Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #5,381
Hili swala la udini litawatafuna sana watanzania siku zote na sema the founder is Nyerere yeye kashatangulia huko hii mbegu yake aliyoipanda ndio imeota
Unasikitishwa na wewe ndio ulioleta huu uzi? maji ukishayavulia nguo uyakoge, Au hujuwi hilo?
Mohamed Said kitabu chake kimetoka Juliasi Nyerere yu hai.
Mwalimu Nyerere sio muasisi wa Udini balii ndie muasisi wa VITA dhidi ya Udini Tanganyika/Tanzania,
Wewe ulivyokuja na huu uzi wako kuwa Mohamed Said mchochezi ulidhani watu watakaa kimya.
Na katika vita hii Mwalimu alijitengenezea maadui wengi mno ambao wamekuwa wakirithishana visasi hivi hadi leo. Hakujawahi kuundwa Cabinet ya nchi hii ambayo ni "all inclusive" kama ile ya kwanza ya Tanganyika huru na nyingine nyingi zilizofuata baada ya hapo. Bado Mwalimu anaambiwa alikuwa mbaguzi! Kweli akutukanae hakuchagulii tusi.Mwalimu Nyerere sio muasisi wa Udini balii ndie muasisi wa VITA dhidi ya Udini Tanganyika/Tanzania,
Ungekuwa mtoto wa Julius Kambarage ningekuambia pitia kumbukumbu zake nyumbani uje utuambia kabla ya Nyerere lini Watanzania walipigana vita vya kidini.
Si lengo langu watu wakae kimya, bali waujue ukweli nao uwaweke huru dhidi ya minyororo ya Mchochezi Mohamed Said!
Ndugu yangu nilikwambia Historia ya Tanganyika huijui na hutaki kujua kabisaaa!
Hivi unajua DINI hizi mnazozililia wewe na Mohamed Said zimekuja lini?
Unajua ukristu wa RC umekuja lini nchini?
Na uislamu umekuja lini?
Na zaidi Mwalimu Nyerere ameingia lini katika mafundisho ya dini ya Kigeni?
Amekuwa madarakani kwa miaka 24 bila vita kama ile ya jana kule Geita kuwepo. Usimamizi wa KATIBA na SHERIA ndio haupo kwa sasa. Mambo haya hayataki nalenale( kama ulipita JKT unalijua neno hili) au kubembelezana.Ungekuwa mtoto wa Julius Kambarage ningekuambia pitia kumbukumbu zake nyumbani uje utuambia kabla ya Nyerere lini Watanzania walipigana vita vya kidini.
Endelea kujifariji tu kwanza wasomaji hawana chochote wanachopata kutoka kwako labda kejeli na dhihaka.
Wewe ni mtupu za sana kwenye anga za historia.
Umeahidi vitu vingi humu jamvini hakuna hata kimoja ulicholeta watu wameamua kukupuza tu.
Amekuwa madarakani kwa miaka 24 bila vita kama ile ya jana kule Geita kuwepo. Usimamizi wa KATIBA na SHERIA ndio haupo kwa sasa. Mambo haya hayataki nalenale( kama ulipita JKT unalijua neno hili) au kubembelezana.
Tutatwangana kidini bado tutajikuta sio wamoja kwani hata nchi za DINI moja kama Uarabuni na Somalia wanauana. Tutaanza kutwangana KIKABILA, KIUKOO,....
Tatizo lako wewe na ndugu yako ni kukurupuka hujui hata huo mjadala ulianzia wapi, hoja hakuna bali ni kurukia rukia tu maneno kama ...., kitabu nilichokitaja hapo umewahi hata kukisikia????? Maana nyie mnafikiri vitabu vya historia ya Tanganyika ni vile anavyotaja mwalimu wenu tu. Tatizo lingine ni kwamba nyie mko hapa kiimani zaidi and that is the main problem, big problem. Toka huu mjadala umeanza hakuna chochote mnachochangia zaidi ya mipasho mkiamini MS anaonewa hahaha ahahahah!!!!!! Sorry I won't have time again kujibizana na wewe kama ndugu yako. Majidiliano na Mzee Said na wengine ambao wako objective.
Kama historia ya Kivukoni kweli siwezi kuijua lakini historia ya Tanganyika unipati kabisa.
Umeshindwa kujua Oscar Kambona alikuwa na cheo gani ndani ya TANU. unasema alikuwa mwanachama wa kawaida tu.
Yericko wewe mchache sana kwenye historia ya Tanganyika.
Mbona unawalisha maneno wasomaji? Wamekwambia kuwa hawajanufaika na chochote kutoka kwangu?
Yaleyale ya Mwalimu wenu Mohamed Said yakulisha watu maneno!
Sema ukweli kuwa wewe ndie hujanufaika na chochote kutoka kwangu, na niukweli huwezi kupendezwa na nilichoandika hapo kwakuwa ninawaharibia mipangu yenu ya uchochezi!
Inawezekana hauelewi maana ya uzi huu mkuu,
Nimeuleta hapa ikiwa ni sehemu ya kumuonya Mohame Said kwa Uchochezi wake!
Na mpaka dakika hii ninaamini nimeokoa watu wengi sana waliokuwa wafuasi wa NGANO za Mchochezi huyu!
Hiyo vita ndio hatuwezi kuongopeana kabisa uwadanganye hawa vijana waliozaliwa miaka ya '70 kuelekea '80. Uongo mzuri ni kama wa mzee Mohamed aliouficha kwenye kanzu na barghashia za wazee wake wa Kariakoo.Vita vya Kagera vilikuwa siyo vita? Nipe kisa chake tuanze kufungua vitabu upya.
Mimi nitamkumbuka zaidi Mshume Kiate kwa maharage, dagaa na mchicha wake alookuwa akipeleka Magomeni kwa Mwalimu.Mpaka sasa wewe ndiye uliyejifunza mengi sana, mpaka unataka kuendelea kujifunza kwa kwenda kutafuta data za kina Mkwawa, mikanda ya hotuba, historia ya Abushiri na mengineyi mengi.
Nna uhakika uzi huu umekuwa na faida kubwa sana kwa jamii. Wengi leo wanamjuwa Mshume Kiate, Mashado Plantan, Iddi Tosiri. Lakini nani kabla ya hapa alikuwa akiwajuwa? na nani alikuwa hamjuwi Nyerere? tulilosoma jipya kuhusu Nyerere ni jinsi alivyowageuka Waislaam na kuwaweka ndani, kuwavunjia jumuia yao ya EAMWS na mambo kadha wa kadha.
Nakupa heko na nakupa hongera. Ni faida kubwa sana huu mjadala. Uzuri ni kwamba umeshindwa mpaka dakika hii kuonesha uchochezi na dhihaka za Mohamed Said kwa wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, tunachokiona ni dhihaka na kejeli mnazowafanyia wewe na wenzako na tunaona Mohamed Said akiwatukuza na kuwaenzi.
Imekula Kwako.
Haahaa aisee kweli nimeamini wewe na kundi lenu likiongozwa na Mohamed Said ni hatari kwa Taifa,Vita vya Kagera vilikuwa siyo vita? Nipe kisa chake tuanze kufungua vitabu upya.
Wewe wamekuambia wapi wamenufaika na mchango wako au ndiyo unasema unaamini wanaamini.
Mimi nitamkumbuka zaidi Mshume Kiate kwa maharage, dagaa na mchicha wake alookuwa akipeleka Magomeni kwa Mwalimu.