajabu pia kwani taasisi dhulmati huwa ni nchi nzima hukuhitaji kwenda Johanesburg kuprove uwepo wa apartheid au DC kwenda kuuona utumwa.

Hoja ya waislamu kunyimwa elimu mifano mingi sana ameitolea kutokea Dar. Sasa twende nyuma kidogo mwanzoni mwa miaka ya 80. Nimechagua kipindi hiki kwani nilishuhudia nayotarajia kuyaandika. Kifupi Dar enzi zile elimu haikuwahi kupendwa na wala haikuwa ujanja. Shule ilikuwa ni kimbilio ya mijitu ya kuja ambayo ilikuwa haina namna nyingine zaidi ya kusoma ili ije mjini. That was the perception of the day. Wajanja enzi hizo walikuwa mabaharia, Ma Dj, wachezaji (Simba, Yanga, Pan), Wanamuziki wa dansi na Wafanyakazi wa Bandari (kama akina Mohamed Said mwenyewe). Shule haikuwa na nafasi, role models kwa vijana wadogo enzi hizo walikuwa akina Gerry Kotto, Kalikali, Seydou, Makochela etc. na si wasomi. Baadae walikuja wauza unga, clearing and forwarding agents etc. Perception hizi potofu kuhusu umuhimu wa elimu ziliathiri vijana wote waislamu kwa wakristo na zilienea mpaka mijini kwingine nchi nzima. I know some fools watarukia kwamba see "they are now blaming it on ubaharia, samba, yanga, dansi etc." lakini ukweli ndiyo huo kuhusu perception ya shule by then jiini.

Mwanzoni mwa miaka ya 80 kukaruhisiwa kuanzisha shule binafsi, ungetegemea nafasi hiii kutumiwa nchi nzima tena hasa kule kulikokuwa na shule chache za serikali. Lakini haikuwa hivyo shule binafsi zikashamiri kule kule kulikokuwa na shule nyingi za serikali Kilimanjaro, Mbeya, Kagera, Iringa Mwanza etc
na si Dar why? (Wateja wakuu wakiwa ni locals kutoka maeneo hayo zilikojengwa shule hizo binafsi) Kifupi ni kuwa Dar hakukuwa na local demand period. Maana hata hapa pia supply and demand rules. Lakini pia wazee wetu "wa kuja" hawakuiona Dara kama sehemu muafaka ya kusomesha watoto wao kutokana na shule kutothaminiwa. Dar ukichanganya na pwani kukawa na shule chache binafsi ukilinganisha na wilaya kama Moshi vijijini au Rungwe. Ikumbukwe kuwa hizi ni enzi "ukipasi" darasa la saba unafanyiwa sherehe nyumbani.

Ni sometimes mwanzoni miaka ya 90 ndio shule ikaanza kuonekana muhimu tena, "twisheni" kila mahali hadi "uswazi". Sera za soko huria zikapelekea influx ya uwekezaji mfano mabenki binafsi, makampuni ya sm yaliyokuja bidae, migodi, uchumi kukua. Na huu ndio ukawa mwisho wa umaarufu wa mabaharia, wachezaji, wafanyakazi wa bandari. It's just shule shule, shule. Sasa akina Mohamed badala ya kufanya utafiti wa kitaalamu na mikakati ya kujenga shule zaidi na nzuri, kuongeza vyuo, kupanua nafasi za ajira na kuhakikisha vijana wa kitanzania wanakuwa na bright future mbeleni wao wanatafuta wachawi kwa mgongo wa dini.

Ungetarajia basi kwa kuwa kuna hiyo alleged dhulma iliyo wazi basi akina MS wangemobilize taifa zima (Wakristo kwa Waislamu) tupambane na hiyo dhulma. Kama ilivyokuwa South Africa au US, wazungu wengi tu walikuwa wakizipinga serikali zao kwa mifumo ile dhalimu pamoja na wao kufaidika nayo. Unaweza kuwa mjinga kufikiri kuwa Mzee Said hajawahi kunavigate into those waters hell no!!!!!!!!!!Msisitizo kuwa mfumo kristo chini ya kanisa katoliki ulikuwa na lengo la kuwapendelea wao kuliko watu wengine ilikuwa ni careful move kuwafanya walutheri, wasabato, wahindu ect. wa-sympathize na hoja zake. Bahati nzuri na mbaya kwake hilo halijawezekana.

Kinachoshindikana hapa ni kuwa hiyo alleged dhulma kutoka mfumo kristo haijawa substantiated, wala kutolewa ushahidi usio na mashaka na haipo. That is why ni marehemu tu ndiyo wanaotumiwa na Mzee said kujengea hoja

Jingine ambalo hatuhitaji kulinyamazia ni hii tabia ya Tambo za Mohamed Said kujustfy Authority ya hoja zake. Hii ni staili ambayo amekuwa akiitumia sana kwenye majukwaa yake ya wale wanaomsikiliza tu. Mfano aliposema kitabu chake kipo mpaka library of congress, Mohamed Said hii kwake ni sifa mno na justification kwamba alichoandika ni facts tupu. Lakini kwa taarifa yake ni kuwa ndani ya library of congress kuna vitabu chungu nzima vya simulizi based on conspiracies, uzushi, hila etc. Mfano ni hivi hapa chini:

1. Obama's America : unmaking the American dream / Dinesh D'Souza.

2. Roots of Obama's rage / Dinesh D'Souza.

3. Demonic : how the liberal mob is endangering America / Ann Coulter.

4. Way things ought to be / Rush Limbaugh.

5. Real America : messages from the heart and heartland / by Glenn Beck.


Ndani ya hiyo Obama's America mwandishi amemtuhumu marehemu mama ya sitting president Obama kwamba alikuwa Malaya aliyependa kujirusha na wanaume wa thirld world. Sasa kwa wasikilizaji wa hadithi za Mohamed Said ni vema watambue kuwa maktaba hiyo ina vitabu mpaka vinavyomtukana raisi kwa uzushi ilhali MS anatumia uwepo wa kitabu chake mle kama authority.
Lakini pia kuna watanzania mfano Musiba, Hammie Rajab, Eric Shigongo etc. wana vitabu ndani ya Library of congress (Bofya hapa) na tumbukiza majina yao kwenye search utaviona. Hatujawasikia watanzania hawa wakitoa tambo kama hizi za MS.

Tukija kwenye suala zima la Nyerere kuwa alitaka aonekane yeye tu kama anavyotuhumu Mohamed Said hili ni kichekesho. Mwalimu by then na to the African politics of the day kama hii ingelikuwa hulka yake asingeshindwa kuuita UD university of Nyerere, same to the airport, port and all the major roads na wala isingeonekana kuwa jambo la ajabu. But hakuwa hivyo na historia yake itamsimamia.

Kiujumla sidhani kama kuna anayepinga hadithi za MS, kinachopinga ni kule kutaka ku-institutionalize hadithi hizo kuwa historia. Na pale anapoombwa ufafanuzi huchagua maswali ya kujibu, ukiombwa ushahidi aliyemwambia ni marehemu so and so. Mohamed said you just need to come clean juu ya agenda unaoipigania. Adios.

Hili ni bandiko langu la mwisho kwenye mjadala huu.
 
Back
Top Bottom