Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar



moja hiyo...


Maelezo ya Abdulwahid katika kuanzishwa kwa Africa Association inasemekana hayakumpendeza Nyerere, kwa kuwa mwanzo wa harakati dhidi ya ukoloni jina la baba yake Abdulwahid, Kleist Sykes, lilikuwa likitawala.

mbili hiyo...


Historia hii inasemekana haikumpendeza Nyerere na baadhi ya viongozi wa TANU.

Tatu hiyo...


umejuaje kuwa alitambua hivyo?


Abdulwahid alipong'amua hili haraka akajitoa katika kazi ile. Hata hivyo Dr Kleruu aliendelea na utafiti na akaandika historia ya TANU. Historia hii inasemekana ilifuta mchango mzima wa akina Sykes katika kuunda TAA na baadae TANU.

Ya nne hiyo...

[/quote]Uandishi wa kitabu kile haukutofautiana sana na kitabu cha TANU kilichotoka mwaka 1981 kilichoandikwa na Chuo cha TANU cha Kivukoni.

........
[/QUOTE]

Kilichoandikwa na Kivukoni sicho kilichoandikwa na kufanyiwa utafiti na Dr. Kleruu?
 

J,

Nakuelewa vizuri sana.
Hata mie kote ninakohadhir maswali kama hayo hukutananayo.

Naulizwa si Sheikh Hassan bin Amir na Abdu Sykes walomjenga
Nyerere?

Adam Nasibu si ndiyo aliyekuwa anapiga vita EAMWS?

Lakini Adam Nasib alikuwa na usaidizi wa serikali na vyombo
vyake pamoja na fedha kukamilisha kazi ile.

Mambo ni mengi na sakata hili ni katika mitihani migumu jamii
ya Kiislam kukutananayo.
 

Kilichoandikwa na Kivukoni sicho kilichoandikwa na kufanyiwa utafiti na Dr. Kleruu?[/QUOTE]


MM,

Wala isikupitikie kuwa mimi naweza nikabadilika kwa kutaka
kushinda mjadala.

Hiyo "inasemekana" utakutananayo kwingi katika kalamu yangu.

Maalim wangu kanifunza kuwa mnakasha ni mahali pa kusoma
na kusomesha usiongope.

Si pahala pa kutafuta ushindi.

Sema ulokuwa na yakini nalo na lile usojua lichukue ulitie katika
hazina yako.

Ndo maana unaona nikiulizwa jambo silijui nasema hivyo silijui.
 


Unapoandika historia huwezi kutumia "inasemakana" kama ushahidi. Inawezekana ni mawazo yako tu ndiyo yanasema hivyo kwa sababu hauna ushahidi wa moja kwa moja wa madai yako?

Kwa mfano sasa hivi inasemekana wewe ndio mfadhili mkubwa wa mihadhara ya kidini nchini. Na kwa kufanya hivi umekuwa ukichangia katika kuleta chuki katika jamii.

Inaaminiwa kuwa unapokea fedha kutoka nje ili ulete uchochezi.
 

mpagani akifariki huwa hazikwi kwa sala. Hapa unaitaji data gani mimi kuthibitisha ukweli huo?

Kama huwezi changia kuwa mtazamaji.
 
Inasemekana hata zikiwa elfu moja kuelekezwa kwa mtu ambaye ni mzima na akashindwa kujibu basi huwa inaaminika.
Katika mafunzo ya uislamu kutafuta mchumba pindi binti ambaye ni mwari anapokaa kimya kwa mume aliyeletewa inachukuliwa kuwa amekubali.Ndoa nyingi zinazofungwa kwa mafunzo hayo ya kiroho huwa zinadumu na kuwa na baraka nyingi.
Hata mfumo wa mahakama uko hivyo hivyo.Mtuhumiwa anaposhindwa kujitetea kwa kila shutuma mwisho hufungwa kwani huwa imethibitika kuwa ni mkosa.
Kwa maelezo hayo jipime wewe mwenyewe,Nyerere wenu na historia ya Mohammed Said.
Kwa upande mwengine wewe binafsi imethibitika kuwa ni mtetezi wa mfumokristo hapa JF na huoni haya kujiabisha kwa hilo hata unapokuwa huna hoja.
 

Halafu we ritz jana 14/02 nlikuona unakatisha mitaa ya posta na sutti yako nyeusi.
 
Last edited by a moderator:

Huyo anapingana mradi apinge tu, ukiwauliza, mnaopinga nini? Hawajui.
 

Huyu ndie anataka kuandika kitabu cha historia sahihi na matusi yote haya lakini sio makosa yako ni aliyekuleta mjini kutoka BUTIAMA nono sense kabisa
 
mpagani akifariki huwa hazikwi kwa sala. Hapa unaitaji data gani mimi kuthibitisha ukweli huo?

Kama huwezi changia kuwa mtazamaji.

Ueleweki unasema nini pole sana kama unakereka na michango yangu.
 
Mohamed, si unajua kuwa hapa watu wanasoma kila neno kwa maana yake halisi! Si umefanya utafiti sasa hili neno ''inasemekana'' linahusiana vipi na utafiti.
Hivi hujaliona tatizo hapo, maana ukisema ''inasemekana'' maana yake unajiondoa katika ushahidi na kuweka mzigo kwa mwingine.

