Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nikushukuru kwakutambua mchango wangu hapa jamvini,

Nitawashawishi wenzanggu hapa jamvini tuufanyie kazi ushauri wako kadiri tuwezavyo!

Niukweli usio na mawaa kuwa historia yoyote ya nchi haiandikwi na mtu mmoja!

Kinachoandikwa na mtu mmoja na kikakubalika bila kupingwa ni utafiti wa kisayansi tu kwakuwa kila atakaetaka kuthibitisha, atathibitishiwa kisayansi!

Historia ya nchi huandikwa kwa kushirikisha fikra na kumbukumbu za wengi wanaoamua kuwekeza akili yao ktk lengo moja!

Mohamed Said hata kama awali alikuwa na wazo zuri, lakini alizdiwa na hiisia binafsi hasa zakiimani na hivyo kuharibu zaidi maana ya alichotaka kuueleza ulimwengu!

Kweli mkuu Yericko Nyerere ata mimi nampongeza sana ndugu Mohamed Said kwa kuibua changamoto hii ya kuitizama upya historia ya taifa letu lakini amefail kwa kiasi fulani kwa kua amekwisha chagua upande wa kuegemea hivyo ata kama ni data anatafuta atakua anatafuta zile zinazo suit ktk kile anachotaka kukipresent tu,ni kawaida kwa sisi binadamu ukishachagua upande ni lazima uutete kufa na kupona ata ikikubidi wakati mwingine kupotosha kwa makusudi ili lile lengo lako litimie.
 
Last edited by a moderator:
Inategemeana na maana ya kufanikiwa. Hivi ni kweli Nyerere alitoka Magomeni kwenda Kariakoo bila hata senti mfukoni?
Hivi ni kweli Nyerere alisoma hotuba UN kama kasuku aliyeandikiwa na Abdulwahid Sykes na kwenye kitabu chake akaiandika in the first person? Hiyo ni mifano michache tu ufanisi wetu wa kuumbua upotoshaji wa Sheikh Mohamed.

Sasa wewe andika Nyerere alitoka Magomeni akiwa na pesa mfukoni na hakukutana na Mshume. Na pia andika kuwa hotuba ile aliiandika Nyerere akiwa Pugu au vyovyote vile ujuavyo.

Kuna mtu alikulazimisha uyakubali aliyoyaandika Mohamed Said? aidha yakubali au usiyakubali, yaamini au usiyaamini, Mohamed Said kisha andika ajuavyo yeye. Wewe unaweza andika ujuavyo wewe kama unaona ya Mohamed Said hayakuingii. Mohamed Said kaona ya historia ya kivukoni hayamuingii akapekuwa makabrasha ya wazee wake na ya wengine wengi, akaja na kitabu kinachoeleza ajuavyo yeye wazee wake walivyopigania Uhuru.

Ulilazimishwa uamini? Unangoja nini kuandika unavyojuwa wewe kuwa ndio sahihi?
 
Sasa wewe andika Alioki Magomeni Akida na pesa mfukoni na hakukutana na Mshume. Na pia andika kuwa hotuba ile aliiandika Nyerere akiwa Pugu au vyuo vote upendavyo.

Kuna mtu alikulazimisha usafiri aliyoibandika Mohamed Said, aidha yakubali au usiyakubali, yaamini au usiyaamini, Mohamed Said kisha andika ajuavyo yeye. Wewe unaweza andika ujuavyo wewe kama unaona ya Mohamed Said hayakuingii. Mohamed Said kaona ya historia ya kivukoni hayamuingii akapekuwa makabrasha ya wazee wake na ya wengine wengi, akaja na kitabu kinachoeleza ajuavyo yeye wazee wake walivyopigania Uhuru.

Ulilazimishwa uamini? Unangoja nini kuandika unavyojuwa wewe kuwa ndio sahihi?

Kaka,
Mimi si mwandishi. Na si kila mtu ana kipawa cha uandishi. Lakini hilo halininyimi haki yangu ya kufichua upotoshaji. Tungekuwa sote waandishi nani angekuwa na nafasi ya kumsoma na kumkosoa mwenzake?
 
