Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 51,303
- 40,190
Are you really serious? Kweli M Said kawaweza; kawaaminisha kuwa watu hawa wote yeye ndio kawataja kwa mara ya kwanza katika historia. Na la kusikitisha zaidi ni kuwa mpo mnaoamini kabisa kuwa Mohammed Said ndiye mtu wa kwanza kuwataja watu hawa na nafasi yao katika historia. That is really sad. Ukiondoa majina machache ambayo labda yanahusiana na watu wa Gerezani na Kariakoo majina ya washirika wa harakati za Uhuru kutoka sehemu mbalimbali nchini yanajulikana kwa muda mrefu yameandikwa kwa kiasi kikubwa tu.
Alichofanya Mohammed Said katika kujaribu kuiandika upya historia hiyo ni kuwagawa wazee wetu kwa misingi ya dini (Waislamu Vs. Wakristu). Anafanya kile ambacho baadhi ya wazee wake wa Kariakoo walijaribu kukifanya mwaka 1958 walipojaribu kuzigawanya harakati hizo za uhuru kwa misingi hiyo ya dini na matokeo yake wakatimuliwa miaka michache baadaye.
Kama unaamini kuwa Mohammed Said ndiye anawataja hawa - tena kwa dharau kuwa hawakuwa na central role kwenye harakati hizo ila wanatajwa tu kama waigizaji kwenye mchezo wa kuigiza - it is in itself tragic.
Wewe kweli Nyerere kakuweza. Hebu tuambie wewe hao wazee wametajwa kwenye historia ipi ya Tanzania.
Tena Mohamed Said kafanya la maana sana kuwaandika kwenye kitabu chake mpaka wale wazee waliokuwa viongozi wa TANU majimboni miaka mwaka 1955.
Hawa wazee wametupwa kabisa ikiwa Kambona hatambuliki mchango wake wa TANU watakuja kuwa hawa wazee.