kibol
JF-Expert Member
- Apr 24, 2012
- 4,521
- 2,747
Nikushukuru kwakutambua mchango wangu hapa jamvini,
Nitawashawishi wenzanggu hapa jamvini tuufanyie kazi ushauri wako kadiri tuwezavyo!
Niukweli usio na mawaa kuwa historia yoyote ya nchi haiandikwi na mtu mmoja!
Kinachoandikwa na mtu mmoja na kikakubalika bila kupingwa ni utafiti wa kisayansi tu kwakuwa kila atakaetaka kuthibitisha, atathibitishiwa kisayansi!
Historia ya nchi huandikwa kwa kushirikisha fikra na kumbukumbu za wengi wanaoamua kuwekeza akili yao ktk lengo moja!
Mohamed Said hata kama awali alikuwa na wazo zuri, lakini alizdiwa na hiisia binafsi hasa zakiimani na hivyo kuharibu zaidi maana ya alichotaka kuueleza ulimwengu!
Kweli mkuu Yericko Nyerere ata mimi nampongeza sana ndugu Mohamed Said kwa kuibua changamoto hii ya kuitizama upya historia ya taifa letu lakini amefail kwa kiasi fulani kwa kua amekwisha chagua upande wa kuegemea hivyo ata kama ni data anatafuta atakua anatafuta zile zinazo suit ktk kile anachotaka kukipresent tu,ni kawaida kwa sisi binadamu ukishachagua upande ni lazima uutete kufa na kupona ata ikikubidi wakati mwingine kupotosha kwa makusudi ili lile lengo lako litimie.
Last edited by a moderator: