Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Umenigusa sana.Nguruvi3 Mimi ni kijana na kwa bahati nimeyaona pasi jicho la udini yanayoendelea nchi hii. Nakumbuka nikiwa sijafikisha umri wa kupiga kura mwaka 1995 nilikuwa nasikiliza na kufuatilia yale yaliyokuwa yanatokea kwenye uchaguzi ndani ya chama. Kwa kweli nilikuwa shabiki wa Kikwete tena kwa sababu tu alikuwa anaonekana kijana.
Sikumuona kuwa ni Muislam na hata miongoni mwetu walikuwepo wengi sana waliokuwa wanamtaka Kikwete au Salim japo hakuingia kwenye kinyang'anyiro. Na kumbuka hapo nilikuwa Musoma kwa akina Nyerere na hakuna niliyemuona akionyesha hisia za kidini. Rudi 2005 kwangu Salim ndio alikuwa chaguo na nafikiri wajumbe wengi tu wa NEC na mkutano mkuu walikuwa kwenye pande mbili kubwa za Salim na Kikwete...........humo wamo wakristo wengi tu na hawakuuona Uislam wa Kikwete/Salim.
Sasa hapo ndipo naposhangaa hivyo vyanzo vya MS ni vya aina gani. Na hapo huwa najiuliza:
Inawezekana wanaomwambia wanajua anapenda kusikiliza nini kwa hiyo wanampa ukweli uliopindishwa.
Au ni mtunzi mzuri wa ngano mwendelezo, unampa habari kidogo anaongezea nyama kwa wingi ili kufurahisha hadhira yake.
Au kuna mradi anoutumikia ambao unamtaka kujenga ovu lolote kuhusu Mwalimu/Ukristo kufurahisha wenye mradi.
Au ni njia rahisi ya kuwafanya Waislam wajione dhalili na kutofikiria kuweka mikakati ya kujikwamua ki-elimu ili yeye na wenzake wabaki "star" miongoni mwa wajinga!
Au ni chuki aliojengewa na yeye kuikuza kutokana na masimulizi na sasa anaweka "platform" ya kulipa kisasi.
Huwa siishi kujiuliza maswali napowasikia watu kama MS wakiweka jitihada ya kubomoa na kufarakanisha Taifa. Na kwa kweli ukimsoma katikati ya mstari utagundua kuna mwangwi wa wa moja ya maovu hapo juu. Na akishatia neno Uislam basiii wanyonge wake wananywea......Umpinge mtetezi wa "dini" thubutuuu.
Kwasisi wa old school, tumeona wazee wakivaa viatu vimetoboka, shati moja anasubiri likauke aende kazini na mama akijisetiri kwa kitenge kimoja ili watoto wapate ada za sekondari tena za kulipia.
Nimeona kijana aliyefiwa na nduguye ambaye alishauriwa abaki shuleni akihudumia miradi ili msiba ukiisha aongezewe pesa alipe ada. Think about that! kwamba kwenda kuhani msiba itatokea maajaliwa, la muhimu kwanza apate elimu kwasababu nduguye keshatangulia. Katika hali ya ubinadamu haya nimetosa makubwa! kwenye wenye akili haya ni mateso kwenye busara
Nimeona mtu akichukua nduguze bila kujali imani zao ili aende nao Lindi kwasababu nafasi za kufaulu ni kubwa ukilinganisha na mkoani kwake. Nyumba yake ikawa na akina Mwanaidi, Angela, Patrick, Shwaibu n.k. leo wote wapo safi.
Nimeona kule kwetu Mjasani Tanga mtoto akiondolewa shule eti akapate ndoa kwasababu keshavunja ungo.
Vijana wakihimizwa kuvusha magendo kwasababu elimu utaishia kuwa nesi au mwalimu.
Nenda kivinje shule haina wanafunzi, nenda Mkuranga shule ina mwalimu mkuu mmoja anayeitwa Mbwambo akiondoka anakasimu madaraka kwa kiranja mkuu.
Think about that! Mkuranga mahali ambapo Mshume kiYate alipita kwa baikeli akienda rufiji leo Mohamed hajui hilo lililotokea.
Badala ya kwenda kwenye tatizo na kuomba ushauri ni jinsi gani na kitu gani kifanyike(angeungwa mkono sana) Mohamed yupo mezani bize na laptop na tablet akitafuta hadithi za kuamsha hisia, akiwaficha watu ukweli.
Baada ya hapo anapanda ndege kwenda kuonge Ulaya kwa mfumo kristo kwa kutumia lugha ya mfumo kristo.
Nyuma ameacha frustrated society na kwa kuchomeka hisia zake jamii inaanza kurusha mawe.
Mohamed anakimbia ulaya kuonyesha utabiri wake ulivyotimu na kuandika tole la saba.
Wale wasiofahamu tatizo wanabeba magunia wanatoa pesa zao ili kusoma hisia zaidi za uchochezi, Mohamed anaenda toleo la nne. Inakuwa vicious circle! It's immoral, pathetic and libertine.