Mwalimu wetu Mohamed Said, wanafunzi wapo darsa wanasubiri kusoma.
 
Last edited by a moderator:
Kaka,
Mimi si mwandishi. Na si kila mtu ana kipawa cha uandishi. Lakini hilo halininyimi haki yangu ya kufichua upotoshaji. Tungekuwa sote waandishi nani angekuwa na nafasi ya kumsoma na kumkosoa mwenzake?

Sasa si uoneshe huo upotoshaji? wewe unapinga kuwa hivi si sawa lakini hicho kilicho sawa hukiandiki.

Mohamed Said ameshasema mara nyingi humu jamvini, ni wengi hawaamini kama haya kayaandika yeye. Wewe unaweza ukaamini unaweza usiamini, basi hata unachokijuwa ndio ukweli huwezi kukiandika kwa kuwa si mwandishi? mbona kupinga unaweza kuandika? Si lazima uandike kitabu kama Mohamed Said, hata mistari miwili mitatu ya kutuonesha ukweli unaoujuwa wewe inatosha, tutakuelewa.

Lakini leo unapinga kuwa huamini Mzee Nyerere aliweza kutoka Magomeni bila hata senti, sasa jiulize alikuwa na kazi ipi wakati huo ya kumuingizia pesa? ulitaka aibe? hakuwa mtu wa aina hiyo. Au unapinga kuandikiwa hotuba? leo hii duniani karibu Marais wote wana waandishi wao wa hotuba, nini cha ajabu? Fikiri!

Kama unaujuwa ukweli zaidi ya huo aliouandika Mohamed Said tujuze, si kupinga tu mradi upinge.
 
Sasa si uoneshe huwa upotoshaji? wewe unapinga t, kuwa hivi si sawa lakini hicho kilich sawa hukisemi.

Mohamed Said ameshasema mara nyingi humu jamvini, ni wengi hawaamini kama haya kayaandika yeye. Wewe unaweza ukaamini unaweza usiamini, basi hata unachokijuwa ndio ukweli huwezi kukiandika kwa kuwa si muandishi? mbona kupinga unaweza kuandika? Si lazima uandiki kitabu kama Mohamed Said, hata mistari miwili mitatu ya kutuonesha ukweli unaoujuwa wewe inatosha, tutakuelewa.

Lakini leo unapinga kuwa huamini Mzee Nyerere aliweza kutoka Magomeni bila hata senti, sasa jiulize alikuwa na kazi ipi wakati huo ya kumuingizia pesa? ulitaka aibe? hakuwa mtu wa aina hiyo. Au unapinga kuandikiwa hotuba? leo hii duniani karibu Marais wote wana waandishi wao wa hotuba, nini cha ajabu? Fikiri!

Kama unaujuwa ukweli zaidi ya huo aliouandika Mohamed Said tujuze, si kupinga tu mradi upinge.

Zomba,
Kama wewe kweli unaamini Nyerere aliondoka Magomeni kwenda sokoni Kariakoo kuwanunulia watoto wake chakula huku hana hata senti tano mfukoni basi ama wewe ni mwendawazimu au Nyerere ndiye alikuwa na wazimu.
Na hotuba za Nyerere, hasa ile ya kwanza UN tunajua aliiandika mwenyewe. Kama TANU walimpa point of references na draft hilo ni jambo jengine ambalo Mohamed hakusema kabisa. Alitaka tuamini kuwa aliisoma kama kasuku huko UNO.
 
Zomba,
Kama wewe kweli unaamini Nyerere aliondoka Magomeni kwenda sokoni Kariakoo kuwanunulia watoto wake chakula huku hana hata senti tano mfukoni basi ama wewe ni mwendawazimu au Nyerere ndiye alikuwa na wazimu.
Na hotuba za Nyerere, hasa ile ya kwanza UN tunajua aliiandika mwenyewe. Kama TANU walimpa point of references na draft hilo ni jambo jengine ambalo Mohamed hakusema kabisa. Alitaka tuamini kuwa aliisoma kama kasuku huko UNO.