Kwangu mimi ukishasema inasemekana basi moja kwa moja akili inanituma kuwa jambo fulani ni simulizi isiyo na ushahidi.
 

MM,

Hizo propaganda za "kupokea fedha" kutoka nchi za nje zimepitwa na wakati sana tena sana.

Propaganda za Sheikh Hassan bin Amir anataka kupindua serikali ya Nyerere zimepitwa na wakati.

Kwa sababu kama litakujaletwa suala la kupokea fedha kutoka nje basi si Waislam watakaosimama
kizimbani.

Ila nitakufahamisha kitu.
Mimi nafahamika katika jamii.

Yangu yote yanajulikana kwani sijapata kujificha.
Unaona hapa nimeingia na jina langu kamili.

Usiniletee mambo yasiyo na maana kwa hisani yako.
Kawatishe wengine siyo mimi.
 

Nguruvi,

Chukua hivyo hivyo hapana shida.
 

Ndo Mohamed Said aje atueleze ni kwa vipi Nyerere hakuitambua familia ya Sykes halafu washiriki katika uongozi ndani ya nchi na nje ya nchi. Waislam kwa kulalalmika, hata mtu asiyejua kusoma na kuandika lakini ameweza kuriri juzuu bila hata kujua anakariri nini, watadai Nyerere ndiye aliyesababisha kwa sababu alikuwa ni MKATOLIKI.
 

Povu la nini mkubwa?
Mzee Mwanakijiji hajasema unapokea pesa kutoka nje kufadhili mipango ya kuleta vurugu na chuki miongoni mwa jamii, ametoa mfano tu madhara ya kusema jambo huku ukitumia maneno INASEMEKANA KUWA, INAAMINIWA...NK. Kuwa huwezi kutumia maneno hayo kama una uhakika jambo unalolisema ni kweli. lakini kama ni fix utayatumia ili kumpa mwanya anayehusika aje aseme ni kweli au si kweli kama ulivyokuja kukanusha mara moja. kuwa makini na argument zako mkuu
 
huyu mfia dini anayejiita mzee mwanakijiji
ni kweli anatumiwa na kanisa na cdm ili kuleta uchochezi
na ndio mana hawezi kuweka jina lake halisi
kama alivyofanya Mohamed Said
 
Last edited by a moderator:
Joka Kuu,

Hata mie nazikumbuka siku hizo.
Kimetokea kitu gani?

Nani kasababisha fitna hii?
nyeje tujikwamue na dhahama hii?

Jibu unalo wewe Mzee Mohamedi. Wewe na wenzio wenye mawazo ya kibaguzi na kichochezi ndio mliotufikisha hapa. Kwa sababu zako tu za kichoyo unaeneza propaganda za chuki badala ya kutafuta maelewano.
Mimi pia nimesoma shule za serikali kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu, na kote nimesoma na waislamu. Sikuwahi kuona wakionewa katika jambo lolote. Katika mitihani yetu ya mwisho kuna waliofeli na waliofaulu, na katika makundi yote mawili ya kufeli na kufaulu walikuwapo wakristo na waislamu.
Huu uchochezi wako unakusaidia nini?
 
Mkuu, hili swali Mohamed amelikwepa sana. Alichokifanya ni kuaminisha umma kuwa Nyerere alikuwa mwendawazimu siku moja akaamka na kuanza kushambulia masheikh kwa vile alitumwa na kanisa.

Ukweli ni huo hapo juu na Mohamed anaujua. Katika kitabu chake ameandika wazi ''radical muslims''.
Sheikh Amir alitaka kung'oa Nyerere kwasbabu tu ni Mkristo mara mbili. Jaribio liliposhindwa wakajificha chini ya kivuli cha EAMWS ambayo nina kuhakikishia haikuwa ya waswahili! Historia yake inaanzia Pakistan,mwaka 1945 na Mombasa.

Nyerere alipogundua hilo na baada ya kunusurika majaribio kabla ya uhuru akautumia uungwana na busara kumuondoa sheikh Amir! vinginevyo angeweza kumdhuru kwasababu uwezo alikuwa nao! hakufanya hivyo.

Mabaki ya Sheikh ndiyo yalimalizwa kabisa 1968 kwa kuua kichaka cha uhalifu EAMWS. Mohamed, tofautisha EAMWS na Uislam, UAMSHO na Uislam, CUF na Uislam.

Kitu kimoja watu wakumbuke, haya tunayoyaona leo ya akina Ilunga na Mohamed kutaka maaskofu wauawe(na wameua Geita) ni zao la Mpakistani mmoja aliyekuwa Mwalimu anaitwa Malik.
Mohamed ni mmoja wa wale watu wa Warsha waliofundishwa utafiti wa elimu ya Tanzania na huyu Mpakistani.

Mpakistan huyu hakujulikana mara ya kwanza na aliishi kama ''zezeta'' lakini alikuwa na ushawishi mkubwa sana hasa katika mambo ya vurugu za kidini. Serikali iliposhtuka tayari alishatoa wahitimu akina Mohamed, it's too little too late.

Kwahiyo unganishe dots za EAMWS, Maliki, Uamsho na Shura za Maimamu.
Fanyeni uchunguzi kidogo, masheikh wote radicals wamesomea Pakistan na kule mwenyeji wao alikuwa Malik.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…