Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
J,
Ngoja nikupe kitu.
Soma hapa chini na unganisha:
Kwa mara ya kwanza historia ya TANU ilitaka kuandikwa na Abdulwahid mwenyewe.
Baada ya kupatikana kwa uhuru mwaka 1961 na TANU ilipokuwa sasa inataka kujiimarisha kama chama cha umma, inasemekana Nyerere wakati ule Waziri Mkuu alimuomba Abdulwahid aandike historia ya harakati ya Waafrika wa Tanganyika dhidi ya ukoloni wa Waingereza.
moja hiyo...
Maelezo ya Abdulwahid katika kuanzishwa kwa Africa Association inasemekana hayakumpendeza Nyerere, kwa kuwa mwanzo wa harakati dhidi ya ukoloni jina la baba yake Abdulwahid, Kleist Sykes, lilikuwa likitawala.
mbili hiyo...
Historia hii inasemekana haikumpendeza Nyerere na baadhi ya viongozi wa TANU.
Tatu hiyo...
Haukupita muda Abdulwahid akatambua kuwa viongozi wapya walioshika nafasi katika TANU kwa kweli hawakuwa na nia hasa ya kutafiti na kuandika historia ya Tanganyika bali nia na azma yao ilikuwa na kumjenga Nyerere na kumkuza kwa sifa ambazo hazikumstahili.
umejuaje kuwa alitambua hivyo?
Abdulwahid alipong'amua hili haraka akajitoa katika kazi ile. Hata hivyo Dr Kleruu aliendelea na utafiti na akaandika historia ya TANU. Historia hii inasemekana ilifuta mchango mzima wa akina Sykes katika kuunda TAA na baadae TANU.
Ya nne hiyo...
[/quote]Uandishi wa kitabu kile haukutofautiana sana na kitabu cha TANU kilichotoka mwaka 1981 kilichoandikwa na Chuo cha TANU cha Kivukoni.
........[/QUOTE]
Kilichoandikwa na Kivukoni sicho kilichoandikwa na kufanyiwa utafiti na Dr. Kleruu?