Hasira na kuitana wendawazimu inahusu nini? si uandike ukweli uujuavyo wewe. Hebu jikumbushe kidogo kuwa Mshume alishajitolea kabla ya siku hiyo;
Tumkumbuke Marehemu Mzee Kiyate Mshume

  • Dalali wa Samaki Kariakoo na Mfadhili wa TANU na Nyerere



Mohamed Said

Napenda nieleze kisa hiki cha kusisimua cha marehemu Mshume Kiyate kama nilivyoelezwa na mzee wangu Ahmed Rashad Ali, kisa ambacho yeye alihadithiwa na Mwalimu Julius Nyerere kwa kinywa chake mwenyewe. Ahmed Rashad anasema siku aliyosikia kisa hiki yeye alikuwa pamoja na Dossa Aziz na Lucy Lameck. Ilikuwa mwaka wa 1965 siku ile mlowezi Ian Smith alipojitangazia uhuru kutoka kwa Waingereza. Ahmed Rashad wakati ule alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi Idara ya Habari na alikwenda nyumbani kwa Mwalimu Msasani ili apate kauli ya Mwalimu Nyerere na msimamo wa serikali kuhusu mgogoro wa Rhodesia. Walimkuta Mwalimu Nyerere nyumbani kwake katika maktaba yake anaandika. Ahmed Rashad anasema Nyerere aliwaeleza kuwa katika kutafakari mambo yaliyokuwa yakiendelea Rhodesia, Uingereza haitofanya lolote dhidi ya Ian Smith kwa kujitangazia uhuru wa maguvu. Ahmed Rashad alinieleza kuwa Mwalimu Nyerere alisema, "Hawa ni mtu na mjomba wake," akikusudia kuwa Waingereza na walowezi wa Rhodesia walikuwa ndugu wa damu kwa hiyo Waingereza hawatatia jeshi pale kuwang'oa walowezi.

Baada ya Mwalimu Nyerere kumaliza kutoa msimamo wake wakawa sasa wamekaa wanapiga gumzo huku wakinywa vinywaji na Mwalimu alikuwa mtu hodari sana wa kustawisha baraza. Waliokuwa karibu na Nyerere wanamjua kwa sifa hii. Mwalimu Nyerere alianza kuhadithia kisa chake na Mshume Kiyate. Haifahamiki hasa ni lini Nyerere alijuana na Mzee Mshume lakini huenda ilikuwa hata kabla ya kuaisiswa kwa TANU siku zile za TAA Nyerere alipokuwa nakwenda ofisini kwa Abdulwahid Sykes pale Kariakoo sokoni ambako Abdulwahid alikuwa Market Master. Mzee Mshume alikuwa ndiye dalali wa samaki soko la Kariakoo na alikuwa mzee aliyeheshimika sana mjini Dar es Salaam na baadae alikuja kuwa mmoja wa wazee katika Baraza la Wazee wa TANU. Nyerere alianza kukihadithia kisa chake na Mzee Mshume kwa kusema kuwa siku moja wakati wa kudai uhuru alikuwa anatoka nyumbani kwake Magomeni Majumba Sita kwa miguu kuelekea Kariakoo ili kupata mahitaji yake lakini katika safari hiyo mfukoni mwake alikuwa hana hata senti moja. Akiwa njiani karibu na sehemu inayoitwa Mwembe Togwa (hapa kwa leo ni pale Fire makutano na Morogoro Road na Barabara ya Umoja wa Mataifa)Mwalimu alikutana na Mzee Mshume Kiyate. Mwalimu Julius Nyerere akamfahamisha Mzee Mshume kuwa alikuwa anakwenda sokoni Kariakoo lakini hana fedha za kununulia mahitaji yake. Mzee Mshume Kiyate aliingiza mkono katika koti lake akatoa shilingi mia mbili na kumpa Nyerere. Ukitaka kujua thamani ya fedha hiyo kwa wakati ule, naitoshe kujua kwamba ilimgharimu mtu shilingi mia tano tu kujenga nyumba ya vyumba sita katika eneo la Kariakoo.

