Mohamed Said anatoa hoja based on some very wrong premise ambayo ni hatari katika ustawi wa taifa letu. Kwamba eti waislamu ambao hawajafanikiwa ni kutokana na dhulma ya mfumo kristo na wakristo waliofanikiwa basi ni kutokana na kupendelewa na mfumo kristo. Hii ni premise ya aibu kabisa and makes u fail hata kabla safari haijaanza. Lakini ndugu yetu huyu na mashabiki wake kwao huo ndiyo ukweli. Je ni vipi kwa waislamu waliofanikiwa na wakristo walioshindwa na kukata tamaa?????????
Turudi nyuma kidogo, Mohamed katika kujenga hoja zake juu ya mfumo kristo amebase zaidi Dsalaam kitu ambacho ni cha ajabu pia kwani taasisi dhulmati huwa ni nchi nzima hukuhitaji kwenda Johanesburg kuprove uwepo wa apartheid au DC kwenda kuuona utumwa.
Hoja ya waislamu kunyimwa elimu mifano mingi sana ameitolea kutokea Dar. Sasa twende nyuma kidogo mwanzoni mwa miaka ya 80. Nimechagua kipindi hiki kwani nilishuhudia nayotarajia kuyaandika. Kifupi Dar enzi zile elimu haikuwahi kupendwa na wala haikuwa ujanja. Shule ilikuwa ni kimbilio ya mijitu ya kuja ambayo ilikuwa haina namna nyingine zaidi ya kusoma ili ije mjini. That was the perception of the day. Wajanja enzi hizo walikuwa mabaharia, Ma Dj, wachezaji (Simba, Yanga, Pan), Wanamuziki wa dansi na Wafanyakazi wa Bandari (kama akina Mohamed Said mwenyewe). Shule haikuwa na nafasi, role models kwa vijana wadogo enzi hizo walikuwa akina Gerry Kotto, Kalikali, Seydou, Makochela etc. na si wasomi. Baadae walikuja wauza unga, clearing and forwarding agents etc. Perception hizi potofu kuhusu umuhimu wa elimu ziliathiri vijana wote waislamu kwa wakristo na zilienea mpaka mijini kwingine nchi nzima. I know some fools watarukia kwamba see they are now blaming it on ubaharia, samba, yanga, dansi etc. lakini ukweli ndiyo huo kuhusu perception ya shule by then jiini.
Mwanzoni mwa miaka ya 80 kukaruhisiwa kuanzisha shule binafsi, ungetegemea nafasi hiii kutumiwa nchi nzima tena hasa kule kulikokuwa na shule chache za serikali. Lakini haikuwa hivyo shule binafsi zikashamiri kule kule kulikokuwa na shule nyingi za serikali Kilimanjaro, Mbeya, Kagera, Iringa Mwanza etc na si Dar why?
(Wateja wakuu wakiwa ni locals kutoka maeneo hayo zilikojengwa shule hizo binafsi) Kifupi ni kuwa Dar hakukuwa na local demand period. Maana hata hapa pia supply and demand rules. Lakini pia wazee wetu "wa kuja" hawakuiona Dara kama sehemu muafaka ya kusomesha watoto wao kutokana na shule kutothaminiwa. Dar ukichanganya na pwani kukawa na shule chache binafsi ukilinganisha na wilaya kama Moshi vijijini au Rungwe. Ikumbukwe kuwa hizi ni enzi ukipasi darasa la saba unafanyiwa sherehe nyumbani.
Ni sometimes mwanzoni miaka ya 90 ndio shule ikaanza kuonekana muhimu tena, "twisheni" kila mahali hadi "uswazi". Sera za soko huria zikapelekea influx ya uwekezaji mfano mabenki binafsi, makampuni ya sm yaliyokuja bidae, migodi, uchumi kukua. Na huu ndio ukawa mwisho wa umaarufu wa mabaharia, wachezaji, wafanyakazi wa bandari. Its just shule shule, shule. Sasa akina Mohamed badala ya kufanya utafiti wa kitaalamu na mikakati ya kujenga shule zaidi na nzuri, kuongeza vyuo, kupanua nafasi za ajira na kuhakikisha vijana wa kitanzania wanakuwa na bright future mbeleni wao wanatafuta wachawi kwa mgongo wa dini.
