zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,930
Kwa kweli Ritz kama umeweza kushabikia hayo ya zomba...! sina la kuongeza kwenye hilo...ila siku moja tusije kushtuka mtoto wa Sheikh Ponda akifuata nyayo za mtoto wa Salum Abdalla, naye akifanya utafiti aweze kuandika historia ya harakati za wazee wake katika mapambano ya kuupinga utawala wa Kikwete. Watoto wetu na wajukuu zetu nao watajikuta wakiikosoa hiyo histohisia kama tunavyokosoa histohisia ya Mohamed Said huku wajukuu wa Ritz na zomba nao wakimtetea mwalimu wao kama tunavyoshuhudia.
Ila wakati huo kutakuwa na tofauti, dhihaka na kejeli za wajukuu wenu hazitaelekezwa kwa Kikwete aliye madarakani akiiongoza serikali ya CCM bali zitajikita katika kuulaumu mfumo Kristo wakisahau kuwa shida na taabu walizozipata wananchi kutokana na uongozi dhaifu hazikuangalia dini ya mtu. Inasikitisha sana kuwa chuki zilizopandikizwa vichwani mwao kwa simulizi za barazani toka utotoni kutoka kwenye vinywa vya wazee wao, ndizo zilizowaongoza katika uandishi wao ingawa wenyewe watadai waliyoyaandika ndio ukweli.
Wewe umeandika nini na kipi? kama unao ukweli unaoujuwa wewe si uandike, mpaka sasa hoja zako hazina mshiko, eti nyumba, eti mgogoro. Mohamed Said alikwambia anaandika kuhusu migogoro ya nyumba?
Saa nyingine huwa najiuliza uwezo wenu wa kufikiri. Hapo ndipo ulipoishia?
Kivukoni waliyaandika hayo?