Mzee Mshume alifadhaishwa sana na hali ile ya Nyerere kuwa anahangaika na kuikimu familia yake na huku wamemtwisha mzigo wa kuendesha TANU. Kutokana na hali hii Mzee Mshume aliona itakuwa ni kumtaabisha Nyerere bila sababu ikiwa atakuwa anashughulika na kuwatafutia wanawe chakula na wakati huohuo akiwa na jukumu la kufanya kazi za TANU. Hapo ndipo Mzee Mshume alipojitolea kuihudumia nyumba ya Mwalimu Julius Nyerere. Kila asubuhi Landrover ya TANU inapiga breki Karikaoo sokoni pale na Mzee Mshume ananunua mahitaji yote ya siku anamkabidhi dreva wa TANU jina lake Said lakini watu wakampachika jina wakimwita TANU. Said TANU anachukua vitu vile anapeleka vile Magomeni Majumba Sita kwa Mama Maria. Mzee Mshume alifanya hivyo hadi uhuru ulipopatikana. Baada ya uhuru Mwalimu Nyerere sasa akiwa Waziri Mkuu alimwomba Mzee Mshume aache kumnunulia chakula lakini Mze Mshume alikataa na badala yake akamtafadhalisha Mwalimu Nyerere aendelee kupokea chakula chake na kile ambacho kinatolewa na serikali kwake yeye, kama mkuu wa nchi alimuomba Mwalimu awakirimu wageni wake. Mwalimu Julius Nyerere alikiita kisa hiki ‘the TANU spirit' – yaani moyo wa TANU – akieleza mapenzi na moyo waliokuwanao wana TANU wakati ule wa kudai uhuru.

Kisa hiki kwa mara ya kwanza kabisa kilihadithiwa hadharani na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa wakati ule marehemu Ditopile Mzuzuri Mkiwaona kada wa Chama Cha Mapinduzi. Ditopile alikieleza kisa hiki kama alivyokieleza Mwalimu Nyerere kwa Ahmed Rashad na Lucy Lameck kwa nia ya kuonyesha moyo wa TANU na mchango wa wazalendo katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Kisa hiki kwa Dossa hakikuwa kipya. Dossa akimjua Nyerere nje ndani. Kwa bahati mbaya waandishi wa magazeti wakapotosha kisa kizima. Badala ya kutoa umuhimu kwa moyo wa ukarimu wa Mzee Mshume na kumueleza kama mzalendo aliyejitolea katika kupigania uhuru, magazeti yakageuza maneno ya Ditopile kuwa masimango dhidi ya Mwalimu Nyerere. Kwa ajili hii nafasi ambayo ingeliweza kutumiwa ili kueleza umuhimu wa Mzee Mshume na historia ya TANU ikapotezwa.

Tuendelee na Mzee Mshume na Mwalimu Nyerere. Tarehe 20 Januari 1964 wanajeshi waliasi ikabidi Nyerere aombe msaada kwa Waingereza waje kuwanyang'nya silaha askari. Baada ya uasi ule kuzimwa na jeshi la Kiingereza, TANU ilifanya mkutano mkubwa sana katika Viwanja vya Jangwani Dar es Salaam. Mzee Mshume kwa niaba ya wazee wa TANU alipanda jukwaani na kumvisha Nyerere kilemba kama ishara ya kumuunga mkono. Hakuna picha alioyopiga Nyerere kati ya mwaka 1955 na 1961 ambayo Mzee Mshume asiweko ndani yake. Mzee Mshume alikuwa mstari wa mbele katika harakati za uhuru na kumuunga mkono Nyerere kwa kila jambo kwa hali mali. Picha ya Mzee Mshume akimvisha Nyerere kilemba ilichapishwa katika magazeti mengi. Halikadhalika picha nyingine mashuhuri ya Mzee Mshume na Mwalimu Nyerere ni ile iliyopigwa Novemba 1962 wakati wa Uchaguzi Mkuu.Picha hiyo inamuonyesha Mzee Mshume akiwa amevaa koti, kanzu na kofia na huku amemshika Mwalimu Nyerere mkono akimsindikiza kupiga kura. Magazeti ya Chama na Serikali – Uhuru na Daily News yamekuwa yakiitumia picha hii kila baada ya miaka mitano katika uchaguzi wa rais kama njia ya kuwahamasisha watu kupiga kura na kumchagua Mwalimu Julius Nyerere. Kwa bahati mbaya picha ile siku zote hutoka bila maelezo na kwa hiyo wengi hawafahamu yule mzee aliyefuatana na Mwalimu Julius Nyerere ni nani. Kadhalika si wengi wanaoufahamu mchango wa Mzee Mshume Kiyate katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa sababu Mwaka 1995 Jiji lilipoamua kubadilisha jina la mtaa aliokuwa akiishi Mshume Kiyate – yaani Mtaa wa Tandamti ili uitwe Mtaa wa Mshume Kiyate kama ishara ya kumuenzi na kuthamini mchango wake katika kupinga ukoloni, baadhi ya magazeti yalipinga kitendo hicho na hadi leo mtaa ule haujawekewa kibao kilicho na jina la Mshume Kiyate.