Ungetarajia basi kwa kuwa kuna hiyo alleged dhulma iliyo wazi basi akina MS wangemobilize taifa zima (Wakristo kwa Waislamu) tupambane na hiyo dhulma. Kama ilivyokuwa South Africa au US, wazungu wengi tu walikuwa wakizipinga serikali zao kwa mifumo ile dhalimu pamoja na wao kufaidika nayo. Unaweza kuwa mjinga kufikiri kuwa Mzee Said hajawahi kunavigate into those waters hell no!!!!!!!!!!Msisitizo kuwa mfumo kristo chini ya kanisa katoliki ulikuwa na lengo la kuwapendelea wao kuliko watu wengine ilikuwa ni careful move kuwafanya walutheri, wasabato, wahindu ect. wa-sympathize na hoja zake. Bahati nzuri na mbaya kwake hilo halijawezekana.
Kinachoshindikana hapa ni kuwa hiyo alleged dhulma kutoka mfumo kristo haijawa substantiated, wala kutolewa ushahidi usio na mashaka na haipo. That is why ni marehemu tu ndiyo wanaotumiwa na Mzee said kujengea hoja
Jingine ambalo hatuhitaji kulinyamazia ni hii tabia ya Tambo za Mohamed Said kujustfy Authority ya hoja zake. Hii ni staili ambayo amekuwa akiitumia sana kwenye majukwaa yake ya wale wanaomsikiliza tu. Mfano aliposema kitabu chake kipo mpaka library of congress, Mohamed Said hii kwake ni sifa mno na justification kwamba alichoandika ni facts tupu. Lakini kwa taarifa yake ni kuwa ndani ya library of congress kuna vitabu chungu nzima vya simulizi based on conspiracies, uzushi, hila etc. Mfano ni hivi hapa chini:
1. Obama's America : unmaking the American dream / Dinesh D'Souza.
2. Roots of Obama's rage / Dinesh D'Souza.
3. Demonic : how the liberal mob is endangering America / Ann Coulter.
4. Way things ought to be / Rush Limbaugh.
5. Real America : messages from the heart and heartland / by Glenn Beck.
Ndani ya hiyo Obamas America mwandishi amemtuhumu marehemu mama ya sitting president Obama kwamba alikuwa Malaya aliyependa kujirusha na wanaume wa thirld world. Sasa kwa wasikilizaji wa hadithi za Mohamed Said ni vema watambue kuwa maktaba hiyo ina vitabu mpaka vinavyomtukana raisi kwa uzushi ilhali MS anatumia uwepo wa kitabu chake mle kama authority.
Lakini pia kuna watanzania mfano Musiba, Hammie Rajab, Eric Shigongo etc. wana vitabu ndani ya Library of congress (Bofya hapa) na tumbukiza majina yao kwenye search utaviona. Hatujawasikia watanzania hawa wakitoa tambo kama hizi za MS.
Tukija kwenye suala zima la Nyerere kuwa alitaka aonekane yeye tu kama anavyotuhumu Mohamed Said hili ni kichekesho. Mwalimu by then na to the African politics of the day kama hii ingelikuwa hulka yake asingeshindwa kuuita UD university of Nyerere, same to the airport, port and all the major roads na wala isingeonekana kuwa jambo la ajabu. But hakuwa hivyo na historia yake itamsimamia.
Kiujumla sidhani kama kuna anayepinga hadithi za MS, kinachopinga ni kule kutaka ku-institutionalize hadithi hizo kuwa historia. Na pale anapoombwa ufafanuzi huchagua maswali ya kujibu, ukiombwa ushahidi aliyemwambia ni marehemu so and so. Mohamed said you just need to come clean juu ya agenda unaoipigania. Adios.
Hili ni bandiko langu la mwisho kwenye mjadala huu.
Hizi kweli ngano ni vizuri liwe bandiko lako la mwisho watu wanajadili mambo mazito wewe unaongelea habari za Madj's kina Chogo, Saydou.
Wewe huijui Dar eti unasema miaka ya 80 watu walikuwa hawapendi shule ni kichekesho nakutajia shule za Ilala tu Bunge, Gerezani, Amana, Boma, Ilala, Lumumba, Mnazi Mmoja, Msimbazi, Mtendeni, Muhimbili, Uhuru, Upanga, Zanaki, Olympio, Agha Khan, Tambaza, Kisutu, hizi shule walikuwa wanasoma kina nani hapa sijataja Kinondoni, Temeke.
Halafu darasa la saba kulikuwa hakuna kupasi wanachaguliwa tu bila hata ya kuona matokeo hapa ndiyo mfumo kristu unafanya kazi, umeishajiuliza wale ambao hawajachaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza walikuwa wanaenda wapi au ndiyo hawa hawataki shule.
Unalalamika kuhusu mabaharia wakati Dar kuna bahari hii ingekuwa Moshi, Iringa wangekuwepo mabaharia tu.
Kama Nyerere hakuandika jina lake uwanja wa ndege na chuo kikuu basi hana matatizo mengine.