Hofu iliyotanda katika vyombo vya habari na kwa wengi wasiojua historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa mbona majina ya mitaa yote yanapewa majina ya Waislamu? Lakini kubwa zaidi la kushangaza sana ni kuwa hata pale magazeti yalipokuwa yameingia katika malumbano ya kupinga majina yale mapya ya wazalendo katika mitaa kama vile Kleist Sykes, Max Mbwana, Mshume Kiyate, Tatu Bint Mzee, Omari Londo nk. Mwalimu Nyerere ambaye yeye ndiye akiwajua vyema mashujaa hawa alikuwa kimya. Katika mahojiano aliyofanyiwa Meya wa Dar es Salaam, Kitwana Selemani Kondo na Serah Dumba wa Radio Tanzania kuhusu mabadiliko ya majina ya mitaa, Mzee Kondo alisema hao wanaosema hawawajui hao walioenziwa kwa kupewa majina yao kupewa mitaa waulize watu hao walikuwa nani wataelezwa.

Mzee Mshume amekufa pweke Hospitali ya Muhimbili na katika maziko yake hawakuonekana wale waliokuja faidi matunda ya uhuru. Akiwa kitandani mgonjwa pale hospitali alisikika mara kadhaa akimwambia mwanae akiitwa Kiyate, "Kiyate umewapa taarifa wenzangu (anawataja majina) kuwa mimi nimelazwa?" Mazishi ya Mzee Mshume yalifanyika mtaa wa Matumbi kwenye nyumba ya Sheikh Maguno aliyekuwa ndugu yake. Sheikh maguno ndiye alikuwa muadhini wa msikiti wa Shadhly kwa miaka 35. Mazishi ya Mshume Kiyate yalikuwa ya kawaida sana na wala hapakuwa na hotuba wala rambirambi. Kwa miaka mingi Mzee Mshume alipumzika kaburini kwake kwa amani hadi pale alipoenziwa na Kitwana Kondo kwa jina lake kupewa mtaa.
3 Oktoba 2011


Punguza ghadhab, utaona Mohamed Said anatowa kisa alichokihadithia Nyerere mwenyewe, sasa Mohamed Said atowe kitabu na Nyerere yuko hai amzulie? Nyerere huyu Nyerere? Fikiri!
 
Jina la kitabu

HISTORIA YA KWELI YA TANGANYIKA

Waadishi ni Yericko Nyerere, Mag3, Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Nyambala, nyiondo, WildCard, kibol, Jasusi,


Kitabu kipo njiani wakati wowote kitatoka. Watanganyika jiandaeni kuisoma historia yenu jopo la waandishi vichwa wa JF kwa pamoja wanaunganisha nguvu kuandika kitabu.

Una matatizo mdogo wangu; historia ni historia hakuna cha ukweli au uongo. Ukisema uongo kuhusu historia hujaandika historia. Kwa hiyo kwenye historia ukweli peke yake husimama. Sasa tafsiri ya matukio mbalimbali ya historia ndio huwa ni mjadala. Alichofanya Mwalimu wenu hapa Mohammed Said ni kuweka tafsiri yake katika matukio ya historia. Ndio maana uandishi wake umejaa "inasemekana".. "iliaminiwa"... "ilisemwa"... nyingi mno. Wakati wowote hakuwa na ushahidi Mohammed anachomokea "Iliaminiwa" hata asipotaja na kina nani na kwanini...

Hatuhitaji kuandika kitabu kingine kwani historia ya Tanganyika imeandikwa kwa kirefu sana na watu wengi tayari - tatizo ni kuwa Mohammed Said peke yake ndio kajaribu kuiandika kwa kutumia prism ya udini. Matukio yote ya historia yetu (au karibu yote) ameyamulika kwa kutumia dini na hivyo mwanga huo wa dini umemfanya aone kila kitu kikiwa na dini hata kisichokuwa cha kidini.
 
Una matatizo mdogo wangu; historia ni historia hakuna cha ukweli au uongo. Ukisema uongo kuhusu historia hujaandika historia. Kwa hiyo kwenye historia ukweli peke yake husimama. Sasa tafsiri ya matukio mbalimbali ya historia ndio huwa ni mjadala. Alichofanya Mwalimu wenu hapa Mohammed Said ni kuweka tafsiri yake katika matukio ya historia. Ndio maana uandishi wake umejaa "inasemekana".. "iliaminiwa"... "ilisemwa"... nyingi mno. Wakati wowote hakuwa na ushahidi Mohammed anachomokea "Iliaminiwa" hata asipotaja na kina nani na kwanini...

Hatuhitaji kuandika kitabu kingine kwani historia ya Tanganyika imeandikwa kwa kirefu sana na watu wengi tayari - tatizo ni kuwa Mohammed Said peke yake ndio kajaribu kuiandika kwa kutumia prism ya udini. Matukio yote ya historia yetu (au karibu yote) ameyamulika kwa kutumia dini na hivyo mwanga huo wa dini umemfanya aone kila kitu kikiwa na dini hata kisichokuwa cha kidini.

Nimeyaandika haya baada ya Yericko kusema atawasiliana na nyie muandike kitabu cha uhuru.
 
Una matatizo mdogo wangu; historia ni historia hakuna cha ukweli au uongo. Ukisema uongo kuhusu historia hujaandika historia. Kwa hiyo kwenye historia ukweli peke yake husimama. Sasa tafsiri ya matukio mbalimbali ya historia ndio huwa ni mjadala. Alichofanya Mwalimu wenu hapa Mohammed Said ni kuweka tafsiri yake katika matukio ya historia. Ndio maana uandishi wake umejaa "inasemekana".. "iliaminiwa"... "ilisemwa"... nyingi mno. Wakati wowote hakuwa na ushahidi Mohammed anachomokea "Iliaminiwa" hata asipotaja na kina nani na kwanini...

Hatuhitaji kuandika kitabu kingine kwani historia ya Tanganyika imeandikwa kwa kirefu sana na watu wengi tayari - tatizo ni kuwa Mohammed Said peke yake ndio kajaribu kuiandika kwa kutumia prism ya udini. Matukio yote ya historia yetu (au karibu yote) ameyamulika kwa kutumia dini na hivyo mwanga huo wa dini umemfanya aone kila kitu kikiwa na dini hata kisichokuwa cha kidini.
Ndio maana kuna habari ambazo Mohamed hataki kuziongelea.
Mfano, ataongelea sana Nyerere kuishi kwa Sykes lakini hata jibu swali kuhusu mzozo wa umiliki wa Nyumba inayosemekana ilijengwa na Sykes.

Ameshindwa kukanusha yasijetokea yale ya Maryknoll na Mkutano mkuu wa AA 1946.

Mag3 ameuliza sana kuhusu Cecil Matola kilichofuata ni Mohamed kusema huyo alifariki mwaka 1939. Mohamed hakufanya utafiti kuhusu Cecil na jitihada zake kama kiongozi wa chama isipokuwa historia imeruka toka kwa Sykes kwenda kwa Sykes.

Mohamed antuambia role ya Mshume Kiyate( na tunaiheshimu sana) ni kubwa kuliko Cecil Matola.

Mohamed ameongelea kurasa nzima kuhusu Mwapachu na jinsi alivyotoka Makerere kiasi kwamba role ya Kyaruzi kama president wa TAA imekuwa kama haipo.

Ninarudia tena na tena Mohamed hajaweza kuthibitisha kuhusu sehemu kubwa ya historia na inabaki kuwa simulizi tamu la wahenga na malenga kama si ngano.

Mkuu Mkandara ameongelea vizuri sana jinsi wakoloni walivyotufanya tukawa hatujielewi na kwa bahati mabya miaka 50 baada ya wao kurudi makwao wametokea wakoloni wengine wanaotaka kutugawa kama wakoloni kwa kutumia dini.

Baada ya kusema hayo ''inasemekana'' Mkandara si mwislam safi kwasababu hakubaliani na maoni ya viongozi wa dini ya kiislam, naye pia amekuwa BAKWATA!
Hakubaliani na maoni ya msemaji wa waislam bwana Mohamed anayeeleza upande wa pili wa waislam

Hiyo ndiyo philosophy inayotumika kutisha watu!
 
hivi kama red maana yake ni hiyo blue, kwanini usingetumia hiyo red tu au blue tu?
dini yenu lazima ukitaja sentesi kwa lugha ya kiarabu lazima utafsili ndo utaeleweka?
Si anakusaidieni nyie msiojua Kiarabu!!
Kwani nyinyi mkiongea kisambaa kwa waswahili simnatoa tafsiri pia.
 
umejuaje kama wote humu hawajui kiarabu?

MM ubishi wako wakitoto!
Kwahio kama baadhi ya watu hapa wanajua kiarabu plus wewe zisitolewe tafsiri kwa Kiswahili kwa wale ambao hawajui kiarabu?
Haya tuseme wewe umegraduate darasa la kiarabu, je umewafundisha wote hapa kiarabu kufanya kila mtu asihitaji tafsiri.
 
Kaka yangu naona sasa hivi unajadili mpaka Like.
Kwa kweli Ritz kama umeweza kushabikia hayo ya zomba...! sina la kuongeza kwenye hilo...ila siku moja tusije kushtuka mtoto wa Sheikh Ponda akifuata nyayo za mtoto wa Salum Abdalla, naye akifanya utafiti aweze kuandika historia ya harakati za wazee wake katika mapambano ya kuupinga utawala wa Kikwete. Watoto wetu na wajukuu zetu nao watajikuta wakiikosoa hiyo histohisia kama tunavyokosoa histohisia ya Mohamed Said huku wajukuu wa Ritz na zomba nao wakimtetea mwalimu wao kama tunavyoshuhudia.

Ila wakati huo kutakuwa na tofauti, dhihaka na kejeli za wajukuu wenu hazitaelekezwa kwa Kikwete aliye madarakani akiiongoza serikali ya CCM bali zitajikita katika kuulaumu mfumo Kristo wakisahau kuwa shida na taabu walizozipata wananchi kutokana na uongozi dhaifu hazikuangalia dini ya mtu. Inasikitisha sana kuwa chuki zilizopandikizwa vichwani mwao kwa simulizi za barazani toka utotoni kutoka kwenye vinywa vya wazee wao, ndizo zilizowaongoza katika uandishi wao ingawa wenyewe watadai waliyoyaandika ndio ukweli.
 
Last edited by a moderator:
Hasira na kuitana wendawazimu inahusu nini? si uandike ukweli uujuavyo wewe. Hebu jikumbushe kidogo kuwa Mshume alishajitolea kabla ya siku hiyo;


Punguza ghadhab, utaona Mohamed Said anatowa kisa alichokihadithia Nyerere mwenyewe, sasa Mohamed Said atowe kitabu na Nyerere yuko hai amzulie? Nyerere huyu Nyerere? Fikiri!

Samahani kama kutumia neno "mwendawazimu" ni ghadhab. Nilitaka kusisitiza kwamba haingii akilini kwa mtu mwenye akili timamu kwamba Nyerere ataondoka Magomeni, achape mguu hadi Kariakoo kutafuta chakula cha wanae huku hana hata senti tano mfukoni. Ingeandikwa kwamba alikuwa amepungukiwa hela, ingeeleweka. Lakini kusema hakuwa na hela ni beyond imagination. Kuhusu hotuba, imo katika kitabu cha Nyerere, Freedom and Unity. Mohamed anao wajibu sasa wa kutuletea draft iliyoandikwa na Abdulwahid ili tulinganishe tuone ni maneno gani ya Abdulwahid ambayo Nyerere ali incorporate katika hotuba yake.
 
Siku zote huwezi ficha pembe la ng'ombe.

haya sasa yale yaliokuwa yamefichikana sasahivi yapo dhwahir shahir. Je umesikia yale ya kule Buseresere na katoro?
ndicho alichopanda kwa kificho JKN. sasa kipo hewani.
Udini wa Buseresere na Katoro umepandikizwa na Kikwete. Katuambia hapa hapa Mohamed jinsi Waislamu walivyokuwa wakinong'onezana misikitini katika uchaguzi wa 2010 wamchague muislamu mwenzao na siyo yule kasisi wa katoliki. Angekuwepo Nyerere upuuzi kama huu usingetokea. Lakini, but then, ulishatuambia kuwa huna akili kwa hiyo sishangai kwa kauli yako.
 
Samahani kama kutumia neno "mwendawazimu" ni ghadhab. Nilitaka kusisitiza kwamba haingii akilini kwa mtu mwenye akili timamu kwamba Nyerere ataondoka Magomeni, achape mguu hadi Kariakoo kutafuta chakula cha wanae huku hana hata senti tano mfukoni. Ingeandikwa kwamba alikuwa amepungukiwa hela, ingeeleweka. Lakini kusema hakuwa na hela ni beyond imagination. Kuhusu hotuba, imo katika kitabu cha Nyerere, Freedom and Unity. Mohamed anao wajibu sasa wa kutuletea draft iliyoandikwa na Abdulwahid ili tulinganishe tuone ni maneno gani ya Abdulwahid ambayo Nyerere ali incorporate katika hotuba yake.

Jasusi,

Mimi singependa kulirejea suala la Mshume Kiyate na Nyerere.
Halina maana.

Pili suala la pale Kariakoo wana TANU kusaidia harakati kwa hali
na mali ni suala ambalo wala si letu sisi kukaa tukabisha kubwa
khasa ni kwa kuwa hayo yote yalikuwa mambo ya ikhsani.

Ila pale alikuwapo Abdu Sykes, Shariff Attas, Sharif Mbaya Mtu,
Shariff Mohamed na hawa ni watu waliokuwa karibu sana na TANU
na Nyerere.

Kuhusu ile document ni suala nyeti na wengi humu wameumizwa na
taarifa mpya za suala hili.

Kama nilivyoeleza chanzo cha document ile ni TAA Political Sub Committee
iliyoundwa mwaka 1950.

Document hii Abdulwahid Sykes kaitaja katika taarifa yake ya mwaka 1950
kwa wanachama wa TAA na akaeleza mchango wa Earle Seaton katika
kuiandika.

(Huyu Earl Seaton ndiye aliyeandika ''petition ya Wameru iliyosomwa na Japhet
Kirilo UNO katika Meru Land Case 1952).

Sasa document hii ya TAA Political Sub Committee ilizungumzwa katika kuunda
kwa TANU mwaka 1954.

Document hii imepotea haipo popote.

Maktaba ya CCM Dodoma hii document haipo wala Nyaraka za Taifa haionekani
ingawa jalada lipo lakini document imenyofolewa.

Nyaraka za Taifa jalada lipo document haipo na microfilm vilevile haipo.

Binafsi nimeandika makala iliyochapwa katika Africa Events kuhusu kupotea
kwa document za kihistoria.

Sina zaidi cha kuongeza kuhusu document hiyo na hotuba ya Nyerere UNO 1955.
 
Back
Top Bottom